TAKUKURU: Kwenye TFF kuna hela zimetumika vibaya

TAKUKURU: Kwenye TFF kuna hela zimetumika vibaya

Sasa tunamtaka Mwakyembe ambaye ndio waziri mwenye dhamana ya Michezo aje hadharani na kutuambia wazi, zile pesa ziliingia akaunti gani, nani alipewa au zilitumikaje?
 
Kama Pesa zile zilitolewa na serikali ili kutumika katika maandalizi ya mashindano yaliyokuwa yanaratibiwa na TFF, na TFF hawakuzipokea, kwanini TFF walikuwa kimya muda wote huo?
Kwanini hawakuhoji ziliko hizo pesa?
 
Hope hao TAKUKURU wanajua masuala ya football huwa hayapelekwi mahakama za kawaida, ndio maana wanawaambia direct warudishe hizo fedha.

Wakijichanganya tutafungiwa na wenye mpira wao.

Sent using Jamii Forums mobile app
Fedha siyo suala la mpira wa miguu (Football) bali ni wizi kama wizi mwingine. Kwa kuwa TFF wamekanusha kuwa fedha za serikali hazikuingia kwenye akaunti yao basi TAKUKURU wafuatilie kwa Doto wa hazina, huenda zilipigwa juu kwa juu au ni ahadi hewa ya kujitafutia umaarufu wa kisiasa.
 
nilimuonya karia kitambo sana !
Juzi jana kashinda nyumbani kwa Naibu Rais Daud Bashite akimlilia amwambie mtukufu magufuli amlinde awambie Takukuru wapige kimya waseme wamechunguza wakakuta aliyeiba pesa kakimbia Nchi au kafa.
 
Kama Pesa zile zilitolewa na serikali ili kutumika katika maandalizi ya mashindano yaliyokuwa yanaratibiwa na TFF, na TFF hawakuzipokea, kwanini TFF walikuwa kimya muda wote huo?
Kwanini hawakuhoji ziliko hizo pesa?
Zanzibar-ASP umeuliza swali la msingi kabisa. Na hapo ndipo kuna giza au UKAKASI
 
Wallace Karia alitumia hila mbaya sana kupata kuwa Rais wa TF. Alitumia nguvu za Serikali kupitia Mkurugenzi wa Mchezo ambaye ni Katibu wa BMT kuhakikisha kuwa wakati wa uchaguzi wa TFF May 2017, Jamal Malinzi anakuwa rumande kwa mashtaka yasiyo na dhamana. Kweli Jamal Malinzi alikamatwa akudunguliwa mashtaka ya kutakatisha fedha (AML).

Kwenye uchaguzi Karia akapita dhidi ya ushindani hafifu. Pia na Michael Wambura naye anashinda kama Makamu wake. Baada ya miezi 6 Karia akamuengua Wambura aliyechaguliwa kihalali kama Makamu wa Rais wa TFF. Hatimaye naye Wambura akaanza kutafuta haki yake kwa kupitia mifumo ya ndani ya TFF na BMT lakini akashindwa. Wambura anaamua kwenda Mahakamani ambako suala lilikuwa lina dalili zote kuwa angeshinda.

Karia alamuwahi kwa kumpeleka TAKUKURU na kifunguliwa mashtaka ya kutakatisha fedha pia. Kiufupi wote Wambura na Malinzi wako huru kwa namna tofauti ila ukweli ni kwamba Wllace KARIA aliwabambikizia zile kashfa ili apate ile nafasi aje kufanya UFISADI bila kudhibitiwa.

Ngoja tusubiri nini kitajiri kutoka TAKUKURU
Ukiua kwa upanga lazima ufe kwa upanga. Daadadadekiiiii
 
Hope hao TAKUKURU wanajua masuala ya football huwa hayapelekwi mahakama za kawaida, ndio maana wanawaambia direct warudishe hizo fedha.

Wakijichanganya tutafungiwa na wenye mpira wao.

