TANESCO yaingia mkataba wa kukodi software kutoka India kwa USD 30M

TANESCO yaingia mkataba wa kukodi software kutoka India kwa USD 30M

200% deal wuuu,
Walikuwa na haki kusema vyuma vimekaza,
Walikuwa na haki kumuajiri kigogo ili apambane kwa ajiri yao wakati wa mwendazake!
Kwani mmesikia siku hizi Wanasema vyuma vimekaza?
No no noooo Wanakula kuku kwa mrija,
kigogo nae anaelea kwenye mafuta Ana imba na kusifu!
Binaadamu tuna dhambi!
 
Hiyo ERP ina features gani special kushinda nyingine, wanatakiwa watueleze

Unaweza kudhani umeuliza jambo la maana kumbe limeonesha hujui kitu. Unataka Tanesco aje hapa kueleza features??? Hutapata hilo na sijui ni mihemko au kushindwa kujikontrol?!

Tanesco ni wazi alitoa scope of works na anataka kufanya nini. Softare designers wakajitokeza na huyu bwana kashinda tu hilo shindano!!

Laumu aina ya elimu ya nchi hii ambayo inafundisha vitu majina na haina mazingira ya uvumbuzi!! Si unaona unadhani ERP unayoijua ndio Tanesco anapaswa kuitumia pia??!! [emoji23][emoji23][emoji23]

ERP ni tailor-made! It is not a one-size-fits-all thing! Hao uliwauliza wakikujibu nishtue.
 
Watanzania naona tulisahau kabisa ajenda ya ufisadi wakati wa Magufuli, mpaka sasa kuna ufisadi umefanyika fasta fasta bila ya watu hata kushtuka.

Mkataba uliosainiwa baina ya Serikali ya Tanzania (kupitia TANESCO) na kampuni ya Tech Mahindra ya India wenye thamani ya dola milioni 30 ni wa kukodisha software ya Enterprise Resources Planning (ERP) - ambayo wahindi hawa wenyewe wanaiita Corporate Management System (CMS), kama inavyosomeka kwenye bango pichani chini.

Software ya aina hii huwa inaunganisha vitengo vyote vya taasisi katika software moja kwa ajili ya urahisi wa kuendesha taasisi. Hivyo basi kwa lugha nyingine ni kwamba Wahindi hawa watafunguliwa milango ya kuingia kila mahali ndani ya TANESCO, na hivyo kuwa na siri zote za mfumo wetu wa umeme.

Jambo kama hili ni hatari sana kwa usalama wa taifa. Hakuna njia rahisi ya kuiangusha nchi bila ya kufyatua hata kombora moja kama kuangusha mfumo wa nchi wa umeme.

Software kama hizi serikali inatakiwa iwawezeshe wataalam wa ndani kupitia Mamlaka ya Serikali Mtandao kutengeneza, kama vile mfumo wa malipo serikalini ulivyotengenezwa na wataalam wetu wa ndani kwa kuwezeshwa na serikali.

Zabuni ya kukodisha software hii ilianzaga kwenye dakika za lala salama za utawala wa Kikwete. Hivyo basi kitendo cha zabuni hii kukaa benchi kwa miaka mitano ya Magufuli kinaonesha kuwa hakuwa amekubaliana nayo. Baada ya Magufuli kufa naona wadau wa zabuni hii wameiendeleza na kuimwagia wino fasta, kama wanavyotaka kufanya kuhusu bandari ya Bagamoyo.

img-618a884f193e3.jpg
Cha ajabu hutasikia hata bunge likihoji huu ujinga.
 
Ma ma mae walai nchi hii, bilioni 65 tunaAZIMA(KODI) software wakati huo umeme vijiji kibao hakuna!!![emoji848]

Je tumekodi kwa muda gani!?[emoji856]

Unampaje mtu wa nje kitu adimu kama hii, maana yake huyu mfumo wetu wa tanesco atakuwa anaujua kimK..ndu mk..ndu.
Vitu vya hovyo mnoo, taifa hili, kadri wanachi tunavyojilegeza ndio wanazidi kutupapasa, hatimae watatushika makalio kabisa. [emoji35]
 
Tuliza puru usome uelewe!

USD 30 million ni equivalent na billion 69.5 za kitanzania! Hizo pesa ni nyingi mno kuna vichwa viko UDSM,DIT,IFM ambavyo with a fraction of that amount of money wangeweza ku develop system nzuri tu kwa msaada kidogo tu wa hao wahindi!

