MtazamoWangu
JF-Expert Member
- Apr 25, 2009
- 313
- 7
Other members of the TANESCO board of directors are Victor Mwambalaswa, Agnes Bukuku, Juma Bakari, Vintan Mbiro, Semindu Pawa, Beatus Segeja, and Ngosi Mwihava.
Hivi hawa wote kuna hata mmoja mwenye ABC za mambo ya umeme?
mkataba kati ya tanesco na richmond ulikuwa June 23, 2006.Hasara ya mwaka 2006 haiwezi kuwa inahusiana na mkataba wa Richmond ila inaweza kuwa imeongezeka kutokana na mgawo wa mwaka 2006. Mkataba ulivunjwa mwaka 2007 mwezi Oktoba na hivyo lazima kuangalia hesabu za miaka 2007 na 2007 ili kuweza kujua madhara ya mkataba ule. Mkataba ule umeletaje hasara kwenye shirika? Ninaamini hasara imepungua kutokana na uongozi mpya wa TANESCO kuongeza juhudi za kukusanya madeni na kusafisha vitabu kwa kuondokana na matumizi yasiyofaa na ndio kilichofanyika.
sawa rashid hausiki lakini keep in mind kwamba ametoka vodacom akaenda tanescoDr. Rashidi hahusiki na Richmond maana yeye amekuta mkataba tayari umesianiwa na chini ya uongozi wake ndio walivunja mkataba na Dowans baada ya TANESCO kupata ushauri wa kitaalamu kutoka REX attorneys. Kwa hiyo si sahihi kusema Rashidi anahusika na Richmond maana hahusiki kwa njia yeyote ile.
kutokana na maneno yako(zitto) mtu ambaye amepewa mkopo wa bil 400 anataka kununua mitambo ambayo wewe mwenyewe ulisema itaifishwe kwa ajili ni mali yetu. na wewe unamuita huyu mtu the best ceo. the best ceo anataka kununua mali yake mwenyewe. unadhani watu wangekataa kama angeenda kununua GE mipya.Suala la Dowans limejadiliwa sana na kifupi ni kuwa Rashidi alitaka mitambo ile ili kuongeza uwezo wa TANESCO kuzalisha umeme wake mwenyewe badala ya kununua kutoka kwa wazalishaji kwani hali aliyokuta TANESCO ni ile ambayo nimewahi kuieleza hapa kuwa TANESCO walikuwa wanalipa asilmia 84 ya mapato yao kwa wazalishaji binafsi wa umeme ambao walikuwa wanazalisha asilimia takribani 45 tu ya umeme wote ambao TANESCO walikuwa wanauza kwa wananchi.
mwanzoni mwa mwaka jana tanesco imepandisha bei kwa 23% na ilikuwa inataka 40%. connection charges zimepanda kwa 100%.mjadala unakuwa mtamu kama tutajikita kwenye facts badala ya maneno ya mtaani na kisha kuyaweka kama facts.
Lukule,
kusema nimekuwa shallow ni kunionea tu. Labda useme ninajengea hoja taarifa ambazo sio sahihi nk. Ripoti za fedha ninazo semea hapa ni ripot zenye nyaraka zote kabisa na zilizochambuliwa na wataalamu. Wakaguzi wa TANESCO ni PwC, ambalo ni shirika lenye heshima kubwa katika kazi ya ukaguzi. Kama wao walikuwa shallow na baadaye CAG naye akawa shallow katika ripoti yake basi nitakubaliana nawe.
Mimi kwa taarifa nilizo pata toka wakati ule alipokuwa BOT ni i.e Governor alikuwa ni Mtu Competent sema miaka ya Mwanzo, lakini wana siasa walimuharibu na yeye akakubali kuharibiwa, kwa sasa namuona hafai hata, labda tusema kwamba wana siasa wana muhitaji kwa shughuli zao za kifisadi.
Sasa tukiachana na Historia yake huko nyuma, tuangalie utendaji wake wa hapo Umeme ambao upo wazi, kama yeye angekuwa mtu makini, tusinge ingia mkataba wa Richmond, na kama alilazimishwa, basi asinge kuja kutetea ununuzi wa Dowans na matawi yake, jingine tusinge ingia kwenye mgao wa sasa, jingine ni matumizi mabaya ya fedha tena za mkopo kwenye shughuli ambazo si za uzalishaji au zilizotarajiwa kuwezeshwa kutokana na huo mkopo.
