TANROADS hawana uwezo wa kudesign barabara nzuri kama za Kenya?

Wapi hakuna uhitaji? Dodoma Kuna congestion ipi kuzidi junction ya Mafiat au CBD ya Mwanjelwa au Junction ya Meta?

Au hayo mahitaji unayaona wewe punga peke yako?
Wewe tulia akili zako ni ndogo[emoji23][emoji23]
 
Bongo huwezi kutana na watu wa mamlaka wanaotumia akili inapopaswa kutumia akili...

Mbezi Mwisho pale tu kuweka zile over pass ilikuwa ni baada ya kupigiwa kelele...
Unadhani hawatumii akili?wanatumia akili kuliko unavyodhani kupanga mbinu zao za kupata ulaji
 
Kuhusu gharama bado sijafanya tafiti ila kwa Tanzania gharama zimepaa kutoka Milioni 800 mwaka 2014 hadi kufikia shilingi 1.6Bilioni mwaka 2022

Tatizo ninaloliona ni kukosekana kwa Uzalendo miongoni mwa Wataalamu wetu na Viongozi wetu wa Kitaifa
Narudia tena hicho ni kisingizio Cha kijinga.Kwani ujenzi wa Barabara hapa Tzn una jipya lipi kiasi kwamba wengine waweze ila Tzn ndio ishindikane?

Mpaka hapo unaona Kuna shida huko TanRoads Kuna Majitu majinga tuu yamekariri maisha.

Jiti limeshupaa kabisa kwamba eti miundombinu haijengwi kupendezesha Mji 😂😂

Angalia hicho kituko Cha Ubungo mnaita flaiova kwanza ni hovyo hara gharama kubwa kulinganisha na interchange 4 level ya Ghana.
 
Hawa Tanroads ni Janga, nikikaa na kuona sifa wanazopewa huwa nasikitika sana, Kwani ni wataalamu ambao wamejitoa ufahamu!! Wao priority ni Matumbo Yao TU, kutumia taaluma Yao wameweka pembeni!! Niseme TU, wataalamu washauri kazi Yao ni kusikiliza mahitaji ya mwenye kazi ambaye ni Tanroads, ila mwenye KAZI akiwa shortsighted na mshauri anamletea a short sighted design!!
Natoa mfano mdogo, Kwa hapa DSM barabara za mwendokasi, barabara mchanganyiko WA magari (mixed lane) huwa baada ya bus stops za brt huwa hizi barabara zinarudi na kuwa sambamba na Lane ya brt, huku kurudi baada ya stand katika huwa sio rafiki sana hadi michanga inakuwepo kwenye hizo Kona Kali!! Tatizo lilionekana Brt ya Kwanza, huwezi amini tunakwenda brt ya Tano Hilo tatizo wameshindwa kuliona!! Je Kuna any reviews yoyote wanaifanya kwenye michoro wakipewa!? Jibu ni hawana muda, Yao madili tuu!!
 
Ni wapi mna eneo la ukubwa huo kuweka bara bara …mnachojua ni kulaumu na kulia lia mnataka maendeleo mkidhani kuongea ni rahisi!
Watu siwanalipwa kupisha mradi mbona una mawazo yakitoto sana kaka,,,,jknia imepanuliwa vipi watu hawakulipwa???
 
Wewe ni zezeta narudia zezeta[emoji23][emoji23][emoji23] Akili huna!
Miundombinu inajengwa kwasababu ya uhitaji na katika kujengwa huko kwasababu ya uhitaji ndiyo watazingatia beautification.

Huwez kujenga miundombinu out of nowhere ukilenga beautification na hamna uhitaji.

Damn people are really this stupid[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Hawa itafikia wakati wawe wanawajibishwa haiingii akilini barabara imedesigniwa na kufikia standard lakini baada ya mwaka imeharibika halafu wanaomba tena pesa za matengenezo. Fikiri wewe ni mhandisi umedesign jengo halafu lifeli nakuambia utasota jela maisha yako yote ila kwenye barabara tunachukulia kawaida huku serikali ikiingia gharama kubwa kwa uzembe wa wahandisi na hawachukuliwi sheria hata siku moja
 
Umesema sahihi

Suala la kupungua kwa maadili limechangia pakubwa kufikia huku.

Ndiyo maana leo hii barabara yenye design life ya miaka 20 unakuta baada ya miaka 5 tu unakuta imeshaanza kuzibwa Viraka
 
Sasa tunachoangalia nibhela au huitaji wa sasa maana kama issue ni gharama magufuli asingeanzisha mradi wa SGR ambao ni multi trilion tsh...
 
Unadhani hawatumii akili?wanatumia akili kuliko unavyodhani kupanga mbinu zao za kupata ulaji

Hizo sio akili Joannah, matumizi sahihi ya akili yanapaswa kuwa na matokeo chanya...

Mfano mwingine, BRT ya Kimara hadi Kibaha haina kituo cha basi ndani ya barabara ya BRT...

Basi la BRT ili lipakie au lishushe, itabidi litoke upande wa kushoto kabisa, yaani lita interfere flow ya magari binafsi ili kushusha au kupakia...
 
Viongozi wetu waanze kuwa waadilifu ili kurudisha uadilifu Serikalini maana sasahivi mambo ya business as usual ndiyo yameshika hatamu.

Mungu atusaidie tutoke hapa tulipo maana Nchi ni kama imekosa Visionary leaders
 
Ni wapi mna eneo la ukubwa huo kuweka bara bara …mnachojua ni kulaumu na kulia lia mnataka maendeleo mkidhani kuongea ni rahisi!
Mkuu, Tanzania ina eneo la ardhi ya square kilometers 945,087 na square kilometers 61,000 ya eneo la maji na mito. Ni eneo kubwa kiasi gani TANROAD wanahitaji kujenga barabara za mfano?...Eneo lote la JMT limehodhiwa na Serekali inayoshindwa kujenga barabara kuu pana na za viwango vya kimataifa ...Hii ni aibu kwa mainjinia wetu na taasisi zote zinazopokea mafungu ya pesa kwa ajili ya kufanya maendeleo ya miundombinu. 🤔
 
Sasa tunachoangalia nibhela au huitaji wa sasa maana kama issue ni gharama magufuli asingeanzisha mradi wa SGR ambao ni multi trilion tsh...
Mahitaji ndiyo hupelekea gharama

Mfano rahisi ni kuwa ujenzi wa nyumba ya chumba 1 utakuwa rahisi kuliko nyumba ya Vyumba 3.

Kwasasa tuna tatizo la kifedha Serikalini japo najua itakuwa vigumu wao kukiri hili hadharani.

Maana Viongozi wanawaza Uchaguzi Mkuu hapo Mwakani na Mwaka huu Serikali za Mitaa
 
Harafu yamekaririshwa ooh gharama.Nchi maskini kama Rwanda inajenga barabara nzuri na za Kisasa kwenye Miji Yao ,Je huko gharama hazihusiki?

Ushamba,ujinga na local thinking ndio zinawasumbua.Maofisi ya Serikali yamejaa watu wengi sana wasio na uwezo wa kufikiria na wamekariri ila kujiongeza hamna.

Kuna Jamaa wa TanRoads Kigoma yule RM wao ameamua kwenda kinyume na hayo mambumbu kiasi kwamba kila mtu anamsifu na mara kadhaa wameambiwa wakajifunze kule.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…