Tetesi: TAKUKURU, TISS wadaiwa kuchunguza rushwa ya Wizara ya Nishati kwa Wabunge

Tetesi: TAKUKURU, TISS wadaiwa kuchunguza rushwa ya Wizara ya Nishati kwa Wabunge

Warofo

Member
Joined
Mar 15, 2011
Posts
81
Reaction score
79
MAKAMBA.png

Taarifa kutoka ndani ya TAKUKURU zinadai kuwa taasisi hiyo imefungua jalada la uchunguzi wa tuhuma kuwa Waziri wa Nishati, January Makamba, alitoa rushwa kwa wabunge ili wapitishe bajeti ya wizara yake ya 2023/24 wiki iliyopita.

Inadaiwa Makamba alitumia taasisi zilizo chini ya Wizara yake ikiwemo TANESCO, EWURA na TPDC kugawa rushwa kwa wabunge kwa kisingizio cha kufanya semina ya wabunge siku mbili mfululizo kabla ya kuwasilisha bajeti ya wizara yake.

Pia aligawa mitungi 100 ya gesi kwa kila mbunge kama sehemu ya rushwa hiyo, iliyofanikisha bajeti yake kupitishwa licha ya malalamiko makubwa ya wabunge kuhusu huduma mbovu za kukatikatika kwa umeme na usimamizi hafifu wa sekta ya nishati.

Tayari baadhi ya wabunge wameanza kuhojiwa na TAKUKURU ili kukusanya ushahidi wa rushwa hiyo ya mchana ambayo inakadiriwa kutumia karibu Shilingi Bilioni 2.

Idara ya Usalama wa Taifa, TISS, nayo inasemekena kuwa inachunguza taarifa hizo ili iweze kupeleka faili kwa mamlaka ya uteuzi.
 
Mimi ningewaona hawa Wanaochunguza wana Akili kama wangeanza Kwanza kumchunguza anayetoa Pesa hovyo kwa Klabu ya Yanga SC, anatoa Ndege kufanya Majukumu ya Kipuuzi yasiyo ya Faida huku Fedha za walipa Kodi Masikini zikitumika kuzilinda.
 
Mimi ningewaona hawa Wanaochunguza wana Akili kama wangeanza Kwanza kumchunguza anayetoa Pesa hovyo kwa Klabu ya Yanga SC, anatoa Ndege kufanya Majukumu ya Kipuuzi yasiyo ya Faida huku Fedha za walipa Kodi Masikini zikitumika kuzilinda.
Kwako wewe kuwapa simba mil 35 kwa ushindi wa bao 7 halikuwa jambo baya! Wakipewa wengine nongwa. Afu unajiita una akili kubwa? Akili kubwa hujui hata maana ya MOTIVATION?
 
Umeahidiwa Cheo huko Serikalini au?
Mm sifungwi n vyeo. Ila mtu mwenye akili kubwa hawezi kujadili watu kunywa juice ikulu. Hujui kwamba ofisi ya raisi ikulu ina bajeti yake? Sasa tangu lini matumizi ya bajeti iliyopitishwa na bunge yawe matumizi mabaya? Akili kubwa ya wapi hii???
 
Yawezekana ndio maana ule mwaka watu 40, mpaka wakulima wa vijijini, walichukua fomu za kugombea ukuu wa nchi.
 
Mimi ningewaona hawa Wanaochunguza wana Akili kama wangeanza Kwanza kumchunguza anayetoa Pesa hovyo kwa Klabu ya Yanga SC, anatoa Ndege kufanya Majukumu ya Kipuuzi yasiyo ya Faida huku Fedha za walipa Kodi Masikini zikitumika kuzilinda.
Wewe ni hamnazo.
 
Makamba alitumia taasisi zilizo chini ya Wizara yake ikiwemo TANESCO, EWURA na TPDC kugawa rushwa kwa wabunge kwa kisingizio cha kufanya semina ya wabunge siku mbili mfululizo kabla ya kuwasilisha bajeti ya wizara yake
Kila mara tunasema huyu mtu ni muumini mkubwa sana wa rushwa, kuanzia kuipokea na kutoa pia!
Sioni kama hata Takukuru na TISS watakuja na la maana kwani huenda hizi Taasisi nazo zikaishia walikoishia wabunge wala rushwa wa ccm
 
Back
Top Bottom