TANESCO: Umeme tunaozalisha ni mwingi mahitaji ni madogo nchi nzima, hakuna mgawo kwa sasa

TANESCO: Umeme tunaozalisha ni mwingi mahitaji ni madogo nchi nzima, hakuna mgawo kwa sasa

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
images - 2024-04-23T221841.609.jpeg

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limesema limelazimika kuzima mitambo mitano kwakuwa majitaji ya umeme yapo chini huku uzalishaji wa umeme ukiwa ni mwingi.

TANESCO imesema hayo wakati Afisa wa Shirika hilo akiongea mbele ya Waziri Mkuu kwenye Maonesho ya Wiki ya Nishati yaliyofanyika Viwanja Vya Bunge Jijini Dodoma.

“Mh. Waziri Mkuu kwa sasa hivi tunavyopngea tuna mitambo karibu mitano ipo nje, haifanyi kazi yoyote ni kwamba tu mahitaji yapo chini uzalishaji upo mwingi kwahiyo tumeiweka tu stand by kwa ajili ya kusubiria mahitaji yakiwa juu tunaiwasha, karibia megawats 175, umeme tunaozalisha ni mwingi mahitajii ni madogo Nchi nzima, narudia tuna mitambo mitano minne Kituo cha Kinyerezi I na mmoja Kituo cha Ubungo III, hii mitambo tumeizima kwasababu mahitaji yapo chini na uzalishaji wa umeme ni mwingi imebidi tuizime, kuhusu mgao hamna mgao kwa sasa”

PIA SOMA
- Waziri Mkuu Majaliwa: TANESCO imezalisha umeme zaidi ya mahitaji

- Biteko: TANESCO inanunua umeme wa Megawati 31 kutoka Uganda na Zambia

Millard Ayo
 
Tanga mjini leo umekatika zaidi ya mara 4 kuanzia asubuhi mpaka usiku saa 2 na ni kawaida kila siku kukatika
 
Wangesema hivi, Mh PM,

Demand ya nchi ni...........
Installed capacity ni............
Active units ni sawa na MW..........

Mh PM, kutokana na Active and available units kuwa uwezo wa MW...., zaidi ya demand ya nchi kwa kiasi ....., tumeamua kuzima mtambo A wa ukubwa wa MW..., B, C, D na E ambazo zina juml ya MW...

Majuzi mmesema mnazima mitambo Bwawa, juzi mkasema mnawasha mingine, jana mkasema bwawa linasababisha mafuriko, tutazima..kumaanisha kurudi kwenye mgao, leo mnasema MNAZIADA bila kutupa data kamili, kesho mtasema TANESCO inakabidhiwa Dubai haina ufanisi.
 
Back
Top Bottom