TANESCO achana na Solar Energy, ni wizi na hasara kwa Taifa

TANESCO achana na Solar Energy, ni wizi na hasara kwa Taifa

Wewe your outdated,tekinologia ya solar imeishapiga hodi katika mataifa mengi, na zimefanyika breakthrough ya solar panel hata battery.
Hata ujenzi wa nyumba kwenye watu makini wanaezeka kwa solar panels.
Kama hiyo haitoshi wenye nyumba wanazalisha umeme wa ziada kuliko matumizi yake na kuuzia makampuni makubwa ya ugavi wa umeme.
Lakini solar tekinologia imehujumia na makampuni yanayozalisha mafuta.
Wewe ndio hujui kitu. Unasema wenye nyumba wanazalisha umeme? Umeme wa nyumbani wa kuwashia bulb tano na TV energy saving ndio unataka utumike kuendeshea vinu vya kuchana mbao?

Nitajie kiwanda kinachoendeshwa na umeme wa jua hapa duniani. Kisha nani kakwambia makampuni ya mafuta yanahujumu.

Tatizo ni moja: Gharama za kuendeshea umeme wa jua ni ghali. Unajua kwa nini mtu atakayegundua njia mbadala na more convenient kutunzia charge zaidi ya Lithium ion batteries atakuwa the next billionaire?

Investors hawatumii kelele na siasa nyingi. Hawana porojo hata siku moja, hakuna mfanyabiashara kichaa atanunua batteries za kuhifadhi umeme kwa gharama kubwa kisha baada ya miaka miwili zipoteze nusu ya uwezo wake, baada ya miaka minne azitupe anunue nyingine. Wakati huo panels zilimuweka gharama kubwa, wataaalam wana kazi nyingi ni wengi na wana elimu kubwa hivo kuchangia staff kuwa kubwa na gharama sana. Staff wa HEP station ni mgambo kuzuia wewe usijitupe uko na stress zako. Mitambo inakaa mihongo hata minne haijaguswa kabisa.

Unajua zile pikipiki za umeme za LINKAL zinauzwaje na zikiisha battery yake ile ambayo hupungua uwezo baada ya miezi hata 20 inauzwaje? Sasa battery heavy za viwanda ziuzwe bei gani hapo kwa comparison.

Nitajie bwawa lolote la kufua umeme hapa Tanzania ambalo lishawahi fanyiwa ukarabati tangu yajengwe. Kule DRC wanatumia umeme wa HEP ambayo haikuwahi kamilika hata. Uganda, Owen Falls iliporekebishwa watu tulitangaziwa wakati imetumiwa miongo kadhaa. Nchi yako inashindwa DART sembuse miradi ya kuharibu kabisa uchumi kama umeme. Umeme na mafuta havina majaribio ya kubahatisha, inflation ya hapo hutoiweza.
 
Wewe ndio hujui kitu. Unasema wenye nyumba wanazalisha umeme? Umeme wa nyumbani wa kuwashia bulb tano na TV energy saving ndio unataka utumike kuendeshea vinu vya kuchana mbao?

Nitajie kiwanda kinachoendeshwa na umeme wa jua hapa duniani. Kisha nani kakwambia makampuni ya mafuta yanahujumu.

Tatizo ni moja: Gharama za kuendeshea umeme wa jua ni ghali. Unajua kwa nini mtu atakayegundua njia mbadala na more convenient kutunzia charge zaidi ya Lithium ion batteries atakuwa the next billionaire?

Investors hawatumii kelele na siasa nyingi. Hawana porojo hata siku moja, hakuna mfanyabiashara kichaa atanunua batteries za kuhifadhi umeme kwa gharama kubwa kisha baada ya miaka miwili zipoteze nusu ya uwezo wake, baada ya miaka minne azitupe anunue nyingine. Wakati huo panels zilimuweka gharama kubwa, wataaalam wana kazi nyingi ni wengi na wana elimu kubwa hivo kuchangia staff kuwa kubwa na gharama sana. Staff wa HEP station ni mgambo kuzuia wewe usijitupe uko na stress zako. Mitambo inakaa mihongo hata minne haijaguswa kabisa.

