Tangazo kwa wale wote mtasafiri kutoka mjini kwenda vijijini, hapa kuna mambo ya msingi ya kuzingati

Tangazo kwa wale wote mtasafiri kutoka mjini kwenda vijijini, hapa kuna mambo ya msingi ya kuzingati

DungaMawe

JF-Expert Member
Joined
Jul 31, 2022
Posts
1,522
Reaction score
4,630
🇹🇿TANGAZO TANGAZO.🇹🇿

Kwa wale mnaokuja kula christmas vijijini zingatia yafuatayo:

1. Huku pia tuna TV lakini chaneli zetu ni TBC na ITV hakuna mambo ya kuangalia series na TV tunawasha kuanzia saa 2 usiku hivyo mkae kwa kutulia.

2. Mje na dada wa kazi huku hakuna mtu wa kubeba mtoto wako.

3. Hakuna kuchotewa maji ya kuoga mtoni unaenda mwenyewe.

4. Mje na midoli ya kuchezea watoto wenu wasije kutunyongea vifaranga.

5. Hakuna kuchinjiwa kuku hadi siku ya christmas.

6. Ukimaliza kuoga toka na sabuni kwa sababu hiyo hiyo ndo tunaoshea vyombo.

7. Ukija na mke au mume wako asianze kusema mboga hii akila anaumwa tumbo sisi tunakujua tangu ulivyokuwa mdogo ulikuwa unakula maembe yenye wadudu na haukuwahi kuumwa tumbo kwa hiyo mtakula chochote kitakachopikwa.

8. Huku hakuna kumbembeleza mtoto wakati wa kula akikataa kula sisi tunakula na tunamaliza.

9. Usiku hakuna kumulikiwa tundu la choo unapapasa na mguu tu.

10. Hakuna Kutupa ugali uliolala huo ni mkate wetu asubuhi.

11. Hakuna mto wa kulalia huku unalalia mikono tu.

12. La mwisho wale mliopo kwenye ajira zaidi ya miaka 10 na huku nyumbani hamjajenga mtakuwa mnalala kwa mwenyekiti.

Ahsanteni na karibuni sana 🙏🙏
 
Back
Top Bottom