Tangu tupate Uhuru mwaka 1961 hatujawahi kuwa na madarasa ya Shule za Serikali ya aina hii

Tangu tupate Uhuru mwaka 1961 hatujawahi kuwa na madarasa ya Shule za Serikali ya aina hii

Jesusie

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2021
Posts
1,466
Reaction score
766


==
Baada ya kutazama kipande hiki kifupi cha Video hii wacha sasa nitete na wale tuliosoma Shule za Msingi na Sekondari za Serikali ya Tanzania.

Naamini tutakubaliana kuwa "Tangu Tanzania iwe huru hatujawahi kuwa na shule za Serikali za Msingi na Sekondari zenye hadhi na mwonekano kama hizi zinazojengwa leo na Rais Samia Suluhu Hassan".

Mnaweza kukubaliana na mimi kuwa Rais Samia Suluhu Hassan amekuja na aina mpya kabisa ya utawala na anafanya mambo yake kitofauti sana.

Mtakumbuka Rais Samia Suluhu Hassan ametoa jumla ya madarasa kama haya elfu 18 yaani elfu 15 ya Sekondari na elfu 3 ya Shule za Msingi Shikizi.

Tunaamini, madarasa haya yataongeza hadhi ya wanafunzi na walimu lakini pia yataamsha ari na nguvu ya wanafunzi kupenda shule na madarasa yao.

Tuweni wakweli, hakuna kama Rais Samia Suluhu Hassan na huenda ikatuchukua miaka mingi kumpata mwingine mwenye upendo kama wake.
 
eti ametoa, kwani zile pesa ni zakwake? huu upumbavu ndo unawafanya watawala wajione miungu mtu akati wamepewa tu dhamana ya uongozi.
Yaani nyie mataahira kweli unafikiri mungeambiwa zinatumika kutoa elimu ya corona tu mngembishia? acheni ujinga kajioa kuwaeleza anazianyia ktu gani chamuhimu kwenu bado mnaongea utumbo nyau nyie
 
Enzi hizo Tuliosoma primary school Muhimbili, Forodhani, Bunge, Zanaki, Upanga, Jamhuri na Kisutu tunajisikia kucheka sana kwa watu wa aina yako shule za ghorofa wewe unajidai na mabanda? Lumumba, gerezani na kule bungoni nako madarasa ya juu yamesakafiwa taa na feni juu...
 
Unasifu madarasa ya mkopo? Unajua Serikali imetoa nini kupata huo mkopo? Unadangayika kirahisi sana wewe, Serikali imegawa cobalt ( moja kati ya rasilimali aghali na zinazotafutwa sana leo hii kutengeneza electric cars, cell phones, computer chips Serikali imegawia Mzungu karibia bure), Gold, Gas ili ujengewe cheap madarasa halafu unasifu?

Hayo madarasa hata kwa kodi ya kunywa bia tu tunayokatwa inatosha kujenga na zaidi, …
 
eti ametoa, kwani zile pesa ni zakwake? huu upumbavu ndo unawafanya watawala wajione miungu mtu akati wamepewa tu dhamana ya uongozi.
Mkuu zile pesa angeamua kununua BARAKOA ingekuwaje?? Ndio maana wanasema ametoa kujengea hayo madarasa, maana bila amri yake huwezi chukua hizo pesa. Chuki kama hizi ndio mpewe NCHI??
 
Back
Top Bottom