TANESCO yaingia mkataba wa kukodi software kutoka India kwa USD 30M

TANESCO yaingia mkataba wa kukodi software kutoka India kwa USD 30M

Sheria ya kunyonga ipoo, sasa ikiwa hata hujui sheria za nchi utamuongoza nani wewe?
Kwa wahujumu na mafisadi au wewe ulifikiri kwa wabakaji na Nani alinyongwa lete maeleze acha kuropoka Kama upo usingizini
 
TAtizo la mtoa Uzi ni mshamba, mill 30 kwa software ni ya kawaida kwa kampuni kubwa kama TANESCO

Mmezoea kutumia software za uwizi unafikiri kampuni kubwa kama TANESCO nao watatumia hapana
Hukuelewa kwamba unakodishiwa,sio unauziwa.Unajua cha kukodishiwa kinaishiaga wapi.Labda mtoa post hajaelewa vizuri.Usd milioni 30.halafu watakuja na training programme kwa Watanesco kwa kulipwa.Sipati picha jamani nosaidieni.

Halafu tutakuwa tunawalipa mpaka lini.Sijaelewa,muda wa kukodisha ukiisha wanachukua software yao au inakuwaje.Wakati wa matumizi iki co rrupt lazima waje au tunawaajiri.Nisaidieni sielewi. Watu wa IT Kina shahidi wa Kingai wa Tigo toa tena upupu hapa.
 
Mbona mifumo kama hii saivi serikalini watu wanafanya Tena sema tu hapa Kuna interest za watu. Na hata kama serikalini wakishindwa Kuna kampuni kibao tu za humu humu ndani pia zinafanya
 
Tena hata huko IFM, UDSM , DIT umeenda mbali, hapa hapa JF mbona tupo watu tunapiga hizo kazi...mimi kwenye hiyo 69.5 billion wanipe 0.5 tu naunda timu yangu ya ushindi tena kuna wakongwe humu humu wapo wakikubali tunaungana tunatoa hiyo ERP kama wanavyotaka na kama hawaamini waseme hata kifungu cha mkataba nikishindwa wanifunge na tukimaliza kazi tunawafanyia knowledge transfer wanakuwa na control nzima ya mfumo🐒
Kama ni hivyo kwanin software nyingi za watanzania ni flop sio rahisi kama unavyotaka kuaminisha watu unafikiri hawana sample za software zilizotengenezwa Tanzania
 
Hukuelewa kwamba unakodishiwa,sio unauziwa.Unajua cha kukodishiwa kinaishiaga wapi.Labda mtoa post hajaelewa vizuri.Usd milioni 30.halafu watakuja na training programme kwa Watanesco kwa kulipwa.Sipati picha jamani nosaidieni.

Halafu tutakuwa tunawalipa mpaka lini.Sijaelewa,muda wa kukodisha ukiisha wanachukua software yao au inakuwaje.Wakati wa matumizi iki co rrupt lazima waje au tunawaajiri.Nisaidieni sielewi. Watu wa IT Kina shahidi wa Kingai wa Tigo toa tena upupu hapa.
Naweza nikawa nimekosea, lakin pia mtoa Uzi ameelezea jujuu sana
 
Kama ni hivyo kwanin software nyingi za watanzania ni flop sio rahisi kama unavyotaka kuaminisha watu unafikiri hawana sample za software zilizotengenezwa Tanzania
Sioengelei hizi software zinazotengenezwa na makajanja anayekuambia anatoa app kwa 30,000 au kila siku yeye ana punguzo kuna watu wakongwe wapo wamefanya mambo makubwa na hakuna longolongo na wapo wanaoamini zimetengenezwa na wazungu ila ukiambiwa historia yake ndio utaelewa. Tatizo ni watu wamevamia fani na kumekosekana regulation ya maana ya nani ni nani ndio maana wengi mnakuwa na hiyo perception. Unafikiri hakuna software zilozochukuliwa kutoka nje ambazo zimeflop pia ? ukiambiwa ndio utashangaa zaidi gharama zilizoingiwa
 
Kwanini wakodi ?? Hawawezi inunua kabisa? Bcs watakodi mpk lini?
Siku hizi software nyingi zinakodishwa badala ya kuuzwa moja kwa moja. Faida ya kukodi ni kwamba kila wakati unapate updates na latest version ya hiyo software. Ukinunua, inakubidi kila mara ununue mpya. Hii ni gharama kubwa sana. Shida ya kukodi ni kuwa inategemea na vifaa vingapi unataka kufunga/kuunganisha hiyo software. Nyingine ni kuwa ukiacha kulipa kodi basi access yako nayo inakwenda na maji. Kwa mantik hii ni kuwa hii pesa iliyotajwa ni ya kila mwaka au kila baada ya kipindi walichokubaliana.

Amandla...
 
Watanzania naona tulisahau kabisa ajenda ya ufisadi wakati wa Magufuli, mpaka sasa kuna ufisadi umefanyika fasta fasta bila ya watu hata kushtuka.

Mkataba uliosainiwa baina ya Serikali ya Tanzania (kupitia TANESCO) na kampuni ya Tech Mahindra ya India wenye thamani ya dola milioni 30 ni wa kukodisha software ya Enterprise Resources Planning (ERP) - ambayo wahindi hawa wenyewe wanaiita Corporate Management System (CMS), kama inavyosomeka kwenye bango pichani chini.

Software ya aina hii huwa inaunganisha vitengo vyote vya taasisi katika software moja kwa ajili ya urahisi wa kuendesha taasisi. Hivyo basi kwa lugha nyingine ni kwamba Wahindi hawa watafunguliwa milango ya kuingia kila mahali ndani ya TANESCO, na hivyo kuwa na siri zote za mfumo wetu wa umeme.

Jambo kama hili ni hatari sana kwa usalama wa taifa. Hakuna njia rahisi ya kuiangusha nchi bila ya kufyatua hata kombora moja kama kuangusha mfumo wa nchi wa umeme.

Software kama hizi serikali inatakiwa iwawezeshe wataalam wa ndani kupitia Mamlaka ya Serikali Mtandao kutengeneza, kama vile mfumo wa malipo serikalini ulivyotengenezwa na wataalam wetu wa ndani kwa kuwezeshwa na serikali.

Zabuni ya kukodisha software hii ilianzaga kwenye dakika za lala salama za utawala wa Kikwete. Hivyo basi kitendo cha zabuni hii kukaa benchi kwa miaka mitano ya Magufuli kinaonesha kuwa hakuwa amekubaliana nayo. Baada ya Magufuli kufa naona wadau wa zabuni hii wameiendeleza na kuimwagia wino fasta, kama wanavyotaka kufanya kuhusu bandari ya Bagamoyo.

img-618a884f193e3.jpg
Nenda baba nenda Magufuli lala salama!
 
Back
Top Bottom