Taifa la Israel halina uhalali wa kumiliki Gaza

Taifa la Israel halina uhalali wa kumiliki Gaza

Kama tukienda kwa staili hii lazima ufahamu Joshua alipowaleta hao wayahudi hapo alikuta kuna watu wanaishi tayari na hta Abraham alihamia tu hapo akikuta kuna wakazi wengine.

Meaning original inhabitants ni 13 tribes of canaan kuanzia gilgashites,Hivites n.k

Ni sawa na leo Wanyarwanda wanavyoidai Kivu eti kisa Mwami wao aliwahi itawala mashariki ya congo miaka 100+ iliyopita!!

Kma ni asili wayahudi hapo sio asili yao bari ni huko Mesopotamia/Iraq alipotoka baba yao. Na kma kigezo cha kwamba waliwahi kuishi hapo leo Wahispania kma taifa wanaweza rudi US nakudai yote kisa to columbus ndio aliivumbua?

Embu tuache dini pembeni tunapojadili hili suala
Hamna banaaaaa.

ISRAEL THE LAND JEWS THE PEOPLE

PERIOD!
 
Watu wamevamia msikiti na kuwanza kuwarushia mabomu ya machozi na kujeruhi, utaacha kurudisha!!! Umeondokewa na wazazi, wakaka, wadada na watoto utakaa kimya!!!! Hata kama ni wewe huwezi vumilia haya mateso.
Shauri zao hayataki kujua ukweli sasa unategemea nini? Tangu miaka zaidi ya 4000 wanatandikwa na kushindwa
 
Sikutaka sana kuingia into details; alicho kisema bwn zitto Jr ndicho hsa historia ya taifa hili la Israel; iko hivi; baba wa taifa hili ndio hasa baba wa Waarabu (Iran, Iraq kwa asili sio waarabu) aliitwa Ibrahim baba yake akiwa mzee Tera, huyu mzee alibahatika kuzaa watoto wa kiume 3, wa kwaza akiwa ndio huyu Ibrahimu ambae ndie focal point ya mjadara huu; hawa watu walikua wenyeji wa nchi ya Uli ya Ukaldayo ambayo ndio Iraq ya leo, Ibrahimu katika kutafuta maisha alihamia nchi ya Caanan ambayo ndio hi inaitwa Palestina au Israel ya leo; mzee huyu aliingia hapo akiwa na mtoto wa mdogo wake anaitwa Lutu, hawa watu 2 walikua na mifugo yao mingi, yaelekea wenyeji wa hapo hawakua wafugaji kiviile kama hizi 2 people, wachungaji wa hawa ndugu 2 wakagombana huko machungani, mzee Ibrahimu akaona isiwe shida, dogo akahamia Sodoma wakati mzee akabaki hapo hapo Caanani/Palestina, kumbuka kipindi chote hiki huyu mzee Ibrahimu hakua na mtoto though alikua na mke, walihamia Misri kwa kukimbia njaa ilioibuka hapo mashariki ya kati, finally alirudi tena hapo this time akiwa na house girl wa Kimisri; miaka kadhaa baadae huyu mzee Ibrahimu alimzalisha huyu house girl wake mtoto wa kiume, huyu mtoto ndio alikuja kutengeneza mataifa 12 ya Kiarabu; miaka 12 baada ya huyu mtoto wa beki 3 kuzaliwa, mkewe Sara nae akashika mimba nae akaza mtoto wa kiume na huyu ndio hasa aliyekuja kutengeneza taifa la Israel na Jordan cause huyu mtoto wa mzee Ibrahimu kwa Sara mkewe alizaa mapacha, mmoja aliitwa Yakobo na mwingine Esau, huyu Esau ndiye hasa baba wa Edom (sasa Yordan/Jordan ) ingawa historia ya nchi hi ni uzao wa watoto wawili, mabinti wa Lutu wale waliozalishwa na baba yao na huyu Esau. Yakobo baadae alibadiri jina kutoka Yakobo kwenda Israel, huyu mwamba alipiga copy za kiume 12 na ndio hayo makabila 12 ya Israel ya leo, waliishi hapo baadae walikimbilia Misri kwasababu ya njaa na nabiii Musa kutoka kabila la Walawi ndiye aliowaongoza ndugu zake kurudi nyumbani though hakuwafikisha na ndipo Joshua kutoka kabila la Yuda ndiye aliyewafikisha hapo panapoitwa leo Israel/Palestina/Caanan; kumbuka haya mambo yametokea miaka zaidi ya 1000 kabla ya Yesu Kristo; wameishi hapo miaka na miaka, mara wapigwe na nchi jirani, sometimes walitekwa mateka baadhi ya vijana wao kwenda nchi zingine nk.
Now confusion inayokuja kuhusu mwaka 1948 iko hivi; kipindi Yesu anazaliwa, dunia ya wakati huo ilikua inatawaliwa na dola ya Kirumi (sasa ni Roman empire au Itali ukipenda) baada ya Yesu kwenda zake huko tunakosoma kwenye vitabu vya dini, hawa jamaa walivamiwa na kupigwa vibaya, wengi wao walikimbilia mataifa mbalimbali, wengine Italy, Africa (Africa hasa Ethiopia, kumbuka Ethiopia/Kushi ilikua na mahusiano ya kibiashara na Israel/mashariki ya kati siku nyingi) wengine walikwenda Asia na Amerika, i hope uliwahi kuiona ile movie ya Escape from Sobibo, inaeleza vizuri, is a true story but also tunasoma katika historia kwamba Hitler aliwaua almost Wayahudi 6,000,000, vita kuu ya pili ya dunia ndio iliwalazimisha wengi kurudi nyumbani hasa kutoka mataifa ya Ulaya, Wayahudi wengi waliobaki huko walikokua ni wale wa Amerika.
Kwa leo niishie hapo
Chief.. Ismael sio baba wa waarabu wote, Ismael kazaliwa kakuta waarabu wapo.
Yeye anasehemu tu ya makabia machache katika waarabu, lakini si waarabu wote.
 
