TAKUKURU, Polisi waja na muarobaini wa rushwa za barabarani wakishirikiana na wadau

TAKUKURU, Polisi waja na muarobaini wa rushwa za barabarani wakishirikiana na wadau

Ushauri wangu ziwekwe camera za kudumu barabarani kama Nairobi zitasaidia kupunguza rushwa ya speed na haya wizi Wa Magari.pili vituo vya polisi USA river,pia ni shida askari wawe wanahamishwa Mara Kwa mara
Utaweka kamera hadi porini? Wanachotakiwa kufanya ni kuwapa motisha watu watakaopeleka vidhibiti vya askari wanaotoa rushwa.
 
Magari yetu ndo kitega uchumi,jiulize kwann daladala ndo zinaonewa sana,ukifika vituoni asubui daladala zimejaa jioni uzioni zishaacha pesa kuingia bure kutoka hela plus ya breakdown hata kama gari ni nzima watalazimisha ivutwe.Wanapenda daladala sababu daladala hawana mda wa kusimama mahakamani watapoteza muda huku gari imezuia kituoni hata kama ni haki yake yuko radhi atolewe pesa kuokoa siku maana kulala kituoni kusubiria haki yako utaipata kwa kuchelewa lkn nawe utapata hasara mfano ukikaa siku 10 utapoteza hesabu ya milioni moja kwa siku kumi,hivo radhi kutoa hata laki 2 ili gari isilale kituoni thus wanapenda daladala sababu ya pesa ya haraka na ya uhakika.Wakifukuzwa kazi au wakistaafu utawaonea huruma sana maana hakuna mirija ya zuluma.
 
Tuta acha je kutoa Rushwa? Rushwa tunatoa kwa sababu ya utatu huo huo.
Mosi, Serikali (faini 30,000), dereva hana uwezo wa kutoa faini ya 30,000 na askari yuko tayari kupokea rushwa ya 5,000-10,000. Binafsi nitatoa rushwa kuliko kulipa faini ambayo kiuhalisia hiyo fedha sina. Wakifanya faini 10,000 nitailipa.

Pili, ili tuache kutoa rushwa, ni lazima serikali ipambane kuhakikisha kuwa polisi wanaacha kubambika makosa kwa waendesha vyombo vya barabarani. Trafiki anaanza, leseni (hiyo), triangle (hiyo), sticker ya usalama (hiyo), breki (zipo), siti (haina mchubuko), kwanini umepakia mzigo umepita urefu wa bodi? Unatakiwa ulipe faini (30,000).

Au tairi zinaelekea kuisha (faini), gari rangi imebabuka (faini), kioo kimegongwa na changarawe na kuonyesha kanyota bila kupasuka (faini), pale nyuma uliovertake pasiporuhusiwa (wakati gari uliovertake ilipaki pembeni).

Hii inakuwa karaha sana kwa kuwa huwezi kuwa mtakatifu kwa haya watakayo askari wetu wenye njaa kali. Mwisho wa siku ni kuishia kutoa rishwa ili japo ubakize hela ya sembe kwa ajili ya watoto. Ningekuwa naweze nisingepita barabarani kabisa kuepukana na polisi hawa wenye kero za kutosha.
Hata uchukue gari zero kilometers wataitoa kasoro lzm iliwe.
 
Tuta acha je kutoa Rushwa? Rushwa tunatoa kwa sababu ya utatu huo huo.
Mosi, Serikali (faini 30,000), dereva hana uwezo wa kutoa faini ya 30,000 na askari yuko tayari kupokea rushwa ya 5,000-10,000. Binafsi nitatoa rushwa kuliko kulipa faini ambayo kiuhalisia hiyo fedha sina. Wakifanya faini 10,000 nitailipa.

Pili, ili tuache kutoa rushwa, ni lazima serikali ipambane kuhakikisha kuwa polisi wanaacha kubambika makosa kwa waendesha vyombo vya barabarani. Trafiki anaanza, leseni (hiyo), triangle (hiyo), sticker ya usalama (hiyo), breki (zipo), siti (haina mchubuko), kwanini umepakia mzigo umepita urefu wa bodi? Unatakiwa ulipe faini (30,000).

Au tairi zinaelekea kuisha (faini), gari rangi imebabuka (faini), kioo kimegongwa na changarawe na kuonyesha kanyota bila kupasuka (faini), pale nyuma uliovertake pasiporuhusiwa (wakati gari uliovertake ilipaki pembeni).

