TAKUKURU: Faili la Uchunguzi wa aliyekuwa Mkurugenzi wa TPA lakamilika, imebaki ofisi ya CAG kumaliza mchezo

TAKUKURU: Faili la Uchunguzi wa aliyekuwa Mkurugenzi wa TPA lakamilika, imebaki ofisi ya CAG kumaliza mchezo

Wasukuma kazi mnayo,,kwaiyo unataka uyo jambazi Kakoko asishtakiwe
Kwa bahati mbaya nje ya utani sijawahi kuwa na ukaribu wa vinasaba(kwa maana ya mimi kuwa msukuma) wala kimaslahi(kwa maana ya mimi kuwa mmoja ya waliokuwa wanufaika wa sukuma gang)

Hoja ya msingi hapa TAKURU waache kufanya kazi kufuata upepo na matamko ya kisiasa enzi za meko tulisikia wengi uchunguzi wao umekamilika matokeo yake hatuoni kesi zao mahakamani ndio maana napata wasiwasi na hili pia ndio maana natoa tahadhari
 
Hii kesi ya hawa mabwana ni uhuni mtupu!
Hakimu wa kweli ni Mola, kwake haki itapatika siku moja, ni jambo la muda tu.
 
Dar es Salaam. Taasisi ya Kuzuia na Kupamabana na Rushwa (Takukuru) imesema imekamilisha faili la uchunguzi kuhusu tuhuma zinazomkabili aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Deusdedit Kakoko.

Machi 30, mwaka huu taasisi hiyo ilimkamata Kakoko ili kuhojiwa kuhusu tuhuma za ufisadi zilizomkabili ikiwa ni siku mbili baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kuagiza asimamishwe ili kupisha uchunguzi kuhusu udokozi wa fedha za umma.

Rais Samia alimwagiza pia Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Dk Charles Kichere kuchunguza jinsi Sh bilioni 3.6 zilivyotumika kwenye mamlaka ya bandari.

Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Brigedia Jenerali John Mbungo amesema uchunguzi dhidhi ya bosi huyo na maofisa wengine umekamilika kwa asilimia 98.

“Asilimia mbili zilizobakia ni taarifa ya CAG ambayo ni muhimu sana, bila hiyo hatuwezi kwenda mahakamani.”

Mbungo alisema ripoti ya uchunguzi huo inahusisha pia sehemu ya taarifa ya CAG ili kudhibitisha tuhuma zinamkabili.

Chanzo: Mwananchi

Pia soma:
Sukuma Gang watakuja kupinga na hii!!
 
Hao nafikiri, next appearance wataachiwa huru either kwa mashsrti au bila masharti. Mbaya wao hayupo tena.
Hela wamechukuwa wao , na nchi ndio ili guaranty mkopo, hivyo standard charted bank Malaysia wana subiri hela yao.
Ina maana serikali ikiwachia jamaa , unalipa hiyo hela mara mbili
 
Hivi ule uchunguzi wa akina Andengenye(kwasasa ni RC alikuwaga kamshina wa zimamoto) na kangi uliishia wapi? Takukuru waache kufanyia kazi maagizo ya kisiasa haya ya viongozi wa kitaifa
Andengenye alizuga kwa kuomba msamaha baadae jiwe akamzawadia uRC.
Kangi uelekeo wake ndo sikuufuatilia ila kiufupi hakukuwa na mwendelezo wa kesi.
 
Andengenye alizuga kwa kuomba msamaha baadae jiwe akamzawadia uRC.
Kangi uelekeo wake ndo sikuufuatilia ila kiufupi hakukuwa na mwendelezo wa kesi.
Kabisa TAKURU nayo inabidi iangaliwe upya either kwa kuiongezea meno kisheria na kikanuni au ufumiliwe upya kwenye safu yake ya uongozi
 
Dar es Salaam. Taasisi ya Kuzuia na Kupamabana na Rushwa (Takukuru) imesema imekamilisha faili la uchunguzi kuhusu tuhuma zinazomkabili aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), Deusdedit Kakoko.

Machi 30, mwaka huu taasisi hiyo ilimkamata Kakoko ili kuhojiwa kuhusu tuhuma za ufisadi zilizomkabili ikiwa ni siku mbili baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kuagiza asimamishwe ili kupisha uchunguzi kuhusu udokozi wa fedha za umma.

Rais Samia alimwagiza pia Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Dk Charles Kichere kuchunguza jinsi Sh bilioni 3.6 zilivyotumika kwenye mamlaka ya bandari.

Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Brigedia Jenerali John Mbungo amesema uchunguzi dhidhi ya bosi huyo na maofisa wengine umekamilika kwa asilimia 98.

“Asilimia mbili zilizobakia ni taarifa ya CAG ambayo ni muhimu sana, bila hiyo hatuwezi kwenda mahakamani.”

Mbungo alisema ripoti ya uchunguzi huo inahusisha pia sehemu ya taarifa ya CAG ili kudhibitisha tuhuma zinamkabili.

Chanzo: Mwananchi

Pia soma:
CAG anaingiaje hapo tena sasa
 
Hakuna serikali isiyokuwa na madudu hata hii utakuja kusikia tu ni Jambo la muda.
Uzuri serikali hii haijifanyi kuongozwa na malaika mkuu kama ile iliyopita,ndio maana hata yakitokea madudu hakuna atakayeshtuka.
 
Back
Top Bottom