Israel haina mamlaka juu ya Gaza wala Jerusalem wala West bank. Israel ilivamia tu maeneo hayo ya Palestine toka miaka ya 1960s.

Palestine ilikuwepo na kihistoria ilitawaliwa na Uingereza. Je Taifa la Israel lilitawaliwa na nani?

Maana ijulikanavyo kuna jamii ya wana wa israel ila hakuna na hakukuwahi kuwa na taifa la Israel.

USA inalazimisha illegal westbank settlements zilizojengwa na Israel kwa uvamizi ziwe legalized ilhali yale maeneo waisrael wamevamia.
SOma upya historia. Kabla ya Uingereza kuivamia Yuda na Samaria, kisha kuiacha mikononi mwa Jordan, Eneo hilo lilijulikanaje. Usije na propaganda za kijinga za karne ya 19 za arab League
 
srael haina mamlaka juu ya Gaza wala Jerusalem wala West bank. Israel ilivamia tu maeneo hayo ya Palestine toka miaka ya 1960s.

Palestine ilikuwepo na kihistoria ilitawaliwa na Uingereza. Je Taifa la Israel lilitawaliwa na nani?

Maana ijulikanavyo kuna jamii ya wana wa israel ila hakuna na hakukuwahi kuwa na taifa la Israel.
Kwa historia hii ni nchi yao tangu mwanzo na sio kama wewe unavyoaminisha watu. Nenda ktk historia.
 
Sina tatizo la kuwaita wengine HARAMU cause kila mtu ana mtazamo wake; nina tatizo kidogo juu ya uelewa wako wa mambo; yaani unaanza kuizungumzia Israel wakati wa ukoloni? So kwa maneno mengine hujui chochote kuhusu mfalme Daudi, nabii Musa, Suleiman, Yesu nk?
Mkuu tatizo watu hawautaki ukweli huu, kwa asili hii ni nchi yao. Watu wanaangalia kunzia 1900 na sio historia ya nchi hii ya Uyahudi. Jurusalem yote tangu mwanzo (kabla ya Kristo) ilikuwa nchi ya Uyahudi.
Wapalestina walikuwa na wafanyabiashara waliokuja uyahudi kufanya biashara na kuondoka baadae wakayapenda mazingira na kuhamia.
 