Hii inakuwa karaha sana kwa kuwa huwezi kuwa mtakatifu kwa haya watakayo askari wetu wenye njaa kali. Mwisho wa siku ni kuishia kutoa rishwa ili japo ubakize hela ya sembe kwa ajili ya watoto. Ningekuwa naweze nisingepita barabarani kabisa kuepukana na polisi hawa wenye kero za kutosha.
Mi saa 12 asubuhi natoka home kurudi lazima iwe saa 1 usiku na zaidi,sitaki kabisa kukutana nao.
 
Kuna mtindo umekuja polisi wanajificha porini na kutumia simu zao za smart phone kupiga Magari over speed, ukifika mbele unasimamishwa unaonyeshwa Picha ya gari lako na speed yako kwenye siku ya trafic mwingine, wanakudai rushwa na faini hawataki kukuandikia, mfano kuna eneo LA low gear, kule babsti mkoani kuelekea kateshi, pale polio ni kitovu cha kuombea na kukusanyia rushwa, tunaomba takukuru Mkoa wawe pale kusaidia wananchi.

RTO na RPC wapi pale wanajifanya hawaone wananchi wanavyonyanyaswa ,imefika mahali au wakati penye traffic point awepo MTU mmoja Wa takukuru,hali sio mzuri haya kidogo.pili kwanini serikali isiweke camera barabarani ili Picha ikipigwa isome na kupeleka Picha moja Kwa moja ofisi za polisi Mkoa na wilaya badala ya sasa Picha kuwepo kwenye siku za watu binafsi na kutoza faini au rushwa?

Je RPC anajua ni Picha ngapi zimepigwa Kwa siku au anasubiri tu kuambiwa kilichotokea? Ushauri wangu ziwekwe camera za kudumu barabarani kama Nairobi zitasaidia kupunguza rushwa ya speed na haya wizi Wa Magari.pili vituo vya polisi USA river,pia ni shida askari wawe wanahamishwa Mara Kwa mara
Camera hazipunguzi rushwa,nani atakaekaa mda wote anaangalia camera aache kuchat.Elimu itolewe zaidi nadhani wasikimbilie kulipisha fine bali kutoa onyo ukirudia kosa fine ndo ifuate.Pia fine haipunguzi ukiukaji wa sheria maana mwenye uwezo yeye kulipa si tatizo kama watu wanazinunua torch ili wawahi wanapokwenda nn fine.Fine hazijapunguza makosa ya barabarani labda kuongeza makusanyo,mamlaka zinahaja ya kubuni mbadala utakaowafanya watu waheshimu sheria za barabarani.
 
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Nchini (TAKUKURU) leo imefanya maongezi ya kimkakati na Wadau mbalimbali wakiwemo Sekta Binafsi, Sekta za Umma, Asasi za Kiraia, Taasisi za Dini, Vyombo vya Habari, Viwanda vya Uchapaji na Uchapishaji, Kampuni za Simu, Wamiliki wa Vyombo vya Usafiri, Wasanii, Madereva wa Vyombo vya Moto na Wananchi kuelezea Kampeni inayotarajiwa kuzinduliwa ya kupunguza ama kutokomeza kabisa rushwa Barabarani.

TAKUKURU imeeleza kuwa Kampeni hiyo imepewa jina la ‘UTATU’ ikimaanisha ni muunganiko wa pande Kuu tatu: TAKUKURU, Jeshi la Polisi na Wadau

Imedaiwa kuwa lengo kuu la kampeni ni kuzuia rushwa za barabarani ambayo imebainika ni kisababishi kimojawapo cha ajali zinazotokea barabarani; tatizo ambalo limekuwa likikemewa sana na viongozi mbalimbali wa Serikali. Aidha imesema UTATU huo unatakiwa kuweka mikakati ya pamoja na endelevu ya kutibu tatizo la ajali badala ya kulaumiana na kunyoosheana vidole.

Kampeni hiyo imejiwekea mambo malengo mahususi manne, ikiwa kila lengo linatakiwa kutekelezwa na kila mdau kwa nafasi yake:
  • Kudhibiti vitendo vya rushwa miongoni mwa wasimamizi wa sheria za barabarani
  • Kuandaa mkakati wa kuzuia vitendo vya rushwa barabarani
  • Kushirikisha Umma kuzuia vitendo vya rushwa barabarani
  • Matumizi ya TEHAMA kudhibiti vitendo vya rushwa barabarani
Kuhusu matumizi ya TEHAMA kudhibiti vitendo vya rushwa barabarani, TAKUKURU imesema tayari limeanza kutekelezwa kwa kutengeneza mfumo utakaotumika kuchukua matukio ya vitendo vya rushwa kwa kutumia simu ya mkononi (Mobile App).