Unajua zile pikipiki za umeme za LINKAL zinauzwaje na zikiisha battery yake ile ambayo hupungua uwezo baada ya miezi hata 20 inauzwaje? Sasa battery heavy za viwanda ziuzwe bei gani hapo kwa comparison.

Nitajie bwawa lolote la kufua umeme hapa Tanzania ambalo lishawahi fanyiwa ukarabati tangu yajengwe. Kule DRC wanatumia umeme wa HEP ambayo haikuwahi kamilika hata. Uganda, Owen Falls iliporekebishwa watu tulitangaziwa wakati imetumiwa miongo kadhaa. Nchi yako inashindwa DART sembuse miradi ya kuharibu kabisa uchumi kama umeme. Umeme na mafuta havina majaribio ya kubahatisha, inflation ya hapo hutoiweza.
Mkuu kwanza jipange upstairs.
 
Asante kwa kujibu maswali kama livyouliza.

Mkuu, kwa haraka kabisa ninaona kosa kwenye namba 5 na 6. Na makosa haya yamefanywa sehemu nyingi tena sehemu nyingine unakuta ni mradi mkubwa kabisa lakini namba sita na namba tano zako zimewapiga chenga. Makosa haya uchangia pakubwa kwa sababu yanaathiri uzalishaji wa umeme kutoka kwenye panel.

Ipo hivi, panel uweza kuzalisha umeme kwa kiwango cha juu sana endapo muale wa jua utaipiga panel kwa pembe mraba yaani katika nyuzi tisini. Kwa kuwa jua ubadilika orientation kwa siku ( asubuhi jioni) au majira ya mwaka ( March Ikweta, Juni Tropiki ya Kansa September Ikweta na December Tropiki ya Kaprikoni), ili kufanisha zoezi la kuhakikisha muale wa jua unagonga panel katika nyuzi tisini yahitajika tracking system ya kugeuza panel kulifuata jua. Hii uongeza gharama kwa system ndogo ya umeme jua.

Hata hivyo, wataalamu walishafanya ukokotozi wa kupata muale wa jua kwa kiasi kikubwa kwa siku na mwaka bila tracking system. Kwa upande wako ambaye upo Arusha. Arusha Latitude yake nadhani ni mbili au tatu na ipo kusini mwa Ikweta. Kwa hiyo unatakiwa utege panel yako katika nyuzi 10 kujumlisha nyuzi za latitude ya Arusha. Tukichukulia Arusha Latitude yake ni tatu, basi panel itegwe nyuzi 13 kutoka uso wa aridhi ulio sawa ( horizontal surface). Na itegwe hiyo panel kwa ukuangalia upande wa Kaskazini kwa sababu Arusha ipo upande wa kusini mwa Ikweta hivyo muda mwingi jua litakuwa upande wa kaskazini mwa Arusha. Cha msingi pia, usilaze panel yako juu ya bati. Inyanyue kwa kuiwekea stendi ambayo ni zaidi ya sentimeter ishirini kutoka uso wa bati. Joto likizidi upunguza uzalishaji wa umeme kutoka kwenye panel. Kwa viwango maalumu vya utengenezaji wa panel, Joto la nyuzi joto 25 ndilo hutumika kupimia hiyo kiwango kikubwa cha umeme ( maximum power) kizalishwacho na panel. Joto likiongezeka in away power upungua.

Kwa uchache hayo tu ni baadhi ya matatizo yanayoweza kuwa yamefanya system yako kutofanya vizuri kadiri ulivyotarajia. Kwa masuala mengine tuwasubiri nguli wa utaalamu wa mambo ya umeme huu wa jua watuelimishe.

Nikutakie siku kuu zote njema. Amina.
Thanks Mkuu ngoja kesho nimtafute fundi nimpe hayo maelezo yako ayafanyie kazi.
 
Nakazia TANESCO kuwekeza kwenye Njia hizi za Umeme hasa wa Solar ni gape la upigaji...