Sent using Jamii Forums mobile app
Karia na kidau wameagiza kamati za ufundi toka Somalia Sudan kusini pia na wamemuomba Le mutuz awasaidie ile kamati ya ufundi ya Daud Bashite na cyprian Musiba iweze kuwasaidia Takukuru wasione kitu.
 
Kama Pesa zile zilitolewa na serikali ili kutumika katika maandalizi ya mashindano yaliyokuwa yanaratibiwa na TFF, na TFF hawakuzipokea, kwanini TFF walikuwa kimya muda wote huo?
Kwanini hawakuhoji ziliko hizo pesa?
Kuna vitisho hutolewa chini kwa chini na wafuasi wa serikali wenye nidhamu ya woga ambao wanaweza kuzuia kuihoji serikali!
 
Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa imesema shirikisho la mpira(TFF ) kuna hela zimetumika vibaya,baadhi ya watuhumiwa wameitwa kuhojiwa na nyaraka mbalimbali zimechukuliwa .

TAKUKURU imesema watu hao wana hiari ya kurudisha hela au kusubiri uchunguzi ukamilike.

Mkurugenzi wa TAKUKURU Brigadia John Mbungo amesema Kwenye shirikisho la Mpira nchini TFF Kuna Fedha zimetumika vibaya amesema baadhi ya wameitwa na kuhojiwa na nyaraka mbalimbali zimechukuliwa

> Amesema kuwa watu hao wana hiari ya kurejesha fedha ama kusubiri uchunguzi ukamilike

>. Amesema kuwa miongoni mwa fedha hizo ni zile zilizo tolewa na Rais John Magufuli

TFF wajibu > Baada ya TAKUKURU kusema itawahoji TFF kuhusu Bilioni 1 ya AFCON ya vijana iliyotolewa na Rais Magufuli, TFF yasema haijawahi kupokea fedha hizo


NB: Kuna nini TFF kwanini kila awamu inayoingia lazima ipige hela .
KARIA ni mtu wa system, wanajua aliyekula hela , hazijaliwa TFF, makada wamepiga na itaisha mama msabilioni ya kikwete yalipigwa na watu kwa sasa wanajiita MATAGA
 
Ila kuna uhakika wowote kama Rais alitoa hiyo hela ?isije ikawa changa la macho,kama alitoa alimpa nani wakati TFF wamesema haikuingizwa kwenye account yao
KARIA ni mtu wa system, wanajua aliyekula hela , hazijaliwa TFF, makada wamepiga na itaisha mama msabilioni ya kikwete yalipigwa na watu kwa sasa wanajiita MATAGA
 
Ila kuna uhakika wowote kama Rais alitoa hiyo hela ?isije ikawa changa la macho,kama alitoa alimpa nani wakati TFF wamesema haikuingizwa kwenye account yao
Umesema vyema sana, assuming ametoa hiyo hela, mlipaji mkuu ni HAZINA kupitia mpwa wake bwana DOTTO, sasa mpwa wa MAGUFULI Ndiye aseme aliweka akaunti ipi?
Huo uchunguzi unafanywa na mwanafunzi wa sekondari Marekani ila hapa haukamiliki ndani ya miaka 10.
Kumbuka suala la Kangi lugola mpaka leo wanachunguza, ukiwauliza wanakwambia usitupangie, by the way, wameiba hilo swala kuwafanya msahau KOONA na ujinga wa microphone ya dodoma kuwapa watu ubunge ambao walisha jiuzulu huku MATAGA wakipiga makofi bila kujua ni fedha zao
 
Juzi jana kashinda nyumbani kwa Naibu Rais Daud Bashite akimlilia amwambie mtukufu magufuli amlinde awambie Takukuru wapige kimya waseme wamechunguza wakakuta aliyeiba pesa kakimbia Nchi au kafa.
Hapo Bashite lazima amtoe mkwanja alionao mpaka afirisike. Hiyo ndiyo kawaida ya Bashite
 
Back
Top Bottom