Haiingii akilini mtu alipe zaidi ya 70 billions kwa kukodi system mara mia angekuwa amaeinunua mazima! Hapo kuna upigaji wa kutisha sana! Hio system nauhakika haina thamani zaidi ya billion 10 kwa kuikodisha tu.
Tena hata huko IFM, UDSM , DIT umeenda mbali, hapa hapa JF mbona tupo watu tunapiga hizo kazi...mimi kwenye hiyo 69.5 billion wanipe 0.5 tu naunda timu yangu ya ushindi tena kuna wakongwe humu humu wapo wakikubali tunaungana tunatoa hiyo ERP kama wanavyotaka na kama hawaamini waseme hata kifungu cha mkataba nikishindwa wanifunge na tukimaliza kazi tunawafanyia knowledge transfer wanakuwa na control nzima ya mfumo🐒
 
Sio kwamba ufisadi ulikufa wakati wa Dikteta Magufuli, tatizo hapakuwa na vyanzo vya habari kuelezea mambo ya serikali.
Hata jamii foram ilifungwa? Magufuri alikuwa na maadui wengi kungelikuwa na ufisadi akina kigogo wasingelishindwa kuandika,acha unafiki.
 
Hili tatizo linaanzia kule juu kabisa, unapokuwa na kiongozi asietaka kushughulisha akili yake kwa chochote zaidi ya kusubiri kuletewa taarifa na wasaidizi wake huyo ndie chanzo.

Wasaidizi wake wanaweza kumpelekea mawazo ya hovyo yenye malengo ya "kutupiga", na kwasababu kiongozi mwenyewe hawezi kuhoji chochote anayakubali tu mawazo hayo kutokana na namna pumba anazolishwa zitakavyokuwa zimepangiliwa.

Matokeo yake ndio haya, unaona habari ya kukodi software ya $ 30 milion, baada ya kutoka kule kwenye mradi wa LNG ambao nao naamini alipigwa sound akaukubali bila kujua chochote, wala asijue hao anaowatuma ndio wajanja wenyewe, anachofanya Rais ni sawa na kumkabidhi fisi bucha sasa tunavuna tulichopanda.
2025
 
Waongo, ukisoma specifications za ERMS ya eGA inasema wazi kuwa ni interoperable na mifumo mingine.

Huu mkataba una harufu nzito ya Ufisadi
Hii serikali ya Samia mbona inageuka ya Kipigaji mapema namna hii kulikoni?
Halafu interoperability ni kitu ambacho kinaweza kuongezwa hata kama haikuwepo as long as hao ega ndio walioitengeneza... labda waseme mfumo wa ega haukuwa interoperable na matumbo yao
 
Huo mkataba unanuka ufisadi.

Hiyo software ingeweza kuwa developed humuhumu nchini na kuleta ajira kwa watu wetu.

Kitu walichokifanya TANESCO ni kucreate ajira kwa wahindi badala ya watu wetu
Sijawahi kusikia hapa nchini software imetengenezwa na kuuzwa hata kwa majirani zetu, au wewe umewahi sikia?
 
Kuna Halmashauri niliwahi kufanya kazi Idara ya Ardhi waliibia Halmashauri huku madiwani wakimwaga sifa nyingi kwa ubunifu wa ile Idara. Walidownload Google Map wakadai wamenunua software kwa gharama ya Sh 20 milioni ili kusaidia mipango mji.

Lile dude tulilibeba mpaka Maonesho ya Nane Nane kuwaonesha wananchi jinsi Halmashauri yetu ilivyopiga hatua katika Idara ya Mipango Miji. Sidhani mpaka leo kama ile Halmashauri ilishagundua iliibiwa. Tuligundua vijana wawili tu kitoka Idara nyingine ambao tulikuwa ndo tumepata ajira.

Just imagine kama Halmashauri inaibiwa kienyeji namna hiyo hali ikoje katika mambo makubwa ambayo Watanzania wengi hawana utaalam nayo?
Na unaweza kukuta hapo wanaogopa hiyo software mpya itawaumbua na kuziba mianya yao ya kuiba mapesa.
 
Kuweka 'ERP system' katika TANESCO siyo kitu kibaya lakini nachelea matumizi ya huu mfumo hayatazidi 33% ya uwezo wake.
Hivyo watakuwa wanalipia 'full' lakini matumizi 'only a third..'.
Zaidi ya hayo kuna ERP nyingine zenye kujulikana zaidi na 'support' unapata ulimwenguni pote hata hapa TZ kama SAP, SAP Hanna n.k.
Pia kuna 'firms' lukuki na 'madogo' kibao wa ki-TZ wanatengeneza na ku-'support' mifumo kama hiyo.
Na pia TANESCO na Wa-TZ hawahitaji 'heavy softwares' kama hizo..
Lakini siyo mbaya kumpa MD Chande 'benefit of doubt' kwani naye ana utaalam katika Mifumo ya Komputa..
Je kwenye hizo gharama kuna ukweli hapo?
 
Tuna vijana wa kitanzania wamesomeshwa vizuri mambo ya IT, walanguzi wamerudi kazini...
 
Back
Top Bottom