Kwa wauza vifaa vya umeme wa solar Tafadhali msiwadanganye wananchi wakawaida wasiofahamu kuhusu mambo basic ya kiufundi wakawekeza pesa nyingi kwenye umeme huu huku mkiwapotosha kwa sababu mwanga wa jua ni bure na umeme wa maji unakatika katika ovyo hasa vipindi vya kiangazi na jua kali...

Nawaachia wachangiaji wa mada hii andiko zuri kuhusu HVDC (high-voltage, direct current (HVDC)) na kwa nini kuamua kuitumia at high scale kwa Nchi nyingi Africa ni sifa za kijinga na wizi usiojali kesho ya wengine HVDC Transmission Systems
 
Wengi tukisikia solar energy tunajawa na hisia kwamba ni jambo la maana sana! Ni umeme mzuri kwa mwanakijiji anayetaka mwanga wa kufukuza wanyama watembeao gizani tu! Kwani nchi zetu hizi maskini hatuhitaji miradi mikubwa kiasi hicho kinacholengwa na Tanesco.

Ni uharibifu wa pesa kwa kujidai kuingia kwenye renewable energy. Ni biashara ya makampuni ya kigeni kujipenyeza ndani ya TANESCO, nao wanaandika eti by 2050 Tanzania itatumia renewable energy, wakimaanisha wind na solar. Huu naweza kuita ni upuuzi.

Solar na wind bado ni luxurious energy sources ambazo tunawaachia nchi zilizoendelea kufanya majaribio. Ni aibu kwa shirika kama Tanesco kujiingiza kwenye miradi ya gharama kubwa kiasi hicho. Maneno kama renewable energy na alternative energy ni kujiridhisha tu na kuwazubaisha wanasiasa na kunufaisha makampuni ya nje ambayo yanatuuzia hizo pannels.

Katika East Africa walianza Uganda. Kwa mikogo wakatangaza kuwa na solar farm, ukweli ni kwamba hilo ni shimo la fedha. Wangeweza kupata umeme mwingi kutoka Nile kuliko hizo pannels. Sasa wameingia Tanesco nao kwa mikogo wanatangaza tender ya kufunga mitambo ya solar. Spain Andalusia inajigamba kuwa na solar farm ya kisasa kabisa na technolojia za kisasa lakini bado ni umwamba tu, wana umeme mwingi kwa njia za nuklia na mafuta.

Je, kwa nini Tanesco inajiingiza kwenye solar? Jibu ni rahisi: Kwanza hawaijui kiuhakika kiasi hicho zaidi ya kusimuliwa na makampuni yanayouza pannel na kutoa mifano ya nchi jirani na ulaya ambako hakuna nchi hata moja ilnayotegemea solar. Mfano mzuri ni ujerumani ambako Angela Merkel aliahidi kuondoa mitambo yote ya nuklia ili kuweka renewable kama hizi wanazokimbilia Tanesco. Tangu 2005 hadi leo hajafika kokote! Kumbuka huyu ni mfizikia, syansi anaijua sana. UK wao waliongeza nuklia na ikajengwa na kampuni ya China. Hivi karuibuni Afrika kusini imejenga nyuklia mpya na ni mitambo itakayokuwa mikubwa kuliko yote duniani.

Pili Tanesco kuna tamaa ya kupewa kitu kidogo na makampuni ya nje ili kubeba techolojia ya aina hii ambayo kwa tender kama hiyo, lazima itajengwa na makampuni ya nje.

Bila kujali 2050 nani atakuwa hai, Munachokifanya ni wizi mtupu na hasara kwa kizazi kijacho. Kama mna ubavu jengeni mitambo ya nyuklia.
Kama kawaida ya waTanzania, unazungukazunguka tu huelezi kitu kikaeleweka vizuri na wasomaji. Sababu kuu ni kwamba hujui chochote juu ya teknolojia hiyo.

