Tanzania inafuata misingi yote ya Demokrasia ya vyama vingi

Tanzania inafuata misingi yote ya Demokrasia ya vyama vingi

Kwa mujibu wa tafiti za wataalamu wa mambo ya siasa Tanzania ni nchi ya tano duniani kwa utawala bora unaozingatia haki na misingi ya kidemokrasia , utafiti huo umeonyesha nchi ya Guatemala, Honduri na Malta kushika nafasi tatu borašŸ’
 
Mapungufu madogo madogo na kasoro chache zilizopo, vipo pia kila mahali inapotekelezwa demokrasia ya aina ya Tanzania, mathalani Marekani na kwingineko.

Na kwasababu hiyo uchaguzi huru na wa haki Tz upo, Tume huru ya uchaguzi Tz ipo, Utawala wa Sheria na utawala bora Tz upo, heshima kwa haki za binadamu na makundi maalumu Tz vipo, uhuru wa maoni, habari, vyombo vya habari na mawasilino Tz vipo, uwazi na uwajibikaji Tz upo, bunge na mahakama huru Tz vipo, usawa na haki ya kupata huduma za msingi Tz vipo, ulinzi na usalama wa watu, mali na makazi yao Tz vipo, uhuru wa kuabudu na kuabudiwa Tz upo, uhuru wa kutoa na kupokea sadaka na misaada Tz upo, nakadhalika nakadhali, nakadhalika, nakadhalika.....

Tunaweza kutofautiana kwa kiwango cha kuridhika cha utekelezaji wa Demokrasia hii ya vyama vingi Tanzania na ufanisi wake. Na hiyo ni haki na ni Demokrasia ya maoni, kutofautiana na kukubaliana kutofautiana.
Mathalani, wingine anaweza kusema hakuna kabisa demokrasia, mwingine akasepa ipo kidogo, mwingine akasema ipo sana, na mwingine akasema hana maoni kabisa juu ya Demokrasia Tanzania, nakadhalika, nakadhalika, nakadhalika...

Lakini, ukweli usemwe,
Amani, Utulivu na utangamano miongoni mwa waTanzania ni matokeo na matunda matamu ya utekelezaji wa Demokrasia nchini. Ni muhimu sana hali hii ya ustahimilivu na kuvumiliana kuimarishwa zaidi ndani ya mioyo ya wanasiasa na watanzani wote ile umaja wetu usitetereke.

Maendeleo ya watu na makazi yao, maendeleo ya biashara, utalii, miundombinu ya barabara, anga, maji, reli, afya elimu, michezo na vyote vinavyoonekana na visivyo onekana kisiasa, kiuchumi na kijamii ni zao la Demokrasia ya vyama vingi nchini.

Kwa kiwango kikubwa sana maendeleo yanayonekana hivi sasa yamechochewa pakubwa sana na utekelezaji wa demokrasia ya vyama vingi. Mathalani uwazi, uwajibikaji, ulinzi na usalama serikalini.

Changamoto ndogo ndogo na kasoro chache zilizopo na mara nyingi huonekana nyakati za uchaguzi, zinarekebishika na kutatulika ikiwa tu utashi wa kisiasa na dhamira ya kweli miongoni mwa wanasiasa utawekwa kwenye mizania sawa kwa maneno na matendo, kwa maslahi mapana ya umoja na mshikamano wa Tanzania.

Njia zinazotumiwa na wanasiasa kujaribu kushinikiza marekebisho ya mapungufu na kasoro za kidemokrasia nchini, zinarefusha zaidi kupata majawabu. Ushari wa maneno ya wanasiasa dhidi ya serikali, amri na matakwa ya lazima ya wanasiasa dhidi ya serikali, ubabe na utoto wa wanasiasa dhidi ya serikali, nakadhalika nakadhalika nakadhalika.....

