Tangu juzi nipo mitaa ya Barcelona kashinda derby 4-0 lakini sijaona mabango ushamba mzigo

samahani mkuu uliye jijini Barcelona hivi mtu akifanya vitu kwa namna yake na njia zake anazo ona yeye ni sahihi inakuwa ndiyo ushamba?🤔
 
hatari, hadi leo bango linauma

marudio jichanganyeni tena mle 4-5 ***** linawekwa tena

alafu upandishe uzi mwingine
 
Kwani nyie simba mkishinda mbona hua mnapita mitaani na vigoma huo utaratibu spain pia upo? Na vile mna uchu wa kushinda siku mkishinda hayo makelele mtaani na boda boda yaani hakuna watu washamba wa ushindi kama mashabiki wa simba.
 
Kwani hao wanaofanya hayo unawachangia kiasi gani kutokana na maumivu yako
 
Wa wazungu ni bora kuliko wetu wa ushamba ni mzigo kule kufikiri tu kuweka bango ni upuuzi pili kuchemsha nyama za kuoza ni ulimbukeni nani bora hapo mzungu au wewe!
Wazungu wanakwambia gender is a wide concept, there are no two gender (I hope na wewe unaamini ivyo) , most Europeans wanatumia tissue na wanashangaa watu wanaotumia maji kujitawaza (by your logic nawewe utabidi utushangae kwanini tunatumia maji) , wahispania wanaamini Jumanne ni siku ya mikosi, kuna haka kamsemo "En martes, ni te cases, ni te embarques, ni de tu casa te apartes" wanakwambia hakuna kuoa, kusafiri majini wala kuondoka nyumbani kwako siku ya jumanne (Wewe huoni kama ni ujima kuamini upuuzi kama huo).
?
Kila sehemu watu wanadesturi zao, watu washamba kama nyinyi ndo mnaona desturi za watu wengine ni bora zaidi, alafu mnavyojikutaga wasomi sasa mkianza kusifia wazungu, sisi tunawaangalia tunawaona wakuja sana wenetu
 
Hii itakuwa ni Barcelona ya kwa Mtogole.
 
Unaandika tu lakini ukikaa peke yako unakiri hapo ulipo mifumo yako ya maisha yote unatumia utamaduni wa mzungu!
 
Na Espanha onde voçè vive?
 
Sasa unadhani tabia na mienendo ya waTZ inafanana na waspain...! kila mtu na ustaarabu wake na haimaanishi ustaarabu wa wazungu ni bora kuliko wetu..
Cc ndo hatuna ustarabu ungekuwa unalinganisha na Australia kidg ningekuelewa
 
Hata sisi hatuna huu utamaduni wale uliowaona wamefanya ni furaha iliwazidi maana walivuka malengo ya mwaka kwa kishindo, timu yao ilianzishwa kwa malengo hayo, kushinda akicheza na mnyama, sasa kashida 5. We hushangai hawajawahi weka bango la kombe lolote ila huu ushindi kaweka?
 
Uko upareni huko unakula kande unazuga upo Spain.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…