TAKUKURU mchunguzeni Mkuu wa Wilaya Morogoro, anaitumia ofisi yake vibaya

TAKUKURU mchunguzeni Mkuu wa Wilaya Morogoro, anaitumia ofisi yake vibaya

Nasema hivi, Msando alikubali hicho cheo sio kwa ajili ya mshahara, bali ni sehemu ya upigaji. Sijawahi kusifia wahuni wa aina ya Msando.

Nimekuelewa, lakini hili jambo hata mamlaka haiwezi kulivumilia. Mbaya sana kutumia cheo kutapeli wananchi unaowaongoza badala ya kuwasaidia kutatua changamoto zao.
 
Si waliambiwa wale kwa urefu wa kamba zao!! Wana kibali cha kufanya hayo wafanyayo.

Mh unataka kuleta siasa tena, urefu wa kamba ni kuridhika na kipato chako (mshahara + benefits)
 
Kuna tofauti kati ya kufukuzwa na kufukuzishwa. Soma kwa umakini.

Halafu migogoro ya DCs na Wakurugenzi haipo Morogoro tu, unajua sababu ni nini?

Think.
Sababu ya migogoro ni pesa na madaraka.
Kwenye suala la kufukuzishwa kazi ina maana mamlaka zinazoteua na kutengua hazifanyi uchunguzi kabla ya kufukuza kazi watu au kutengua teuzi?
 
Sababu ya migogoro ni pesa na madaraka.
Kwenye suala la kufukuzishwa kazi ina maana mamlaka zinazoteua na kutengua hazifanyi uchunguzi kabla ya kufukuza kazi watu au kutengua teuzi?

Huijui fitna wewe
 
SIRI IMEFICHUKA! Kumbe vile vibanda vya wajasiriamali (Wamachinga) katika Soko Kuu la Chifu Kingalu vilivyojengwa na Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Albert Msando kwa kushirikiana na benki fulani, vimegeuzwa mradi wa kupigia pesa na kuiibia serikali? Hatari sana.

Itakumbukwa kuwa DC Msando alisema anakatwa kiasi fulani cha mshahara wake kila mwezi kulipia deni la benki alilokopa ili kujenga vibanda vile, tena alisema anajitolea.

REJEA: Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albert Msando anasema anakatwa rejesho la mkobo wa kujenga vibanda

Imekuwaje leo anadai alipwe na Halmashauri? Lengo lake lilikuwa ni kufanyabiashara? Kuilaghai Serikali? Kusaka umaarufu wa kisiasa au kutapeli Wajasiriamali?

Tetesi zilianza kuenea kutoka kwa wajasiriamali wenyewe ambao walidai DC aliwaelekeza kulipia kati ya laki 5 mpaka laki 7 kila mwezi kwa kila kibanda, tena fedha hizo alitaka zilipwe kwenye akaunti yake binafsi. Tetesi hizo zikadaiwa ni uzushi.

Yakaibuka madai mengine kwamba baada ya kushindikana kuwalipisha machinga kiasi hicho kufuatia serikali ya mkoa kuelekeza wamachinga walipe tu bei elekezi kwa soko ili kuipatia halmashauri mapato, DC kuona amekwama akaagiza H/Manispaa imrudishie fedha zake takribani milioni 106 ili alipe deni la benki kwa sababu zilitumika kwenye mradi wa maendeleo, jambo ambalo lilipingwa pia kwa sababu sio utaratibu wa serikali mtu binafsi kukopa na kuja kudai bila kufuata sheria na kanuni. Madai hayo nayo akayakanusha kupitia vyombo vya habari na kudai Mkuu wa Mkoa na Mbunge wanakwamisha jitihada za serikali (yeye) kuwasaidia wamachinga.

REJEA: DC Alberto Msando akopa milioni 106 benki ili kuwajengea wamachinga sehemu ya kufanyia biashara

Hivi sasa yapo madai mengine kwamba ameagiza alipwe jumla shilingi milioni 279, huku akitaja majina ya wazabuni wawili waliojenga vibanda hivyo, majina ambayo hayatambuliki na Halmashauri wala mchakato wa zabuni haukufanyika. Na madai haya atayakanusha?

Mbaya zaidi, inasemekana Mkurugenzi na watumishi wa Halmashauri wametishiwa kufukuzishwa kazi endapo hawataidhinisha malipo hayo batili. Kama ni kweli, lazima kuna vielelezo vya barua, wasiogope, waweke mambo wazi.

