TANESCO wameanza kutuandaa Kisaikolojia. Unakuja Mgao wa Umeme siku zijazo na Watu wanaanza kuingiza Nchini Majenereta

TANESCO wameanza kutuandaa Kisaikolojia. Unakuja Mgao wa Umeme siku zijazo na Watu wanaanza kuingiza Nchini Majenereta

Mtu Asiyejulikana

JF-Expert Member
Joined
Sep 11, 2017
Posts
2,254
Reaction score
5,161
Huu ni mwanzo... Tuanze kujiandaa na yale yajayo siku za usoni. Maji yameanza kupungua tena kwenye mabwawa.

Tulicheleweshwa sana kimaendeleo. Sasa tutaweza kuifungua nchi vizuri na kurudisha uchumi uliokwama.

Screenshot_2022-09-15-13-05-19-777_org.mozilla.firefox~2.jpg
 
Hii nchi siku hizi raia wenye furaha ni mawaziri, wabunge, Rais, na wafanyabiashara wakubwa, raia wengine nje ya hapo tuhamie Burundi.

Nchi imejaa matatizo kila upande ajabu tunaaminishwa tuone tuna serikali, hata sielewi mambo yanavyoenda; pale tozo, huku uraiani panya rodi wanaua, ukienda polisi kuwekwa mahabusu, polisi nao wanakuua...

Ukigeuka upande mwingine kuna mgao ambao haueleweki chanzo chake, kama ni upungufu wa kina cha maji kwenye hayo mabwawa, au ni marekebisho ya kiufundi, wanajua wakisema tatizo ni marekebisho pekee wataulizwa mbona yalishafanyika juzi tu?

Basi ni vurugu tupu, wanatafuta sababu nyingine za kuunganishia, muhimu majenereta yaanze kuuzwa tena, kwangu hata yote yanasababishwa na udhaifu wa kiongozi wa serikali aliyepo madarakani, tunachezewa.
 
Kwa nini hatujatumia vizuri fursa ya gesi tuliyo nayo kuzalisha umeme wa kutosha badala ya kutegemea sana maji?
 
Huu ni mwanzo... Tuanze kujiandaa na yale yajayo siku za usoni. Maji yameanza kupungua tena kwenye mabwawa.

Tulicheleweshwa sana kimaendeleo. Sasa tutaweza kuifungua nchi vizuri na kurudisha uchumi uliokwama.

View attachment 2357800
Waendelee kukaza tu😂😂😂 hamna namna ingine mlishangilia sana Magufuli kufa.
 
Haya maji hayakupungua kwa takribani miaka 6
 
sababu ya kukatika: matengenezo ya mashine

Hivi Ulaya mashine hazifanyiwi maintaenance ??????

Mbona wao hawakati umeme kufanya maintenance ????
 
1.Waliwahi kusema umeme unazalishwa karibia mara 2 ya matumizi yake. Hio ziada kwanini usitumike kipindi hiki kufidia.

2. Haya matengenezo hayaishi? Kila siku marekebisho mpaka mwaka unaenda kuisha?
 
We should all commit suicide that's the only solution to stop this suffering Forever.
 
Gesi wameshachakua mabeberu, alisikika mzaRendo mmoja kutoka Chattle akiwaambia ndugu zake.
Kwa nini hatujatumia vizuri fursa ya gesi tuliyo nayo kuzalisha umeme wa kutosha badala ya kutegemea sana maji?
 
Back
Top Bottom