Tamko la Baraza la Maaskofu wa Kipentekoste (PCT) kumjibu Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi

Tamko la Baraza la Maaskofu wa Kipentekoste (PCT) kumjibu Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi

Ki ukweli ktk hili mimi niseme tu sijakubaliana na viongozi wangu wa PCT,kirahisi hivyo kukubali kuletewa
katiba bila uwakilishi wa wapentekoste eti "tunakubali yaishe" ili iweje???? sijapenda'

Hata mimi sijapenda,ila tuache kuwakejeli wapakwa mafuta wa Bwana.
 
Wakiulizwa watasema wametumia hekima na wameongozwa na roho. Ukiniuliza mimi nitasema biblia haiwaagizi wao kuwa waoga kiasi cha kushindwa kusema kweli na kutetea maslahi ya wanyonge. Hivyo kwa msimamo huo waelewe wamekubaliana na upuuzi wote utakaofuatia ambao serikali imeshaanza kuufanya na itakaoendelea kuufanya.

Naunga mkono maelezo yako wamesoma biblia nusu nusu na hawakuwatendea haki waumini wao kama walijua si vyeme kufunua uchi wa baba si wangekaa kimya toka zamani. Na wasiwasi na hili tamko halina uhalali wowote wao walipaswa kudai haki yao na wala sio dhambi. Imekula kwao. Kidumu chama cha Mapinduzi.
 
Ni kweli hata wao wanajua hilo. Lakini mimi tatizo langu hasa halikuwa nani kasema nini. Langu lilikuwa ile haki iliyopotea inakuja kwa kukubali yaishe?

Hivi bado kuna wanoamini kuwa usawa unaombwa? Hakuna heshima ya bei rahisi.

huku kwetu mtu akikupiga kushoto unampa na kulia akupige,ndio maana hatuna tabia ya kujilipualipua kisa kuliliza kisasi,tunamaliza kwa usalama
 
Hata hivyo ufalme wetu sio wa dunia hii, sasa hii katiba ni ya Kaisari. Mwachieni Kaisari.
Mungu tupe hekima katika hili. Sijui wakipitisha, marufuku watu kunena kwa lugha, itakuwaje.
 
Mimi nafikiri ingekuwa Busara kwa baraza hilo sio kuishia kusema tu tulipeleka majina ya watu tisa. Ila wangeenda mbali kidogo na kusema ni tarih Ngapi walipeleka majina hayo. Ili Serikali ifanye kazi zake kwa kuangalia katika dispatch.

Poleni sana
Ukisoma vizuri utaona kama wanasema "kuna kzai maalum imefanyika" kwa hiyo ni useless kusema unayosema.
Kulingana na andiko lao, ni kuwa kwa kuwa serikali imefanya makusudi ikiwa ni kazi "maalum", kuna haja gani ya ku-disclose hizo details?

Hii ndio ninaipata nikisoma kati ya mistari...!
 
Jamani ndo tumenyang'anywa haki yetu kirahisi hivi?? Mbona mimi sisikii kukubali kirahisi hivi? Maweeeeeeee!! Uwiiiii !! Huu ni ukandamizaji....
Askofu wangu Gwajima na Askofu Kakobe vipi jamani.... Haki zetuu.... PCT why are you backing down??
They are probably avoiding further embarrasment from the truth that the never submitted names for the Constitutional Assembly.
 
attachment.php

Teh teh teh!

Hawa wanaonekana washakatiwa kidogo dogo!

Mbona wamekuwa wapole ghafla??

Halafu Agano la kale sikuzote hawataki kulitumia! Iweje lea kwenye hii issue watuletaa mambo ya walawi hapa!??

Hebu ngoja tuwaulize hawa waparoko wengine! Huenda wakawa na habari nyeti!

Cc matumbo mgen Nyenyere Cureone 2013 Eiyer Remote
 
Last edited by a moderator:
Nawashauri hawa wanaojiita maaskofu wakasome maneno ya Yesu aliposema "Call no man your father on earth, for you have one Father, who is in heaven" (Matt. 23:9).
 
Mambo ya Walawi 18:7
Utupu wa baba yako, wala utupu wa mama yako, USIUFUNUE, maana ndiye mama yako; Usiufunue utupu wake.

"Call no man your father on earth, for you have one Father, who is in heaven" (Matt. 23:9).
 
