TANESCO achana na Solar Energy, ni wizi na hasara kwa Taifa

TANESCO achana na Solar Energy, ni wizi na hasara kwa Taifa

Katika umeme ambao siupendi ni wa SOLAR ,gharama za kuwekeza kubwa halafu mwanga hafifu hauna uhakika wa kulast 24hrs.......Ni wizi bora wainvest kwenye Nuclear Reactor.
Kwa wataalamu wanaweza kukutengenezea mfumo wa kuwa na umeme huo hata zaidi ya siku saba bila kutegemea jua. Kikubwa ni mfuko wako wa kutunisha sehemu ya kuhifadhi umeme huo ( batteries) na chanzo cha kuzalisha umeme huo( Solar PV modules). Pia si kweli kuwa umeme huu unazalisha nguvu ya mwanga hafifu. Mwanga wa taa ndani ya chumba inategemea chanzo cha mwanga huo( bulb) kina kani ( lumens) ya kiasi gani kutosha kujaza mwanga unaotakiwa chumbani humo. Kwa hiyo si kweli kuwa huu umeme wa jua hauwezi kuzalisha umeme kwa uhakika.
 
Kwa wataalamu wanaweza kukutengenezea mfumo wa kuwa na umeme huo hata zaidi ya siku saba bila kutegemea jua. Kikubwa ni mfuko wako wa kutunisha sehemu ya kuhifadhi umeme huo ( batteries) na chanzo cha kuzalisha umeme huo( Solar PV modules). Kwa hiyo si kweli kuwa huu umeme wa jua hauwezi kuzalisha umeme kwa uhakika.

Sasa Gharama ya hiyo investiment si bora niongee na tanesco waniletee nguzo hadi kwangu hata kama ni 50 na transfomer juu....Maana hiyo investiment yake zaidi ya 10m.
 
Kwa taarifa yako tu ni kuwa kadri siku zinavyoongezeka kupungua kwa gharama za vifaa vinavyotumika kuzalisha umeme jua inazidi kupungua siku hadi siku kutokana na uboreshaji wa teknolojia. Mfano, miaka ya tisini solar panel bei yake ilikuwa karibu shilingi TZS 10,000/ Wp lakini kwa sasa inakaribia shilingi TZS 1,300/Wp. Na inazidi kushuka. Hii hali inaenda hata kwa vifaa kama batteries, charge controller, inverters, nakadhalika.

Kwa msingi huo, ni makosa kupiga kampeni dhidi ya matumizi ya umeme wa solar kwa sababu ya eti gharama kubwa za umeme huo wakati trends zinaonyesha bei ya umeme huo inashuka kadri siku zinavyosonga.
Mzee Baba let talk in technical point of view

Kweli Jua ndio chanzo Kikuu cha Nishati zote Kwenye Solar System Inatengeneza nishati yake kwa Njia ya Nuclear Fusion (Hydrogen inavunjwa Kuwa Helium) Hii process imefanikiwa na binadamu kwa mara ya Kwanza miaka ya 50 na Kuunda Hydrogen bomb...

Lets go back to how solar panel generate Energy.. Solar panel zinafanya kazi kwa njia inayoitwa photon emission kutokana na Solar light kutokuwa monochromatic, ina radiation zenye wavelengths tofauti hadi leo hakuna solar panel inayoweza kukusanya all energy from sun.

Hiyo process ya kutengeneza hizo panel za ni ghali sana kiasi kwamba itakuwa ghali kuunda solar panel inayoweza kuzalisha hata volt 200 kuliko kuzalisha Generator la volt 400 hii inapelekea Solar Energy kuwa na unit price kubwa sana.

Ukiacha Hivyo DC haibadiliki per second hivyo basi ukisafirisha volt nyingi umbali mrefu itakuwa hatari na itahitaji kubadili waya zinasafirisha kila wiki kama sio kila siku... In short umeme wa solar Africa ni kuchajia simu na kuwashia taa usiku
 
Sasa Gharama ya hiyo investiment si bora niongee na tanesco waniletee nguzo hadi kwangu hata kama ni 50 na transfomer juu....Maana hiyo investiment yake zaidi ya 10m.
Lakini operating cost ni ndogo zaidi ya theluthi mbili ya hiyo Tanesco! Na hapa unasahau mambo ya kuwa umeme utakatika ghafla muda wowote.
 
Lakini operating cost ni ndogo zaidi ya theluthi mbili ya hiyo Tanesco! Na hapa unasahau mambo ya kuwa umeme utakatika ghafla muda wowote.

Ok umeme wa solar yenye uhakika ni kwa matajiri tu ila wa sie pangu pakavu tia mchuzi tunaonunua solar za kuwasha taa nne na kuchaji simu tunateseka sana!! Umeme utafiriki wa balb ya baiskeli unaozalishwa na Dynamo.
 
Ni kweli gharama za kuzalisha umeme wa jua ziko juu kidogo kulinganisha na umeme huo wa AC.

Lakini kwa taarifa yako kusafirisha umeme wa DC ni bei ndogo zaidi kuliko kusafirisha AC. Na hapa ndipo panatia hasara maana loss njiani ni kubwa kwa AC. Suala la gharama za umeme si uzalishaji tu hata usambazaji. Pia gharama za uendeshaji za umeme wa solar ni ndogo kuliko za huo umeme unaopigia kampeni ya kufa na kupona!
Kusafirisha DC ni rahisi Kuliko AC, Bro are you serious?

How can you transmit constant (0 frequency) electricity kwenye Nguzo ya KM 20??
 
Lakini operating cost ni ndogo zaidi ya theluthi mbili ya hiyo Tanesco! Na hapa unasahau mambo ya kuwa umeme utakatika ghafla muda wowote.

Ok umeme wa solar yenye uhakika ni kwa matajiri tu ila wa sie pangu pakavu tia mchuzi tunaonunua solar za kuwasha taa nne na kuchaji simu tunateseka sana!! Umeme utafiriki wa balb ya baiskeli unaozalishwa na Dynamo.
 
Ni kweli gharama za kuzalisha umeme wa jua ziko juu kidogo kulinganisha na umeme huo wa AC.

Lakini kwa taarifa yako kusafirisha umeme wa DC ni bei ndogo zaidi kuliko kusafirisha AC. Na hapa ndipo panatia hasara maana loss njiani ni kubwa kwa AC. Suala la gharama za umeme si uzalishaji tu hata usambazaji. Pia gharama za uendeshaji za umeme wa solar ni ndogo kuliko za huo umeme unaopigia kampeni ya kufa na kupona!
Kusafirisha DC ni rahisi Kuliko AC, Bro are you serious?

How can you transmit constant (0 frequency) electricity kwenye Nguzo ya KM 20??
 
nionavyo mimi ni kwamba Tanesco kwanza wamechelewa sana kuingia kwenye renewable energy hili ni suala lililotakiwa kufanyika walau miaka 10 iliyopita, mataifa makubwa kama vile Marekani na China yalishaanzisha michakato kama hii siku nyingi sana sio vibaya na sisi tukianza na hali yetu hii hii ya kiuchumi, jambo ni zuri shida ni management ndani ya Tanesco
 
Ok umeme wa solar yenye uhakika ni kwa matajiri tu ila wa sie pangu pakavu tia mchuzi tunaonunua solar za kuwasha taa nne na kuchaji simu tunateseka sana!! Umeme utafiriki wa balb ya baiskeli unaozalishwa na Dynamo.
Mkuu, sijui upo tayari kujibu maswali yangu haya?

Mkuu, unatumia system ya Watts ngapi( PV module), taa nne za watt ngapi ?
Je. Taa nne zote umezifunga kwenye chumba kimoja ama kila taa ipo kwenye chumba chake? Naweza kujua ukubwa wa chumba zilimo/ ilipo taa yaani upana, urefu na kimo!? Je. Mtambo/ system yako hiyo ipo maeneo gani/ mkoa gani Tanzania!? Je. Panel hiyo/ hizo umezifunga katika uelekeo upi/ orientation ( pembe ya kuinama na uso wa panel umeangalia upande upi yaani upande wa kaskazini, kusini , magharibi, ama mashariki)

Kwa ufafanuzi zaidi, ninaomba maelezo ya vifaa vyote vinavyounda mfumo/ mtambo/ system yako hiyo ya solar.

Nina uhakika ukinipa majibu ya maswali haya kwa ufasaha, wataalamu wetu wa mifumo hii watatupa sababu kwa nini mfumo wako huo haukidhi kiu ya mahitaji yako ya mwanga hapo nyumbani/ofisini.
 
Ukiacha Hivyo DC haibadiliki per second hivyo basi ukisafirisha volt nyingi umbali mrefu itakuwa hatari na itahitaji kubadili waya zinasafirisha kila wiki kama sio kila siku... In short umeme wa solar Africa ni kuchajia simu na kuwashia taa usiku
Kuna usafirishaji wa umeme wa DC kati ya Msumbiji na Afrika ya Kusini. Taarifa zilizopo ni kuwa hakuna ubadilishaji wa nyaya kila wiki kwa sababu tu kuwa umeme unaosafirishwa ni wa DC.
 
Lakini operating cost ni ndogo zaidi ya theluthi mbili ya hiyo Tanesco! Na hapa unasahau mambo ya kuwa umeme utakatika ghafla muda wowote.
Huo umeme wa solar unawashia nini na nini tuanzie hapa
Kuna usafirishaji wa umeme wa DC kati ya Msumbiji na Afrika ya Kusini. Taarifa zilizopo ni kuwa hakuna ubadilishaji wa nyaya kila wiki kwa sababu tu kuwa umeme unaosafirishwa ni wa DC.
Share picha ya Njia zake ulinganishe na power cables za AC tunazotumia
 
Kusafirisha DC ni rahisi Kuliko AC, Bro are you serious?

How can you transmit constant (0 frequency) electricity kwenye Nguzo ya KM 20??
Sipo JF kusema uongo, nipo hapa kujifunza. Ni kupitia changamoto zenu mnazonipa najibidisha kujielimisha kadri nanvyoweza. Kuhusu swali lako, naomba upitie maelezo yote ya mwana blog wa mambo ya umeme hapa chini. Link imeambatanishwa.
===
 
Kuna usafirishaji wa umeme wa DC kati ya Msumbiji na Afrika ya Kusini. Taarifa zilizopo ni kuwa hakuna ubadilishaji wa nyaya kila wiki kwa sababu tu kuwa umeme unaosafirishwa ni wa DC.
AC reactive losses become great for really long distances and are also the practical solution to differing frequencies.

DC to DC converter are very expensive also huwezi ukatumia transformer kwenye DC current so transmitting AC kwenye long distance ni very practical
 
Sipo JF kusema uongo, nipo hapa kujifunza. Ni kupitia changamoto zenu mnazonipa najibidisha kujielimisha kadri nanvyoweza. Kuhusu swali lako, naomba upitie maelezo yote ya mwana blog wa mambo ya umeme hapa chini. Link imeambatanishwa.
===
Sasa ndio uwaambie watu HVDC cost ni kiasi gani.. na Kuwa Power towers za AC ni kiasi gani...
 
Sipo JF kusema uongo, nipo hapa kujifunza. Ni kupitia changamoto zenu mnazonipa najibidisha kujielimisha kadri nanvyoweza. Kuhusu swali lako, naomba upitie maelezo yote ya mwana blog wa mambo ya umeme hapa chini. Link imeambatanishwa.
===
First, the AC power must be converted to DC to begin the transmission process, and then when it gets to the desired tie-in destination, the DC power must be converted back to AC to be utilized on the grid. (Ni menukuu)

So Practically why we need to expensive converter wakati we can transmit AC direct na katikati tukawa na vituo vya kupoza umeme
fig-3_hvdc-converter-hall_siemens.jpg

Kwenye Blog uliyoshare hiki ni kituo cha kubadili AC/DC sasa tuwaache wachangiaji walinganishe Investment kama kwa ajili kupata 1,000 MW na ile ya Hydropower ya kupata 2500 MW ya Bwawa la Mwalimu Nyerere, ipi ina high return of Investment na economical
 
First, the AC power must be converted to DC to begin the transmission process, and then when it gets to the desired tie-in destination, the DC power must be converted back to AC to be utilized on the grid. (Ni menukuu)
Mkuu, Solar PV arries si zinazalisha DC? Hizo converters tutaziweka huko mwishoni, maana hatuna haja ya kubadili AC ambayo hatuzalishi kwenye solar pv modules!! Kumbuka mada iliyopo mezani ni Solar Energy.
 
