Informer
JF-Expert Member
- Jul 29, 2006
- 1,606
- 6,672
Watumishi watano wa Kituo cha Afya cha Mikanjuni kilichopo Jijini Tanga wamesimamishwa kazi kupisha uchunguzi baada ya kufanya uzembe uliosababisha kifo cha Mama mjamzito Fatuma Mussa Suleiman (36) Mkazi wa Magaoni, aliyefariki baada ya kuwekewa damu ambayo hakustahili kupewa na hakuwa na uhitaji nayo kwa wakati huo.
Mkuu wa Wilaya ya Tanga, James Kaji amesema kuwa Mama huyo alilazwa katika Kituo cha Afya Mikanjuni March 27, 2204 saa kumi alfajiri kwa tatizo la uchungu ambapo damu aliyowekewa Marehemu ilikuwa ni ya Mgonjwa mwingine ambaye alikuwa amelazwa kwenye kituo hicho akipatiwa matibatu ambapo baada ya kupatiwa damu hiyo Fatuma alianza kuonesha dalili za Mtu mwenye mzio mkali (Allergic reaction) kisha akafariki.
Watumishi hao waliosimamishwa kazi kupisha uchunguzi ni pamoja na Wauguzi watatu Fadhila Ally Hozza aliyekuwa zamu ya mchana, Restitua Kasendo Deusdedit na Muya Ally Mohamed walioingia zamu ya usiku na pia Madaktari waliomfanyia upasuaji Andrew Eliasikia Kidee na Hamis Mohamed Msami.
“Mgonjwa alifanyiwa upasuaji ambapo alifanikiwa kupata Mtoto wa kike wa kilo 3.4 na hakuwa na changamoto yeyote na baada ya upasuaji na aliendelea kupatiwa matibabu chini ya uangalizi wa Wauguzi na Madaktari wa zamu, katika wodi aliyokuwa amelazwa marehemu kulikuwa na mgonjwa ambaye alikuwa anahitaji kuwekewa damu na damu yake ilikuwa tayari imeandaliwa, Muuguzii aliyekuwa zamu alimuwekea Marehemu damu ambayo hakustahili kupewa na hakuwa na uhitaji huo, baada ya kuwekewa damu marehemu alipatwa na mzio mkali (Allergic reaction) iliyopelekea kifo chake”
Mkuu wa Wilaya ya Tanga, James Kaji amesema kuwa Mama huyo alilazwa katika Kituo cha Afya Mikanjuni March 27, 2204 saa kumi alfajiri kwa tatizo la uchungu ambapo damu aliyowekewa Marehemu ilikuwa ni ya Mgonjwa mwingine ambaye alikuwa amelazwa kwenye kituo hicho akipatiwa matibatu ambapo baada ya kupatiwa damu hiyo Fatuma alianza kuonesha dalili za Mtu mwenye mzio mkali (Allergic reaction) kisha akafariki.
Watumishi hao waliosimamishwa kazi kupisha uchunguzi ni pamoja na Wauguzi watatu Fadhila Ally Hozza aliyekuwa zamu ya mchana, Restitua Kasendo Deusdedit na Muya Ally Mohamed walioingia zamu ya usiku na pia Madaktari waliomfanyia upasuaji Andrew Eliasikia Kidee na Hamis Mohamed Msami.
“Mgonjwa alifanyiwa upasuaji ambapo alifanikiwa kupata Mtoto wa kike wa kilo 3.4 na hakuwa na changamoto yeyote na baada ya upasuaji na aliendelea kupatiwa matibabu chini ya uangalizi wa Wauguzi na Madaktari wa zamu, katika wodi aliyokuwa amelazwa marehemu kulikuwa na mgonjwa ambaye alikuwa anahitaji kuwekewa damu na damu yake ilikuwa tayari imeandaliwa, Muuguzii aliyekuwa zamu alimuwekea Marehemu damu ambayo hakustahili kupewa na hakuwa na uhitaji huo, baada ya kuwekewa damu marehemu alipatwa na mzio mkali (Allergic reaction) iliyopelekea kifo chake”