Mfumo huo (Mobile App) utakaozinduliwa pamoja na Kampeni hii ya UTATU, utapakuliwa kutoka Play Store au App Store ya simu ya mkononi kisha mtu ataweza kupiga picha za video, mnato au sauti na kuzituma TAKUKURU.

Baadhi ya Majukumu ya Wadau wa Kampeni hii yametajwa kuwa:

Wasimamizi wa sheria na miundombinu ya Barabara (TANROADS, TARURA, LATRA na wengine)
Wanalo jukumu la kusimamia ubora wa miundombinu na Vyombo vya Usafiri ikiwa ni pamoja na
  • Kuboresha sheria, kanuni na miongozo
  • Kuboresha miundombinu ya barabara na mizani
  • Kusimamia usajili wa Vyombo vya Usafiri
  • Kuhakikisha alama za usalama barabrani zinaonekana vizuri
  • Kutoa taarifa za vitendo vya rushwa barabarani
Wasanii wa fani mbalimbali
  • Wana jukumu la kuhamsisha watumiaji wa barabara kupitia Sanaa zao zinazosisimua na kuburudisha huku ujumbe wao ukisaidia kubadili mitazamo ya watumiaji wa barabara kuacha vitendo vya rushwa
  • Wanatarajiwa kutoa michango yao ya kuandaa Sanaa zitakazohusiana na kampeni ya UTATU

AZAKI wao wametajwa kuwa wahamasishaji ambapo majukumu yao yatakuwa:
  • Kuhamasisha wananchi kutuma taarifa za vitendo vya rushwa barabarani
  • Kuhamasisha wananchi waache uoga wa kutoa taarifa za rushwa
  • Kutumia mtandao wao kutoa taarifa za vitendo vya rushwa
  • Kuhamasisha wananchi kuacha kutoa rushwa kwa masimamizi wa sheria za usalama barabarani
Wamiliki wa Vyombo vya Usafiri ambao majukumu yao ni
  • Kusimamia Vyombo vya Usafiri ili kutoruhusu magari mabovu kuingia barabarani
  • Kuajiri madereva wenye sifa na kuwalipa vizuri
  • Kuacha kutoa Rushwa ili wapate leseni bila kufuata utaratibu
  • Kuwachukulia hatua madereva wazembe
  • Kuwasimamia madereva kuacha kutoa rushwa kwa wasimamizi wa sheria za usalama barabarani
Wamiliki wa Vyombo vya Habari ni kundi lingine ambalo katika Kampeni hii majukumu yake yamebainishwa kuwa
  • Kuelimisha wananchi kupitia Vyombo vyao vya Habari
  • Kusaidia kutoa nafasi kwenye Vyombo vya Habari na kurusha matangazo kuhamasisha kampeni
  • Kutoa taarifa za vitendo vya Rushwa

Wamiliki wa Viwanda vya Uchapishaji na Uchapaji wao wataweza kushiriki kwa:
  • Kusaidia kuchapa machapisho ya kuhamasisha kampeni
  • Kutoa taarifa za vitendo vya rushwa
Vingozi wa dini wao wana majukumu muhimu ya
  • Kufundisha maadili kwa waumini wao ili wasitoe rushwa kwa wasimamizi wa sheria za usalama barabarani
  • Kutumia Vyombo vya Habari vinavyomilikiwa na dini zao ili kuhamasisha kampeni
  • Kutoa taarifa za vitendo vya rushwa

Katika mkutano huu, wadau walioshiriki kutoa maoni wamedokeza haya:-

Kwanza, wamesema Rushwa ni mtazamo wa ndani ya Polisi na nje ya Polisi, watu wanaona Polisi ni fursa. Kwenye vitengo vinavyoongoza kwa rushwa ni pamoja na kwenye kutoa leseni, ukaguzi wa barabarani. Polisi walio kwenye Pikipiki maarufu kama ‘tiGO’ na madereva wa magari ya Kirikuu wanaodai kuwa wakipita ni lazima wasimamishwe na kuombwa rushwa

Aidha, wengine wamehoji kwanini TAKUKURU hawapo barabarani? Huku wengine wakisema ni bora adhabu ziongezwe kwenye makosa ya barabarani na adhabu ya fedha iondolewe kabisa.

