Tangazo la Kondomu au Pedi likirushwa nikiwa karibu na binti yangu huwa napata tabu sana

Nyie watu mnachekesha sana.
Ukiwa unaangalia movie pale juu huwa wanaweka kabisa rating .

Kwa mfano utakuta wameandika 18 SNLV maana yake hiyo movie iangaliwe na watu wazima kuanzia miaka 18 na ina contain Sex, Nudity, Strong Language na Violence ,,sasa wewe movie kama hiyo utakaa uangalie na mwanao kweli? Utakua huna akili

Movie za kuangalia na watoto na mama mkwe ni ambazo zimeandikwa FAM au G ikiwa na maana ya suitable for family and general audience

Kuhusu matangazo ni kweli matangazo hayo ya condom na pedi huwa yanaleta ukakasi sana
 
Binti ana umri gani?
 
Enzi hizo!! hiyo shopRite ina miaka mingapi toka ijengwe au hujui maana ya "enzi hizo"
 
macho yote wameelekeza kwa uchaguzi, hata lile tangazo la "mwalimu ananitongoza kila nikienda shuleni" linanikera sana.
Ajabu Wanasema Matangazo Yanapitiwa Ndiyo Yanarushwa Sijui Wanakwama Wapi
 
macho yote wameelekeza kwa uchaguzi, hata lile tangazo la "mwalimu ananitongoza kila nikienda shuleni" linanikera sana.
Linawadhalilisha walimu sana, imagine mzee ni mwalimu half mpo wote mnaangalia hilo tangazo utajiskiaje au mzee atajiskiaje.
 
Linawadhalilisha walimu sana, imagine mzee ni mwalimu half mpo wote mnaangalia hilo tangazo utajiskiaje au mzee atajiskiaje.
TCRA Kimya Utafikiria Haipo Hapa Dodoma, Halioni Hilo Tangazo
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Wakati nipo sekondari baba yangu alikuwa ananinunulia pedi, lakini si kwa kumtamkia kwa mdomo ni ile ikifika kipindi cha kufungua shule naandika list ya mahitaji na pedi ikiwemo ananiletea bila shida yoyote.

Baba yangu pia alikuwa anatuletea chupi na bra kila anapotoka safari za nje ya nchi.

Sikuwahi kuona tatizo lolote na heshima na adabu inabaki kuwa pale pale.

Ila sikuwahi kutamka kwake kuomba ninunuliwe pedi au chupi. Ilikuwa ni katika situation hizo mbili tu, kikawaida nilikuwa namwambia mama.
 
Kuna tamthilia inaitwa panguso duh!! Wanaume wanaitana majina ya kike, kuna siku niko na familia kuna sehemu jamaa anazungumzia mwanamme kushughulikiwa huku akirekodiwa, sitaki kuangalia tena.
Aisee hii tamthilia ni shida. Niseme ukweli kuwa ni nzuri sana sana ina story nzuri.
Tatizo ni lugha na violence. Ingepaswa iwe rated 18+ na ionyeshwe usiku kuanzia saa sita.
Yaani maneno yote wazi wazi...kulawiti, ngono, mauaji. Ni bonge la tamthilia ingawa mwanzoni niliidharau.
 
Hebu tuondolee ubishoo wako hapa...sie ving'amuzi vyetu havina hayo makitu ebo!
 
Wasipojitathmini wataanza kurusha matangazo ya vumbi la congo soon.
 
Wewe unazungumzia mambo ya nje, ni tamthili au sinema zipi zinazoonyeshwa katika channel ya sinema zetu ushawahi kuona wameandika au hata kutangaza kwamba itazamwe na watu wa umri gani?
 
πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…