Tanzania haina Mapato ya kubeba ongezeko la Mishahara yote kwa asilimia 23.3%

Tanzania haina Mapato ya kubeba ongezeko la Mishahara yote kwa asilimia 23.3%

Eti mtu anashangilia kuongezeka kwa 23% this is pure poverty mentality.
Tujadili ni namna gani
1) tutabana matumizi ya serikali
2) dhibiti upotevu wa fedha Report ya CAG
3) kuongeza mapato ya nchi
4) kusbsidize hudumu muhimu
5) kupunguza inflation
Hizi ni contraction policies ambazo hazina nafasi katika uchumi wa kisasa uliojaa supplies. Supply cannot be independent of demand.
Sasa contraction policies zinataka kutenganisha na ndio maana hukaza vyuma. Serikali za kujibana zinataka kodi feom supplies lakini hawapendi kutengeneza demand.
Sasa serikali zenye kupenda expansionery policies zinatumia sera zake za kikodi na za kifedha kutengeneza demand ya supplies halafu inapata kodi kutoka kwa hao suppliers and maufacturers.
Huwezi kuacha uchumi umesinyaaa kwa kubana matumizi hadi kwenye ajira halafu utarajie muujiza wa kukusanya zaidi katika uchumi huo huo ili uweze kuendesha serikali na kutoa huduma.
 
Wewe ambaye hukukariri unataka kujiendesha kwa kuiga mambo hovyo hovyo bila kujua madhara yake iwapo role model yako ni Turkey. Huyo jamaa Ergodan kapandisha mishahara hiyo kwa sababu za kisiasa tu, siyo kwa sababu za kiuchumi. Yeye ni mtawala mmoja corrupt saba ambaye yuko madarakani kwa mabavu tu na anabana sana vyama vya upinzani. Ingawa uchumi wa Turkey siyo mbaya, lakini kutokana na corruption kuna fedha nyingi sana mitaani inayosababisha inflation iwe juu sana. Wakati anapandisha mishahara hiyo kwa kudai kuwasaidia wafanyakazi kutoka na inflation ambyo wakatio huo ilikuwa 54%, ndipo inflation ikapanda zaid sasa hivi ni 70%. Kama huo ndio mfano unaiga, basi bado tun safari ndefu sana. Turkey imekatailiwa kuingia kwenye European Union kwa sababu hiyo.
Rubbish 🚮🚮🚮🚮
 
Hili ongezeko linafikirisha na huu uchimi wa leo mmmh mama ngoja tuone
 
Mimi nadhani pamoja na yote uliyoyasema. Mama hajakurupuka. Hivyo ninaamini kamati yake iliyokuja na mapendekezo imeamua kwa kuangalia situation na kuconsider factor zote muhimu. Bora wale watumishi maana tunaona PESA mingi inaingia midomoni mwa wachache na huwezi jua.
Waafrika wanaakili sana. Ila labda ungesema wabinafsi.
 
Baada ya Mwinyi ilibidi aje Mkapa, baada ya Kikwete ilibidi aje JPM, baada ya Samia atakuja mtu kama JPM/ Mkapa.

Ili kuweka mambo sawa, kujenga miundombinu,taasisi, uchumi, nchi kuwasaidia maskini, majority, kuweka nidhamu serikalini.

Huwezi kuendelea kutembeza bakuli, kuishi kwa mikopo kwa muda mrefu sana kama mtu binafsi, biashara au nchi. halafu hufanyi miradi ya kimkakati, muhimu, maendeleo kama elimu, afya, barabara, umeme, maji, kutokomeza rushwa, ufisadi kuweka nidhamu serikalini, kufutulia mbali mikataba ya hovyo, ya kiunyonyaji kwenye rasilimali zetu iliyokuwa inatetea maslahi ya wageni zaidi ya Watanzanis wenzetu. Akaweka mikataba ya win-win, pia na sisi tufaidike na rasilimali zetu. Alipigwa vita sana.

At some point itabidi kuanza kuishi kwa kipato chetu, kurudi kwenye uhalisia.

Kuondoa mambo ya kuweka familia yako, washkaji kwenye chama na serikalini.

Viongozi, matajiri, connected, mafisadi, machawa watakuwa wamezoea kulamba asali, itabidi atumie mkono wa chuma, ubabe, kuwarudisha kwenye mstari, kuwatuliza.

Watakasirika watamuita majina yote, Kumuombea kifo, ikiwezekana kumuua.
 
Chawa mnachoweza ni matusi tuu na kupaza sauti 🤣
Huyu The Sunk Cost Fallacy ni mpuuzi namba moja hapa JF. Amelewa kwa kulamba asali. Kuzitafuna kodi zetu yeye na genge lake.

Anataka tuendelee hivyo hivyo anachojua ni matusi kunyamazisha wengine.
 
Kazi ya serikali ni kujenga capacity, uwezo, mazingira, ngazi, kuwazesha watu kujiinua, kuinuka.

