TAKUKURU mchunguzeni Mkuu wa Wilaya Morogoro, anaitumia ofisi yake vibaya

TAKUKURU mchunguzeni Mkuu wa Wilaya Morogoro, anaitumia ofisi yake vibaya

Anajiharibia sana

Anajiharibia kwa nani mkuu? Kumbuka hicho cheo ni kichaka cha upigaji na hakuna hatua zozote za maana huwa zinachukuliwa. Huyu aliingia CCM kipindi cha siasa za uzalendo wa kiki. Lengo lake la kujiunga CCM ilikuwa ni kusaka ulaji, na sasa amepata nafasi hiyo.
 
Mbona unaleta hoja halafu ni wewe huyo huyo unajibu na kutetea hoja? Nina mashaka na wewe utakuwa umetumwa.

Sisi wanyonge ametundea makubwa na tunamshukuru mno. Endelea kuhongwa na wanasiasa wanaohofia ubunge wao

Unataka kuspin mjadala? Hebu kuwa serious. Hoja hapa ni uhuni unaofanyika kinyume na sheria. Kuiomba TAKUKURU kuchunguza madai haya kutasaidia kujua mbivu na mbichi. Hutaki?
 
Kumiliki law firm ndio sababu ya kuvunja sheria na kufanya ulaghai? Unajua hii ishu iko serious sana na pengine ikamgharimu nafasi yake? Umeandika kama ni jambo la mzaha vile
Ikiuma chomoa.
 
Aliuaminisha umma. Naachaje kumuamini kiongozi aliyepewa dhamana na taifa?

Hapo ndio unapokwama, mtu akipewa dhamana ndio umwamini? Kwenye mfumo ambao wanaoteua wanaingia madarakani kwa wizi wa kura tena wa wazi unategemea uadilifu gani hapo?
 
Hapo ndio unapokwama, mtu akipewa dhamana ndio umwamini? Kwenye mfumo ambao wanaoteua wanaingia madarakani kwa wizi wa kura tena wa wazi.

Ukipewa dhamana tafsiri yake umeaminiwa.
 
Ukipewa dhamana tafsiri yake umeaminiwa.

Uko sahihi, lakini nasema wanaokupa hiyo dhamana ni wasafi? Unadhani Msando hajui kuwa mfumo umeoza? Kwa taarifa yako Msando alikuwa ni mtu mwenye shughuli zake zinazomuingizia kipato, mshahara wa uDC kwake si kitu, bali alikubali hicho cheo kwa kujua fika ni wapi atapigia pesa.
 
Stendi ya Mafiga ameigeuza bar. Huyu jamaa hatari sana, yaani kachukua stendi kaifanya bar.
 
Uko sahihi, lakini nasema wanaokupa hiyo dhamana ni wasafi? Unadhani Msando hajui kuwa mfumo umeoza? Kwa taarifa yako Msando alikuwa ni mtu mwenye shughuli zake zinazomuingizia kipato, mshahara wa uDC kwake si kitu, bali alikubali hicho cheo kwa kujua fika ni wapi atapigia pesa.

Najaribu kuelewa position yako kwenye hili; unamsifia DC kwa kupiga pesa za umma?
 
Stendi ya Mafiga ameigeuza bar. Huyu jamaa hatari sana, yaani kachukua stendi kaifanya bar.

Basi inawezekana ana makandokando mengi sana. Ndio maana nashauri achunguzwe kujua mbivu na mbichi.
 
Si waliambiwa wale kwa urefu wa kamba zao!! Wana kibali cha kufanya hayo wafanyayo.
 
Najaribu kuelewa position yako kwenye hili; unamsifia DC kwa kupiga pesa za umma?

Nasema hivi, Msando alikubali hicho cheo sio kwa ajili ya mshahara, bali ni sehemu ya upigaji. Sijawahi kusifia wahuni wa aina ya Msando.
 
Mbaya zaidi, inasemekana Mkurugenzi na watumishi wa Halmashauri wametishiwa kufukuzishwa kazi endapo hawataidhinisha malipo hayo batili.
Nilipoona mkurugenzi kutishiwa kufukuzwa kazi na mkuu wa mkoa wakati mamlaka ilyomteua ni raisi nikapata wasiwasi huenda hizi ni fitina za kumchafua Msando.