Watanzania tumezoea sana kulalamika tu sirini... Mfano humu JF .... Lakini mkiambiwa tujitokeze kupinga kitu fulani mnakaa majumbani... Serikali inasubiri msemo wa wananchi sio Maaskofu... Serikali itajuaje msimamo kuwa ni wa wapentekoste wote na sio wa maaskofu wachache tu....???
 
Kulikuwa na mkutano pale PTA jumamosi lakini umati uliojitokeza haulingani na tulivyo sisi wapentekoste...
 
Nimechoka na tamko hilo halafu tamko dhaifu hilo linatufanya tuonekane wanyonge kweli. kukubali aliyetumwa majina hakufikisha kabisa ingekuwa busara za kuongozwa na roho. Lakini kupindisha maandiko kuwa serikali ni baba yao haki ya kweli wakati wenu utafika. pengine haya makanisa wengi wakimbizi ambao hawana sifa kutunga katiba
 
kwa taarifa kama hii, ni haki majina yenu kutupwa kapuni. Unatoa taarifa kama hii kwa umma halafu hata jina la mtoa taarifa hakuna!!!. Ukitoa taarifa kama hii lazima uweke jina na sahihi tujue nani kaiandika. Hapa yawezekana hata mlipopeleka majina hamkuonesha nani kaorodhesha majina ya waliopendekezwa, na wachambuzi wakaona aliyetuma ni mhuni tu.
 
Naunga mkono maelezo yako wamesoma biblia nusu nusu na hawakuwatendea haki waumini wao kama walijua si vyeme kufunua uchi wa baba si wangekaa kimya toka zamani. Na wasiwasi na hili tamko halina uhalali wowote wao walipaswa kudai haki yao na wala sio dhambi. Imekula kwao. Kidumu chama cha Mapinduzi.


Hawajasoma nusu nusu. Wamefanya makusudi tu. Na nakubaliana na hoja kuwa tangu walipoanza kukosoa uteuzi walishaanza kufunua. So why a sudden change? Kama waliona wamekosa haki na wakaamua kuidai so why this dilemma now? Hapana hawa sijawaelewa kabisa. Na tukiendelea hivi tutapata shida sana nchi hii kufikia hatua ya kuwa na hadhi sawa.
 
huku kwetu mtu akikupiga kushoto unampa na kulia akupige,ndio maana hatuna tabia ya kujilipualipua kisa kuliliza kisasi,tunamaliza kwa usalama

Yesu hakumaanisha tuwe wapumbavu kaka. Kama unadhani mtu akikufanyia uovu unatakiwa umruhusu akufanyie zaidi ni kwa nini Yesu alipowakuta wanafanya biashara Hekaluni alikuwa mkali?

Kuna upole na kuna ujinga. Kuna hekima na kuna upumbavu. Vinginevyo huchelewi kujiwa na jirani yako akakwambia kama we umeokoka kweli nipe hicho kibaba cha unga mimi nikale na familia yangu wewe kalale njaa na familia yako kwa kuwa imeagizwa tuwe na upendo na akuombaye mpe!

Hapana walichemsha. ukiona umedhulumiwa haki yako, ukaamua kudai...dai mpaka upate, kama kweli ni haki yako.
 
"IF YOUR LEGS CAN'T TAKE YOU TO PRAYER,THEN HOW DO YOU EXPECT THEM TO CARRY YOU TO PARADISE??"
nimeipenda hiyo hapo juu.

Lakini ukweli wa MUNGU kabisa kama kweli maaskofu wametumia mstari huo ku-justify tatizo hili naomba niwe wazi kabisa kuwa wamekosea saaaana na waombe radhi waumini wote wa kanisa la Tanzania kwa mhusika aliyetumwa kufanya kazi hiyo na asifanye!!!

1. Inapaswa maaskofu wajue kuwa waumini wana akili zao na wanamjua MUNGU sana na wanayajua maandiko vizuri sana. wao kuwa hapo walipo si kwa akili zao hata kidogo! kwanini wanataka kutumia akili zao wakati wanajua hawana za kutosha pasipo MUNGU??? Hata mimi naamini serikali haikusema uongo kuna kosa tu limefanywa na maaskofu.