Unachanganya mambo ambayo yote huyajui. Unaufahamu wowote kuhusu umeme unaotokana na nuklia? Unachanganya makubaliano ya kimikataba kati ya Tanesco na makampuni na kuviweka fungu moja na teknolojia za kufua umeme..., jambo linaloonyesha wazi hakuna unachojua kuhusu mada uliyowasilisha hapa.

Duniani kote hakuna nchi inayotegemea njia moja pekee ya kufua umeme. Solar, upepo, nuklia, maji, makaa ya mawe, n.k., zote ni njia zinazotumika kufua umeme, na mara nyingi hutumiwa kwa mchanganyo ili kutotegemea njia moja tu.

Kama Tanesco wanaingia mikataba mibovu na makampuni yanayozalisha umeme kwa kutumia jua, hiyo haina maana kwamba njia hiyo ya solar haiwezi kutegemewa kuzalisha umeme nafuu kuliko njia zingine.

Mada yako haielezi chochote mbali ya kuchanganya mambo na kukufanya uonekane huna ufahamu wowote juu ya mambo uliyoandika juu yake.
 
Kama kawaida ya waTanzania, unazungukazunguka tu huelezi kitu kikaeleweka vizuri na wasomaji. Sababu kuu ni kwamba hujui chochote juu ya teknolojia hiyo.

Unachanganya mambo ambayo yote huyajui. Unaufahamu wowote kuhusu umeme unaotokana na nuklia? Unachanganya makubaliano ya kimikataba kati ya Tanesco na makampuni na kuviweka fungu moja na teknolojia za kufua umeme..., jambo linaloonyesha wazi hakuna unachojua kuhusu mada uliyowasilisha hapa.

Duniani kote hakuna nchi inayotegemea njia moja pekee ya kufua umeme. Solar, upepo, nuklia, maji, makaa ya mawe, n.k., zote ni njia zinazotumika kufua umeme, na mara nyingi hutumiwa kwa mchanganyo ili kutotegemea njia moja tu.

Kama Tanesco wanaingia mikataba mibovu na makampuni yanayozalisha umeme kwa kutumia jua, hiyo haina maana kwamba njia hiyo ya solar haiwezi kutegemewa kuzalisha umeme nafuu kuliko njia zingine.

Mada yako haielezi chochote mbali ya kuchanganya mambo na kukufanya uonekane huna ufahamu wowote juu ya mambo uliyoandika juu yake.
Umeme wa jua hauwezi kuwa nafuu kuliko Umeme wa maji, Mafuta na Gesi per unit price.

China ni nchi ya pili duniani kuwa na Solar plant kubwa lakini Waliamua Kutengeneza artificial sun (“artificial sun,” a nuclear fusion reactor ). Kwa sababu itawapa alot of Energy kuliko mwanga wa jua..
 
Wakati mwingine ni uungwana kukubali kuwa wewe ni mjinga na pengine mpumbavu inapotokea kitu unachofahamu kuhusu jambo fulani ni matokeo ya ujinga ulio nao.
Sielewi kwa nini uliona kuna umuhimu wa kuanza mchango wako na haya maneno uliyoweka kwenye mstari huo!

Nimesoma ulichochangia katika mistari iliyofuata na kuona angalau mchango wako ni bora kidogo kuliko wake; lakini sikuona "upumbavu" wowote katika mada yake. Lakini pamoja na unafuu kidogo katika mchango wako, sioni maelezo yaliyo muhimu zaidi kukufanya wewe usiwe na "ujinga" wa kiasi kikubwa katika mambo uliyochangia.
 
Umeme wa jua hauwezi kuwa nafuu kuliko Umeme wa maji, Mafuta na Gesi per unit price.

China ni nchi ya pili duniani kuwa na Solar plant kubwa lakini Waliamua Kutengeneza artificial sun (“artificial sun,” a nuclear fusion reactor ). Kwa sababu itawapa alot of Energy kuliko mwanga wa jua..
Eeeeh? Hebu sema tena?

Kwamba: "Umeme wa jua hauwezi kuwa nafuu kuliko umeme wa Mafuta per unit price"? Hebu weka tarakimu zako hapo tuanzie mjadala kwenye hilo!

