Pre GE2025 Tanesco yadaiwa kuhujumu Mkutano Mkuu wa CHADEMA. Yakata umeme Lissu akihutubia

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Your browser is not able to display this video.

Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika amesema kuwa Menejimenti ya Ukumbi wa Mlimani City imewaaleza kwamba changamoto hiyo imetokana na TANESCO ambapo umeme unakatwa na kurejeshwa.

Amesema kufuatia changamoto hiyo menejimenti ya ukumbi imewahakikishia itatumia jenereta ili kuepuka changamoto hiyo ambayo imejitokeza zaidi ya mara tatu.

Pia soma ~ Yanayojiri Uchaguzi Mkuu CHADEMA nafasi ya Mwenyekiti & Makamu Mwenyekiti 2025: Ni Mbowe au Lissu?
 
Halafu wanaimba maridhiano.
Hayo ni mapungufu ya serikali kusimamia demokrasia. Juzi na jana station zote ziliangazia mikutano ya CCM. Leo hata TV ya taifa haioneshi mkutano mkuu wa upinzani.
 
ni jambo la kawaida sana kutokea 🐒
 
Hahaha anatumia nguvu nyingi sana, apunguze jazba. Tunamsikia tu.
 
Inadaiwa wanakata umeme na kuwasha mara kwa mara

Taarifa hii ni kwa Mujibu wa Katibu Mkuu wa Chadema aliyoitoa Ukumbini hapo.

Nashauri wazime umeme wa Tanesco wawashe Generator.

Hii ni sababu ya kijinga sana kwa uongozi wa hapo Mlimani city(wana back up Generator za maana kwa nini wasiwashe? ) Mbona hakuna sherehe iliwahi katikiwa umeme.

Waambieni sio watanzania wote ni Mazwazwa. Na Jambo jingine tunafahamu kuwa wanatengeneza mazingira ya hii hali kuzoeleka ili baadae wapitishe makaratasi yao. Hii njama tumezisoma.

Ndugu mleta taarifa naomba unifikishie ujumbe hapo.

Ahsante.
 
TANESCO watakuwa wanafanya rehasal. Hata kwenye majenereta wapo
 
Tatizo sio tanesco, tatizo ni ukumbi kukosa standby generator
 
Hahaha Lisu anatumia nguvu nyingi sana kuzidi grid ya taifa, apunguze mori.
 
Umeme kukatika maeneo ya Mlimani City ni kawaida sbb wala sio Lissu
 
Tundu Lissu Wakati akitoa Neno la Shukrani Umeme ulikatika na uliporejea akaendelea na hotuba yake na kusema " tutafika tu"

Ukumbi mzima ukazizima kwa vifijo na vigelegele
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…