Israel haina mamlaka juu ya Gaza wala Jerusalem wala West bank. Israel ilivamia tu maeneo hayo ya Palestine toka miaka ya 1960s.

Palestine ilikuwepo na kihistoria ilitawaliwa na Uingereza. Je Taifa la Israel lilitawaliwa na nani?

Maana ijulikanavyo kuna jamii ya wana wa israel ila hakuna na hakukuwahi kuwa na taifa la Israel.

USA inalazimisha illegal westbank settlements zilizojengwa na Israel kwa uvamizi ziwe legalized ilhali yale maeneo waisrael wamevamia.
Waizrael kwao ni wapi?
 
Ndivyo unavyofikiri, Biblia ni kitabu cha ahadi na unabii pamoja na mambo mengine. Mungu wa Biblia Yahweh aliwaahidi mababa wa Israeli kwamba amewapa eneo hilo kwa ahadi ya milele. Wakimkosea atawahamisha na kuwaondoa hapo ila ni kwa muda tu, baadaye atawarudisha. Kumkosea walimkosea, wakaabudu miungu na misanamu, kuwaondoa aliwaondoa. Lakini wengi wao aliwarudisha miaka takriban 450 kabla ya Kristo. Wakajenga hekalu upya lakini walikuwa chini ya Waajemi, baadaye Wayunani na mwisho Warumi (wakiwa na utawala wa ndani wakati wa Herode). Baadaye wakamkosea Mungu tena wakamuua Masihi. Mwaka 70 AD Warumi wakaja tena wakawahamisha na eneo lao lijabadilishwa jina na Warumi kutoka Yudea kuwa Philistine Asia. Jina Palestine lilianzia hapo, walibaki wahayudi wachache pamoja na Wagiriki wachache. Baada ya mwaka 600AD Waarabu walianza kutanua mipaka yao na baadaye wakaeneza dini ya Kiislamu. Kwa hiyo Wapalestina wa leo ni hao Waarabu wachache walioishi eneo hilo wakichangamana na Wakristo na Wayahudi. Huu mgogoro wa sasa ni tunda la dunia kukataa na kujaribu kubadili hiyo ahadi ya milele kwa Wayahudi kwenye eneo hilo.
Nilisemahapo mwanzo kwamba Mungu wa Biblia ni Mungu wa unabii: nabii zote zinazohusu siku za mwisho duniani hapa zinawaona wayahudi wakiwa na taifa lao na Yerusalem mji wao mkuu.
Sasa tunapata shida sana kwa kujaribu kwa nguvu zote kubatilisha ahadi ya Mungu kwa mababa wa Israel (Abraham, Isaka na Yakobo ndio Israel). Hakuna nguvu, hata dunia yote ikiungana hatuwezi kuwatoa hao jamaa Yersalem. Sio kwa sababu ni wakali wa vita ila tutakuwa tunapingana na ahadi ya Mungu pamoja na neno la unabii. Ninafahamu wapo ambao haya niliyoandika hawayaamini - na ndio chanzo cha shida zote hizo zinazotokea Palestine leo. Ningetamani Dunia yote ingekubali kwamba Mungu ndio mtawala ana haki kumpa mtu yoyote eneo atakalo yeye Mungu. Sisi tukipinga tutakuwa tunapiga mateke mchongoma. Wenye masikio ya kusikia na wenye hekima wanaojitakia amani wao na watoto wao huiombea Israel amani na ustawi. Kwa sababu huwezi kumlanii mtu ambaye Mungu amembariki na tena "hakuna uchawi juu ya Yakobo".
una uhakika waisrael waliosemwa kwenye biblia ni hawa kina netanyahu wanaoukubali ushoga?
 
una uhakika waisrael waliosemwa kwenye biblia ni hawa kina netanyahu wanaoukubali ushoga?
Kwa sababu hamkubali ndio maana amani haitakuwepo. Mmeshaona mara nyingi hakuna muungano wowote wa kijeshi dhidi ya Israel unaofanikiwa. Kwa hiyo kama mnadhani hao ni feki haya endeleeni lakini tusisikie mnalia wala kulalamika. Mimi nilitoa ushauri tu: mtu akitaka amani na mafanikio aitakie amani Israeli. Kama unaona akina Netanyahu ni feki basi tafuta waisraeli halisi uwaunge mkono. La sivyo mtakuwa mnapingana na mpango wa Mungu.
 
