TANGA: Watumishi wabainika kuongeza idadi ya Wagonjwa wa VVU ili kunufaika na Fedha za AMREF

TANGA: Watumishi wabainika kuongeza idadi ya Wagonjwa wa VVU ili kunufaika na Fedha za AMREF

Yanarudi yale yale ya Covid-19,kwahiyo kumbe kuna michezo ya kupikwa takwimu ili muonekane wagonjwa wengi,watu wapige hela.
Siku ukisikia idadi ya watu waliochanjwa chanjo za uviko kuanzia Sept, Oct na Novemba mwaka huu utazimia...hii ndio Tanzania iliyofunguliwa!

Jiwe alikuwa sahihi kuzuia baadhi ya NGO hapa nchini. iCap, Marie Stopes, nk wanachokifanya hapa Kanda ya ziwa Mungu anawaona!

Ona sasa watumishi wameamua kupika takwimu za waathirika kisa 20,000/= kwa siku, huku WHO inatuweka kwenye "nchi zenye wahonjwa wengi wa ukimwi" Kisha Madelu anaenda kukopa pesa za "kuongeza kasi ya mapambano dhidi ya ukimwi" na kununua ma vx V8!
 
Watumishi wa afya katika wilaya ya Muheza waliohusika kusajili wagonjwa hewa 313 wa virusi vya Ukimwi (VVU) ili kuonyesha takwimu zipo juu za wanaoishi na VVU kwa maslahi yao binafsi ikiwemo kujinufaisha na fedha zinazotolewa na shirika la afya la AMREF.

Awali akitoa taarifa kwa waandishi wa habari ofisini kwake, Kamanda wa TAKUKURU mkoa Tanga Zainabu Bakari, amesema walibaini udanganyifu huo baada ya uchunguzi na kugundua watoa huduma za afya wilayani Muheza wanahusika na kusajili majina hewa ya wagonjwa wa Virusi vya Ukimwi ili kuzidisha takwimu za ugonjwa huo kwa maslahi yao binafsi.

Alisema wahudumu wa afya wanaohusika na zoezi la kusajili na kuwafuatilia watu wanaoishi na VVU wilayani humo, wamekuwa wakilipwa posho ya gharama ya usafiri na mawasiliano kiasi cha sh. 20,000 kwa siku kila wanapowatembelea wagonjwa hao.

Aidha amesema idadi hiyo ya wagonjwa iliondolewa kwenye mifumo na wahusika waliohusika na usajili wa wagonjwa hewa walipewa barua na kujieleza kwa kitendo cha kusajili wagonjwa hewa ambapo Wizara ya Afya imetoa maelekezo ya kufanya uhakiki kwa wateja wanaotumia dawa ambao sio halisi.

Chanzo: EATV
takwimu ni kitu sensitive sana aisee. hawa wachukuliwe hatua kali kabisa . unakosa uadilifu na kukiuka maadili kwa kiwango hicho... hapana
 
Nataka Kujua, Je zaidi Yaa ARV kuna kingine waathirika wa HIV wananufaika na Fedha za Amref?
 
Hii ni TAKUKURU ya nchi gani? Canada....
Mchezo wa kupika data unaofanywa na NGO za hapa Tanzania ni WA kutisha! Wakifukua chanjo za covid-19, uzazi wa mpango watazimia, nimesema hii ni TAKUKURU ya Canada kwa maana serikali yenyewe wanapika data kuwafurahisha wafadhili na hao hao watumishi wa afya ndio wanaotumika.....

EATV achana na maigizo hayo, kupika takwimu hapa Tanzania ni halali na hata sensa upo ushahudi makarani walipika hasa!
Ukijumlisha hata sensa unapata jibu jingine.Hapo hujaingia kwenye MATUMIZI ya mikopo ya fedha za nje
 
Shida ni kutoa Posho kwa kazi ambazo ni wajibu wa Mhusika,
 
Wanajifunza kutoka kwa baba yao CCM anavyoiba na kufoji hesabu za kura wakati wa uchaguzi.
 
Hiyo nikwasbabu hii miradi inatumia pesa nyingi kutaka data io inasababisha watu kupika data
 
Back
Top Bottom