Hakuna ungwana, ustaarbu wala utashi katika kauli na matendo miongoni mwa wanasiasa dhidi ya serikali. Ni kutunishiana misiuli kusiko koma, kutwa kucha ni kiburi na majivuno cha eti chama hiki au kile kina wafuasi wengi kuliko kingine na kwahivyo kina haki zaidi na kinaweza kufanya chochote itakacho.

Hii si sawa.
Huu ni mwanzo wa kuharibu na kumomonyoa demokrasia ambayo tayari imekomaa, imeimarika, inashamiri na kunawiri vizuri sana nchini.

Kama raia wa Tanzania navisihi vyama vya siasa na wanasiasa, vyama vya kiraia, taasisi za dini na makundi mbalimbali ya kutetea haki nchini,
fanyieni vyovyote mfanyavyo kwa mujibu wa sheria.

Lakini chondechonde, matokeo ya hayo yote muyafanyayo iwe ni Amani, Amani, Amani, ya huyu Mama Yetu Tanzania.

wasaalam.....
Upuuzi mtupu.
 
Kwa mujibu wa tafiti za wataalamu wa mambo ya siasa Tanzania ni nchi ya tano duniani kwa utawala bora unaozingatia haki na misingi ya kidemokrasia , utafiti huo umeonyesha nchi ya Guatemala, Honduri na Malta kushika nafasi tatu borašŸ’
shukrani sana kiongozi.
 
Matatizo ya kukulia husweken huko ndaani ndani maporini ndio haya. Siku MTU akija Dar anaona CCM. Imefanya makubwa. Hivi nimuulize, wakati wa chaguzi za 2019/2020 ulikua bado uko porini unakula mizizi na asali au ulishatokeza kwenye mwanga?
 
Matatizo ya kukulia husweken huko ndaani ndani maporini ndio haya. Siku MTU akija Dar anaona CCM. Imefanya makubwa. Hivi nimuulize, wakati wa chaguzi za 2019/2020 ulikua bado uko porini unakula mizizi na asali au ulishatokeza kwenye mwanga?
ndio ule ushari unaochelewesha na kurefusha muda wa kupatikana majawabau ya dosari na kasoro chache zilizopo kwenye demokrasia.
ungwana umekua shari.
 
HAMNA HAJA YA HAYO. NCHI INATAKIWE IWE NA AMANI.
TATIZO NI KATIBA::
MMOJA ANAMTEUA MSIMAMIZI KUAMUA JAMBO AMBALO NAE ANALITAKA
una hoja muhimu sana ndugu. na ni kweli kabisa hamna haya ya kuvuruga amani. Ni ungwana tu.

kinachotokea na kuonekana kinasikitisha sana, yaani uwasilishwaji wa hoja na malalamiko panapo husika unafanywa na mwanadamu na unakua katika hali ya ushari mno na wa kulazimisha.
sasa na mpokea hoja na malalamiko pia ni mwanadamu, Sasa wanadamu tulivyo nae anavimba. Hakubali kulazimishwa.

kinachotokea ni kuvimbiana na mambo yanagoma kwenda kabsaa. inakua ni kulalama kutwa kucha
 
Kwamba huwa hatuoni hujuma na upuuzi unaofanywa kwa mawakala wa upinzani ama?
ukiona hvyo ndyo culture ya muafrika,sisi bado hatujafka kutaka pure democracy na ikifika tutaipata,kwa sasa msilete fujo
 
Tanzania imekubali kuwa na mfumo wa vyama vingi,imekataa demokrasia.
 