2. Mtu anaetaka kujibu hoja zozote kihekima lazima apime mambo makuu ya hoja hiyo! Hoja hapa ni kupata katiba ya Nchi itakayotumiwa na watu wote wa imani zote, mtu mwenye kujibu kwa kumtumia Roho Mtakatifu katika hoja kama hii hawezi kabisa kutumia mstari huo!! huko ni kuchoka kiroho kabisa wala haihitaji kuuliza mtu!!!

3. Je Nabii nathan angesema nini mbele ya mfalme Daudi kama ukweli wa kuzini na mke wa Uria ulikuwa kumkosea MUNGU?

4. jE, Musa alipoamriwa kuwatoa wana wa Israel katika utumwa kule Misri angesemaje mbele ya Mfalme Farao? tena alimlazimisha mfalme awatoe watu wake!

5. Je, Shedrack, Meshak na Abednego tungewajuaje kama wangetoa majibu kama haya wakati wa utumishi wao kwa Bwana? maana wao walimwambia ukweli mfalme kama kufa na wafe lakini Mungu akawasimamia kwa kuwa walijua wajibu wao kwa Mungu wao na watu wao! mbona ninyi maaskofu mmshindwa kabisa kusimamia ukweli mbele ya Taifa hili lote? mimi nalia na mstari mlioutumia kujustify TAMKO lenu, it is not right at all!!!

6. Kama Daniel (mkuu wa wilaya wakati huo) huku akiwa Nabii na mtumishi wa MUNGU aliyetukuka alitupa chini heshima yake yote ya ukuu wa wilaya akadharauliwa ili Mungu atukuzwe ndani ya tundu la simba, vipi leo ninyi watumishi wa MUNGU mnasita kusema ukweli? kutetea wanyonge wa nchi hii? kutetea imani? kutetea haki za msingi za watu!, Je hamjui kuwa mwoga na mchawi na mzinzi wamewekwa kundi moja??? maandiko hayo mliyoyatumia hata kama mmekuwa waoga hamwoni kuwa sii sawa kabisa? tena mkatumia andiko moja tuuu! Hamkusoma YESU alisema ushahidi wa watu wawili wakubalika?

7. Je Stephano hakuuwawa kwa kutetea imani dhidi ya watawala? je aliwavua nguo wazazi wake?

8. Je Petro hakufungwa gerezani kwa kuwaambia ukweli watawala? YESU hakuwajibu mafarisayo juu ya hukumu zao na sheria zao juu ya watu? Soma Math. 23: 1 - 29 uone alivyowapa haki yao.

9. Je Paulo hakupigwa viboko 40 kasoro kimoja kwa kuwaambia ukweli watawala? kwanini ninyi mmeshindwa ilhali ni viongozi wa IMANI?

10. JE Yohana hakukatwa kichwa sababu ya kumwambia Mfalme ukweli?

11. Je kwanini mmetia mashauri giza?? enyi wana wa kizazi cha upotevu!!!

12. Mumewatwika watu wa Mungu mzigo mzito ambao ninyi wenyewe hamkuweza kuuchukua!! NENO hili lawafaa ninyi hasa katika wakati huu , Yer. 23:1 - 9!!! mmekumbuka mafungu ya 10 tu na kuwaita watu mbele ili muwaabishe wala si sheria ya MUNGU, lakini serikali mmeistahi! mumetubisha watu hadharani lakini serikali mumeiogopa!!

Kwasababu hiyo ya unafiki na kutenda haya yote mbele za watu, BWANA WA MAJESHI, MUNGU MWENYE NGUVU MFALME WA AMANI, amewaondolea kilicho chenu mahali pake!!! wala hamtafikia upeo wa mafanikio yake aliyowakusudia tena! ama sivyo mtubu na kuliambia kweli KANISA LA MUNGU hapa Tanzania! Nayo yamekuwa.
huu ni ujumbe wa BWANA anaetaka aweza kunipigia 0765 118 221

 
...kwa kuwa viongozi wa Kipentekoste hawakuwa na nalengo yanayofanana na magamba,ilikuwa sio raisi mwenyekiti wa chama chakavu kuwateuwa...

Eti Kingunge anawakilisha Waganga wa Kienyeji............ CCM wana mambo ya ajabu.
 
mimi naamini Rais Hakuyapata majina hayo, angeyapata hangeacha kuteua mtu wa Mungu kuwakilisha Taifa.
 
Back
Top Bottom