Taifa Star kufungwa, tatizo ni uwezo mdogo wa kocha?

timu yetu imefungwa na algeria bao 7-0 na kuondolewa mashndanoni kwa bao 9-2 badala ya kutafuta mchawi mi nazani huu ni wakati muafaka kwa serikali kurekebisha mtazamo kuhusu michezo serikali izingatie kua zaidi ya kuleta furaha kwa sasa michezo pia nia ajira kwa kua tunataraji kupata baraza la mawaziri hv karibuni bas nashauri wateule waje na mikakati ya kuibua na kulea vipaji kwa kuongeza nguvu kwenye michezo ikiwemo kupeleka mashuleni wataalam na vifaa vya michezo vya kutosha lakini pia kujenga vituo maalum vya serikali kwaajili ya kulelea na kukuzia vipaji vya watanzania ikiwa 2tafanya hivyo tutasahau kushndwa
 
This is News Alert: Baada ya kufunga Taifa stars niliondoka kwenda kulala, binafs sikuumizwa na matokeo ni kama niliyahisi kabla. Lakini Ajabu na kweli leo usiku nikiwa nimelala nimepokea Njozi (sio ndoto) njozi.

Njozi imenifunulia tatizo la Timu hii sio Wachezaji, ni CCM, watanzania wengi wananung'unika, wanachuki, wana hasira na CCM na viongozi wake hasa JM, mungu anasikia vilio vyao nchi ina laana. Haiwezi kufanikiwa kwa hakika.

Ikifaniikiwa basi itakuwa mambo ya uzinzi tu kama Big brother lakin napo kuanzia sasa ni ndoto.

Haki wanayonyimwa Watanzania wengi nchi inalaaniwa. Nimeoneshwa mengi ikiwepo suala la zanzibar, warning ilikuwa

MZEE HATOFANIKIWA,
tusisubiri neema. HAIPO.
Manung'uniko ya Wengi walio wasafi yataisimamisha nchi hii kwa muda.

KILIO cha viongozi wa kiroho walio safi, Na wananchi wa kiroho walioombea Taifa hili likapita salama, wameelekeza kwa mungu tena sala zao kumuuliza mungu kwa haki ya walio wengi. AMESIKIA, nimefunuliwa.

HII NYUMBA ITAKWAMA KWA MIAKA MI 5. Tuombe sana.
 
kufungwa 7 ni hatua ya mwisho kabisa ya makosa mengi yaliyopo.. saba sio ishu mbona.. na unapozungumzia 7 zingatia aina ya timu tuliyocheza nayo na kariba ya wachezaji wao..
swala la kocha mkwasa ni kumuonea tu kwa kweli kajitaidi mnooo kuibadilisha timu. goli la mapema lilituchanganya..tatizo linaanza katika mfumo mzima wa uendeshaji soka..
hakuna youth program yoyote ile ya maana tupo tupo tuu.. club hazina misingi mizuri ya kukuza vipaji, ligi ya magumashi, hatuna exposure kwa kuuza wachezaji wengi nje(kwa kina samatta tumeona umuimu wa kuwa na wachezaji nje)
yoooote haya hatuyasemi na kama kawaida yetu tukimbwela tunatafuta mnyonge tunamlisha pilau la miba na kachumbari ya vioo..
tumuache kabis c b mkwasa katika hili..
msilete upumbavu huo kabisa wakumsema mkwasa
 
Sasa Tanzania tunahitaji kocha wa kigeni mwenye rekodi nzuri ya ufundishaji na mwenye kukizi viwango vya kimataifa.
Wabongo hamuwezi kukaa na kocha wa kigeni hata siku moja, sHIDA YENU HAMNA UVUMILIVU
 
7 bila,aibu kubwa sana,uzuri mi ni shabiki wa Nigeria Na Uholanzi,pia Mnazi Wa Arsenal.
 
wtz weng wamekata tamaa sbb ya ccm kila kukicha ni huzun moyon hawana amani ndyo kila jambo halifanikiwi
 
we we ni mpuuzi kocha mbovu INA maana scolari nae alikuwa mbovu mana Brazil walipewa saba..acha ujinga
 
Algeria waliwaheshimu tu marais wetu,ndo maana wakaachia iwe droo wakijua kuwa watawafunga kwao
 
Maximo alianza vizuri na stars na matokeo yalionekana,soka letu lilipanda, tulishiriki CHAN hadi robo fainali. Lkini majungu yamemuondoa tukaishia kuambulia makocha vimeo.
 
Hayo ya Taifa Stars ni matokeo tu ya tatizo na wala sio tatizo lenyewe.Tatizo hasa ni MFUMO MZIMA WA UENDESHAJI WA SOKA katika nchi yetu.Kwa mfano wachezaji wote hao wa timu ya taifa ni ZAO LA KUZUKA,hawana misingi ya kisoka tangu wakiwa wadogo.Bila ya kuangalia mfumo wetu,hata wakina Mourinho na Guardiola timu yetu itawashinda vile vile.
 

Tatizo sio kocha,tatizo ni mfumo wetu wa soka.Hakuna kocha atakayetufaa duniani kama tutaendelea na mtindo wetu huu wa kuendesha soka.Na huyo Maximo hakuwa mzuri kiufundi bali alikua ni muhamasishaji zaidi.
 
Watu wa Dar bila kujali tofauti zenu za kisiasa CCM na UKAWA, kwa pamoja jitokezeni kwa wingi leo usiku uwanja wa ndege kuipokea Stars wakiwa na gunia zito wanaitaji msaada wa kulibeba. Sio tu wakishinda mnajitokeza kwa wingi ata sasa fanyeni ivyo. Huu ni wakati wa kuisoma namba tuisome namba wote kwa pamoja.
 
Vipi magu hajafanya ziara ya kushitukiza TFF? Maana watanzania tumezoea vibaya sisi tumezoea vya kunyongwa sasa vya kuchinja vinatushinda, tumuombe jeche afute matokeo maana sio halali ahahahahaha, Wareno wanasema sete azero.
 
mpira fani za watu sie fani yetu kufuta matokeo ya urais zanzibar
 
Halafu mnasema hapa kazi tu. Mambo ni yale yale chini ya ccm msitegemee jambo jipya lolote lile. Labda maigizo kuwa mengi.
 
Tatizo sio kocha,tatizo ni mfumo wetu wa soka.Hakuna kocha atakayetufaa duniani kama tutaendelea na mtindo wetu huu wa kuendesha soka.Na huyo Maximo hakuwa mzuri kiufundi bali alikua ni muhamasishaji zaidi.

umeongea ukweli ambao wengi hawataki kuukubali,
kuwa kufanya vibaya kwa stars ni mfumo mbaya wa sok
tulio nao hapa nchini, kuanzia kuvumbuavipaji, kukuza vipaji ,
kuvitafutia fursa nzuri (hasa ulaya) vipaji vyetu,
ligi za madaraja ya chini mpaka ligi kuu kuwa mbovu kabisa,

kwahiyo kilichotokea kwa stars ni reflection ya mambo yote hayo.

Kufungwa 7-0 , na hivyo jumla kutolewa kwa goli 9-2 ni aibu kubwa sana
kwa soka letu na kina samata tunawatia gundu baya sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…