John Haramba
JF-Expert Member
- Feb 4, 2022
- 365
- 1,374
Timu ya Tanzania imepoteza kwa bao 1-0 dhidi ya Uganga katika mchezo wa kuwania kufuzu CHA, leo Agosti 28, 2022
Japokuwa kuna mchezo wa marudio baina ya timu hiyo unaotarajiwa kuchezwa Septemba 3, 2022, lakini niwe mkweli ili kufanikiwa kufuzu basi kuna kitu kikubwa cha ziada kinatakiwa kifanyike, tofauti na hapo Uganda wapo mbali zaidi kuliko sisi.
Kuna mambo kadhaa ambayo yamechangia kupoteza mchezo huo:
WACHEZAJI HAWACHEZI KITIMU
Kuanzia kipindi cha kwanza hadi dakika 90 zinakamilika bila shaka ilionekana wazi ni kama hakukuwa na chemistry baina ya mchezaji mmoja na mwingine.
MENTALITY YA WACHEZAJI
Ukiangalia vizuri wachezaji wa Uganda walivyokuwa wakifanya baadhi ya vitu vidogovidogo kama kupoteza muda, kucheza na refa, kufanya vitu kadhaa ili wapoteze muda au wawatoe kwenye focus wapinzani wao, ni tofauti kabisa na ilivyokuwa kwa wachezaji wa Tanzania.
Wachezaji wa Tanzania ni kama walikuwa hawategui mitego ya wapinzani wao, na ndio maana nasema mentality ilikuwa tofauti na ilivyotakiwa kuwa.
HAKUNA PASSION
Hii hasa ni kwa wachezaji, asilimia kubwa au wote ni kama hawakuwa na passion ya kuichezea timu hiyo.
Watazame wachezaji walivyokuwa wakicheza, watazame na hao hao wakiwa ngazi ya klabu zao, ni tofauti kabisa, hata bao lilivyofungwa ni wazi kulionekana hakuna passion na focus ya mchezo ilikuwa chini.
KILA MCHEZAJI ANACHEZA KIBINAFSI
Tazama wachezaji wa Uganda walivyokuwa wakicheza ki strategy, kila move walikuwa wanajua inaenda wapi na kwa sababu gani. Nyota wa Tanzania kuuchukua mpira kupiga chenga, madoido ilikuwa kawaida na mengine hata hayakuwa na msingi kulingana na uhalisia uhitaji wa matokeo.
REFA YUPO KWETU LAKINI KAMA YUPO UGENINI
Mwamuzi wa kati hakuwa na presha kutoka kwa wachezaji wetu na ndio maana kuna amtukio yalioonekana wazi angeweza kuifikiria Tanzania, lakini kwa inavyoonekana ‘hawakujua kucheza naye’ matokeo yake katuminya.
ONE v ONE UGANDA WAPO VIZURI
Nguvu ya mchezaji mmoja mmoja wachezaji wa Tanzania wengi hawakuwa na nguvu ya kushindana na Waganda ndio maana mipira mingi ikawa inachukuliwa au kuanza kuguswa na Waganda.
Japokuwa kuna mchezo wa marudio baina ya timu hiyo unaotarajiwa kuchezwa Septemba 3, 2022, lakini niwe mkweli ili kufanikiwa kufuzu basi kuna kitu kikubwa cha ziada kinatakiwa kifanyike, tofauti na hapo Uganda wapo mbali zaidi kuliko sisi.
Kuna mambo kadhaa ambayo yamechangia kupoteza mchezo huo:
WACHEZAJI HAWACHEZI KITIMU
Kuanzia kipindi cha kwanza hadi dakika 90 zinakamilika bila shaka ilionekana wazi ni kama hakukuwa na chemistry baina ya mchezaji mmoja na mwingine.
MENTALITY YA WACHEZAJI
Ukiangalia vizuri wachezaji wa Uganda walivyokuwa wakifanya baadhi ya vitu vidogovidogo kama kupoteza muda, kucheza na refa, kufanya vitu kadhaa ili wapoteze muda au wawatoe kwenye focus wapinzani wao, ni tofauti kabisa na ilivyokuwa kwa wachezaji wa Tanzania.
Wachezaji wa Tanzania ni kama walikuwa hawategui mitego ya wapinzani wao, na ndio maana nasema mentality ilikuwa tofauti na ilivyotakiwa kuwa.
HAKUNA PASSION
Hii hasa ni kwa wachezaji, asilimia kubwa au wote ni kama hawakuwa na passion ya kuichezea timu hiyo.
Watazame wachezaji walivyokuwa wakicheza, watazame na hao hao wakiwa ngazi ya klabu zao, ni tofauti kabisa, hata bao lilivyofungwa ni wazi kulionekana hakuna passion na focus ya mchezo ilikuwa chini.
KILA MCHEZAJI ANACHEZA KIBINAFSI
Tazama wachezaji wa Uganda walivyokuwa wakicheza ki strategy, kila move walikuwa wanajua inaenda wapi na kwa sababu gani. Nyota wa Tanzania kuuchukua mpira kupiga chenga, madoido ilikuwa kawaida na mengine hata hayakuwa na msingi kulingana na uhalisia uhitaji wa matokeo.
REFA YUPO KWETU LAKINI KAMA YUPO UGENINI
Mwamuzi wa kati hakuwa na presha kutoka kwa wachezaji wetu na ndio maana kuna amtukio yalioonekana wazi angeweza kuifikiria Tanzania, lakini kwa inavyoonekana ‘hawakujua kucheza naye’ matokeo yake katuminya.
ONE v ONE UGANDA WAPO VIZURI
Nguvu ya mchezaji mmoja mmoja wachezaji wa Tanzania wengi hawakuwa na nguvu ya kushindana na Waganda ndio maana mipira mingi ikawa inachukuliwa au kuanza kuguswa na Waganda.