TAKUKURU mchunguzeni Mkuu wa Wilaya Morogoro, anaitumia ofisi yake vibaya

Huyo msando ni mwizi anashirikiana na mgambo kukamata bajaj zinazopakia maeneo waliyopiga marufuku kusimama na wakikukamata wanapiga faini wanayoitaka wao kati ya 50000 na 30000 na ukizingua wanakuweka polisi na bajaj inaandikwa asitoke kwa amri ya mkuu wa wilaya, kuna jamaa yangu ilimtokea hii akagoma kulipa hadi msando mwenyewe akaenda pale sentro akamuuliza jamaa kwanini hutaki kulipa ni nani anakupa jeuri?
 

Utaambiwa una chuki binafsi.

Uchunguzi wa vyombo vya dola utasaidia kukomesha haya.
 
Hivi Wakili Msando si ana kashfa ya kutapeli fedha za yule mama mteja wake ambaye alishinda kesi dhidi ya Tigo? Nadhani zilikuwa milioni 165 kama sikosei ambazo alizichepusha zikaingia kwenye akaunti yake binafsi. Au lile soo limeshaisha?

Kama bado, basi jamaa ajiangalie sana. Takukuru ya sasa hivi iko serious mno, CP Hamduni ni muadilifu na hapendi janjajanja. Haya mambo yake ya utapeli yatamcost.

Nakazia hoja; ACHUNGUZWE.
 
Kwani hapati mshahara na malupulupu mengine?Hawa wanaishi kwa starehe kuliko hata mjomba wangu kule namasakata ambaye anaenda kufundisha hadi jumamoc
Mwalimu wa Afrika mashariki mimi huwa namuita masikini na nitaendelea kumuita hivyo! Na hata akijaribu kula hekaluni kwake atashikwa tu afungwe kirahisi kabisa.

Mkuu wa Wilaya mshahara na hayo unayoyaita malupulupu hayatoshi hata kidogo kama una akili za kitajiri
 
Hayo unayosema sio yake. Yeye alinukuliwa akisema anajitolea mshahara wa uDC na hatarajii malipo. Leo anakuja kudai kwa nguvu na vitisho juu ndio inatia mashaka. Na hajahukumiwa, nimewaomba TAKUKURU wachunguze, hilo lina ubaya gani?

Wewe unaona hilo linawezekana? Yani akopee mshahara wake akatwe yeye kwa mslai ya machinga!!! Unaonekana una jambo na huyo jamaa maana unaandika kiudaku udaku alafu ni kama umepaniki kakufanyaje huyu mtu? Haya evidence iko wapi ya Haya unayosema?
 

Bajaji ilikamatwa kwa kosa gani?
 

Hatuwezi kuwa na TAKUKURU ambayo inaendeshwa kwa style hii. Kwamba kila anayeamka na lake kichwani (hata kama ni kujaribu kulipiza kisasi kwa mpenzi aliyebwagana naye) basi hilo ndilo linakuwa agenda ya TAKUKURU. That isn’t how an institution should be run.

Wewe kama ni whistleblower fuata njia sahihi ili taarifa zako zifanyiwe kazi effectively and efficiently!
 

Mimi kama active citizen nimetoa rai, kazi yao wenye vyombo husika kufanyia kazi tuhuma hizi kwa sababu hata humu JF zimekuwa zikitajwa kwa muda mrefu. Mojawapo ya njia sahihi ya kufanya whistle blowing ni kupitia hizi platforms za mitandaoni. Umekariri njia zipi?
 

Kuna hili nalo!?
 
Kwanza sio mchaga ni mpare wa mabogini hapa jiran yangu kabisa

Sawa, lakini sioni umuhimu wa kutaja makabila. Mambo mengine ni tabia binafsi.
 
Wewe unaona hilo linawezekana? Yani akopee mshahara wake akatwe yeye kwa mslai ya machinga!!! Unaonekana una jambo na huyo jamaa maana unaandika kiudaku udaku alafu ni kama umepaniki kakufanyaje huyu mtu? Haya evidence iko wapi ya Haya unayosema?

Kwahiyo aliyesema anakopea mshahara ni mimi au yeye mwenyewe? Labda kama unasoma halafu huelewi.

Hizi ni tuhuma na tahadhari zimeanikwa, kazi ya vyombo vya dola ni kufuatilia na kuchukua hatua kwa sababu haya yanasemwa na hao wajasiriamali wenyewe. Sijui kwanini unataka kuchukulia jambo hili personal wakati linahusisha fedha za umma.

Jitambue.
 

Whistleblowing haifanywi kwa kutoa tuhuma tu bila evidence yoyote. Wapelekee TAKUKURU vielelezo ulivyonavyo. Unaogopa nini kama una ushahidi?

It’s unrealistic kwa TAKUKURU kuchunguza kila tuhuma wanayoiona kwenye social media platforms. Tuhuma nyingi ni majungu au zinatokana na misunderstood information!
 

Hujui maana ya whistle blowing au umekariri. Pia kama ni vielelezo basi kauli za DC peke yake zinatosha kumtilia mashaka na kumchunguza. Mfano sheria gani inaruhusu makato ya zaido ya 80% ya mshahara kulipia mkopo? Acha TAKUKURU wafanye kazi yao.

Hata humu JF tuhuma nyingi zilifanyiwa kazi na zilibezwa hivi hivi. Vipi kama zingepuuzwa?
 

Whistleblowing unayoijua wewe nadhani ni ya referee wa netball.

Jifunze kutofautisha facts na opinions. Kama ni kulalamika na kutoa opinions zako, fanya hivyo tu kama watu wengine, lakini sio kuwaambia “TAKUKURU mchunguzeni Mkuu wa Wilaya ya Morogoro…” wakati authority ya kufanya hivyo huna.
 

Unajua maana ya RAI? Pia ni nani mwenye hiyo authority ya kufanya hivyo? Unaelewa nafasi ya mwananchi kwenye demokrasi na utawala bora?

Wewe inawezekana una maslahi na DC, hujishtukii zaidi ya 80% ya comments za hii thread zinamdiscredit huyo jamaa yako! Angekuwa msafi, angepata watetezi wengi humu na hata thread ingeshapoteza maana.

Jitambue.
 

Kusema, “TAKUKURU mchunguzeni …” ni rai?

Wewe ni mgeni kwenye jukwaa hili kiasi cha kutokujua political vengefulness ya watu waliomo humu?

Mimi sasa hivi nikianzisha campaign dhidi ya Ally Hapi au Dr. Mashinji hapa ndani, kwa kisingizio chochote kile, unadhani sitaungwa mkono na supermajority ya wachangiaji wa uzi wangu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…