Takwimu zinaonesha kila sekunde 24 kuna mtu anafariki kwa ajali ya barabarani

Takwimu zinaonesha kila sekunde 24 kuna mtu anafariki kwa ajali ya barabarani

Kwa mujibu wa Jeshi la Polisi, kati ya Januari hadi Septemba 2023, kulikuwa na matukio ya Ajali za Pikipiki 339 zilizosababisha Vifo vya watu 263

Mkuu wa Dawati la Elimu Usalama Barabarani, Kamishna Msaidizi Michael Deleli amesema Majeruhi walioripoti taarifa za Ajali kwenye Vituo katika kipindi hicho ni 252

Waathirika wakuu katika ajali nyingi za Vyombo vya Moto ni Abiria ambao ni 60% tofauti na makundi mengine yanayoathiriwa na Ajali hizo

Soma Takwimu zinaonesha kila sekunde 24 kuna mtu anafariki kwa ajali ya barabarani
ukipanda boda halafu tangu mwanzo wa safari dereva boda wako ni mwendo wa honi tu pwiiip pwiipwiip hadi mwisho wa safari anataka apite kila gari, kila kizuizi wala Subra, ujue soon mnapukutika nae....

maana semi trela imewasha indicator kabisa kwamba inakunja kulia au kushoto yeye analazimisha kupita huko huko na mihoni kibao kwa speed ya 100 kwenye kona shaaaa ...

Taa za barabarani nyekundu zimewaka kabisa na gari zimesima, anakuja boda na abiria wake pwiipwiip piiii piiii anazitime eti zilizoruhusiwa zipungue halafu eti kwa speed ajatize awahi kulikwepa lililoruhusiwa,

My friend wewe abiria na uyo boda wako soon mnapukutika kuongeza hiyo idadi ya waliopukutika kwa ajali ya boda bila wasi wasi wowote ....
 
Ila imerahisisha sana usafiri,shida ni elimu ya barabarani na wao kujithamini kwamba uhai wao ni muhimu.Sasa unakuta pikipiki imetolewa side mirror,kavaa ndala mregezo ,suruali boxer iko nje kweli atahimili mikiki ya barabarani!Maana yake mtu wa hivyo hata akili haijakaa sawa,chochote barabarani kitakuwa kipengere.
Pikipiki ya mtu alietoa side mirror, Sipandi.
Juzi tar, 12 Alhamis, nilikua natokea kibaha, ukitoka wakati naingia kwenye mataa ya pale, kwa mkuu wa wilaya ya Ubungo, taa zilikua zinaruhusu gari za kutoka kibaha na mjini kupita, kwa kuwa barabara ile haitengenezi foleni, gari zilikua mwendo kiasi.
Mwendesha boda mmoja, alikua anatokea upande ofisi za mkuu wa wilaya zilipo, akataka kukatiza barabara bila kusubiri taa za upande wake kuruhusu.

Kilichotokea akaenda kuigonga gari kwenye mlango wa dereva, ila boda alianguka vibaya sana, aliangukia kichogo, sijui ilikuaje, maana sisi tuendelea na safari.
 
Wiki tatu nyuma asubuhi mida ya saa 1 nawahi town kuna mishe ya muhimu. Nmefika fresh Fire kuna kale kafoleni ka kuingia mjini. Trafiki akaturuhusu mbele yangu zilikuwa gari kama 3 zikapita ile naingiza gari sijui boda alitoka wapi kakatiza shaaaa pembeni yangu kuna noah. Nilishtuka sana nikapiga break yule mwenye noah alikosa kosa yule jamaa ilibidi yule boda achore duara kwenda mbele ili noah asimpasue. Sasa cha kuchekesha nilipopiga break nikawa mkabala na yule trafiki akaniambia unasimama Kwanini wewe peleka moto tu achana nao hao.
Dah mpaka jioni yake nawaza ile kauli ya yule trafiki nikajua hawa watakuwa wameshachoka na hawa boda. Na nikawaza ningembutua yule boda ingekuwaje maana no kupotezeana muda tu kijinga. Na hicho ndio kinachowapa kichwa boda wengi wanajua kuwa ukimgonga utapoteza muda wako na resources nyingine so kuepusha utamuacha tu kama kuchomeka achomeke au umpishe aende zake.
Kwakweli serikali iingilie Kati hili suala ni janga. Huwa narudia kusema hili nawahurumia sana watoto wadogo wanaofundishwa kuruka barabara kwenye zebra wakati hao boda zebra ndo hawazingatii kabisa yani. Wao ni spidi shaaaa na honi tu.
Kifupi wamegeuza honi kuwa break zao
 
Ni elfu 3 au mia 3?

Wiki iliyopita kuna mdogo wangu tumemzika kisa usenge wa bida mmoja mmoja tu mvuta bangi alietaka ku overtake gari akakuta mbele kuna gari nyingine inakuja akakimbilia pembeni na kumgonga huyo dogo, ambae aliangukia kichwa na damu kuvujia ndani.
 
Wiki tatu nyuma asubuhi mida ya saa 1 nawahi town kuna mishe ya muhimu. Nmefika fresh Fire kuna kale kafoleni ka kuingia mjini. Trafiki akaturuhusu mbele yangu zilikuwa gari kama 3 zikapita ile naingiza gari sijui boda alitoka wapi kakatiza shaaaa pembeni yangu kuna noah. Nilishtuka sana nikapiga break yule mwenye noah alikosa kosa yule jamaa ilibidi yule boda achore duara kwenda mbele ili noah asimpasue. Sasa cha kuchekesha nilipopiga break nikawa mkabala na yule trafiki akaniambia unasimama Kwanini wewe peleka moto tu achana nao hao.
Dah mpaka jioni yake nawaza ile kauli ya yule trafiki nikajua hawa watakuwa wameshachoka na hawa boda. Na nikawaza ningembutua yule boda ingekuwaje maana no kupotezeana muda tu kijinga. Na hicho ndio kinachowapa kichwa boda wengi wanajua kuwa ukimgonga utapoteza muda wako na resources nyingine so kuepusha utamuacha tu kama kuchomeka achomeke au umpishe aende zake.
Kwakweli serikali iingilie Kati hili suala ni janga. Huwa narudia kusema hili nawahurumia sana watoto wadogo wanaofundishwa kuruka barabara kwenye zebra wakati hao boda zebra ndo hawazingatii kabisa yani. Wao ni spidi shaaaa na honi tu.
Kifupi wamegeuza honi kuwa break zao
Bodaboda ni wazembe sana acha wafe

Sent from my Pixel 5 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom