Tetesi: Tanzania inalipwa mabilioni ya fedha toka nje ambazo zimefanywa siri na serikali hazina rekodi, tumenunulia ndege, na kujenga SGR na Stiegler nk

Tetesi: Tanzania inalipwa mabilioni ya fedha toka nje ambazo zimefanywa siri na serikali hazina rekodi, tumenunulia ndege, na kujenga SGR na Stiegler nk

Tetesi zlizopo ni kwamba serikali ya Tanzania imekuwa ikilipwa mabilioni ya fedha na kampuni za nje lakini fedha hizi zimefanywa siri bila kuingizwa katika kasri za serikali, na hivyo kuwa nje ya wigo wa ukaguzi wa serikali kutia na CAG. Hili ndilo simulizi lililopo.

Nitawawapa dondoo za mazungumzo yaliyofanyika.

"Asikudanganye mtu, suala la Tanzania kununua ndege kwa fedha za kodi na pia kujenga Stiegler na SGR, daraja la Salenda na hizo flyover na mabarabara na miradi mikubwa inayofanyika, sio kwamba ni fedha za kodi. Tanzania haina ubavu huo wa fedha za kodi kufanya miradi mikubwa kama hiyo. Mnadanganywa. Tanzania imekuwa ikilipwa mabilioni ya fedha ambayo zimefanywa siri, na uongozi wa nchi kutumia fedha hizo kama mtaji wa kisiasa".

Lakini je, fedha hizo zinatoka wapi, na kwa nini Tanzania ilipwe? Simulizi linaendelea.

"Fedha hizo ni fedha za Helium ya Tanzania. Katika nchi ambazo zimebarikiwa rasilimali asili Tanzania labda inaongoza. Kuanzia miaka ya 2010 dunia ilionekana kwamba inaishiwa gesi ya Helium ambayo imekuwa ikitengenezwa viwandani na kuuzwa kwa bei kubwa"

"Kuna nchi sita tu duniani zinazozalisha Helium kwa sasa, na viwanda 14 duniani. Karibu nusu ya hii gesi inatoka USA. na theruthi moja inatoka Qatar. Sasa viwanda vyote hivi 14 vilivyopo duniani, vinazalisha Helium kutokana na natural gas. Tanzania ni nchi pekee duniani ambayo Helium imepetikana ardhini kwa wingi sana na ndio maana sasa iko katika nafasi ya kuongoza soko la Helium duniani".

"Hii gesi inapopatikana ardhini inakuwa na concentration ya wastani wa 2% na hivyo kufanya bei yake kuwa juu sana kwa kuchimba, na ndio maana inazalishwa viwandani. Sasa jambo moja la ajabu lilitokea. Mwaka 2015 wataalamu waligundua hii gesi Tanzania ikiwa inapatikana kwa kiwango cha juu sana, kati ya 5-15%. Hii ilifanya Tanzania kuwa nchi pekee ambayo ina Helium ardhini ambayo inaweza kuchimbwa na kuzalishwa kwa gharama ya chini kuliko inavyozalishwa na viwanda hivi 14 katika nchi 6 duniani. Na matokeo ni kwamba Tanzania ikajikuta katika nafasi ya kuongeongoza soko la Helium duniani, kama ambavyo Saudi Arabia inaongoza soko la mafuta duniani."

"Kwa sasa kuna upungufu mkubwa wa Helium. Kufuatia upungufu wa hii gesi, Marekani hata walianza kuweka hifadhi kubwa ya gesi hii kwa ajili ya matumizi ya baadae. Upungufu wa hii gesi umefanya bei yake uongezeka kwa zaidi ya asilimia 135% kwa mwaka mmoja tu!"

"Hii gesi ya Helium ni muhimu sana na itaipaisha Tanzania kiuchumi kuliko hata kama ingekuwa na mafuta. Matumizi ya hii gesi ni pamoja na kwenye mambo kama welding na hata utaalamu wa space (kwa kiingereza uses of Helium gas: are arc welding, chromatography, medical lasers, optical fiber, intercontinental ballistic missiles, space travel, etc)"

"Lakini sasa kukawa na tatizo. Ikiwa Tanzania ingeruhusiwa kuchimba hii Helium na kuuza, basi ingeuza kwa bei poa kiasi kwamba ingeua kabisa uzalishaji wa hivi viwanda 14, USA akiwa mzalishaji mkubwa. Basi inaonekana kulikuwa na makubaliano kwamba Tanzania icheleweshe uzalishaji wa Helium hadi wakati unaokubalika. Lakini kwa kufanya hivyo, lazima kulikuwa na makubaliano kwamba Tanzaia ilipwe fedha nyingi kama "compensation" ya kuzuia uzalishaji wa Helium ili kunusuru kampuni zinazouza Helium kwa sasa. Hiyo ndiyo fedha inayofanya miradi yenu ambayo wanasiasa wenu wanawaambia eti ni kodi za wananchi ili kuji-promote kisiasa. Habari ya ugunduzi wa Heluim Tanzania na umuhimu wa hii gesi katika soko la dunia, ilipaswa kuwa kubwa kuliko kama Tanzania ingegundua mafuta. Sasa jiulize, kwa nini wanasiasa wenu wamekaa kimya kuhusu huu ugunduzi mkubwa uliofanyika Tanzania? Tanzania ni nchi pekee duniani unapata Helium ardhini na utatawala soko la dunia kama ilivyo kwa Tanzanite, na mnakaa kimya, kwa nini?"

NB: Kwa wale mnaochangia mada hii bila kufikirisha sana ubongo wenu, jiulizeni jambo hili: Je implications za Tanzania kuwa nchi pekee duniani yenye Helium inayopatikana ardhini kwa wingi, ambayo inaweza kuua soko la nchi 6 pekee duniani zinazozalisha Helium kwa sasa, huku Marekani ikiwa imeshikilia zaidi ya asilimia 50% ya soko hilo, ni nini? Jiulizeni pia kwa nini serikali yetu imekaa kimya sana kuhusu huu ugunduzi wa Helium nchini ambayo itatatuweka karibu sawa kimapato na nchi zinazozalisha mafuta?

Pia tafakarini sana kile Bloomberg wamesema kuhusu ugunduzi wa Helium Tanzania, "With such extreme sensitivity in this market, a big new helium source could, just maybe, transform a whole country’s economy. A country such as, say, Tanzania".

Mwisho tafakarini sana matumizi ya Helium, kutia ndani matumizi yake katika makombora ya masafa marefu (intercontinental ballistic missiles), space travel, chromatography, medical lasers, optical fiber nk


Reference:
In Photos: Massive Underground Helium Reserve Found in Tanzania
Reference: That huge helium deposit under Tanzania is even bigger than we thought
Reference: Tanzania could become top helium producer - African Business Magazine

Taarifa ya Bloomberg Businessweek juu ya Helium ya Tanzania
2019-08-28


Among the key uses for helium today are arc welding, chromatography, medical lasers, optical fiber, intercontinental ballistic missiles, and space travel. The Large Hadron Collider, the particle accelerator outside Geneva wrestling with the biggest questions of physics, needs 120 metric tons of helium a week to keep running. Helium can make things superconductive, meaning they can transmit electricity basically forever without generating any heat, and other helium properties make the element essential for semiconductor manufacturing. Every MRI machine in the world bathes its magnetic coils in liquid helium to prevent overheating.

Like the price of lithium, the price of helium is one of the more opaque among commodities, but reports said it jumped 135% from the previous year. With such extreme sensitivity in this market, a big new helium source could, just maybe, transform a whole country’s economy. A country such as, say, Tanzania.

Helium prices

Current price: $37.50 per 1000 cubic feet
View attachment 1331611
Umeandika pumba tupu na katika hilo swala la helium hujui chochote
Kwa taarifa yako tu ipo kiasi cha futi cubic 54 billion ambazo kwenye soko la dunia huo mzigo ni kama trillion 10 hivi hapo hajaingia mkataba na wamiliki wa kitalu kutoa gharama za utafutaji na uchimbaji unakuja potosha umma hapo hizi akili za nyumbu wa DJ

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mara umeisha ukubali huo uzushi billa kufanya utafiti zaidi na kujiridhisha?
Je kama hela hiyo wange iweka kwenye account za nje bila kutengeneza hizo miundo mbinu!
Labda wanaozitoa wanazifuatilia zinafanya nini?
 
Heri mtu yule asiyekwenda Katika shauri la wasio haki; Wala hakusimama katika njia ya wakosaji; Wala hakuketi barazani pa wenye mizaha...Hii mizee yote ife “jangwani”kama Musa ndio tutafikia nchi ya maziwa na asali
 
Habari ya ugunduzi wa Heluim Tanzania na umuhimu wa hii gesi katika soko la dunia, ilipaswa kuwa kubwa kuliko kama Tanzania ingegundua mafuta. Sasa jiulize, kwa nini wanasiasa wenu wamekaa kimya kuhusu huu ugunduzi mkubwa uliofanyika Tanzania? Tanzania ni nchi pekee duniani unapata Helium ardhini na utatawala soko la dunia kama ilivyo kwa Tanzanite, na mnakaa kimya, kwa nini?"
Hili ni swali zuri sana hata kama baadhi ya yaliyoandikwa kwenye mada yanakiasi fulani cha kutoaminika. Kwa mfano, hilo la 'compensation' kupisha viwanda, ni gumu sana, hata kama sio kwamba haliwezekani.

Lakini natamani ingekuwa hivyo, mradi tusidaiwe tu hapo tutakapokuwa tayari kuvuna gesi yetu na kutunufaisha ipasavyo.

Serikali inayopenda kufanya mambo yake gizani kama hii, kila lisemwalo ni vigumu kulipuuza.
 
Lakini kama inatumika kujenga miundo mbinu kwaajili ya taifa sioni Shida. Hapa nampongeza rais mzalendo Coz Ingekuwa enzi zile hii hata kuona tusingeona. Watu wangegawana tu na 10%zao na gesi ingechimbwa bila sisi kujua. Hongera mheshimiwa rais Dr John Pombe Joseph Magufuli mzalendo namba moja kwa kufikiria taifa kwanza wakati wote.

Kulingana na mtoa mada ni kuwa gesi haijaanza kuchimbwa basi ni jambo nzuri. Haichimbwi tunakula faida. Kongole serikali ya awamu ya tano business oriented.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawawezi kufanya hivyo kama kweli hizo fedha hazijaainishwa rasmi kwenye kasri za serikali. CAG ataona kuwa matumizi ni makubwa kuliko mapato, na atashindwa kuelewa fedha za ziada zimetoka wapi, na upinzani utasema serikali inachapisha kiholela fedha ili kuongeza fedha za matumizi ya serikali
Kwenye mishahara haitawezekana lakini kwenye ndege imewezekana?!!!
Haya endelea na kutujuza sie tunaomba na kashata tu tunywee vizuri hii helium.
 
mkuu hakuna kitu kama hiko! hizo taarifa za kijiolojia kuhusu helium gas unazo? kwa ufupi ni kwamba ishu za uwepo wa helium gas ni nadharia na kampuni ya helium one inataka kuuaminisha umma wa kimataifa uwepo wa gas hiyo ili wapate kuuza hisa zao kwa watu binafsi na makampuni.,. nimemaliza.
lost and gone
 
