Tanga, Korogwe: Ajali yaua 17 na kujeruhi 12

Tanga, Korogwe: Ajali yaua 17 na kujeruhi 12

Coaster iliyokuwa imebeba mwili wa marehemu na abiria 26 Ikitokea Dar es Salaam Kuelekea Moshi Kilimanjaro kwa ajili ya mazishi.[emoji848][emoji2827]
Marehemu hakuwa tayari kusafirishwa? Ama kuna mtu hakupenda awepo kwenye msafara?

Kuna watakaokuja kubeza unachowaza....

Ila mara kadhaa tumeshashuhudia waafrika wanagombea maiti kwenda kuzika, ugomvi msibani na kutoelewana kati ya ndugu wa marehemu.

Moja ya maswali yako inaweza kuwa kweli, akipatikana mwana familia wa karibu na marehemu wa kwanza aliyekuwa anasindikizwa kama alikuwa na macho ya rohoni kuna siri mahala.

Kma ni ajali ya kawaida basi kuna liana mahala, ama wazee wa mji/ ardhi anakoenda kuzikwa marehemu hawamtaki....

Mungu awapatie ufumbuzi wapone majeraha ya mwilini na rohoni.
 
View attachment 2505507View attachment 2505508View attachment 2505511
Picha za Ajali

Ndugu waandishi wa Habari na Ndugu wananchi wa Mkoa Wa Tanga na Tanzania kwa ujumla Nimepokea kwa masikitiko makubwa tukio la Ajali Mbaya iliyotokea usiku wa leo. Ajali hiyo imehusisha Magari mawili na kusababisha Vifo vya watu 17 na Majeruhi 12 Pamoja na Uharibifu mkubwa wa Magari hayo..

Ajali ilitokea Tarehe 03/02/2023 Majira ya Saa 4.30 Usiku Eneo la Magila Gereza Kata ya Magila Gereza Tarafa ya Mombo Wilayani Korogwe, Barabara Kuu ya Segera - Buiko.

Magari yaliyohusika na Ajali hiyo ni Gari Na T.673 CUC aina Mitsubish Fuso Ikiendeshwa na Dereva ambaye Jina Lake Halijafamika iligonga na Gari T.863 DXN aina ya Coaster Coaster Iliyokuwa imebeba Mwili wa Marehemu n Abiria 26 iliyokea Dar es Salaam Kuelekea Moshi Kilimanjaro kwa mazishi.

Ajali hii inasababisha Vifo 17 na Majeruhi 12. Ambao Majina yao wote Hayajafahamika. Miili ya Marehemu imehifadhiwa katika Hospitali yetu ya Wilaya Ya Korogwe na Majeruhi 10 Wamehamishiwa Hospitali ya Mkoa wa Tanga Bombo na Majeruhi 2 wamebaki Hospital ya Korogwe Kwa Matibabu.

Chanzo cha Ajali ni Mwendo Kasi na Uzembe wa Dereva wa Gari Na :T.673 CUC M/Fuso Kulipita gari la mbele Bila Ya kuchukua Tahadhari na kugongana Uso kwa uso Gari Na :T.863 DXN T/Coaster

Tukio la Ajali Baada ya kukaguliwa , Magali yote yameshaondolewa barabarani na Sasa Barabara inapitika.

Mgumba T. Omary
Mkuu wa Mkoa Wa Tanga.
Mungu awqsemehe dhambi zao, kifo cha mateso makubwa imetosha.
 
Coaster iliyokuwa imebeba mwili wa marehemu na abiria 26 Ikitokea Dar es Salaam Kuelekea Moshi Kilimanjaro kwa ajili ya mazishi.[emoji848][emoji2827]
Marehemu hakuwa tayari kusafirishwa? Ama kuna mtu hakupenda awepo kwenye msafara?
Inashangaza na huzuni pia, kwa mila yawezekana kabisa, inaogopesha sana, simulizi zijazo tutapata majibu
 
Coaster iliyokuwa imebeba mwili wa marehemu na abiria 26 Ikitokea Dar es Salaam Kuelekea Moshi Kilimanjaro kwa ajili ya mazishi.[emoji848][emoji2827]
Marehemu hakuwa tayari kusafirishwa? Ama kuna mtu hakupenda awepo kwenye msafara?
Kuna namna ngoja tungoje updates zaidi. Hii huwa inatokea sana, hakika kuna vitu huwa havifi unakufa mwili tu
 
Muhubiri 3
1 Kwa kuwa kila jambo na wakati wake, na majira kwa kila kusudi chini ya mbingu.

2 Kuna wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa, wakati wa kupanda na wakati wa kung'oa yaliyopandwa,

3 wakati wa kuua na wakati wa kuponya, wakati wa kubomo na wakati wa kujenga.

4 Kuna wakati wa kulia na wakati wa kucheka, wakati wa kuomboleza na wakati kucheza.

Ufu 14:13
Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, "Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao."


Ayubu 14:1

“Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke Siku zake za kuishi si nyingi, naye hujaa taabu."
 
Narudia tena Tanzania ni miongoni mwa nchi hatarishi uwapo barabarani.
Ajali za namna hii zinaakisi akili za watu wetu kwamba sisi ni taifa la wajinga wengi.

Siku moja, nimepewa lift na ndugu yangu mtu mwenye elimu yake na kazi nzuri, lakini namna alivyokua anaendesha ovyo barabarani nikasema huyu lazima apate ajali. Wamenishusha zangu Moro, wao wakielekea Dodoma, baadaye napata taarifa wamekula mzinga gari haifai, yeye na mkewe wameumia vibaya.
 
Back
Top Bottom