Kwa binadamu au kitu chochote kuna vitu vinavyo onekana na vilivyo fichika, na hivyo ni vashiria vya mtu kuwa mzuri au mbaya, sasa kwa kuangalia hivyo viashiria vinavyo onekana na visivyo onekana kiutendaji utaona Idrisssa hafai amekosa kuwa mtu wa msimamo na ameunga mkono/ na kutekeleza vitu vinavyo dumaza uchumi.
Mbona alimkatalia Mwenyekiti wa Bodi Gari, sasa alishindwa nini kuzui matumizi mabaya ya fedha za Mkopo, Yeye ni mwanauchumi, ana uwezo mkubwa wa kumshauri EL, na JK je aliwashauri nini kuhusu maafa ya mikataba ya Richmond nk.
Ni nani aliyesema kama si wewe mwenyewe?
Haya kaka, unataka asubuhi niamke niangalie upepo unaelekea wapi ndio na mimi nielekee? Tatizo langu wakati mwingine napenda kuwa devils advocate ili watu wafikiri beyond myths that motivate our orientation in looking into things and make opinion. Najua u devils advocate una nicost haswa. Hata hivyo jamii lazima iwe na watu wanaofikiri tofauti kidogo ili mijadala iwepo. Ikifika siku watu wote tukafikiri sawa itakuwa hatari sana.
Ushauri taken kaka
Aliyeandika hayo ni huyu hapo "JF Great thinker" Acha kukurupuka usiwe kama sio mjinga!
na hili ndio tatizo kubwa..tokea mwanzo wakati IR anateuliwa watu wengi walilalamikia uzoefu wake katika masuala ya umeme....walikuwepo watu wenye uwezo hata ndani ya Tanesco ambao walikuwa na uwezo wa kuendesha kampuni....wafanye kama basi TTCL,management ni wafanyakazi wanaojua kampuni nje/ndani....
Other members of the TANESCO board of directors are Victor Mwambalaswa, Agnes Bukuku, Juma Bakari, Vintan Mbiro, Semindu Pawa, Beatus Segeja, and Ngosi Mwihava.
Hivi hawa wote kuna hata mmoja mwenye ABC za mambo ya umeme?
This is classic! watu wanataka uwe kama wao, wanasoma michango ya mwanzo wakiona trend ni kukandika na wao wana bandwagon, ndio JF style ukifanya tofauti wewe fisadi, umetumwa, CCM nk
Sawa Mkubwa, sasa Huyo Dr kapewa hesabu za darasa la pili 1 =1 kashindwa, sembuse za secondary nk. in the context kwamba kapewa mkopo wa kuongeza tija kwa shirika yeye kaenda kukarabati majengo , sasa huyo utamwita CEO anayefaa.Aliyeandika hayo ni huyu hapo "JF Great thinker" Acha kukurupuka usiwe kama sio mjinga!
.......... ninasafiri kwenda Trinidad kwenye Commonwealth. So najua kutakuwa na maswali kibao nitajibu nikifika huko....
Zitto,
Nakukubali sana pale unapolitetea kwa nguvu zako zote jambo ambalo unaliamini kuwa its right, nakushauri sometimes upime utetezi wako kwa public opinion trend usijefika mahali ukaonekana " An Enemy of The People"
Kwenye hili la Tanesco, mimi binafsi nilikuelewa siku nyingi, haswa kwa kuzingatia wewe ni Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma, tangu lile la mitambo ya Dowans, sasa watu wamefurahi tunameza dozi chungu zaidi ya IPTL, itatuumiza zaidi, lakini imefurahisha watu.
Yes sibishi kuhusu track record yake kwenye utendaji, ila watu bado wanaunganisha na kuchafuka kwa jina lake kwenye hayo mengineyo kiasi kwamba kumtetea nkutaonekana kama kumsafisha.
Ndivyo wanavyoonekana watetezi wa Mkapa ama Lowassa, pamoja na madudu yao, walikuwa na mazuri yao ambayo yanastahili pongezi sio kubezwa, na ukiwapongeza kwa mazuri, unageuka adui, ndiyo hali ya Dr. Rashid hapa.
