Tangu Deception aanze kampeni yake kuhusu UKIMWI, kuna yeyote humu ndani ambaye amemuamini?



Mkuu hawa Madaktari wako wa aina nyingi ,
wapo waliosoma lakini hawakuridhika na yale waliyofundishwa tu Wakaamua kujiongeza kwa kufukua yalifichwa. Hawa wanajua HIV ni fix.na UKIMWI upo kwa kila binadamu na ndiyo maana tunaungua magonjwa mbalimbali.
Na tiba ya magonjwa yote yaliyopo hapa duniani ni mimea tu( mbogamboga,matunda, mizizi,majani)

Kuna wanaofaidika na giriba ya makampuni ya madawa ingawa kwa asilimia ndogo lakini kwao inaonekana kubwa.

Kuna walioridhika na kiwango walichofikia ,hawana haja ya kuendelea kuchimbua zaidi kwa kufikiri na kusoma vitabu na machapisho zaidi.
Hawa kwao Ukimwi/AIDS inaletwa na ngono

Kuna wale waliopumbazwa na uwongo wa wazungu na kuukubali nu kuuishi nao , hawa kwao HIV ni kitu cha ukweli.
 
Someni vitabu vya afya zaidi,
someni machapisho yahusuyo afya zaidi.
Angalieni video zihusuzo afya zaidi.
Wapo wazungu wengi sana wana roho nzuri wanauanika ukweli waziwazi juu ya afya zetu.
Wanauanika uhuni na giriba za wapigani wa makampuni naviwanda vya madawa.

Kwa wale mlioelimika kidogo wasaidieni kuwaelimisha ndugu zenu huko vijijini.
 
Wewe jamaa ni kilaz.a sana na ninasikitika kama nchi tuna wataalam wa afya wenye fikra mfu kama zako, Tangu nimefuatilia mjadala huu sijaona hoja ya maana kutoka kwenu madaktari.
Daud1990, sijui una maana gani kuniita kilaza, lakini neno "kilaza" naelewa ni mtu ambaye ni mjinga. Hilo halina shida, tuseme mimi ni mjinga na wewe mwerevu.

Pili, hakuna sehemu yoyote nilishawahi kusema mimi ni Dr. Hakuna. Na nilimkatalia Deception kwamba mimi sio Dr. Lakini pia, hutendi haki kwa madaktari wa kitanzania. Hutendi haki. Mtu hawezi acha kutibu aje hapa aanze kujadili siasa za Deception, never. Kwanza huyo Dr. atakuwa anakinzana na Wizara ya Afya.


Hoja zenu ni Kutia watu hofu, vitisho na huruma na sio tafiti na research za kitabibu kama afanyavyo deception and the likes....

Daudi1990, Deception hana utafiti wowote wa kitabibu. Hana. anapinga kitu ambacho hawezi kuthibitisha. You tube ndiyo utafiti?. Leta hapa paper iliyoandika hayo mnayosema, achana na you tube za miaka ya 1980........ Leta hapa machapisho ambayo yanasema hakuna HIV.

Page 10 zilizopita kabla ya hii deception alikuuliza maswali Mengi sana ulikimbia mbio ndefu sana..
Sikuona umuhimu wa kuendelea kujibizana na mtu ambaye anasema hakuna HIV. Akaawambie wadogo zake hamna HIV na sio vijana wa kitanzania. Vijana wanateketea kwa virusi, nyie mnasema hamna! ili iweje? wakapige kavu? acheni hizo.


Napata shaka na elimu ya madaktari Wetu ,sina imani nao kabisa. Kuna mmoja Jana nilimuuliza anaweza kunithibishia by evidence kuwa amewahi kumuona HIV??? Majibu aliyonipa ni aibu .
Sasa hapo ndipo unapokesea. Kwanza kabisa nilishasema kwenye post zangu huko nyuma kwamba mimi sio daktari na sijawahi kuwa Dr.

