Tamisemi na wizara ya elimu tunaomba mtoe tamko kwa sisi tulio kosa ajira

chemichemi

Senior Member
Joined
Apr 5, 2014
Posts
116
Reaction score
3
Tangu watoe ajira za walimu 2013/2014,kuna wahitimu wengi wa vyuo mbalimbali tumekosa ajira mfano mimi chuo chetu korogwe tupo stashahada takribani 195 tumekosa ajira,hatuwezi kuilazimisha serikali itupatie ajira hapana;lakini swali ni kwanini wengine wapewe ajira na sisi tunyimwe,au sisi sio watanzania,mtoe tamko juu ya swalahili tujue nivigezo gani mmevitumia katika upangaji wa ajira??
 

Sio wewe peke yako ata mimi nawengine wengi ambao maskini ya mungu awajuwi kilio chao wanakipeleka kwa nani. Naongea ivi kama mhanga wa hili jambo ni kwa nini wasitowe tamko tujuwe nini kinaendelea.Inauma sana mpaka saizi tumehitimu alafu atujuwi hatma yetu.
 
Mcharge nahisi hawa jamaa hiki kilio na malalamiko yetu hawayaoni,kwani ingekua wanasoma haya malalamiko yetu hakika wangetoa tamko ilikutupoza mimi hapa nilipo mpaka sasa siamini kilichotokea majina 36071 nimekosekana amakweli!.
 
chemichemi hawa jamaa wanatusikia sana,ila wanachukulia kawaida sababu wao wana maisha mazuri na hawana haraka na hili.
 
Sulle,kweli nimeamini aliye shiba hawazi kumjali mwenye njaa kamwe,najuta kusomea ualimu,na neno ningejua huja mwisho wa safari!!.
 
-------- wewe , ukionna haupo jua ulifeli una sap
 
Mlupembe
unajua mimi sio mjinga ama -------- mpaka nipoteze muda nakuandika haya kama ningekua nimefeli nisingekurupuka kuandika haya yaliotusibu karibuni vyuo vyote,ningekua najiandaa kufanya sapp na sivinginevyo.
 
hawa jamaa hawana huruma kweli walisema watu wajaze form kwa kuandika majina vyuo na namba za simu kwa madai kabla ya tarehe moja watatoa lakini tuliona majina ya st john tu xaxa sijui ndio wenye haki ya kuajiriwa
 
Arstotle;
ile fomu ilikua na lengo la kutuondoa na kuturidhisha kisaikolojia katika ofisi zao,maana mpaka sasa hakuna jipya
HATA TAMKO HAKUNA!!!.
 
Arstotle;
ile fomu ilikua na lengo la kutuondoa na kuturidhisha kisaikolojia katika ofisi zao,maana mpaka sasa hakuna jipya
HATA TAMKO HAKUNA!!!.

mkuu hapa tutafute watu wa magazeti watoe habari ili wajue jambo sio dogo kama wanavyodhani
 
Arstotle;
tafadhili ndugu kama una no.ya mhariri wa gazeti lolote nakuomba uweke hapa
 
labda walikuwa wanafanya sensa jamani ndo maana wakatuambia tuandike majina na vyuo
 
Afu hawa watu wengin wanaokurupuka kutoka usingizin hawafai hum,mi siwezi nkawa nimesupp afu niongee ktk mtandao wa umma
 
Serikali inaajiri kwa idadi na mahitaji. Sasa kama watu wamehenea wakiwaajiri watawaweka wapi? Na kuwalipa nini? Au mnataka kujitolea!
 
hivi we rolla,mahitaji yao ni walimu wangapi na wanahitajika walimu gan?maana umeongea kama msemaji wa tamisemi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…