Taka zimemwagwa Mtaani Msimbazi B, hii ni hatari sana kwa Watumiaji wa Soko la Kariakoo

Amos Gabriel Makala, huu mkoa umekushida mapema sana. Dar es Salaam imekuwa ya hovyo sana. Hebu angalia soko la Ilala ofisi zako metre 50 toka lilipo soko. Nina imani halufu mbaya inayo toka pale inaingia kwenye ofisi zenu. No wonder Ndiyo maana wakati wote mmefunga madirisha yenu. Mh Makala amka, Tembelea jiji uone shida zetu.
 
Duuh mkuu upo ndotoni ama mie ndio nimelala??

Makala si ni katibu wa itikadi na uenezi huko CCM kwa sasa?

Na Albert Chalamila kawa nani kwa sasa huko Dar es salaam?
 
CCM hawataki ulunganishe na SI unit ya mfumo aliokuwa nao JPM. sasa kila wanachofanya kina warudia.Morogoro alikuepo kanjegele ,alifanya usafi manispaa yote hadi huku Pembezoni kuliwekwa wadumpo ya kuchukuliwa na loli la taka,wakamfitini kaondoka sasa kati kati ya mji tu pachafu.huku pembezoni ndio waneondoa yale madampo.
Ni bora tuamue kazi kwa sifa na vigezo na sio presha za mwenye cheo.
 
Ulikuwa jela au ulikuwa kwenye coma sasa ndio unazinduka!
Amos Makala sio Mkuu wa Mkoa wa DSM.
 
Ndg unaandika kwa uchungu kweli ila sasa haujui hata RC wa Dar ni nani
 
Reactions: Tui
Huu si uungwana kabsa unatupaje uchafu karibu na biashara za watu😝
 
Ndg unaandika kwa uchungu kweli ila sasa haujui hata RC wa Dar ni nani
Ndugu yangu matatizo ya Dar ni mengi mno yametupasua vichwa. Ni nani mkuu wa mkoa?...... Ahaa Albert Chalamila. Ana maneno meeengi sana huyu vitendo vidogo
 
Duuh mkuu upo ndotoni ama mie ndio nimelala??

Makala si ni katibu wa itikadi na uenezi huko CCM kwa sasa?

Na Albert Chalamila kawa nani kwa sasa huko Dar es salaam?
DAR ni pasua kichwa.... Ni Chalamila
 
"Suala la uchafu Dar ni technical mno, watanzania hamuwezi kulielewa"

Ndiyo ufafanuzi utakaotolewa na wenye mamlaka yao.
 
Amos Makala unisamehe huko uliko. Nime kutuhumu bure kwa matatizo ya watu ambao mnatakiwa kuwa simamia.
 
Khaaa mbona dar wachafu sana ni jini Hilo kweli?🥺 🥺
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…