Sisimizi kwanza nashukuru kwa mchango wako, na kama utaweza kurejea kwenye moja ya post zangu kuhusu huyu Dr, ni kwamba on the Face value ni mzuri, ninasema hivyo kutokana na kwanza na elimu yake, na pia hatua alizochukua huko nyuma alipoingia NBC, za kuwauliza wazee wazamani kuhusu wepesi wa file zao, kutokana na hilo namfagilia, lakini tukija kwenye matokeo ya kazi zake, EG Bot U-governor zaidi ya kusisitiza watu wawe na qualification naomba utupe nyama kuonyesha aliweza kufanya hiki , na kile alizui wizi, aliinvest vizuri mali zetu nk nk., lakini navyo kumbuka BOT kulikuwa na ile Kashfa ya DCP na mambo ya akina Chavda/Jetu Patel etc, zaidi ya Hapo kulikuwa na Mkataba wa IPTL, sasa hapa namuingiza Governor wa BOT kwa sababu Mikataba mikubwa ambayo inahusisha utoaji wa Pesa nje lazima iruhusiwe na Governor, na hata hii fedha ya Jersey , uwezekano mkubwa imetokana na IPTL na sio ya Radar, sasa alivyo toka BOT bila kuongezewa tuache hivyo hivyo, ndipo akaenda AKIBA commercial Bank, kama MD , lakini hakuka muda mrefu ndipo akaenda VODAcom, sasa mafanikio ya AKIBA Commercial Bank inawezekana yametokana na mambo mengi kwanza effectiveness ya board, pili ya management, na tatu kuwa ni mali ya watu binafsi sio cha Umma ukimaanisha kumilikiwa na serikali.Dr Rashid ninayemfahamu
Kwa bahati nzuri nimeshiriki katika kazi maalum ya pale TANESCO wakati wa kipindi cha NET Group na baada kuingia kwa Dr Rashid pia. Watanzania tuache uchafuzi wa CVs za watu pasipo kuwa na uhakika. Kuna mabadiliko makubwa sana ambayo Rashid ameyafanya ndani ya TANESCO, ambayo ni mazuri na makubwa. Rashid alikabidhiwa mkoba wa lile shirika ukiwa na pumzi inayokaribia kufa. Jambo la kwanza la kuangalia, tazama hati za ukaguzi wa mahesabu za sasa zinazofanywa na kampuni moja ya kimataifa, (Audited financial statements) ambayo imekuwa ikikagua kampuni hiyo tangu wakati wa NETI Group. Utaona kuna mabadiliko makubwa sana. Kutoka Adverse opinions/Disclaimer opinions hadi sasa utaona atleast Qualified opinions. Ukweli ni kwamba Dr Rashid ni kati ya ma CEO makini na wazuri katika nchi hii. Ndiyo, upende usipende, pamoja na kelele nyingi na mapungufu yanayoweza kujitokeza, bado Dr Rashid ni CEO makini. Kwa wanao ongea kwa kutazama maandishi ya kwenye magazeti tu, hawawezi kuelewa!.
Siasa zinapokuwa zimeingia katika professionalism ndipo tunaona kupakwa kwa kinyesi kwa Dr Rashid. Tatizo letu wa TZ mambo ambayo yanahitaji wataalamu tunayawekea kimbelembele cha siasa, hata pasipohitajika!. Tangu tuhuma za Rashid zianze siyo leo, lakini kila siku ni tuhuma tuhuma tuhuma tu!. Hata wasiokuwa na data, ni tuhuma tu.
Jambo la pili, tazama hata maendeleo ya baadhi ya makampuni ambayo Dr Rashid anayasimamia kama Mwenyekiti wa Bodi, kwa mfano benki ya Akiba, tazama miaka miwili ambayo huyu mzee wetu Rashid ameingia kwenye board na kupewa uenyekeiti wa bodi, amefanya mabadiliko makubwa na tunaona benki hii ni kati ya benki ambazo zinakua na kufanya mabadiliko makubwa katika technolojia na utendaji pia, hapa nchini.
