Tajiri MO hebu punguza Sifa katika kipindi hiki cha Usajili, unataka makombe yote ubebe wewe? Bienvenu Valentin NOMA

Tajiri MO hebu punguza Sifa katika kipindi hiki cha Usajili, unataka makombe yote ubebe wewe? Bienvenu Valentin NOMA

Mkono Mmoja

JF-Expert Member
Joined
Jan 26, 2019
Posts
3,359
Reaction score
6,568
Bila ya Salamu.

Huwa najiuliza nilichelewa wapi kujiunga na Simba Sc? Mpaka leo nikifikiria nakosa majibu.

Kifupi katika hiki kipindi cha wiki mbili nimeshuhudia chama langu jipya likifanya usajili wa kufuru. Magugu na mapandikizi yaliyokuwa yakihujumu timu yetu yametolewa na kuletwa vyuma vipya virudishe makali ya Simba.

Wahenga walisema Simba halali na njaa ila anaweza kuchelewa kula na hili nimeliamini kwa sajili za kimataifa zinazofanywa kimafia na Tajiri namba moja kijana Africa, namzungumzia si mwingine bali ni Trilionea Mohammed Dewji.

Leo hii ametangazwa beki wa kushoto ,mzaliwa wa mwaka 2000 (Kidume cha 2000) ,mchezaji wa timu ya Taifa ya Burkina Faso ,kinda mwenye miaka 24 , si mwinngine bali ni VALENTIN NOUMA.

Ni left back mwenye nguvu na kasi ya ajabu ya kupanda kushambulia na kuzuia huku akiwa ni specialist wa mipira iliyokufa , africa hakuna wa kumfananisha nae labda kwa karibu uwezo wake unafanana na kiungo wa westham united ,James Ward prowse. Simba sasa hivi licha ya kuwa itapata mabao mengi kutoka kwa viungo na washambuliaji wake bado pia itafaidika kwa magoli yatakayotokana na mipira iliyokufa (dead balls).

Bienvenu Valentin Nouma (aka Van NOMA)

Kazini kwa Tshabalala kuna Kazi.
IMG-20240707-WA0014(1).jpg
 
mnakuwaga na mbwembwe baadae misamiati inaanza kubadirika! utasikia mangungu toka...😂
Tutakutana katika Live threads.

Hersi yupo pharmacy anatafuta metronidazole baada ya kusikia hizi sajili
 
sawa mbwembwe zenu ndo huwa hivihivi ati mnawachezaji warefu kushinda goli... 🤣
Wachezaji wetu hawaruki wanatulia tu mpira unagonga kichwani unaingia nyavuni....oyaa huyu mwamba Valentin ni NOMA anapiga cross balaa yaani kama Marcelo hivi alivyokuwa real madrid
 
Bila ya Salamu.

Huwa najiuliza nilichelewa wapi kujiunga na Simba Sc? Mpaka leo nikifikiria nakosa majibu.

Kifupi katika hiki kipindi cha wiki mbili nimeshuhudia chama langu jipya likifanya usajili wa kufuru. Magugu na mapandikizi yaliyokuwa yakihujumu timu yetu yametolewa na kuletwa vyuma vipya virudishe makali ya Simba.

Wahenga walisema Simba halali na njaa ila anaweza kuchelewa kula na hili nimeliamini kwa sajili za kimataifa zinazofanywa kimafia na Tajiri namba moja kijana Africa, namzungumzia si mwingine bali ni Trilionea Mohammed Dewji.

Leo hii ametangazwa beki wa kushoto ,mzaliwa wa mwaka 2000 (Kidume cha 2000) ,mchezaji wa timu ya Taifa ya Burkina Faso ,kinda mwenye miaka 24 , si mwinngine bali ni VALENTIN NOUMA.

Ni left back mwenye nguvu na kasi ya ajabu ya kupanda kushambulia na kuzuia huku akiwa ni specialist wa mipira iliyokufa , africa hakuna wa kumfananisha nae labda kwa karibu uwezo wake unafanana na kiungo wa westham united ,James Ward prowse. Simba sasa hivi licha ya kuwa itapata mabao mengi kutoka kwa viungo na washambuliaji wake bado pia itafaidika kwa magoli yatakayotokana na mipira iliyokufa (dead balls).

Bienvenu Valentin Nouma (aka Van NOMA)

Kazini kwa Tshabalala kuna Kazi.View attachment 3035728
Simba huwa inakuwa team maarufu sana kipindi cha usajiri na kile cha pre-season, ikishaanza ligi tu ni vilio na malalamiko
 
Huyu si alikua GEITA huyu iliyoshuka daraja?

#YNWA
Kwani ajabu,tunasajili uwezo wa mchezaji au timu?

Liverpool ilishawahi kusajili
Xherdan Shaqiri wakati stoke city imeshuka daraja.

Andy Robertson wakati Hull city iliposhuka daraja.

Wijnaldum wakati Newcastle iliposhuka daraja.

Danny Ings wakati burnley iliposhuka daraja

Charlie Adam wakati Blackpool iliposhuka daraja.

Jermaine Pennant wakati Birmingham city iliposhuka daraja

peter crouch wakati Southampton iliposhuka daraja.

Je hawa walikuwa wachezaji wabaya?
 
Back
Top Bottom