Wengine wakiwemo Viongozi wa Dini wametoa maoni kuwa hofu ya Mungu ndio suluhisho pekee la tatizo la rushwa kwa wananchi wanaweza kuwaepuka TAKUKURU na Polisi ili wasikamatwe kwenye masuala ya rushwa. Pia, Polisi wakiwa na hofu ya Mungu wanaweza kukataa rushwa na kuwakamata wanaotaka kutoa na hivyo kuzuia rushwa.

Lakini, kuhusu App TAKUKURU waliyozungumzia wadau wamesihi sana kuwa kunatakiwa kuwe na elimu ya awali itakayotolewa kwa Wananchi kabla ya kuanza kutumia App hiyo na pia kuwapa muda Wananchi kuielewa.

Wametaka pia Makamanda wa Polisi na watumishi waboreshewe maslahi kwa kuwa hiyo inaweza kuwa njia mojawapo ya kuzuia rushwa.
Hakuna anayependa kutoa rushwa ila shida inakuja pale Trafic anapokuambia anakuandia kosa fulani TZS 30,000 ambalo wewe kabisa unajua ni uongo ila kwa kuwa una haraka badala ya kupoteza muda kubishana naye unaamua kumpa TZS 5,000 akanywe nayo konyagi ifupishe hayo maisha yake.

Mfano hizo tochi zao kuna namna hata kama unatembea 45km/kwa saa yeye atakuonyesha ulikuwa unatembe 55Km/ saa ukipinga sana anakwambe akipe mzunguko wa matairi yako
 
Ukinunua gari lazima mkubali kugawana faida kati ya serikali na askari. Tena askari wanavuta nyingi kuliko mmiliki na serikali. Watu wa daladala ndo twajua.
 
Kwakweli traffic wamekuwa kero barabarani sana sana, kuna sehemu kabla ya kufika Mafinga kuna jamaa huwa anakaa kabisa na kamera yake kajificha angle ambayo haonekani kirahisi na kamera ina stand kabisa.

Sehemu ilivyokaa ni vugumu sana kwa dereva kwanza kuona kibao halafu in zebra haionekani vizuri na wala si sehemu yenye movement ya watu. Magari mengi pale yanapigwa kamera hata kama ulikuwa 51km/h utapigwa faini tena mbili, faini ya kwanza utaambiwa umevuka zebra bila kusimama, faini ya pili utaambiwa umevuka na speed say 55km/h.

Hao ni traffic wengine utakaowakuta mbele na picha zao kwenye simu, ukibishana anakuambia turudi akakuoneshe kibao kilipo! halafu utaambiwa umesamehewa kosa moja lingine unaandikiwa maana wewe ni mbishi sana, hapo mnaanza mjadala sasa wa kupunguziana mpaka anavuta mpunga wake unasepa zako,kuna siku tulishikwa magari zaidi 20, wabishi wanakomolewa kwa kulipa na waungwana wanajadili wanatoa mpunga wanasepa.

Kwa hiyo rushwa ya barabarani haiwezi kuisha sababu ya advantage ya traffic ya kukomoa madereva, naunga mkono labda faini baadhi ya makosa iwe pesa kidogo mfano elfu tano mpaka elfu kumi. Hatari yake lakini ni maderava wabaya na wakorofi wata take advantage kuendesha hovyo maana hawataogopa.

Kiujumla jambo hili lina utata kidogo na busara inahitajika kusolve kwakweli.
 
Watunza sheria wengine wamekuwa wakitumia udhaifu wa sheria kama fursa kwao kushiba.
 
Siungi mkono hoja.Yaani badala ya kumtoa trafiki na huku 5 nilipe faini ya elfu 30 au 50?
 
Njia peke ni kupunguza faini badala ya 30000 wekeni 5000 hapi watu watalipa uzuri. Lakini kwa 30 000 tabu sana kutatua tatizo
Kweli mkuu,tena mi hua sitaki shida akinipiga mkono tu wkt ananiambia lete leseni naiambatanisha na 'kishika uchumba' hapohapo kwny hio leseni,wala hutasikia maneno mengi,atajifanya anazungukia gari afu huyo anasepa zake.
 