una uhakika waisrael waliosemwa kwenye biblia ni hawa kina netanyahu wanaoukubali ushoga?
Halafu kuhusu Wayahudi kuukubali ushoga: kwanza ni wachache sana ambao pia sio wayahudi kwa dini. Watu wa jinsi hiyo wapo kote duniani. Kuna maeneo serikali zao (hii ikiwa pamoja na Israeli) wanakubali kwamba wapo. Kuna serikali nyingine duniani zinakana - ila wapo, ndio sababu zinaweka adhabu kwa atakaye patikana. Dhambi imo ndani ni mioyo ya watu mahali popote palipo na watu utakuta dhambi za aina zote, la maana wewe binafsi umeishinda dhambi? Na si ushoga pekee hata ufisadi, kupenda pesa, uzinifu, uongo, chuki na visasi, uchawi. Hao watendao hayo wote wametenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.
Tukirudi kwa Israeli: wao hawawi taifa teule kutokana na haki yao hapana bali kwa ahadi ya Mungu kwa mababa wa Waebrania. Haya mambo ni tanzi na kisiki cha kujikwaa, wengi wameumia kwa kushindwa kujua Mungu anavyoona mambo.
 
Suleyman Ni mwarabu sio mwana wa Israel kijana. Acha kupotosha umma.KUANZIA MWAKA 1947KUSHUKA CHINI HAKUNA ARCHEOLOGICAL EVIDENCE IONESHAYO WAISRAEL WALIWAHI KUISHI PALESTINA KABLA. ILA KUNA MISIKITI ILOGUNDULIWA TOKA KIAKA YA 600 NDUGU USILETE BVITABU VYA PAUKA NA PAKAWA.KIPINDIPALESTINA IKIWA CHINI YA OTTOMAN NA OMAN IKIGUNDULIKA KM SHIRAZ NA DUBAI IKIJULIKANA KAMA HIJAZ ISRAEL ILIKUA NI MOJA YA ASILI YA KILOWEZI UJERUMANI.EMBU NIPE HISTORICAL EVIDENCE USINIPE HADITH ZA PAUKA NA PAKAWA Yeslikua wafalme wa Palestine but hao walikua ni Waisrael, kumbuka mfalme Daudi alipewa ufalme baada ya kumuua kamanda mkuu wa vikosi wa kivita wa Wapalestina, zamani walijulika kama wafilisti, au Philistines ambao ndio hawa hawa Wapaletina wa leo; kwa ufupi hawa watu wana ugomvi wa miaka na miaka na sio issue ya kutawaliwa na Uingereza au laa. Labda nikupe story ndogo ya huyu waziri mkuu wao wa sasa hivi huyu bwana Benyamini Netanyahu; Huyu jamaa baba yake mzee Netanyahu alikua mwalimu wa dini (rabi) moja kati ya wanae huyu mzee ni huyu waziri mkuu wa sasa na kaka yake aliitwa Jonathan, huyu Jonathan ndiye aliyeongoza ile kitu inaitwa 90 minutes in Entebe, Benyamini alizaliwa hapo hapo mashariki ya kati/Israel/Palestine na huyo kaka yake alizaliwa USA, why USA ni kwamba huyo mzee alikua anatakiwa kwenda kufundisha Wayahudi wenzie huko oversees na wakati mwingine anatakiwa kurudi nyumbani, remember wote hawa wamezaliwa enzi za ukoloni wa Uingereza.
 