Kuhusu hao waChina "kutengeneza 'artificial sun'" hili hujaeleza chochote mbali ya kutaka kutukoga tu kuonyesha kwamba umeisoma mahali. Sijui kama unaufahamu wa kutosha kutokana na hiyo "artificial sun."

Sijui kwa nini huoni 'contradiction' katika hayo uliyoandika kuhusu "China kuwa nchi ya pili duniani kuwa na solar plant kubwa...," na hayo mengine uliyoendelea kuyaandika. Wasingeona umuhimu wa 'solar plant' isingewalazimu kuwa na "solar plant kubwa".

Hukusoma niliyoandika hapo juu kuhusu ulazima wa nchi kuwa na "energy mix"?
 
Kwa mtazamo wangu njia rahisi ya kumaliza tatizo la umeme hapa nchini ni kuruhusu makampuni mengine yaje kuleta ushindani kwa tanesco,
Eenheee. Utatufanya tulie sana tena mkuu. Mara hii unatufanya tusahau waliyotufanyia IPTL?

Ninakubaliana nawe kuhusu ubovu ulipo Tanesco. Hebu tujaribu kuwarekebisha na wengine tuwaweke ndani wanapokengeuka.
Lakini pia sikatai pendekezo lako la kuwapa ulaji hao makampuni, mradi tu pawe na mbano wa mikataba tunayoingia nao. Hii ya kuja kuvuna hapa na kutuachia majonzi kama tulivyokwishashuhudia na majaribio yaliyofanyika haikubaliki.
 
Mkuu ingawa binafsi nina bifu na Tanesco ila bado hujatoa maelezo ya kitaalam kutushawishi sisi raia ambao ndio wamiliki wa hilo shirika kuona ubovu wa huo mradi wa Solar Energy.

Nilichokiona hapa ni title tu na content ambayo iko very weak iliyojaa malalamiko tu lakini hakuna lolote la kitaalam humo ndani lenye faida.

Jaribu kuleta sababu za kitaalam tukuelewe kuwa huo mradi ni mbovu.

Labda nikusaidie kidogo tu tueleze kitaalam;

1. Hasara za Solar energy vis a vis hydro electric power, gas , oil.

2. Gharama zake.

3. Unit moja itauzwaje compared na ya sasa.

Mpaka hapo baadae,
Utakapokuja na uchambuzi wa kina hii ni ngonjera kama zingine tu.
 
Eeeeh? Hebu sema tena?

Kwamba: "Umeme wa jua hauwezi kuwa nafuu kuliko umeme wa Mafuta per unit price"? Hebu weka tarakimu zako hapo tuanzie mjadala kwenye hilo!

Kuhusu hao waChina "kutengeneza 'artificial sun'" hili hujaeleza chochote mbali ya kutaka kutukoga tu kuonyesha kwamba umeisoma mahali. Sijui kama unaufahamu wa kutosha kutokana na hiyo "artificial sun."

Sijui kwa nini huoni 'contradiction' katika hayo uliyoandika kuhusu "China kuwa nchi ya pili duniani kuwa na solar plant kubwa...," na hayo mengine uliyoendelea kuyaandika. Wasingeona umuhimu wa 'solar plant' isingewalazimu kuwa na "solar plant kubwa".

Hukusoma niliyoandika hapo juu kuhusu ulazima wa nchi kuwa na "energy mix"?
Labda kama unaulewa wa Masuala ya umeme...

Otherwise naweza nikaongea na wewe kilayman...

Charger ya Simu na battery which one is costly than the other one?


Solar is DC in nature, production ya volt 1 ya DC ni ghali kuliko production ya 1V AC, so technically we gharama haziwezi kuwa sawa kamwe
 
Mkuu ingawa binafsi nina bifu na Tanesco ila bado hujatoa maelezo ya kitaalam kutushawishi sisi raia ambao ndio wamiliki wa hilo shirika kuona ubovu wa huo mradi wa Solar Energy.