Demokrasia gani katika Uchaguzi Mkuu 2020 Mkuu wa Polisi alitumia muda mwingi kumfuatilia mgombea mmoja wa upinzani. Huyo Mkuu hata akajisahau akaelekeza mgombea huyo popote alipo ajisalimishe Polisi. Tume ya Uchaguzi ikaagiza tuhuma husika ni wajibu wa Tume sio Polisi.
Mahakama Kuu ilitoa uamuzi katika kesi ya wanaharakati kuwa si sahihi Wakurugenzi wa Wilaya kuwa wasimamizi wa uchaguzi. Uamuzi huo ulitupiliwa mbali, Wakurugenzi wakahakikisha wagombea Uchaguzi Mkuu wa 2020 toka vyama vya upinzani wanawekewa vikwazo kila hatua ya mchakato wa kujisajili hadi kutangaza matokeo. Kilichotokea ni BUNGE la chama kimoja lililokorogewa Covid 19. Katika mfumo huo maendeleo kwa uma wa Watanzania itabaki kuwa sarabi ("mirage").
Mapungufu madogo madogo na kasoro chache zilizopo, vipo pia kila mahali inapotekelezwa demokrasia ya aina ya Tanzania, mathalani Marekani na kwingineko.

Na kwasababu hiyo uchaguzi huru na wa haki Tz upo, Tume huru ya uchaguzi Tz ipo, Utawala wa Sheria na utawala bora Tz upo, heshima kwa haki za binadamu na makundi maalumu Tz vipo, uhuru wa maoni, habari, vyombo vya habari na mawasilino Tz vipo, uwazi na uwajibikaji Tz upo, bunge na mahakama huru Tz vipo, usawa na haki ya kupata huduma za msingi Tz vipo, ulinzi na usalama wa watu, mali na makazi yao Tz vipo, uhuru wa kuabudu na kuabudiwa Tz upo, uhuru wa kutoa na kupokea sadaka na misaada Tz upo, nakadhalika nakadhali, nakadhalika, nakadhalika.....

Tunaweza kutofautiana kwa kiwango cha kuridhika cha utekelezaji wa Demokrasia hii ya vyama vingi Tanzania na ufanisi wake. Na hiyo ni haki na ni Demokrasia ya maoni, kutofautiana na kukubaliana kutofautiana.
Mathalani, wingine anaweza kusema hakuna kabisa demokrasia, mwingine akasepa ipo kidogo, mwingine akasema ipo sana, na mwingine akasema hana maoni kabisa juu ya Demokrasia Tanzania, nakadhalika, nakadhalika, nakadhalika...

Lakini, ukweli usemwe,
Amani, Utulivu na utangamano miongoni mwa waTanzania ni matokeo na matunda matamu ya utekelezaji wa Demokrasia nchini. Ni muhimu sana hali hii ya ustahimilivu na kuvumiliana kuimarishwa zaidi ndani ya mioyo ya wanasiasa na watanzani wote ile umaja wetu usitetereke.

Maendeleo ya watu na makazi yao, maendeleo ya biashara, utalii, miundombinu ya barabara, anga, maji, reli, afya elimu, michezo na vyote vinavyoonekana na visivyo onekana kisiasa, kiuchumi na kijamii ni zao la Demokrasia ya vyama vingi nchini.

Kwa kiwango kikubwa sana maendeleo yanayonekana hivi sasa yamechochewa pakubwa sana na utekelezaji wa demokrasia ya vyama vingi. Mathalani uwazi, uwajibikaji, ulinzi na usalama serikalini.

Changamoto ndogo ndogo na kasoro chache zilizopo na mara nyingi huonekana nyakati za uchaguzi, zinarekebishika na kutatulika ikiwa tu utashi wa kisiasa na dhamira ya kweli miongoni mwa wanasiasa utawekwa kwenye mizania sawa kwa maneno na matendo, kwa maslahi mapana ya umoja na mshikamano wa Tanzania.

Njia zinazotumiwa na wanasiasa kujaribu kushinikiza marekebisho ya mapungufu na kasoro za kidemokrasia nchini, zinarefusha zaidi kupata majawabu. Ushari wa maneno ya wanasiasa dhidi ya serikali, amri na matakwa ya lazima ya wanasiasa dhidi ya serikali, ubabe na utoto wa wanasiasa dhidi ya serikali, nakadhalika nakadhalika nakadhalika.....