Halafu kuhusu Wayahudi kuukubali ushoga: kwanza ni wachache sana ambao pia sio wayahudi kwa dini. Watu wa jinsi hiyo wapo kote duniani. Kuna maeneo serikali zao (hii ikiwa pamoja na Israeli) wanakubali kwamba wapo. Kuna serikali nyingine duniani zinakana - ila wapo, ndio sababu zinaweka adhabu kwa atakaye patikana. Dhambi imo ndani ni mioyo ya watu mahali popote palipo na watu utakuta dhambi za aina zote, la maana wewe binafsi umeishinda dhambi? Na si ushoga pekee hata ufisadi, kupenda pesa, uzinifu, uongo, chuki na visasi, uchawi. Hao watendao hayo wote wametenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.
Tukirudi kwa Israeli: wao hawawi taifa teule kutokana na haki yao hapana bali kwa ahadi ya Mungu kwa mababa wa Waebrania. Haya mambo ni tanzi na kisiki cha kujikwaa, wengi wameumia kwa kushindwa kujua Mungu anavyoona mambo.
Nani kakudangaya ww km hautaki amani usiitakie mema Israel???ndivyo mnavyodangamyana kanisani?Mbona mwaka 1973Misri aliipoga Israel mpk Waziri wao Golda meir akaomba maridhiano?Halafu nyie mnasema Israel ni taifa teule mbona hao waisrael wenyewe hawaitambui biblia na wanawapinga wakristo?Hilo taifa waliloahidiwa na Mungu mbona wamelitafuta kwa kumwaga damu? Ardhi yao walioahidiwa wazayun ni ipi Sinai ya misri walioipora 1967 na kunyang'anywa 1974,ya gollan heights waloipora 1967,Lebanon ama Syria ama palestina?
Kama wao waliahidiwa ardhi kwann hawakuenda ktk hyo ardhi moja kwa moja bali walianza kuleta vita kwanza?
Mbona ukifata archeological evidences haioneshi km Israel waliwahi kukaa plestina nyuma ya miaka 1947???
Kaka watu sio wajinga km udhaniavyo! Nipe majibu ya hayo maswali.
 
Vitabu vya kiimani na kihistoria vinasema Daudi na Suleman ni wafalme wa kiYahudi (Jews). Palestina kma eneo limetambuliwa wakati wa ukoloni lakini kihistoria miji ya kiyahudi kma Nazareth, Yudea, Galilaya ilikiwepo tangu wafalme wa kale wa Wayahudi. Ni kweli wayahudi ambao ndo taifa la Israeli walisambaa na kupoteza utaifa ila eneo walilopo sasa kijiografia na historia ndio haswa asili yao na vizazi vyao viliishi hapo hakuna pengine.
Kitabu kipi cha kiimani kinasema Suleyman myahudi?Km Ni biblia wala usisumbuke kunilaghai maana imejaa vtu unrealistic.
Hao wayahudi hawaitambui biblia wala msahafu madai yenu ya kusema Israel taifa teule hawayatambui na wanatambulika km wapinga dini.
Kama palestina ndipo walipoanzia kukaa miaka ya zamani kwann akat wanarudi middle East hawakuenda palestina directly bali walianzisha vita maeneo tofauti tofauti?
Mwaka 1967 Israel aliipora Misri Sinai na akaipora Syria gollan heights kwa vita iitwayo six days war.Mwaka 1973 misri akampiga Israel na kuwaeka mateka ili waiachie Sinai waisrael wakaondoka vita inaitwa October war ama yomkippur war.
Km Israel kwake kiuhalisia Ni palestina Misri na Syria alifata nn na kwann alihangaika kupora maeneo????
MAJIBU TAFADHALI.
 
... hakuna nchi; wala kabila; wala taifa; wala kipande chochote kiwacho cha ardhi ambacho mipaka yake imejulikana tangu kale; mipaka yake ni imara; ramani ya mipaka yake imetunzwa kwenye droo za Kiti cha Enzi kama ilivyo mipaka ya Taifa la Israel.

Yaani iko hivi, Mwenye Kiti cha Enzi, "akivuta droo" lenye ramani mbalimbali za uumbaji wake, ni Taifa la Israel pekee ambalo ramani yake OG inapatikana kwenye droo hizo tofauti na mataifa mengine ambayo ramani zake utazipata UN na kwenye makabati yaliyojaa vumbi na mende.
Mbona hawakuleta archeological evidence kuthibitisha?
Mbona ukiwahoji waisrael wenyewe wakutajia mlolongo wa historia ya kizazi chao kabla ya Zionism hawajui na hawana???
Chunga kauli bro usimalize maneno wasaidie hayo maswali waisrael kujibu.
 