MY TAKE: Kwa sababu hili ni jambo lenye harufu ya rushwa, wizi na matumizi mabaya ya ofisi na fedha za umma; ipo haja ya TAKUKURU na vyombo vya dola kufika Morogoro na kulichunguza kwa undani.

Inaumiza kusikia watu wanataka kuibia Serikali kwa sababu tu wameaminiwa na kupewa dhamana. Watanzania wa leo sio wajinga kiasi hicho. HILI LISIACHWE LIPITE HIVI HIVI!
Yaani mbuzi amchunguze fisi?
 
SIRI IMEFICHUKA! Kumbe vile vibanda vya wajasiriamali (Wamachinga) katika Soko Kuu la Chifu Kingalu vilivyojengwa na Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Albert Msando kwa kushirikiana na benki fulani, vimegeuzwa mradi wa kupigia pesa na kuiibia serikali? Hatari sana.

Itakumbukwa kuwa DC Msando alisema anakatwa kiasi fulani cha mshahara wake kila mwezi kulipia deni la benki alilokopa ili kujenga vibanda vile, tena alisema anajitolea.

REJEA: Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albert Msando anasema anakatwa rejesho la mkobo wa kujenga vibanda

Imekuwaje leo anadai alipwe na Halmashauri? Lengo lake lilikuwa ni kufanyabiashara? Kuilaghai Serikali? Kusaka umaarufu wa kisiasa au kutapeli Wajasiriamali?

Tetesi zilianza kuenea kutoka kwa wajasiriamali wenyewe ambao walidai DC aliwaelekeza kulipia kati ya laki 5 mpaka laki 7 kila mwezi kwa kila kibanda, tena fedha hizo alitaka zilipwe kwenye akaunti yake binafsi. Tetesi hizo zikadaiwa ni uzushi.

Yakaibuka madai mengine kwamba baada ya kushindikana kuwalipisha machinga kiasi hicho kufuatia serikali ya mkoa kuelekeza wamachinga walipe tu bei elekezi kwa soko ili kuipatia halmashauri mapato, DC kuona amekwama akaagiza H/Manispaa imrudishie fedha zake takribani milioni 106 ili alipe deni la benki kwa sababu zilitumika kwenye mradi wa maendeleo, jambo ambalo lilipingwa pia kwa sababu sio utaratibu wa serikali mtu binafsi kukopa na kuja kudai bila kufuata sheria na kanuni. Madai hayo nayo akayakanusha kupitia vyombo vya habari na kudai Mkuu wa Mkoa na Mbunge wanakwamisha jitihada za serikali (yeye) kuwasaidia wamachinga.

REJEA: DC Alberto Msando akopa milioni 106 benki ili kuwajengea wamachinga sehemu ya kufanyia biashara

Hivi sasa yapo madai mengine kwamba ameagiza alipwe jumla shilingi milioni 279, huku akitaja majina ya wazabuni wawili waliojenga vibanda hivyo, majina ambayo hayatambuliki na Halmashauri wala mchakato wa zabuni haukufanyika. Na madai haya atayakanusha?

Mbaya zaidi, inasemekana Mkurugenzi na watumishi wa Halmashauri wametishiwa kufukuzishwa kazi endapo hawataidhinisha malipo hayo batili. Kama ni kweli, lazima kuna vielelezo vya barua, wasiogope, waweke mambo wazi.

MY TAKE: Kwa sababu hili ni jambo lenye harufu ya rushwa, wizi na matumizi mabaya ya ofisi na fedha za umma; ipo haja ya TAKUKURU na vyombo vya dola kufika Morogoro na kulichunguza kwa undani.

Inaumiza kusikia watu wanataka kuibia Serikali kwa sababu tu wameaminiwa na kupewa dhamana. Watanzania wa leo sio wajinga kiasi hicho. HILI LISIACHWE LIPITE HIVI HIVI!
Abood
 
Takukuru hawana mipaka kwenye kazi zao hata kwa wateule wa Rais mkuu.
Hayo ni maneno tu ya mkosaji, mbona walimshindwa Sabaya mpaka pale alipotenguliwa uteuzi wake? Hii nchi imejaa sanaa sn angekuwa Mtendaji wa mtaa mbona sahivi angekuwa mahakamani
 
Hebu zitaje mkuu maana miye Moro nakujua.

Hawezi kujibu kwa hoja huyo, atakupotezea muda tu na kuleta ushabiki.

