GoldDhahabu
JF-Expert Member
- Apr 29, 2023
- 7,189
- 10,375
- Thread starter
-
- #21
Mkuu, ndivyo ilivyokuwa? Mbona hatukufundishwa hayo mashuleni?Sii kweli!, baada ya yale Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, Manowari za Uingereza zilitia nanga Mombasa tayari kuivamia Zanzibar, kuikomboa. Karume akaja kwa Nyerere kuomba ulinzi, ndipo, Nyerere akamshauri Karume tuungane kuwa nchi moja, Karume akajibu hata leo, wewe Rais mimi Makamo.
Inavyoonekana, ni Tanganyika ndiyo inayoung'ang'ania Muungano! Unataka kusema Tanganyika inawapenda sana Wazanzibar hivyo imeamua kuendelea kuwasiaida hata kama hawana shukrani?Viongozi kutoka Zanzibar hata rais wa Zanzibar ndio wanaojua madhara ya kuvunja muungano, hao wengine wanajisemea tu. Zanzibar haijaweza bado kujitegemea kifedha siku wakiweza muungano utavunjika hapo hapo!
Wazanzibar wanasema nyie ndiyo mnaowatawala, tena kimabavu.Mi naona Tanganyika tunatawaliwa tena kwa kasi tuu
Kwani hapana wasomali wenye mali nyingi bara? Tumeungana nao? Wahindi wangapi wanamiliki mali nyingi sana hapa Tanganyika, hadi bank of India, tumeungana nao?Umwambie Samia na Mbarawa na mawaziri wa Zanzibar waliopo serikali ya muungano kwamba muungano uvunjwe sasa hawatakubali ila baada ya wao kustaafu tena shingo upande manake wana mali nyingi bara.
Tanganyika hatuna la kupoteza muungano ukivunjika ila Zanzibar watapoteza bajeti, nafasi tele za uteuzi, biashara, ajira nyingi, na mali nyingi ikiwemo ardhi wanazomiliki huku bara.Inavyoonekana, ni Tanganyika ndiyo inayoung'ang'ania Muungano! Unataka kusema Tanganyika inawapenda sana Wazanzibar hivyo imeamua kuendelea kuwasiaida hata kama hawana shukrani?
Ukiacha hizo semekana zako, wewe mwenyewe unadhani ukweli upoje kwa kutazama tu hali ilivyo, ni nani mnufaika mkubwa wa MuunganoInasemekana, hata yale yanayoitwa Mapinduzi Tukufu ya Zanzibar, yalikuwa ni mauaji katili, na yaliratibiwa na kusaidiwa, kwa sehemu kubwa, na Tanganyika. Hata silaha zilizotumika kwenye mapinduzi zilitoka Tanganyika.
Inasemekana, mapinduzi hayakulenga kumwondoa Mwarabu, bali Serikali halali kwa lengo la kukiweka madarakani Chama kilichokuwa kikiungwa mkono na Tanganyika.
Inasemekana, tokea mfumo wa Vyama vingi uanze, chama kinachoungwa mkono na Tanganyika kimekuwa kikishinda uchaguzi bila ridhaa ya wapiga kura. Kwamba kishinde kisishinde, lazima kiingie madarakani, maadam tu kinaungwa mkono na Tanganyika.
Inasemekana, hata huu Muungano uliopo kwa sasa si Muungano bali ni Ukoloni. Kwamba Tanganyika inaitawala nchi nyingine kimabavu.
Na kuna Watanganyika wenye majumba na Mali zinginezo nje ya mipaka ya Tanganyika - Zanzibar, South Africa, Dubai n.k.Kwani hapana wasomali wenye mali nyingi bara? Tumeungana nao? Wahindi wangapi wanamiliki mali nyingi sana hapa Tanganyika, hadi bank of India, tumeungana nao?
Wapo wazungu wanamiliki mahoteli kadhaa hapa bongo, tumeungana nao?
Kumiliki mali sio lazima muungano.
Watawala.Ukiacha hizo semekana zako, wewe mwenyewe unadhani ukweli upoje kwa kutazama tu hali ilivyo, ni nani mnufaika mkubwa wa Muungano
Kwa nini Tanganyika haitaki kuwarejeshea uhuru wao?Tanganyika hatuna la kupoteza muungano ukivunjika ila Zanzibar watapoteza bajeti, nafasi tele za uteuzi, biashara, ajira nyingi, na mali nyingi ikiwemo ardhi wanazomiliki huku bara.
Kuwapa uhuru wao!?? Ambaye hana uhuru si huwa anaudai au kuupigania? Waliwahi kuudai?Inasemekana, Wazanzibar wanatamani kuwa huru, hata leo ikiwezekana. Tatizo ni Tanganyika ndiyo haitaki kuwatejeshea uhuru wao!
Inasemekana
Inasemekana
Inasemekana ...
Sasa tuwekee ushahidi wa hizo habari ulizosema inasemekana
Mnufaika Namba moja ni watawala wa Tanganyika na Zanzibar.Ukiacha hizo semekana zako, wewe mwenyewe unadhani ukweli upoje kwa kutazama tu hali ilivyo, ni nani mnufaika mkubwa wa Muungano
Inasemekana, kuna aliyewahi kutaka kufanya hivyo akashikishwa adabu! Alikuwa nani vile? Ni mzee Jumbe au mwingine?Kuwapa uhuru wao!?? Ambaye hana uhuru si huwa anaudai au kuupigania? Waliwahi kuudai?
Zanzibar wakiambiwa wajitegemee, hata mwaka hauiishi, wataanza kutaka mwungano uvunjike. Lakini kwa sasa, wakati huu wanaoutunzwa na bara, hawawezi kuthubutu kutaka mwungano uvunjike.
Mnapenda mno dezo. Hata Uhuru mnataka mpewe?Tanganyika ipo tayari kuipa Zanzibar uhuru wake?
👍Nchi ya Tanganyika yenyewe imeambulia kilio cha mamba huku watu wake wakiwa na jukumu la kuondoa vyombo mezani baada ya "wakubwa" kumaliza kula.
Mlaumu Mwalimu aliyekufundisha, hayo maneno ya Pascal Mayalla yapo kwenye recordings za audio kama ushuhuda Nyerere mwenyewe akisemaMkuu, ndivyo ilivyokuwa? Mbona hatukufundishwa hayo mashuleni?
Nashukuru mkuu. Nitafuatilia.Mlaumu Mwalimu aliyekufundisha, hayo maneno ya Pascal Mayalla yapo kwenye recordings za audio kama ushuhuda Nyerere mwenyewe akisema
Ni kweli Tanganyika inaitawal Zanzibar kimabavu?Mnapembenda mno dezo. Hata Uhuru mnataka mpewe?
Amandla...
Ni umaskini ndio unawafanya wazanzibari wasingizie muungano na kwa taarifa yako wazanzibari wengi watazimia siku muungano ukivunjika.Kwa nini Tanganyika haitaki kuwarejeshea uhuru wao?
Kwahiyo Zanzibar iwaombe radhi watanganyikaMnufaika Namba moja ni watawala wa Tanganyika na Zanzibar.
Mnufaika Namba mbili ni nchi ya Zanzibar.
Mnufaika namba tatu ni wananchi wa Zanzibar japo hawalitambui hilo!
Nchi ya Tanganyika yenyewe imeambulia kilio cha mamba huku watu wake wakiwa na jukumu la kuondoa vyombo mezani baada ya "wakubwa" kumaliza kula.