Tanroad Iringa, haya ni matumizi mabaya ya fedha za walipa kodi

Tanroad Iringa, haya ni matumizi mabaya ya fedha za walipa kodi

Godman

JF-Expert Member
Joined
Jun 23, 2013
Posts
423
Reaction score
650
Wakuu! Habari za muda huu, sijui ni nani anayewashauri hawa TANROAD wa Iringa, mwezi wa pili mwanzoni waliipa tenda ya kuziba viraka kwenye Barabara ya Iringa to Dodoma Kampuni iitwayo TS Solutions (T) Limited ya Kipunguni, Kizinga area Dar es salaam.

Kampuni hii imefanya kazi hiyo katika eneo la Mlima Nyang'oro hadi karibu na Kijiji Cha Migoli, hivi karibuni Kampuni hii iliishiwa baadhi ya "Material" na walikuwa wanasubiri yaletwe ili waendelee na kazi.

Cha ajabu wakati wanasubiri hayo "Material" Kuna Kampuni nyingine iitwayo Kings ya Madare Dar es salaam nayo imepewa tenda katika eneo ambalo Kampuni ya awali iliziba viraka siku chache nyuma,.

Hii sasa imepewa tenda ya kufumua lami yote takribani kilometa tatu eneo ambalo tayari lilishazibwa viraka na Kampuni ya awali, kwangu haya naona ni matumizi mabaya ya fedha za walipa Kodi.

Iweje kipande hicho hicho zipewe tenda Kampuni mbili tofauti ndani ya muda mfupi? Kwa nini sasa badala ya kuziba viraka siku chache nyuma, wangeamua kuifumua yote kama wanavyofanya sasa? Kama bajeti ilikuwa bado ya kufumua basi baada ya kupata hizo fedha kwa nini wasingeelekeza eneo lingine kuliko eneo hilo hilo kupewa tenda Kampuni mbili tofauti?
 
Izazi - Nduli barabara inatengenezwa
Fufu - Mkonze barabara inatengenezwa tena hichi kipande cha Mpunguzi wamekifumua kirefu sanaaa.

Hii barabara haina hata miaka 12
 
Izazi - Nduli barabara inatengenezwa
Fufu - Mkonze barabara inatengenezwa tena hichi kipande cha Mpunguzi wamekifumua kirefu sanaaa.

Hii barabara haina hata miaka 12
Ni kweli haina muda mrefu, cha kushukuru hatuwezi kurudi tena kwenye vumbi, inafumuliwa lami inawekwa lami, lakini Sisi Watanzania kwa kukosa uzalendo pia kunasababisha vitu vingi kuwa chini ya kiwango, mfano mkandarasi anaweka "ratio"ya mifuko 100 ya Cement kwa kipande cha kilometa 1, badala ya kuweka yote mtu anaiba mifuko 10 hadi 20.
 
Wakuu! Habari za muda huu, sijui ni nani anayewashauri hawa TANROAD wa Iringa, mwezi wa pili mwanzoni waliipa tenda ya kuziba viraka kwenye Barabara ya Iringa to Dodoma Kampuni iitwayo TS Solutions (T) Limited ya Kipunguni, Kizinga area Dar es salaam.

Kampuni hii imefanya kazi hiyo katika eneo la Mlima Nyang'oro hadi karibu na Kijiji Cha Migoli, hivi karibuni Kampuni hii iliishiwa baadhi ya "Material" na walikuwa wanasubiri yaletwe ili waendelee na kazi.

Cha ajabu wakati wanasubiri hayo "Material" Kuna Kampuni nyingine iitwayo Kings ya Madare Dar es salaam nayo imepewa tenda katika eneo ambalo Kampuni ya awali iliziba viraka siku chache nyuma,.

Hii sasa imepewa tenda ya kufumua lami yote takribani kilometa tatu eneo ambalo tayari lilishazibwa viraka na Kampuni ya awali, kwangu haya naona ni matumizi mabaya ya fedha za walipa Kodi.

Iweje kipande hicho hicho zipewe tenda Kampuni mbili tofauti ndani ya muda mfupi? Kwa nini sasa badala ya kuziba viraka siku chache nyuma, wangeamua kuifumua yote kama wanavyofanya sasa? Kama bajeti ilikuwa bado ya kufumua basi baada ya kupata hizo fedha kwa nini wasingeelekeza eneo lingine kuliko eneo hilo hilo kupewa tenda Kampuni mbili tofauti?
Makandarasi "Wazalendo" wanalindwa sana na Tanroads, inawezekana ni kampuni zao au wana ushirika nazo. Wanajenga barabara nyingi chini ya kiwango. Hivi hawaoni aibun kwamba wa nje wajenge kwa viwango. Hivi wanafikiri kwa kiwango cha muda mfupi sana sio kwa kwenda bele kwamba kampuni yangu iwe ya kimataifa.
Acha hizo jamani Wacha kimalizia pesa kwao halafu mnashindwa kumaliza kazi.
Ndio zinabaki Tanzania tu
 
Izazi - Nduli barabara inatengenezwa
Fufu - Mkonze barabara inatengenezwa tena hichi kipande cha Mpunguzi wamekifumua kirefu sanaaa.

Hii barabara haina hata miaka 12
Wenyewe wanajitetea eti malori yanayobeba makaa ya mawe kutoka Songea kwenda Rwanda ndio yameharibu hiyo barabara....sasa cha kushangaza mbona hayajaharibu kipande cha Songea hadi Iringa😀😀
 
Sisi wazalendo tunakubali kupewa kazi kwa bei ya mwajiri si tunayoijua itatosha kufanya kazi nzuri. Matokeo yake kazi inafanyika chini ya kiwango! Unajaza tenda yako unaitwa kwa mazungumzo unaambiwa bajeti iliyopo ni kiasi cha chini ya ulichojaza! unaulizwa utafanya ? Kwa sababu ya njaa unakubali shingo upande na ukifika site ndio figisu zinafanyika!
 
Tatizo linaanzia juu,Sijawahi kumuona Magufuli analalamika,badala yake alichukua hatua lakini wa sasa hivi yeye analalamika sasa Sisi tufanyaje?
 
Back
Top Bottom