Mkuu kama una zijua facts naomba anza na upelelezi wa vitu viwili kuhusu mtukufu wako Tundu Lissu kwanza.
Tanzania tuna left hand Drive but right Hand Driver that means dereva wa gari ambalo lilimwendesha Lissu alikuwa kulia kwake wakati yeye alikaa kushoto kwa dreva. Sasa maajabu yaliyo tokea ni kwamba Lissu ameumizwa zaidi kulia kuliko kushoto, ilikuwaje dreva wake ambaye alikuwa kulia kwake asijeruhuwe badala yake hayo maafa ya kumiminiwa risasi yampate yeye tu?
Mbona wana CHADEMA toka tukio tukio litokee mmeficha dreva asihojiwe na vyombo vinavyo husika? Inakujaje wewe unahoji utekelezaji wa serikali kuhusu kujeruhiwa kwake badala ya kuhoji maelezo kutoka kwa der ja wake ambaye anaushahidi wa kutosha ambao ungeweza saidia kujua wahusika wa hilo tukio ni nani?
Nikupe siri kwenye fuko za bahari karibu kila leo maiti ya watu inaokotwa. Tatizo huzisikii hizo habari kwa sababu hakuna mtu ambaye anazizungumzia. Lakini hizi za Tanzania viongozi wako na watu waliokusudia kumchafua Magufuli waliamua kufanya hivyo ili wakoko na wakoma kama wewe mwone na kukubali kuwa kweli Magufuli nikatili na anaua watu. Watu wanao weza buy hizo hadithi za Abunuawasi ni vichaa ambawo wamekuwa admitted kwenda Milembe na Mazombi wa kwenye Michael Jackson Thriller kama wewe, lakini sio wanaume walio kiona kitabu na kukariri herufi za kurumi na kigiriki na kuzielewa namba za kiarabu kama sisi. Use your common sense please!
Mpaka leo Scotland YARD wa Uingereza wanamtafuta Msichana wa Uingereza Madeleine Beth McCann, aliyeitwa Maddie (aliyezaliwa Mei 12, 2003 katika Leicester), alipotea Mei 3, 2007 kutoka kwenye nyumba ya likizo Praia da Luz ya Ureno mpaka leo hajaonekana wakati kesi yake ilijulikana duniani kote kwa njia ya habari za vyombo vya habari, sembuse Beni Saanane na primitive devices na technic kama za kwetu?
Mkuu kwa jinsi ninayo kusoma wewe ni kijana sana na kwa hali hiyo ningeomba badala ya kupoteza mda wako kulumbana na mimi katika maswala ambayo wewe na mimi hatuwezi kuyatatua ningekuomba kufanya kitu kimoja; tumia ujana wako, akili na nguvu ambazo mungu kakujalia wewe mwenyewe kufight ili uje okoa jahazi ambayo wewe unadhani linazamishwa na Rais Magufuli, kwani Rais Magufuli naye alifanya hivyo hivyo wakati akiwa waziri.
Huo udikteta wa Magufuli mimi binafsi si uoni na hayo mauaji na kitendo cha kudharau katiba mimi siuoni na sikioni pia. Wapinzani wako Bungeni na wanafanya matakwa yao kama kawaida; wanapinga kupitisha bajeti ya matumizi ya fedha kwa ajili ya miradi mbali mbali kama ya maji, umeme, barabara na kadhalika, miradi ambayo wao wenyewe, ndugu zao na hata wapiga kura wao yanawasaidia. That is crazy!
Mahakama mbona inafanya kazi yake kama inavyo paswa? Rushwa imepungua sana na baadhi ya vigogo walio kuwa wamejificha kwenye chama cha Mapinduzi CCM wako kizimbani na wengine wanakuja. Kitu gani kingine unakihitaji zaidi ya hayo? Huna sababu ya kumsifu na kumshukuru Magufuli kwa jitihada zake za kuchukua maamuzi magumu?
Serikali chini ya uongozi wake mbona inatenda kazi zake mbali mbali vizuri kulingana na taratibu za katiba na mujibu wa Chama Cha Mapinduzi na hizo trillions za fedha unazo dai anajichotea kutoka hazina bila idhini ya Bunge wewe unadhani anazitumia kwa ajili gani? Kwa jambo hili mimi nakusihi kuchukua mda wako na kuangalia mambo na matatizo yaliyo ipata nchi yetu siku za nyuma badala ya kuangalia miaka hii mitatu ya utawala wa Rais Magufuli.
Baba wa Taifa Mwalim Nyerere alifanya kitendo hicho hicho ambacho Magufuli amekifanya cha kutumia hela za umma katika kugharamia mambo ambayo yeye aliyaona yanatija katika maendeleo yetu sote. Nakupa mfano, baada ya Wakenya mwaka 1977 kuamua kwa hiari yao bila makubaliano na sisi kuvunja umoja wa East African Community na kuamuru ndege zote ambazo zilikuwa zinamilikiwa na umoja huo kutua Kenyatta Airport, isipokuwa moja tu ambayo iliokolewa na mzalendo wetu Mapunda ambaye hivi karibuni amezawadiwa TZS Milion kumi na Rais Magufuli katika shamra shamra za kupokea ndege yetu ya kisasa ulimwenguni Airbus A220-300, Rais Nyerere aliagiza ndege 14 Cash bila kupata idhini ya Bunge. Kirahisi kuelewa kuwa kuna maamuzi mengine ambayo Rais wa nchi ana mamlaka kuyachukua ikibidi ili kuyaweka mambo sawa. Mpaka sasa naona kelele zote za akina Tundu Lissu zimeisha au kupungua.