Tatizo letu wa TZ tunachonga sana hata pasipokuwa na data za kutosha kuendeleza mchongo!! Utakuta mwandishi wa habari au M- TZ mwenzangu, yeye pekee ni prosecutor, yeye huyo ni Forensic expert, yeye ni Auditor, yeye ni Engineer, yeye Mhasibu nk, huu ni mtazamo hasi. Lazima tufike mahali tuwe tunachonga kwa data, pale panapohitajika, si kuchonga tu!. Tunawasaidia wafanyabiashara kuuza magazeti bure!!. hali wengine wakisubiri pesa za wananchi zitumike kuwanyamazisha kuendeleza uandishi wa habari usiokuwa na tija na uliojaa udaku udaku tu!. Magazeti mengi yanajifanya yanaandika habari za uchunguzi, lakini ukisoma utaona ni UDAKU TU!. Soma hata habari hii ya Thisday, hapo juu; kwa umakini, utaona hakuna investigative journalism inayoonekana katika makala hiyo, zaidi ya kujaa udaku udaku tu!; See this "According to these sources, the TANESCO board of directors chaired by Peter Ngumbulu has already formally recommended the re-appointment of Rashidi - but under controversial circumstances............Ngumbulu was yesterday not available for comment on the implication of a split amongst TANESCO board members (directors) over the Rashidi issue, while acting board chairman Adolar Mapunda flatly declined to comment". Sasa kama hawa Thisday walikuwa wamemkosa Ngumbulu, walikuwa na haraka gani ya kuileta hii habari gazetini, kabla ya kupata uhakika wa taarifa hizi. Hata habari yenyewe haielezi, what are the contravential circumncistances.... Huu ni ubabaishaji katika uandishi wa habari. Hebu angalia, Sources za habari hawajatueleza, hata hizo contravential circumncistances hawajaeleza. Maana yake ni kwamba, sources na taarifa zenyewe wanazotaka kutuhabarisha hawazijui. Isipokuwa wanataka kuuza gazeti tu!
Ninachokiona na ambacho waandishi wengi wa habari wanakosa, ni "Report Writing Skills". Pia ninadhani, wahariri wengi, hawana uwezo mzuri wa kukaachini na kuhariri habari vyema. Pia waandishi wa habari waelewe kwamba kuwa mwandishi mzuri wa habari kunahitaji kuwa na skills zaidi ya taaluma ya uandishi wa habari. Wajitahidi waongeze taaluma, mbalimbali ambazo zitawafanya wawe wanaelewa namna shughuli zinavyofanywa katika makampuni na mashirika. Si ajabu kumkuta mwandishi wa habari aliye andika habari hii katika Thisday, hajui hata Corporate Governance, hajui hata namna masuala mbalimbali yanavyosimamiwa na kutekelezwa katika mashirika na makampuni. Yeye alivyoambiwa Ngumbulu hayupo, basi, akaona ndiyo mwisho wa fikira! Akakimbia kwenda kwenye mtambo kupeleka habari eti Habari hizi nilizoziandika ngumbulu hakupatikana kuthibitisha!!. Hata asijue kwamba suala kama hili ni sensitive, linalohitaji umakini katika kulitolea taarifa kwa maslahi ya taifa. Tatizo wanatoa taarifa kama WANAVYOPEANA TAARIFA ZA MISIBA!!.
Nadhani Thisday nao wamepoteza mwelekeo!! They are more of Majungu, kuliko investigative journalism wanayoiimba kila kukicha!
"For actions speaks louder than words, let us embrace actions more than words!!!!!"
Other members of the TANESCO board of directors are Victor Mwambalaswa, Agnes Bukuku, Juma Bakari, Vintan Mbiro, Semindu Pawa, Beatus Segeja, and Ngosi Mwihava.
Hivi hawa wote kuna hata mmoja mwenye ABC za mambo ya umeme?
Pre-emptive strategy...........!
Umpende usimpende Rashidi, ni one of the best CEOs of our Parastatals.
Siasa...........! tungeacha mashirika yakawa na bodi huru na kuziwekea malengo na kuzipima kutokana na malengo mashirika haya yangeenda vizuri sana. Siasa zinaingia sana na huyu Rashidi ni mmoja wa CEOs anayewakatalia wanasiasa waziwazi. Wanamchukia sana. Mfano kawaambia Wizara walipe pango la jengo la TANESCO, wizara eti hawataki..... CCM nao wameng'ang'ania Rest House ya TANESCO dodoma, amewatimua. Wamekasirika. Basi ni matatizo tu..... Sasa kwenye kampeni wanataka waweke CEO goigoi awape pesa maana Rashidi hatakubali na wao wameshazoea.....