Kwa muda mrefu sasa tumesaidia watu wengi kupitia ukurasa huu. Pamoja na kuwa na majukumu mengine mengi lakini nimejitahidi mara kwa mara kuwa na muda kidogo kwa ajili ya jamii. Ilifika mahali kila mtu mwenye shida alielekezwa kwenye ukurasa huu. Japo hatukuweza kusaidia wote lakini tulijitahidi kwa kadri ya uwezo wetu kugusa maisha ya wale tulioweza kugusa.

Kutokana na wahitaji kuwa wengi ninyi wenyewe mkapendekeza tuwe na Foundation ili tuweze kusaidia watu wengi zaidi. Kwa miaka zaidi ya miwili nimekua nikishauriwa kuwa na Foundation lakini nikasita. Mwaka huu "kelele" za foundation zikawa nyingi sana. Baada ya kutafakari nikaona umuhimu wa kufanyia kazi wazo hilo.

Kwa kuwa sauti za kuanzisha foundation zilitoka kwenu nilitegemea muwe mstari wa mbele kuhakikisha wazo hilo linafanikiwa. Lakini ni bahati mbaya sana imekuwa kinyume. Mwitikio ni mdogo sana, kuliko challege yoyote ambayo tumewahi kuifanya hapa.

Hii imenifundisha kuwa watu wengi wanapenda mabadiliko lakini hawataki kuwa sehemu ya mabadiliko hayo. Mtu akipata shida anataka aje kuomba msaada hapa, lakini hataki kusaidia wazo la kuwa na taasisi itakayomsaidia yeye na wengine wengi zaidi. Hali hii sio kwamba tu inakatisha tamaa, bali pia inavunja moyo kusaidia wengine.

Anyway, kesho tutahitimisha challenge yetu, na tutaeleza msimamo wetu kuhusu huduma yetu ya kusaidia jamii, ambayo tumekuwa tukiifanya kwa muda mrefu sasa. Tujifunze kwamba, unapotaka mabadiliko hakikisha unakuwa sehemu ya mabadiliko hayo. Usipofanya wewe, hakuna wa kufanya kwa niaba yako.

Kama unataka kuona huduma ya #GiftedHeart ikikua na kugusa maisha ya watu wengi zaidi tuma mchango wako kwenda (M-PESA) 0743339247, Gwakisa Mwakitega AU (Tigopesa) 0715568653, Samson Charles Kamnde AU (AirtelMoney) 0787568653, Samson Charles Kamnde.

#GiftedHeart #RudishaTabasamu #LetLoveLead #MalisaGJ
 
Ni vema mkasoma vitabu vya dini kwa umakini mkubwa maana vimejaa udanganyifu kwa waliorafsiri siko hapa kubishana ila kuhusu Mungu na taifa la Israel nendene mkajifunze au kutafuta ukweli wa bara la Afrika historia yake ya kweli mtaacha kubishana hasa kupitia biblia muisrael halisi ni walikua weusi na wapo Afrik ya kati kushuka chini historia imebadilishwa kuanzia kwa adamu na eva majina si yao Kristo wa kweli muda sana sio huyu tuloletewa na Mzungu na alikuja sababu ya mtu mweusi ambae ndio uumbaji halisi wa Mwenyezi hata hayo si majina yao halisi kila kitu kimebadilishwa sisi ndo tulimuasi Mungu wa kweli ndomn mpk leo mpo utumwani weng bado hatujitambui nchi ya maziwa na asali ni Afrika hao waisrael waliopo pale si halisi ni fake

Msinitukane msibishie bali tafuteni ukweli wewe mtu mweusi ndie taifa la Mungu wa kweli hatubagui ila huo ndo ukweli tujifungue kifikra mtanielewa tafuteni ukweli kabla ya utumwa wazee wetu waliishije na kama fuvu la mtu wa kale lilikutwa olduvai pale ngorongoro means maisha yalianzia huko ikawaje mamb yaruk kwenda kwa wazungu ambako hakujawahi kuwa na masalia yeyote ya viumbe vya zamani....? Iko wap historia ya mtu mweusi? Je km sisi ndo uumbaji wa Mungu ni vipi tuambie wazee wetu hawakumjua Mungu? Kuna mengi yamejificha ni vema kbl hatujaadili ya watu tutafute ukweli unaotuhusu sisi toka uumbaji
 
Back
Top Bottom