View attachment 984573
[emoji3] [emoji3] [emoji3] [emoji120] Hizi facts za miaka mitatu iliyopita naziona sana na ndiyo maana nakusisitiza kuwa facts zinazo husu mambo ya dini ya mwaka 47 kulingana na na maelezo yako au miaka 315 baada ya kuzaliwa Yesu Christo au Karne ya 6 mpaka 15 ni za kuzizingatia pia kwani impact zake katika maisha yetu leo ni kubwa sana. Kwani tukijifunza makosa ya wakati ule tunaweza kugarantii amani ya maisha yetu ya sasa na baadae nchini.
Nikupe mfano, wakati wa Middle Age binadam hasa katika bara la Ulaya walisahau maisha ya enzi za warumi, wagiriki, wakatago na ya wa-Agypt matokeo yake walipigana vita vya kinyama na kuuana wenyewe kwa wenyewe kana kwamba sio watu ambao wakati wa Antic walikuwa tayari wameshapata civilization. Dini hapa hasa ya kikristo zili play a major role.
Baada ya kukumbuka maisha ya kidemokrasia ya warumi na wagiriki ya kipindi cha Ancient time diyo walikuja kuunda utaratibu wa kujali haki za maisha ya binadam na kuheshimu mipaka ya nchi zao tena mpaka leo. Na hapo maendeleo yali ibuka tena na kuendelea mpaka leo.
Kwa hiyo hizo ni akili za kuelewa matukio ya ulimwengu ambayo nakusihii wewe kujaribu kuyaiga kwani yanaweza kuja kukusaidia sana kuondoa frustrations zako za maisha. Amka mkuu usitumiwe na wana siasa ambao hawana lolote katika maisha yao bali ni kuwakatishana tamaa nyie vijana wetu na wajenga nchi ya baadae kwa ulafi wa madaraka.
Wewe katika maisha yako unakubali uozo unao lishwa wa kuwa Magufuli anatoa pesa kuwanunua wapinzani kweli? Kwenye uchaguzi wake alikataa hela ya michango ya wafanya biashara ya kutaka kusaidia kampeni yake ya urahisi, sembuse za wabunge na madiwani? Kama una amini hayo basi utakuwa hutumii akili yako katika kuchangia hoja zako. Utakuwa unatumiwa maana ningependa utambue kuwa Magufuli ni mwanamme asiye teteleka kama akina Mkwawa na Mangi Meli, yuko tayari kuweka rehani ya maisha yake kuliko kubabaishwa na huo upuuzi wa kuwanunua wapinzani. Ili Iweje sasa?
Yeye kwa taarifa yako anawaona watanzania wote sawa. Yeyote yule ambaye ana legitimate ya kushika madaraka katika ofisi ya serikali atashika anachotaka utendaji wa kazi kwa ufanisi kwa manufaa ya watanzania wote.
Sasa naomba nikuulize kitu, hivi wewe na mimi nani ni mburula? Yaani unathubutu kuniita mimi ni Mburula wakati wewe hujui hata unacho kiandika kina maanisha nini? Kuchangia hoja kwa mambo ambayo unayarudia rudia kwako ndiyo akili hiyo? Mimi nakuona kama kijana ambaye huna msimamo. Hujui nini unataka. Frustration pure zimekujaa. Wewe kwa ujumla una umasikini wa roho ya upendo kwa nchi yako na watanzania wenzako.
Jifunze kujenga hoja yenye substance na inayo leta maana kwa msomaji. Usitumie kipaji chako cha kuandika maneno mengi ambayo ni irrelevant kwa kudhani kuwa una akili kuliko wengine. Unajidanganya mwenyewe. Kama watu wako wa kijiweni ndiyo wakueleza uozo huo, basi jiulize mara tatu kwa nini watu hawakuelewi na wewe huwaelewi?
Wito wangu kwako, tumia kipaji chako kuandika vitu ambavyo vitakupa mwangaza wa kutambua ulimwengu ulivyo ili ule leta maendeleo yako binafsi, familia yako na nchi yetu. Kwa upande wangu naona history yako ya maisha na mtazamo wa mwenendo wa maisha ya binadam kwako uko narrow sana kwa sababu mara nyingi unapenda hoja ya confrontation na members wenzako wa JF badala ya hoja za kujifunza vitu.
Nikupe Tips, ukipata au kusikia kitu ambacho hukijui toka kwa mtu jaribu fanya research ili ukielewe kwa undani zaidi badala ya kuandika pumba na kuanza kutukana watu. Mimi hata ukiniita Mburula hainiumizi kitu na wala haini saidii kitu, kwani najua uwezo wangu upo wapi na nini nimekifanya kwangu na kwa binadam mwenzangu wanao nizunguka, nikianza na familia yangu, ndugu, jamaa zangu wengine na marafiki.
Kwa vile nina upendo na watanzania wenzangu kama wewe, nakupa nafasi hapa ya kuondoa frustrations zako za maisha kwa kukuambia kuwa kama una qualifications za uhakika hasa za ufundi na uwezo wa kujifunza mengi ya dunia basi angalia hiyo Clip hapo chini na uone kama ina weza ikakuamsha na kuanza peleka maombi yako ya kazi Ubalozi wa Ujerumani ili upate bahati yako. Pengine iko siku utakuja kuwa Rais wetu na kufanya mambo ya ajabu ya kutuletea maendeleo yetu sisi kuliko hata Magufuli. Jitahidi na jaribu bahati yako!!
Sent using
Jamii Forums mobile app