Other members of the TANESCO board of directors are Victor Mwambalaswa, Agnes Bukuku, Juma Bakari, Vintan Mbiro, Semindu Pawa, Beatus Segeja, and Ngosi Mwihava.
Hivi hawa wote kuna hata mmoja mwenye ABC za mambo ya umeme?
Kaka analysis nzuri sana.
However, is it of the national interest to let the dictatorship of the demagogues to win the day?
Unawajua wanasiasa wetu, unajua sekta yetu ya habari na pia unawajua wazee wa data wetu iwe hapa JF ama kwengineko. Unadhani wana uwezo(capacity), haiba (caliber) ama mamlaka ya kimaadili (moral authority) kuachwa kuwa waamuzi wa mawazo ya wananchi na hata kutaka kutuamulia hatma ya nchi yetu?
omarilyas
Tatizo letu wa TZ tunachonga sana hata pasipokuwa na data za kutosha kuendeleza mchongo!! Utakuta mwandishi wa habari au M- TZ mwenzangu, yeye pekee ni prosecutor, yeye huyo ni Forensic expert, yeye ni Auditor, yeye ni Engineer, yeye Mhasibu nk, huu ni mtazamo hasi. Lazima tufike mahali tuwe tunachonga kwa data, pale panapohitajika, si kuchonga tu!. Tunawasaidia wafanyabiashara kuuza magazeti bure!!. hali wengine wakisubiri pesa za wananchi zitumike kuwanyamazisha kuendeleza uandishi wa habari usiokuwa na tija na uliojaa udaku udaku tu!. Magazeti mengi yanajifanya yanaandika habari za uchunguzi, lakini ukisoma utaona ni UDAKU TU!. Soma hata habari hii ya Thisday, hapo juu; kwa umakini, utaona hakuna investigative journalism inayoonekana katika makala hiyo, zaidi ya kujaa udaku udaku tu!; See this "According to these sources, the TANESCO board of directors chaired by Peter Ngumbulu has already formally recommended the re-appointment of Rashidi - but under controversial circumstances............Ngumbulu was yesterday not available for comment on the implication of a split amongst TANESCO board members (directors) over the Rashidi issue, while acting board chairman Adolar Mapunda flatly declined to comment". Sasa kama hawa Thisday walikuwa wamemkosa Ngumbulu, walikuwa na haraka gani ya kuileta hii habari gazetini, kabla ya kupata uhakika wa taarifa hizi. Hata habari yenyewe haielezi, what are the contravential circumncistances.... Huu ni ubabaishaji katika uandishi wa habari. Hebu angalia, Sources za habari hawajatueleza, hata hizo contravential circumncistances hawajaeleza. Maana yake ni kwamba, sources na taarifa zenyewe wanazotaka kutuhabarisha hawazijui. Isipokuwa wanataka kuuza gazeti tu!
Ninachokiona na ambacho waandishi wengi wa habari wanakosa, ni "Report Writing Skills". Pia ninadhani, wahariri wengi, hawana uwezo mzuri wa kukaachini na kuhariri habari vyema. Pia waandishi wa habari waelewe kwamba kuwa mwandishi mzuri wa habari kunahitaji kuwa na skills zaidi ya taaluma ya uandishi wa habari. Wajitahidi waongeze taaluma, mbalimbali ambazo zitawafanya wawe wanaelewa namna shughuli zinavyofanywa katika makampuni na mashirika. Si ajabu kumkuta mwandishi wa habari aliye andika habari hii katika Thisday, hajui hata Corporate Governance, hajui hata namna masuala mbalimbali yanavyosimamiwa na kutekelezwa katika mashirika na makampuni. Yeye alivyoambiwa Ngumbulu hayupo, basi, akaona ndiyo mwisho wa fikira! Akakimbia kwenda kwenye mtambo kupeleka habari eti Habari hizi nilizoziandika ngumbulu hakupatikana kuthibitisha!!. Hata asijue kwamba suala kama hili ni sensitive, linalohitaji umakini katika kulitolea taarifa kwa maslahi ya taifa. Tatizo wanatoa taarifa kama WANAVYOPEANA TAARIFA ZA MISIBA!!.
Nadhani Thisday nao wamepoteza mwelekeo!! They are more of Majungu, kuliko investigative journalism wanayoiimba kila kukicha!
"For actions speaks louder than words, let us embrace actions more than words!!!!!"