Aisee kweli, ila yupo mmoja hivi na nikabila hilohilo, Bwana mmoja akiwa ameoa wake wawili kafa na kuacha mali kibao yakiwemo mashamba ,majumba ,magari, n.k ila yapo mashamba mawili yale hata kwenye Miradhi hayakuepo, yaliwekwa KWa ajili ya mjomba wake aliemlea akiwa mdogo baada ya mama yake kufa, Tanga
Huyu bwana wa kabila hili alikua rafiki wa karibu wa marehem, so baada ya kifo Cha rafiki yake akajisogezea mke mdogo, na huyu ndo alikua na document nyingi za mali ya marehem , akafanya alivyojua familia ikaja jikuta mali zote zimeangukia kwenye mikono ya Mangi
Mwaka flani nikawa Tanga mjomba mtu tukakutanishwa katika harakati za kutafuta shamba Kama eka 20 hivi , jamaa akasema lipo , siku nikaenda kukagua kweli ni zuri, kuanzia udongo , tukapatana bei ,nikamlipa KWa kufuata taratibu zote,
Kama miezi miwili Mangi anajitokeza Kua nalo shamba lao, vitisho kibao, ila uzuri muuzaji yupo, Sasa tokana na vitisho alivyokuja navyo kwangu, na KWa kua nilishaelezwa A-Z ,nilimwambia ukweli, kwamba Sasa naomba tubambane maana shamba nimeisha nunua, na muuzaji atakua shahid YANGU tu ,asisumbuliwe, ila Mimi na wewe na pesa zako tupambane KWa namna yoyote anataka,
Jamaa alitoa povu ,Mara yeye ndo mwenye Tanga , Mara nini, akasema ananipa mwezi mmoja niwe nimedai pesa KWa elieniuzia vinginevyo yatanikuta,
Nami nikamwambia nakupa wiki MOJA utakuja nipigia magoti Hapa, Kama utani hivi, rafiki wakasema niachane na shamba jamaa, sio mzuri hasa kwenye Mambo ya giza, nikawambia nataka nimuone jeuri yake mpaka mwisho, shamba nimeisha nunua sirudishi shamba maana ni utapeli anataka fanya,
Siku sita zikakata huku msg za vitisho vya KILA aina , Mie Kimia,
Siku tisa anatokea lushoto kapiga Mueleka wa Adabu, miguu yote vunjika vunjika, sijui alikua anatoka kufanya nini, badae mwili naambiwa ukaanza umuka Kama mpira hapo Bombo hosp,na ukweli sikumfanyia lolote la kishirikina
Sasa wapambe wakawa wanazileta kwangu nami nakazia kwamba ataondoka si nilimpa siku 7 atakuja niomba msamaa,
Wiki ya pili ndugu zake wananitafuta ,kwamba kawatuma Mambo ya shamba yaishe na angependa nikaonane naye hospital , Wala sikwenda , ila niliwambia mwambie yameisha, alikuja kupona but with much respect to me , mpaka leo shamba lipo ,
Note ,Dhuluma sio nzuri, Kama mtu alikopa bil 1 ,KWa jengo la gharama ya bil 10 au na kuzidi, kwanini basi msikubaliane hata KWa kuliuza upate Chako na KINGINE apewe, haya ni maisha ya kupiga,
Utakua nyumba 100,200 ila utazikwa nazo ? Na je unafikili utaweza fikia miaka mia ukiwa hai ,KWa maisha ya Sasa lazima utakua umefukiwa, tuache tamaa