Wengi tukisikia solar energy tunajawa na hisia kwamba ni jambo la maana sana! Ni umeme mzuri kwa mwanakijiji anayetaka mwanga wa kufukuza wanyama watembeao gizani tu! Kwani nchi zetu hizi maskini hatuhitaji miradi mikubwa kiasi hicho kinacholengwa na Tanesco.

Ni uharibifu wa pesa kwa kujidai kuingia kwenye renewable energy. Ni biashara ya makampuni ya kigeni kujipenyeza ndani ya TANESCO, nao wanaandika eti by 2050 Tanzania itatumia renewable energy, wakimaanisha wind na solar. Huu naweza kuita ni upuuzi.

Solar na wind bado ni luxurious energy sources ambazo tunawaachia nchi zilizoendelea kufanya majaribio. Ni aibu kwa shirika kama Tanesco kujiingiza kwenye miradi ya gharama kubwa kiasi hicho. Maneno kama renewable energy na alternative energy ni kujiridhisha tu na kuwazubaisha wanasiasa na kunufaisha makampuni ya nje ambayo yanatuuzia hizo pannels.

Katika East Africa walianza Uganda. Kwa mikogo wakatangaza kuwa na solar farm, ukweli ni kwamba hilo ni shimo la fedha. Wangeweza kupata umeme mwingi kutoka Nile kuliko hizo pannels. Sasa wameingia Tanesco nao kwa mikogo wanatangaza tender ya kufunga mitambo ya solar. Spain Andalusia inajigamba kuwa na solar farm ya kisasa kabisa na technolojia za kisasa lakini bado ni umwamba tu, wana umeme mwingi kwa njia za nuklia na mafuta.

Je, kwa nini Tanesco inajiingiza kwenye solar? Jibu ni rahisi: Kwanza hawaijui kiuhakika kiasi hicho zaidi ya kusimuliwa na makampuni yanayouza pannel na kutoa mifano ya nchi jirani na ulaya ambako hakuna nchi hata moja ilnayotegemea solar. Mfano mzuri ni ujerumani ambako Angela Merkel aliahidi kuondoa mitambo yote ya nuklia ili kuweka renewable kama hizi wanazokimbilia Tanesco. Tangu 2005 hadi leo hajafika kokote! Kumbuka huyu ni mfizikia, syansi anaijua sana. UK wao waliongeza nuklia na ikajengwa na kampuni ya China. Hivi karuibuni Afrika kusini imejenga nyuklia mpya na ni mitambo itakayokuwa mikubwa kuliko yote duniani.

Pili Tanesco kuna tamaa ya kupewa kitu kidogo na makampuni ya nje ili kubeba techolojia ya aina hii ambayo kwa tender kama hiyo, lazima itajengwa na makampuni ya nje.

Bila kujali 2050 nani atakuwa hai, Munachokifanya ni wizi mtupu na hasara kwa kizazi kijacho. Kama mna ubavu jengeni mitambo ya nyuklia.
Dah...mkuu ….wanaotaka kutumia umeme jua wengi wao hawaangalii gharama kama ilivyo...bali wanalinganisha gharama za umeme dhidi ya uharibifu wa mazingira…..hata tafiti nyingi zimefanywa kuhusiana na umeme wa jua...juu ya kuwepo wa mashamba makubwa ya umeme jua au kuwepo wa umeme jua kwa kila mtu kwake.. ...matokeo yako wazi kabisa kwamba..mashamba makubwa ya umeme jua ni gharama sana...karibu mara 4 kama ukiongeza na gharama za kusafirisha nishati hiyo kwenda kwenye matumizi ukilinganisha kama kila mtu atakuwa na panel yake nyumbani….. Hivyo ni bora waktafuta namna ya kuweka ruzuku kwenye vifaa vya umeme jua ili watu waweze kuutumia kwa wingi...tuweke uzalendo mbele ...10% iwe nyuma 🤭
Tanesco 10% zisiwatoe uzalendo
 
Back
Top Bottom