Hoja za msingi;

1. DC Alijenga vibanda vya wajasiriamali kama mtu binafsi au kiongozi wa serikali? Kama mtu binafsi kwanini?

2. Kwanini aliita ujenzi wa vibanda hivyo ni msaada na kujitolea huku akisema anakatwa zaidi ya 80% ya mshahara wake kila mwezi? Aliudanganya umma? Kwa maslahi gani?

3. Kama alijenga kama kiongozi wa wilaya, alifuata utaratibu gani? Kwanini hakutangaza zabuni kama sheria inavyoelekeza?

4. Kama ilikuwa ni mradi wa serikali, kwanini alichukua mkopo benki kwa jina lake binafsi badala ya kuchukua kwa jina la ofisi na sasa kuitaka Halmashauri kumrejeshea fedha zake pasipo makubaliano yoyote ya awali?

5. Kwanini alitaka wamachinga wamlipe kila mwezi laki 7 kwenye akaunti yake binafsi badala ya kulipa kwa uongozi wa soko ambazo zitaenda moja kwa moja Halmashauri?

Maswali haya ndio yanapaswa kujibiwa na sio blah blah. Kama hakuna majibu, basi TAKUKURU waanzie hapo na hatua zichukuliwe.
 
SIRI IMEFICHUKA! Kumbe vile vibanda vya wajasiriamali (Wamachinga) katika Soko Kuu la Chifu Kingalu vilivyojengwa na Mkuu wa Wilaya ya Morogoro, Albert Msando kwa kushirikiana na benki fulani, vimegeuzwa mradi wa kupigia pesa na kuiibia serikali? Hatari sana.

Itakumbukwa kuwa DC Msando alisema anakatwa kiasi fulani cha mshahara wake kila mwezi kulipia deni la benki alilokopa ili kujenga vibanda vile, tena alisema anajitolea.

REJEA: Mkuu wa Wilaya ya Morogoro Albert Msando anasema anakatwa rejesho la mkobo wa kujenga vibanda

Imekuwaje leo anadai alipwe na Halmashauri? Lengo lake lilikuwa ni kufanyabiashara? Kuilaghai Serikali? Kusaka umaarufu wa kisiasa au kutapeli Wajasiriamali?

Tetesi zilianza kuenea kutoka kwa wajasiriamali wenyewe ambao walidai DC aliwaelekeza kulipia kati ya laki 5 mpaka laki 7 kila mwezi kwa kila kibanda, tena fedha hizo alitaka zilipwe kwenye akaunti yake binafsi. Tetesi hizo zikadaiwa ni uzushi.

Yakaibuka madai mengine kwamba baada ya kushindikana kuwalipisha machinga kiasi hicho kufuatia serikali ya mkoa kuelekeza wamachinga walipe tu bei elekezi kwa soko ili kuipatia halmashauri mapato, DC kuona amekwama akaagiza H/Manispaa imrudishie fedha zake takribani milioni 106 ili alipe deni la benki kwa sababu zilitumika kwenye mradi wa maendeleo, jambo ambalo lilipingwa pia kwa sababu sio utaratibu wa serikali mtu binafsi kukopa na kuja kudai bila kufuata sheria na kanuni. Madai hayo nayo akayakanusha kupitia vyombo vya habari na kudai Mkuu wa Mkoa na Mbunge wanakwamisha jitihada za serikali (yeye) kuwasaidia wamachinga.

REJEA: DC Alberto Msando akopa milioni 106 benki ili kuwajengea wamachinga sehemu ya kufanyia biashara

Hivi sasa yapo madai mengine kwamba ameagiza alipwe jumla shilingi milioni 279, huku akitaja majina ya wazabuni wawili waliojenga vibanda hivyo, majina ambayo hayatambuliki na Halmashauri wala mchakato wa zabuni haukufanyika. Na madai haya atayakanusha?

Mbaya zaidi, inasemekana Mkurugenzi na watumishi wa Halmashauri wametishiwa kufukuzishwa kazi endapo hawataidhinisha malipo hayo batili. Kama ni kweli, lazima kuna vielelezo vya barua, wasiogope, waweke mambo wazi.

MY TAKE: Kwa sababu hili ni jambo lenye harufu ya rushwa, wizi na matumizi mabaya ya ofisi na fedha za umma; ipo haja ya TAKUKURU na vyombo vya dola kufika Morogoro na kulichunguza kwa undani.

Inaumiza kusikia watu wanataka kuibia Serikali kwa sababu tu wameaminiwa na kupewa dhamana. Watanzania wa leo sio wajinga kiasi hicho. HILI LISIACHWE LIPITE HIVI HIVI!
Ashughulikiwe inavyostahili.
 
Back
Top Bottom