Taja JF member au members ambao una hamu kabla hujatangulia mbele za haki angalau uwe umewajua

Taja JF member au members ambao una hamu kabla hujatangulia mbele za haki angalau uwe umewajua

Naamini kabisa kwamba wote tuliopo humu jf tuna umuhimu wetu kwa namna moja au nyingine ila hata hivyo haiondoi ukweli kwamba kuna baadhi ya wenzetu humu ( members ) ambao michango yao na uwasilishwaji wake huwa na mvuto sana kiasi kwamba inafika muda mtu unakuwa una hamu sana siku itokee tu uweze kuonana nae au umuone mubashara kabisa ili roho yako isuuzike.

Hivyo leo nimeona siyo vibaya nikiwashirikisheni nanyi ili kwa pamoja tuweze kuwataja hao members au member ambaye labda unaombea usitangulie kwanza kwa Mwenyezi Mungu Mbinguni kabla bado hujaonana au hujakutana nae kwani labda unampenda kiuchangiaji wake humu na anakuvutia sana na kila mara hukosi kumfuatilia mabandiko yake au mada zake.

Kwa kuanzia tu mimi natamani sana siku moja niweze kuonana na hawa members wa jf wanaonivutia na kunifurahisha mno hasa kwa aina ya michango yao na hata uchangamfu wao wa kiuchangiaji:
  1. Maxence Melo
  2. Mike Mushi
  3. Asha Dii
  4. Bridger
  5. Active
  6. Reserved
  7. Silencer
Karibu na Wewe Mkuu uweze kutaja members wako unaowakubali sana hapa jf.
Hiyo list yako sijui hata mmoja labda huyo namba moja au hao wengine mamluki mkuu
 
Kwa kuanzia tu mimi natamani sana siku moja niweze kuonana na hawa members wa jf wanaonivutia na kunifurahisha mno hasa kwa aina ya michango yao na hata uchangamfu wao wa kiuchangiaji:
  1. Maxence Melo
  2. Mike Mushi
  3. Asha Dii
  4. Bridger
  5. Active
  6. Reserved
  7. Silencer
Karibu na Wewe Mkuu uweze
Wewe unahatari...yani unataka kuonana na Mods..?
 
Back
Top Bottom