Hakuna ungwana, ustaarbu wala utashi katika kauli na matendo miongoni mwa wanasiasa dhidi ya serikali. Ni kutunishiana misiuli kusiko koma, kutwa kucha ni kiburi na majivuno cha eti chama hiki au kile kina wafuasi wengi kuliko kingine na kwahivyo kina haki zaidi na kinaweza kufanya chochote itakacho.

Hii si sawa.
Huu ni mwanzo wa kuharibu na kumomonyoa demokrasia ambayo tayari imekomaa, imeimarika, inashamiri na kunawiri vizuri sana nchini.

Kama raia wa Tanzania navisihi vyama vya siasa na wanasiasa, vyama vya kiraia, taasisi za dini na makundi mbalimbali ya kutetea haki nchini,
fanyieni vyovyote mfanyavyo kwa mujibu wa sheria.

Lakini chondechonde, matokeo ya hayo yote muyafanyayo iwe
 
ukiona hvyo ndyo culture ya muafrika,sisi bado hatujafka kutaka pure democracy na ikifika tutaipata,kwa sasa msilete fujo
Sio kweli, kubalini tu kuwa mmefikia mwisho wa ushawishi wenu kwa umma. Sio kutaka kucheza na maneno.
 
Kwenye demokrasia halisi hakuna mgombea anayeenguliwa bila amri ya mahakama.
 
Tanzania ina mengi mazuri kwa upande wa utawala wa kidemocrasia ila yafuatayo bado yanahitaji kuboreshwa:
1. Tume ya Uchaguzi - iwe huru kweli
2. Mahakama - ziwe mbali na siasa na rushwa
3. Polisi wawe mbali na siasa lakini watekeleze kazi yao ya kuhakikisha nchi ni salama na tulivu
4. CCM wakubali kua kuna siku inabidi ipishe wengine.
5. Mali za CCM walizovuna kabla ya mfumo wa vyama vingi irudishwe serikakini sababu wananchi wote walichangia na zinawapa CCM uwezo kandamizi kwa wapinzani.
6. Wapinzani wajiimarishe na kubainisha kua wanaweza kuaminiwa na watanzania kuunda serikali. Mpaka sasa haioneshi wana huo uwezo.
7. Siasa za visasi ziepukike kabisa. Atakea chukua utawala ajikite kwenye maendeleo na umoja wa taifa.

Mimi naona bora kwa miaka kama 20 ijayo kuchukua mfumo wa serikali ya mseto au maridhiano kufuatana na idadi ya kura vyama vilivopata. Hii itawezeshe kujenga imani na na utamaduni wa kufanya kazi kwa umoja hata baadae tukirudia mfumo wa chama kimoja kilicho shinda uchaguzi kutawala pekee.
 
Demokrasia ya kupitishana bila kupingwa inapatikana Tanzania tu tume huru ya kuengua wapinzani peke yake ipo Tanzania tu,tume huru ya kujaza kura fake kuibeba CCM ipo Tanzania tu,tume huru inayofanyia kazi maelekezo ya kuibeba CCM ipo Tanzania tu,tume huru ambayo wapinzani pekee ndio hawajui kujaza form za uchaguzi inapatikana Tanzania tu,demokrasia ambayo intelejensia yao inaonyesha uvunjifu wa amani ya nchi ni kwa wapinzani peke yao inapatikana Tanzania tu,tume huru ambayo wapinzani ndio wanaotekwa na kuporwa form za uchaguzi na haikemei matukio hayo inapatikana Tanzania tu.
ni vizuri kubainisha dosari na kasoro zote kwa makini, kisha kwa ungwana wa kiwango wasilisha mapendekezo mujarabu kiungwana pia panapohusika.

lawama na ghadhabu dhidi ya udhaifu wa demokrasia nchini, si suluhu hata kidogo.
Malalamiko yatakuepo tu, miaka nenda miaka rudi ,
walalamikaji nnje, walalamikiwa ndani na hakuna kitakachofanyika na mambo yateendelea kama yalivyo.
 
Back
Top Bottom