Pili madaktari wa kitanzania ndiyo huwa wanakutibu ukiumwa. Tatu, hao Madaktari ndiyo waliomtibu Tindu Lissu mpaka akastabilise. Nne, hao hao Madaktari ndiyo walimtibu mke wa Rais Magufuli alipolazwa pale muhimbili. So have respect. Siasa zako na Deception usiwaingize madakatri wa kitanzania.


Msikilize Karry Mullis Mgunduzi wa Kifaa cha PCR ambacho unakitumia ila naamini hujui huyu Mzee ndio inventor akizingumzia myth za HIV
Pamoja na wewe mwenyewe kuweka video lakini hujaelewa ulichokiweka.

Dakika ya 9:06 huyo Karry amesema "PCR came right about the same time that HIV did and it was.........." mpaka hapo amekiri HIV ilikuja muda huo huo. Anaendelea "people started looking with PCR for HIV, that was the only way to see it" Anasema hivi watu wakaanza kutumia PCR kucheck HIV, ilikuwa ndiyo njia pekee ya kuona HIV.

Anaendelea kusema mwaka 1983 - kulikuwa na MaDR. 2 ambao walikuwa wanajua mambo ya HIV, mwaka 1985- kulikuwa na MaDr. 500 tu na mwaka 1986 kulikuwa na MaDr. 500,000 waliokuwa wanajua kuhusu HIV. Kwa maana hiyo msitegemee sana hizo you tube zenu za miaka ya 80, kwa sababu bado maDr. wengi walikuwa hawana ufahamu.

Mwishoni kabisa huyo Karry anasema academy ya science ya marekani ni bunch of idiots. Hawana tafiti za maana zilizoandikwa. Kila mtu anaruka ruka. Huyu anasema vile, huyu anasema vile. Ni siasa kwenye utafiti.

Kasikilize 16:42 Peter Duesberg anasema "Chemotherapy iligunduliwa 30 years ago long before AIDS was known to kill human cells" kumbe mnajua AIDS inaua human cells. hahahaha


Madaktari wa Tanzania mnatutia aibu someni Basi mbona vitu vipo mtandaoni

Msihusishe maDr. wa kitantanzia kwenye siasa zenu na Deception.
 

Chakochangu, umelishwa matango pori na wewe ukayala.

HIV ni fix?????????????????????????????? tupe ushahidi hapa kwamba HIV ni fix. Achana na you tube za Deception. Leta chapisho.

Kwanini watu wawili wakipima HIV mmoja anaonekana positive na mwingine hana. Hicho kinacho onekana kwa mwingine ni nini?
 
Jiongeze mkuu hakuna hasiyekuwa na ukimwi hapa. Na ndio maana huwa tunaugua mafua.
Hongera kwa kunywa sumu inayokuua taratibu.

Soma vitabu na machapisho mengi ndugu utaelewa siri nyingi chini ya Jua.
Internet kwa faida yako na vizazi vyako.

Kaka kipimo gani unatumia kusema huyu ana ukimwi na yule hana?

Kuumwa mafua ni kuwa na ukimwi? Ukimwi ni nini hasa???
 

Nini huwa positive na nini huwa ni negative.
Tafadhali nieleweshe hivyo vitu kwa kiswahili.
 
Nini huwa positive na nini huwa ni negative.
Tafadhali nieleweshe hivyo vitu kwa kiswahili.
Kaka, tunazungumzia HIV virus. Positive una HIV Virus na Negative huna.

Sasa nithibitishie HIV ni fix.

Au labda niulize hivi, ni kwanini unasema hakuna HIV virus?
 
Hii kitu itafasiri kwa kiswahili. Na ielezee kinaga ubaga hapa. Mfano sijui chochote ila nataka kujifunza kutoka kwako mtaalamu kwa Lugha yangu ya kiswahili nitaelewa vizuri.

Chakochangu, mimi naona hatuendi popote na huu mjadala. Kwa sababu wewe mwenyewe umeandika HIV ni fix, halafu unaniuliza HIV ni nini kwa kiswahili.

Amini unavyotaka, lakini usiwafanye wadogo zetu kufanya zinaa hovyo kwa kuwaaminisha hakuna HIV.

 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…