Nilichokiona hapa ni title tu na content ambayo iko very weak iliyojaa malalamiko tu lakini hakuna lolote la kitaalam humo ndani lenye faida.

Jaribu kuleta sababu za kitaalam tukuelewe kuwa huo mradi ni mbovu.

Labda nikusaidie kidogo tu tueleze kitaalam;

1. Hasara za Solar energy vis a vis hydro electric power, gas , oil.

2. Gharama zake.

3. Unit moja itauzwaje compared na ya sasa.

Mpaka hapo baadae,
Utakapokuja na uchambuzi wa kina hii ni ngonjera kama zingine tu.
Mleta mada yuko sahihi...

Umeme wa solar ni wizi najibu maswali yako
1. Solar Energy vs Hydro electrict

Solar Energy works on principle of Electrons emission by photos... Hii ni process ambayo photons(Light particle zikigonga metallic surface zinasababisha electrons to move)

Sasa zile solar pannels unaziona 98% kama sio zote zimeundwa kwa Silion katika (Layer 3) ya juu ni N-TYPE na ya chini ni P-TYPE ili uweze kuzifanya electrons zitoke kwenye N-Type kwenda P-Type unahitaji only (Visible Spectrum of specific wavelength 300nm hadi 11Knm) na hii ndio challenge ya kwanza kwenye solar energy inaanzia inaitwa Effeciency... Solar cells zote zina effeciency(Uwezo wa solar cells kubadili mwanga wa jua kuwa umeme) currently maximum ni aroung 20% efficiency (in other words 80% ya mwanga wa jua hupotea bure kabisa)

Kuhusu efficiency inategemea na aina ya material iliyotengeza most efficient material ni Mono Crystalline na gharama zake kuziunda ni ghali nakuhakikishia utapita kariakoo nzima usikute solar panel ya hivi, aina ya pili na common ni poly crystalline hii efficiency yake ni around 10% na ya mwisho ni less effecient ni thin-film hizi mtu wa kawaida kabisa anaweza kuuziwa.

Kwa upande wa Hydro electric yenyewe ni AC nina hakika humu ndani ukiomba mtu akusukie generator ya mafuta inayoweza kuzalisha volt 250 hadi 400 from scratch utapata hata watu 10

2. Moja inakaza gharama
 
Namsikitiaga sana mbogo anayeongelea mazingira wakati hana uhakika wa kula yake ya siku/wiki.
Mazingira yanafaida gani kama watu wetu wanakufa na njaa au hawana uhakika wa kula. Serikali ituhakikishie kula kwanza kwa kuwekeza kwenye vyanzo rahisi zaidi ili excess itumike kuendeleza miundombinu mingine ya nchi na kusaidia wananchi wake
 
Wengi tukisikia solar energy tunajawa na hisia kwamba ni jambo la maana sana! Ni umeme mzuri kwa mwanakijiji anayetaka mwanga wa kufukuza wanyama watembeao gizani tu! Kwani nchi zetu hizi maskini hatuhitaji miradi mikubwa kiasi hicho kinacholengwa na Tanesco.

Ni uharibifu wa pesa kwa kujidai kuingia kwenye renewable energy. Ni biashara ya makampuni ya kigeni kujipenyeza ndani ya TANESCO, nao wanaandika eti by 2050 Tanzania itatumia renewable energy, wakimaanisha wind na solar. Huu naweza kuita ni upuuzi.

Solar na wind bado ni luxurious energy sources ambazo tunawaachia nchi zilizoendelea kufanya majaribio. Ni aibu kwa shirika kama Tanesco kujiingiza kwenye miradi ya gharama kubwa kiasi hicho. Maneno kama renewable energy na alternative energy ni kujiridhisha tu na kuwazubaisha wanasiasa na kunufaisha makampuni ya nje ambayo yanatuuzia hizo pannels.