Serikali makini inafanya hivi

1Afya. kuwa na huduma za afya nzuri kwa wote ni muhimu sana. tunazaliwa hospitalini, wote tukiumwa, ajali tunaenda hospitalini, mwisho wetu wengi tunakuwa hospitalini.

2. Elimu. (Elimu bure) ni kitu muhimu sana watoto zaidi ya milioni 10 kwa miaka mitano wameenda shule. Maisha yao, upeo wao, uwezo wao wa kufikiri umebadirika na kubadilishwa na elimu. Bila elimu tusingejua kusoma na kuaandika chochote hata hapa JF, simu yako usingeweza kuitumia.

3. Utawala wa sheria, kupinga rushwa ukiritimba, kusisitiza uwajibikaji,kupunguza kodi zai ili kuwezesha biashara kushamiri.

4. Miundombinu:- Muhimu sana kwa kila kitu. Mfano kutoa mazao yako kijijini kuuza mjini, nchi jirani, Ulaya, Duniani. Kwenda kazini, kurudi nyumbani, kufanya biashara zako. Ukiumwa, ajali kwenda, kuwahi hospitali ili kuokoa maisha yako. Kwenda shule, kununua chakula kwa bei rafiki, biashara zote kukua, kuongeza kodi za serikali.

Maisha yote ya binadamu yanajengwa, kila kitu kinajengwa na kuwezeshwa kwanza na juu ya miundombinu.

Kwahiyo serikali yoyote makini itawapa wananchi wake wote elimu bure, bima za afya rafiki, itawapa umeme, maji bila kuleta sababu za kipuuzi eti kwanini haiwezi kufanya hivyo kila siku. Itajenga barabara, reli ya kasi utoe mazao yako kijijini uuze mjini, Duniani, kuiwezesha biashara yako, kilimo, wewe kufanya kazi, kukua, kustawi.

Sababu ukifanya hivi vitu watu watafanya biashara, kazi, export zitaongezeka, mapato ya nchi yatakua.

Automatically Wafanyakazi wa serikali watalipwa vizuri. Na wale wa sekta binafsi mshahara wao utaongezeka. Nchi itaenda uchumi wa kati, mkubwa.

Sasa kama umeme ni issue, tunarudi kwenye ujima taratibu hata kama tukiongeza mishahara kwa 100%.

Vitu vya msingi vitavyowasaidia na kuwainua wengi Watz tumeviacha. Hatuna muda navyo kabisa. Tunapiga siasa badala ya kuchapa kazi.
 
Kwanini unaipenda, unataka kuhamia nchi fulani, fikiria, kwanini SSH atatembeza bakuli? ni vitu fulani vinakuvutia elimu, afya, mazingira, haki kwa wote, mindombinu, sheria zao ambazo ziko neutral, hazibagua, mweusi au mweupe, maskini au tajiri. Kiongozi na mwananchi wa kawaida. Viongozi, matajiri wote wasingefika hapo bila miundombinu.

Rasilimali za watu zinawezeshwa na miundombinu rafiki.

Ukiangalia Dubai, US, EU, nini kinakuvutia? Barabara, umeme, afya, maji, usalama, mazingira ya kufanya biashara, kazi, kuishi. Kitu cha kwanza muhimu duniani ni miundombinu. Ukijenga nyumba unaweka msingi imara kwanza, vyote vitajengwa juu ya huu msingi imara.

Kuna mtu alijaribu kuwekeza nguvu zake zote kwenye hivi vitu muhimu sana. Vingine vyote vingefuata. Of course kuna vitu alikosea, nani hakosei? Sasa hivi unapata teuzi ukimtukana.
 
Tukiwa na umeme, maji,kodi rafiki, kuthibiti mfumuko wa bei, kuwasaidia wakulima, usalama, usafiri wa kuaminika itasaidia watu wangapi?
 
ila ina uwezo wa kuwalipa wabunge mishahra minono na posho kibao,

ila ina uwezo wa kuwalipa mawaziri mshahara mnono na marupirupu kibao.


ilifika wakati kila mtanzania anatamani kuwa mbunge, sio kwa sababu ana uchungu wa kuwatumikia wananchi bali tamaa ya mshahara wanao lipwa wabunge na posho kedekede, sasa ifike mahali pia watumishi wa umma nao waheshimike ktk jamii.
 
ila ina uwezo wa kuwalipa wabunge mishahra minono na posho kibao,

ila ina uwezo wa kuwalipa mawaziri mshahara mnono na marupirupu kibao.


ilifika wakati kila mtanzania anatamani kuwa mbunge, sio kwa sababu ana uchungu wa kuwatumikia wananchi bali tamaa ya mshahara wanao lipwa wabunge na posho kedekede, sasa ifike mahali pia watumishi wa umma nao waheshimike ktk jamii.
Kama wanataka kuwatumikia kweli wawe kama wenyeviti wa serikali za mitaa
 
Back
Top Bottom