Tamko la Baraza Kuu la Jumuiya za Ansaar Sunnah Tanzania (BASUTA) kuhusu mkataba baina ya Tanzania na DP World

Ahaaa!Kumbe vifua vyenu Ansaar Sunnah mmejaa chuki kwa sababu kuna mikataba ya TEC na Serikali mliyosubiri kuitumia ktk kuutetea huu wa DP World na mnatumika kumlinda wa dini yenu?Kwamba HUKO nyuma ilikuwepo mikataba mibovukuliko huu na huu mbovu uendelee ili iwe saresare maua?BAKWATA nao watakuwa na tamko kama hili la Waislamu?
 
Nchi hii ujinga ni wa kiwango cha juu, waliosema DPW wana mkataba mbovu wa IGA leo hii wapo kimya na pengine wanafaidika katika kupitishia mizigo yao pale TPA.

Oooh IGA hii mbaya na mbovu kabisa!, leo hii Adani yupo hapo hapo bandarini tena yeye ndio anayefanya biashara katika magati nyeti kuliko huyo DPW.

Maaskofu hawawezi kukwepa lawama za wao kutaka kumkwaza Rais SSH katika suala hili la uwekezaji pale bandarini.
 
Leo hii adani yupo hapo bandarini na kampuni yoyote ya kitanzania haijazuiwa kuwekeza muda wowote ule katika bandari yoyote iliyopo ndani ya JMT.

Hiyo IGA tuliyodanganywa na wasomi kwamba inakwenda kuimiliki bandari nzima haina mabavu ya kumuondoa Adani na haitakuwa na mabavu ya kumuondoa muwekezaji mwingine yoyote atakayetaka kuwekeza kule Kigoma, kule Nyasa, kule Mtwara na Lindi.
 
Mkuu. Je ukisema chakula hiki sio kitamu na bado ukawa unakula basi ni shida ? Hwana jinsi na ni haki yao kutumia hiyo bandari
 
Mkuu. Je ukisema chakula hiki sio kitamu na bado ukawa unakula basi ni shida ? Hwana jinsi na ni haki yao kutumia hiyo bandari
Kusema haina maana kama huna uwezo wa kuthibitisha kwamba ni kichungu.

Maaskofu waliingizwa mkenge na watu ambao hawana utaalamu na masuala ya sheria za kimataifa. Pengine ni suala la dini ya hao wamiliki wa DPW kuwa ndio ile ile ya SSH.
 
Watetezi wa mkataba wa Bandari, wanaotaka masai waondolewe na wanaochekelea wakosoaji wa rais wakitekwa, kuteswa na kuuuwa ni watu wanaofanana. Ukiangalia hata wasimamizi wa huu uharamia wote wanafanana...
 
Kusema haina maana kama huna uwezo wa kuthibitisha kwamba ni kichungu.

Maaskofu waliingizwa mkenge na watu ambao hawana utaalamu na masuala ya sheria za kimataifa. Pengine ni suala la dini ya hao wamiliki wa DPW kuwa ndio ile ile ya SSH.
Walioingizwa mkenge ni wewe na unaofana nao ....TLS na wanasherio wote magwiji walisema ni mkataba wa kipumbavu. Hata hukumu ya ile kesi waliofungua akina mwabukusi kuna sehemu inaonyesha mapungufu ya ule mkataba sema walijifaya hawawezi kuingilia mhimilii mwingine. Unafikiri kwanini rufaa ya ile kesi inapigwa danadana?
 
Uelewa wa sheria umepimwa kwa namna walivyoshindwa kuutafsiri huo mkataba, Hao TLS wasikutishe kwa jina lao kubwa walishindwa kuitafsiri IGA wakawapotosha mpaka maaskofu.

IGA haiwezi kuibana bandari eti isitafute mwendeshaji mwingine, pale bandarini kuna Adani, mhindi huyu kaja mwaka mmoja baada ya DPW na kwa sasa wanafanya kazi pamoja hapo hapo bandarini, hiyo IGA ingekuwa inatufunga kama kina Mwabukusi walivyodanganya umma hao Adani wangeweza vipi kuingia mkataba na Bandari wa kufanya shughuli za kiuendeshaji?.

Watu wangu wanateketea kwa kukosa maarifa. Hiyo rufaa haisikilizwi na haiwezi kusikilizwa kwa sababu ni upuuzi mtupu. Huyo Mwabukusi ni mweupe sana kwenye masuala ya kisheria na nia aibu kuiongoza taasisi kubwa ya TLS.
 
Kwani nchi hii kunq kufuata sheria...kwa sababu hao wengine wamekuja bandarini ndiyo umeona akina Issa Shivji na magwiji wengine wamekosea? Wenyewe wameutafsiri mkatabata kama ulivyo na ni rubbish hata kwa mtu asiye jua jua sheria.
 
Kwani nchi hii kunq kufuata sheria...kwa sababu hao wengine wamekuja bandarini ndiyo umeona akina Issa Shivji na magwiji wengine wamekosea? Wenyewe wameutafsiri mkatabata kama ulivyo na ni rubbish hata kwa mtu asiye jua jua sheria.
Wamewaingiza chaka kina nyinyi msioelewa chochote. Huwezi kuutafsiri mkataba kwa kutazama kifungu kimoja tu, Ule ulikuwa na vifungu 24 vinatafsiriwa vyote kwa pamoja.

IGA haiizui serikali yetu kuwa na mwendeshaji mwingine kwenye bandari zetu na pia pale pale bandarini TPA.

DPW anaaendesha magati namba 4 mpaka 8 pekee. Adani anaendesha magati namba 9 mpaka 11. Na TPA kama mwenyeji anaendesha magati namba 0 mpaka namba 3 pekee.

Mfano, wewe na mimi tunaweza kuwa tunaifahamu kampuni nyingine yenye uwezo wa kuendesha bandari tukaenda wizara ya mawasiliano na uchukuzi tukaiomba kuendesha bandari ya Mtwara au ya Tanga na tutapewa tenda ya kuendesha ikiwa lipo tangazo la wizara lenye kuita waendeshaji kwa ajili ya bandari hizo na hiyo IGA ya DP World haina nguvu ya kutufanya lolote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…