Jee huo utaratibu umo katika sheria kuwa mtu akigoma kutoa hati yake unakwenda kutenngeneza nyengine.Na nani anayekupa hiyo nyingine kabla kufutwa ya mwanzo.Ingekuwa ni hivyo majambazi wakitaka nyumba eneo fulani ukigoma kuwapa wanakwenda kutengeneza nyengine halafu unahamishwa.Ikiwa hilo lipo basi kuna kasoro kubwa na sheria ya ardhi lazima ibadilishwe isitoe mwanya kwa utovu wa nidhamu namna hiyo.Uongozi ulioondolewa madarakani uligoma kukabidhi vitendea kazi ikiwamo hati, Viongozi waliochaguliwa wakaenda kuifuta hati na kuprocess hati mpya ipo na ndio imetumika kuombea vibali
Hilo eneo viongozi wa dini walitapeli pia kwahiyo malipo ni hapa hapa
Kuna mambo matatu kwenye uonevu wapaswa kuchagua mojawapo.Pambaneni mpaka kieleweke! Uzuri nyie vita mnaiweza! Si mna ile kaulimbiu kwamba “hakuna kumuachia mungu ni jino kwa jino?!”...haya komaeni sasa
Ile msikiti ni amali iliyo chini ya jumuiya ya Waislam wa Mwenge. Ninaufahamu. Sasa hili la kuubomoa wakati wenye msikiti hawajaridhia ndo tunarudi kule kule kwenye kudhulumu amali za waislam.Salaam Wakuu,
Jamani tunaomba msaada, Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum atatutoa roho.
Baada ya rais Samia kuingia Madarakani, wale watu wa pesa inaongea Wamerudi kwa kasi ya ajabu. Mtu mwenye pesa sasa anaweza kufanya chochote na usimfanye kitu.
Katika Mkoa wa Dar Es Salaam kuna Taajiri amewaweka mfukoni Watendaji wote wa Wilaya ya Kinondoni hawa Wakina Gondwe.
Kipindi cha nyumba, kuna Tajiri alitaka kununua Msikiti ili ajenge maduka, Bodi ya Wadhamini ya Msikiti Wakamkatalia. Ikabidi Tajiri huyo amtumie Sheikh wa Mkoa wa Dar es Salaam, Alhad Mussa Salum ambaye alitetengeneza Bodi mpya ya wadhamni wasio hata waumin wa Msikiti ili Waweze kumuuza Tajiri na Wakafanikiwa. Kumbuka Msikiti unamilikiwa na Taasisi ya Mwenge Mosque & Islamic Centre. Hakuna aliyeshirikishwa kwenye Uteuzi wa Bodi Mpya.
Waumini Walilalamika RITA, Ardhi na kwa Mkurugenzi wa Kinondoni bila mafanikio.
View attachment 2359556
Wakashangaa Hati ya jengo wanayo wao lakini wakashangaa Msikiti unavunjwa na kuanza kujengwa Maduka. Walipojaribu kuzuia, Wakaitwa Polisi wa Oysterbay wakawakamata wote walioonekana kulalamika na kuwekwa ndani bila dhamana. Walikaa sana Polisi kwa kosa la kifanya fujo Msikitini. Aliyekua Msimamizi Mkuu wa Msikiti akafa kifo cha gafla kwani aliteswa sana na Polisi wakitaka aoneshe hati ya kiwanja ilipo kwani aliwanyima.
Je, Tajiri aliwezaje kununua sehemu na kujenga bila ya kuwa na hati?
Je, Kwanini Bodi ya Wadhamni iliundwa haraka bila kufuata kanuni?
Kwanini Polisi Wawashikile watu na kuwanyima dhamana hadi uzio uwekwe?
RITA WALIFIKA KUKAGUA MALI ZETU LAKINI HADI LEO HAWATUPI MREJESHO
View attachment 2359599
Kwanini RITA pamoja na kuja sehemu ya tukio, mbona hawajasitisha ujenzi?
Je kwanini Mkurugenzi alisimamisha ujenzi, lakini baada ya mhusika mkuu kufariki akaruhusu ujenzi uendelee?
Hawa waumini wanatishiwa kubambikizwa kesi ya Ugaidi.
Hapa chini naweka Ushahidi
View attachment 2359543
Hii hapa ni OB ya Polisi waliokamatwa kisa wanazuia Msikiti wao Usibomolewe. Huruma za Polisi ACP Ramadhan Kingai ndo zilifanywa Waachiliwe baada ya kuhoji sababu ya kuwashikilia bila dhamana wala kupelekwa mahakamani. Ni baada ya kuelezwa kilicho nyuma ya pazia.
View attachment 2359556
Hii ni barua iliyowataka Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini(RITA) na BARAZA Kuu la Waislamu wa Tanzania (BAKWATA) kufika mbele ya Mkuu wa Wilaya ili atatue mzozo huu lakini hawajatokea kila Walipoitwa.
View attachment 2359570
View attachment 2359571
Hii ni kibali cha kusimamisha Ujenzi, wiki mbili baada ya alokuwa anatetea Msikiti usibomolewe kufariki, Wakakihuisha
View attachment 2359582View attachment 2359583View attachment 2359581
Na hiii ni hati halali waliyopewaTaasisi ya Mwenge Mosque & Islamic Centre ambayo hadi sasa bado wanayo, ila mtu mwingine kaja kabomoa Msikiti na Kujenga Maduka chini ya Usimamizi wa Polisi. Hawana hata Umiliki.
