Tangazo la kifo cha Benjamin Mkapa, Kurungenzi ya Mawasiliano Ikulu lawamani. Inahitaji kusaidiwa kumsaidia Rais - Jicho Letu Ndani ya Habari

Si jambo la kushangaza sana lakini wakti mwingine tujitahidi kutofautisha msiba na harusi.Msiba wa kwanza wa kitaifa ulikuwa wa Karume na wakati ule Radio ilikuwa moja tu RTD na redio set zikiwa chache sana,sina kumbukumbu vizuri ilikuwaje.Msiba wa pili ni wa Sokoine,haukutangazwa mara moja ili zilipigwa nyimbo za kijeshi mfululizo mno na watu tukahisi labda serikali imeanguka.Kama hiyo haikutosha Sokoine alifia Morogoro lakini Nyerere hakuamini mpaka maiti ilivyopelekwa Ikulu.
Hili sidhani ni jambo kubwa sana kwani wangesubiri mpaka asubuhi wangeipa chat mitandao ya kijamii.
 
Pia sehemu alipokaa wakati wa kutoa tangazo, nyuma kuna socket za umeme. Haipendezi
Hivi hamjui Magufuli? Kwenye hali kama hiyo atawaambia ''natangaza sasa hivi''. Wakimwambia mambo ya dress code, sehemu aliyokaa atawaambia ''natangazia hapa hapa chumbani, kwani nani ataniuliza?''
 
Pascal Mayalla,

Kwa mitandao ya sasa, mida ya saa kumi na mbili asubuhi hiyo isingekua taarifa tena kwa umma maana nchi nzima saa saba au nane ingekua imeshajua! Labda hii ingekua tamko tu la rais ila sio taarifa!

Kuna mida codes tupa kule.
Idadi kubwa ya watu mida ile ya saa 6:30 usiku ninaamini wangekuwa wamelala vitandani mwao, sasa habari za msiba wangezipataje Chief barafuyamoto?
Ndotoni?
 
Corona bado ipo na inaua sana
 
Saa 12 asubuhi?...[emoji23][emoji23][emoji23] wazee wenzangu wa jamii forums usiku wa manane isingekuwa taarifa mpya tena..ingeshakuwa story.

So rais alikuwa anataka kuwa wa kwanza kutoa taarifa, mpaka akatoa taarifa isiyo na kiwango kama tetesi za kifo huku mitandaoni?
 
Mzeee baba hatii shaka kama amiri jeshi mkuu yes..ameshaonyesha hilo kwe vita dhidi ya corona,rushwa na ubadhilifu wa mali ya umma.he is fit " kamanda".but still ni binadamu kama wengine
 
Wangejifunza jinsi Mkapa alipotangaza kifo cha Mwalimu Nyerere

Kulia kwake alikuwepo Waziri mkuu ndugu Sumaye, Kushoto kwake alikuwepo Dr Omar Ali Juma na wote walivaa kimamlaka

Sasa Magufuli anavaa Shati la mchelemchele kututangazia kifo cha Raisi Mstaafu huku tukiwa tumelala usiku na yeye anaongea utafikiri alikuwa usingizini

Kisha anatoka hapo anaenda msibani huku amevaa shati la CCM

Nadhani Mkapa alimtendea haki sana Mwalimu Nyerere jinsi alivyohandle msiba wake kuliko jinsi yeye alivyotendewa na utawala huu
 
Hata Mimi nilitegemea kwanza wimbo wa taifa kupigwa alafu ndo tuanze kujiuliza kuna nini?? Sasa ndo raisi ahutubie taifa kwa kutoa hiyo taarifa,
 
Naunga mkono hoja ,asante kwa kututanabahisha ,
Lakini yawezekana Jiwe alipopata taarifa tuu akakurupuka kuitowa bila ya kufuata taratibu tajwa hapo juu.
Hii ni hulka yake ya pupa na kukurupuka juu ya mambo mingi.
Hata kutumbua ,huwa hafanyi upembuzi yakinifu, yeye akiona kosa ni papohapo,
Yampasa na yeye Mkuu ajiweke sawa, na ashirikishe wenzake ,Maana Uraisi ni Taasisi, si mtu mmoja tuu kama anavyotuaminisha mkuu kuwa Uraisi ni wake peke yake ,hahitaji Mtu amshauri.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…