Watu wengi ni waoga kubishana na traffic na hii ndio inasababisha rushwa. Kwa hili la app halitamaliza tatizo

Halafu ajali nyingi zinasababishwa na hawa hawa wanaosimamia sheria na barabara. Unakuta gari tairi zimeisha kabisa lakini anaruhusiwa kuendelea na safari baada ya kuwatoa buku. Bus linajaza mpaka watu wanashindwa kupumua na likipata ajali na kuuwa wanasema kosa la dereva wakati limepita sehemu na wao wameliona hilo, ila kwa njaa zao na kwa kuwa shangazi zao hawamo humo they don’t give a toss.

Sheria ziwe kali kwa hao wala rushwa na watoaji pia na adhabu iwe kali haswa.
 
Watu wengi ni waoga kubishana na traffic na hii ndio inasababisha rushwa
Kwa hili la app halitamaliza tatizo
Halafu ajali nyingi zinasababishwa na hawa hawa wanaosimamia sheria na barabara
Unakuta gari tairi zimeisha kabisa lakini anaruhusiwa kuendelea na safari baada ya kuwatoa buku
Bus linajaza mpaka watu wanashindwa kupumua na likipata ajali na kuuwa wanasema kosa la dereva wakati limepita sehemu na wao wameliona hilo, ila kwa njaa zao na kwa kuwa shangazi zao hawamo humo they don’t give a toss
Sheria ziwe kali kwa hao wala rushwa na watoaji pia na adhabu iwe kali haswa
Ila bongo bado fine za gari zina ka uafadhali kiaina,niliona majuzi state attorney wa Rwanda ali-overspeed fine yake akapigwa Rwf 150,000 kama 450,000(laki nne na nusu) za kibongo,nikasema hiiiiiiiiiiiiiiiiiii
 
Ila bongo bado fine za gari zina ka uafadhali kiaina,niliona majuzi state attorney wa Rwanda ali-overspeed fine yake akapigwa Rwf 150,000 kama 450,000(laki nne na nusu) za kibongo,nikasema hiiiiiiiiiiiiiiiiiii

Mkuu fines za makosa ni ndogo sana huko ukifananisha na nchi zingine
Ila tatizo kubwa ni rushwa ambayo watu wameifanya kama way of life
Kama sheria zinafuatwa sawa
Na fine za Tz ni ndogo bado
Jamaa yangu hapa [emoji636] alikamatwa na kosa la drink and drive kafungiwa miezi 14 kuendesha gari na fine ya £9000 kama kama 27m hivi

Hawana utani huku ukivunja sheria utakoma
 
Hiiiiiii £9000 aisee hizo zina wenyewe bongo fine kama hio itabidi wakate kwenye mafao tu,hakuna namna tena.,ila DUI kwa wenzetu naona ni kosa heavy sana mkuu.

Nadhani bado utashi wa kutokomeza rushwa huko mabarabarani bado haujawekewa mkazo,pamoja na boss wa Takukuru kuwekwa mjeda lkn tatizo hili limeshakua sugu.


Mkuu fines za makosa ni ndogo sana huko ukifananisha na nchi zingine
Ila tatizo kubwa ni rushwa ambayo watu wameifanya kama way of life
Kama sheria zinafuatwa sawa
Na fine za Tz ni ndogo bado
Jamaa yangu hapa [emoji636] alikamatwa na kosa la drink and driving kafungiwa miezi 14 kuendesha gari na fine ya £9000 kama kama 27m hivi

Hawana utani huku ukivunja sheria utakoma
 
Hiiiiiii £9000 aisee hizo zina wenyewe bongo fine kama hio itabidi wakate kwenye mafao tu,hakuna namna tena.,ila DUI kwa wenzetu naona ni kosa heavy sana mkuu.

Nadhani bado utashi wa kutokomeza rushwa huko mabarabarani bado haujawekewa mkazo,pamoja na boss wa Takukuru kuwekwa mjeda lkn tatizo hili limeshakua sugu.

[emoji23][emoji23]
Yaani fine zinapanda tu hazishuki huku na unaweza usisimamishwe na police hata miaka 10 kama huvunji sheria
Na licence zina point 12 na kila kosa wanafyeka baadhi inategemea na kosa lenyewe
Camera zipo kila barabara na magari yote yapo kwenye system ya serikali hata kama huna insurance unadakwa kirahisi sana
Suala bado ni gumu sana huko kwetu mkuu
Police kusimama barabarani umewawekea mlo tu hakuna kingine
 
Back
Top Bottom