View attachment 2359584View attachment 2359585
Na huu ni Uthibitisho wa Serikali za Mtaa kutoelewa kunachoendelea mtaani kwake
View attachment 2359588View attachment 2359587
Na haya ndo Maduka yanayojengwa sehemu ulipokuwa Msikiti Mwenge mbele ya Magorofa ya Jeshi barabara ya TRA
Tunaomba Serikali Sikivu ya Mama Samia iingilie Kati swala hili. Bado naamini Godwin Gondwe anao uwezo wa kutatua mgogoro huu japo haoneshi jitihada zozote kuhakikisha hili swala linaisha.
Mkuu wa Mkoa Makalla sababu ni rafiki yake na Sheikh Salum, kila siku anasema yupo busy.
Hujaona faida za hii mada ,kuletwa hapa?Habari hii haina ukweli wowote Serikali iko macho sana halafu mleta habari wala hakutakiwa kuileta huku JF alitakiwa aipeleke TAKUKURU moja kwa moja huku kaileta ham a msaada wowote anatafuta huruma ya watu tu
Hilo suala la kufanya biashara misikitini ni jambo limekatazwa na sheria ya kiislaam... MSIKITI KAZI YAKE SI BIASHARA... NA NDIO MAANA ALLAAH ANANYIMA BARAKA KWENYE HIYO MISIKITI NDIO MWISHO WA SIKU MNAISHIA KWENYE MIGOGORO ISIYOISHA...Ukweli ni kuwa eneo hilo linajengwa maduka ya kisasa upande wa mbele halafu Msikiti wa kisasa wa ghorofa 4 unajengwa katika eneo la ndani. Yameanza maduka kwakuwa isingekuwa vizuri uanze Msikiti kisha watu wakianza kufanya ibada huku ujenzi wa maduka ungesumbua wanaofanya ibada kwani ibada inahitaji mahala tulivu( rejea kibali alichopost mleta habari kuwa ni kwaajili ya kujenga Msikiti na maduka ya biashara)
Waleta habari ni viongozi waliopigwa chini kwenye uongozi kwakuwa walikuwa hawaleti maendeleo Msikiti ulikuwa dhalili leo viongozi waliochaguliwa wamekuja na mawazo mapya ya kuuendeleza uislamu Mwenge wanapigwa maneno. Kama wana hoja za msingi wapeleke hili jambo TAKUKURU AU Mahakamani sio kulileta JF kutaka huruma ya watu wasiokuwa na taarifa za upande wa pili
Misikiti imeanzisha utaratibu wa kutengeneza maduka katika uzio ili angalau zipatikane fedha za uendeshaji wa misikiti kwakuwa kiukweli tabia ya utoaji sadaka kwa Waislamu hairidhishi tofauti na wenzetu wa dini nyingine wamejengewa tabia ya kutoa sadaka na zaka ambazo sadaka zinatumika kufinance mambo ya dini kama kulipa mishahara na kununua vitendea kazi.Hilo suala la kufanya biashara misikitini ni jambo limekatazwa na sheria ya kiislaam... MSIKITI KAZI YAKE SI BIASHARA... NA NDIO MAANA ALLAAH ANANYIMA BARAKA KWENYE HIYO MISIKITI NDIO MWISHO WA SIKU MNAISHIA KWENYE MIGOGORO ISIYOISHA...
ukitaka kumuona anakuja mbiombio na baibui lake zungumza jambo lolote ambalo yeye atahisi ni negative, kuhusu dini yake.
Maendeleo ni kwa faida ya uislam na kwa faida ya wanachama wanaomiliki msikiti huo.Hayo maendeleo ni kwa faida yanani?
Nakubaliana na wewe " Msikiti ulikua dhalili" je mmekubaliana kuhusu hayo maendeleo?
Je baada ya hayo maduka kujengwa nafasi inayo Baki inaacha sehem ya Msikiti na uwanja kwa shughuli za mikusanyiko Mikubwa?
Ndio maana yule Mzee semtumbi aliekuwa kang'ang'ania hati kuna muda alikuwa anauliza nini bodi isikope yenyewe ikajenga hayo maduka,alafu yakawa yanalipa hilo deni?hivi unajua pale kwa yale maduka tu kwa mwaka tu sidhan kama walikuwa wanakosa mil 100.na wewe kama ndio kati ya wale wanabodi,hivi mnadhani mngeshindwa kukopa hela na mkajenga wenyewe hayo maduka,kuliko kumpa mtu mkataba wa miaka 30 kweli?Miaka 20 iliyoingiwa mkataba ni upande wa uwekezaji wa Maduka upande wa Msikiti hakuna mkataba unajengwa bure na huyo Mwekezaji wa Maduka amejitolea sadaka ya kujenga Msikiti for free na utakuwa chini ya Wanachama wa Mwenge.
Na haya ndo Maduka yanayojengwa sehemu ulipokuwa Msikiti Mwenge mbele ya Magorofa ya Jeshi barabara ya TRA