Katika East Africa walianza Uganda. Kwa mikogo wakatangaza kuwa na solar farm, ukweli ni kwamba hilo ni shimo la fedha. Wangeweza kupata umeme mwingi kutoka Nile kuliko hizo pannels. Sasa wameingia Tanesco nao kwa mikogo wanatangaza tender ya kufunga mitambo ya solar. Spain Andalusia inajigamba kuwa na solar farm ya kisasa kabisa na technolojia za kisasa lakini bado ni umwamba tu, wana umeme mwingi kwa njia za nuklia na mafuta.

Je, kwa nini Tanesco inajiingiza kwenye solar? Jibu ni rahisi: Kwanza hawaijui kiuhakika kiasi hicho zaidi ya kusimuliwa na makampuni yanayouza pannel na kutoa mifano ya nchi jirani na ulaya ambako hakuna nchi hata moja ilnayotegemea solar. Mfano mzuri ni ujerumani ambako Angela Merkel aliahidi kuondoa mitambo yote ya nuklia ili kuweka renewable kama hizi wanazokimbilia Tanesco. Tangu 2005 hadi leo hajafika kokote! Kumbuka huyu ni mfizikia, syansi anaijua sana. UK wao waliongeza nuklia na ikajengwa na kampuni ya China. Hivi karuibuni Afrika kusini imejenga nyuklia mpya na ni mitambo itakayokuwa mikubwa kuliko yote duniani.

Pili Tanesco kuna tamaa ya kupewa kitu kidogo na makampuni ya nje ili kubeba techolojia ya aina hii ambayo kwa tender kama hiyo, lazima itajengwa na makampuni ya nje.

Bila kujali 2050 nani atakuwa hai, Munachokifanya ni wizi mtupu na hasara kwa kizazi kijacho. Kama mna ubavu jengeni mitambo ya nyuklia.

Very stupid arguments!
 
Labda kama unaulewa wa Masuala ya umeme...

Otherwise naweza nikaongea na wewe kilayman...

Charger ya Simu na battery which one is costly than the other one?


Solar is DC in nature, production ya volt 1 ya DC ni ghali kuliko production ya 1V AC, so technically we gharama haziwezi kuwa sawa kamwe
Haihitaji kuwa mtaalam wa umeme kujua haya unayojigamba nayo hapa mkuu.

Tatizo la watu wa Tanzania ni kwamba, ukiwa na ujuaji kiduchu juu ya jambo fulani, hapo unajiona wewe umemaliza kila kitu katika eneo hilo, huku hata kueleza unachojua watu wakielewe huwezi. Sasa huko ni kujua kweli?

Unaponiwekea mfano wa "charger ya simu na battery" kuonyesha kuwa unajua tofauti ya umeme unaozalishwa kwa jua na 'thermal' inaonyesha kwamba hujui kitu chochote katika maswala haya.
Tena wewe unadhani kuwa tu DC au AC ndio inayotofautisha sana njia hizi mbili za kufua umeme na gharama yake, hapo inakufanya kuwa na elimu ya kuungaunga katika eneo hilo.

Mimi sina utaalamu katika mambo ya umeme, lakini elimu ya sekondary katika physics iliniwezesha kabisa kujua tofauti ya DC na AC na kwamba kugeuza DC kuwa AC sio swala la gharama kubwa kiasi cha kutaka watu waamini kuwa umeme unaozalishwa kutokana na mafuta ni bei nafuu kuliko ule wa Solar.

Kama kweli unayo elimu katika eneo hili, basi utakuwa na tatizo kubwa la kueleza unachokijua watu wakuelewe. Utaalam wa aina hii ndio unaoliangamiza taifa hili.
 
Bora solar energy tu,Tanesco wenyewe na leo krismas lakini umeme hakuna
 
Namsikitiaga sana mbogo anayeongelea mazingira wakati hana uhakika wa kula yake ya siku/wiki.
Mazingira yanafaida gani kama watu wetu wanakufa na njaa au hawana uhakika wa kula. Serikali ituhakikishie kula kwanza kwa kuwekeza kwenye vyanzo rahisi zaidi ili excess itumike kuendeleza miundombinu mingine ya nchi na kusaidia wananchi wake
Unaangalia mbele ya pua yako, unadhani umeona dunia nzima?
 
Back
Top Bottom