Hii habari inaweza kuwa ya kweli lakini kwa maneno hayo hapo juu inaonekana ni ya kimchongo majungu.
 
SIRI IMEFICHUKA! Kumbe vile vibanda vya wajasiriamali (Wamachinga) katika Soko Kuu la Chifu Kingalu vilivyojengwa na Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Albert Msando kwa kushirikiana na benki fulani, vimegeuzwa mradi wa kupigia pesa na kuiibia serikali? Hatari sana.

Itakumbukwa kuwa DC Msando alisema anakatwa kiasi fulani cha mshahara wake kila mwezi kulipia deni la benki alilokopa ili kujenga vibanda vile, tena alisema anajitolea.

REJEA: Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albert Msando anasema anakatwa rejesho la mkobo wa kujenga vibanda

Imekuwaje leo anadai alipwe na Halmashauri? Lengo lake lilikuwa ni kufanyabiashara? Kuilaghai Serikali? Kusaka umaarufu wa kisiasa au kutapeli Wajasiriamali?

Tetesi zilianza kuenea kutoka kwa wajasiriamali wenyewe ambao walidai DC aliwaelekeza kulipia kati ya laki 5 mpaka laki 7 kila mwezi kwa kila kibanda, tena fedha hizo alitaka zilipwe kwenye akaunti yake binafsi. Tetesi hizo zikadaiwa ni uzushi.

Yakaibuka madai mengine kwamba baada ya kushindikana kuwalipisha machinga kiasi hicho kufuatia serikali ya mkoa kuelekeza wamachinga walipe tu bei elekezi kwa soko ili kuipatia halmashauri mapato, DC kuona amekwama akaagiza H/Manispaa imrudishie fedha zake takribani milioni 106 ili alipe deni la benki kwa sababu zilitumika kwenye mradi wa maendeleo, jambo ambalo lilipingwa pia kwa sababu sio utaratibu wa serikali mtu binafsi kukopa na kuja kudai bila kufuata sheria na kanuni. Madai hayo nayo akayakanusha kupitia vyombo vya habari na kudai Mkuu wa Mkoa na Mbunge wanakwamisha jitihada za serikali (yeye) kuwasaidia wamachinga.

REJEA: DC Alberto Msando akopa milioni 106 benki ili kuwajengea wamachinga sehemu ya kufanyia biashara

Hivi sasa yapo madai mengine kwamba ameagiza alipwe jumla shilingi milioni 279, huku akitaja majina ya wazabuni wawili waliojenga vibanda hivyo, majina ambayo hayatambuliki na Halmashauri wala mchakato wa zabuni haukufanyika. Na madai haya atayakanusha?

Mbaya zaidi, inasemekana Mkurugenzi na watumishi wa Halmashauri wametishiwa kufukuzishwa kazi endapo hawataidhinisha malipo hayo batili. Kama ni kweli, lazima kuna vielelezo vya barua, wasiogope, waweke mambo wazi.

MY TAKE: Kwa sababu hili ni jambo lenye harufu ya rushwa, wizi na matumizi mabaya ya ofisi na fedha za umma; ipo haja ya TAKUKURU na vyombo vya dola kufika Morogoro na kulichunguza kwa undani.

Inaumiza kusikia watu wanataka kuibia Serikali kwa sababu tu wameaminiwa na kupewa dhamana. Watanzania wa leo sio wajinga kiasi hicho. HILI LISIACHWE LIPITE HIVI HIVI!
Tafuta Hela bwana mdogo !
 
Nilipoona mkurugenzi kutishiwa kufukuzwa kazi na mkuu wa mkoa wakati mamlaka ilyomteua ni raisi nikapata wasiwasi huenda hizi ni fitina za kumchafua Msando.

Hii habari inaweza kuwa ya kweli lakini kwa maneno hayo hapo juu inaonekana ni ya kimchongo majungu.

Kuna tofauti kati ya kufukuzwa na kufukuzishwa. Soma kwa umakini.

Halafu migogoro ya DCs na Wakurugenzi haipo Morogoro tu, unajua sababu ni nini?

Think.
 
Back
Top Bottom