Nilisema na ninaendelea kusema ya kua, mwanasiasa ni mtu mmoja mshenzi na mnafiki na hasidi , hakuna mwanasiasa yuko kwa ajili ya mwananchi, ni uongo wa kutupwa, nadhani baada ya shetani kuchomwa moto kule jehanamu,atakayefuatia ni mwanasiasa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mkuu hakuna kitu kama hiko! hizo taarifa za kijiolojia kuhusu helium gas unazo? kwa ufupi ni kwamba ishu za uwepo wa helium gas ni nadharia na kampuni ya helium one inataka kuuaminisha umma wa kimataifa uwepo wa gas hiyo ili wapate kuuza hisa zao kwa watu binafsi na makampuni.,. nimemaliza.
lost and gone
Mkuu, tutaongea kila kitu na kukitilia shaka lakini sio suala la uwepo wa gesi ya Helium Tanzania. Hadi sasa waliosimamisha uchimbaji sio Helium One, ni serikali. Na kumbuka taarifa kuhusu uwepo wa hiigesi sio za Helium One
 
Kwa hiyo we unaamin dunia ina miaka hiyo? ..jua tu kwamba toka yesu asaliwe ni miaka 2020 tu
Mkuu, unataka tuongee dini? Unajichanganya sana na kutoelewa ukweli wa kisayansi juu ya Biblia. Kwani Yesu aliumbwa kwa mara ya kwanza alipozaliwa na Mariam? Yesu alikuwapo mabilioni ya miaka kabla ya kuzaliwa na Mariam hiyo miaka 2020 iliyopita unayoitaja.

Na pia tofautisha kati ya dunia kuwepo na kuumbwa kwa vitu kama wanyama na mimea na bahari nk juu ya dunia. Dunia imekuwapo kwa mabilioni ya miaka ikiwa imefunikwa na maji, kabla ya uumbaji unaoongelewa katika kitabu cha Mwanzo.

Genesis 1:1-2: In the beginning God created the heavens and the earth. Now the earth was formless and void, and darkness was over the surface of the deep. And the Spirit of God was hovering over the surface of the waters.

Mwanzo 1:1-2 sio day 1 ya uumbaji, ni mabilioni ya miaka kabla ya day 1 ya uumbaji. Sasa baada ya mabilioni ya miaka katika status hiyo ya Mwanzo 1:1-2, ndipo Mungu siku moja akasema; “Let there be light,”a and there was light. And God saw that the light was good, and He separated the light from the darkness. God called the light “day,” and the darkness He called “night.” And there was evening, and there was morning—the first day (Genesis 1:3-5).

Tatizo mnaenda kanisani kuimba mapambio na kuambiwa uzinzi na kuiba ni dhambi na mnaridhika na hayo mambo madogo bila kuwa watafiti. Na mkikutana na watu wanaojua dini wakakitaka kuwaelimisha zaidi mnakuwa na shingo ngumu.
 
Hili ni swali zuri sana hata kama baadhi ya yaliyoandikwa kwenye mada yanakiasi fulani cha kutoaminika. Kwa mfano, hilo la 'compensation' kupisha viwanda, ni gumu sana, hata kama sio kwamba haliwezekani.

Lakini natamani ingekuwa hivyo, mradi tusidaiwe tu hapo tutakapokuwa tayari kuvuna gesi yetu na kutunufaisha ipasavyo.
Serikali inayopenda kufanya mambo yake gizani kama hii, kila lisemwalo ni vigumu kulipuuza.
Mkuu, kama ungesoma mambo ya business hili la compensation lingekuwa rahisi sana kwako kuelewa.

Fikiria hili. Tuseme una kiwanda cha kutengeneza chupa za chai, na inakugharibu shilingi elfu moja kutengeneza chupa moja ya chai na unaiuza kwa shilingi 1500 ukipata faida ya Shs 500 kwa kila chupa. Na wewe ndio mtu pekee mwenye kiwanda cha chupa za chai duniani.

Sasa anakuja mtu anakuambia, nimegundua njia ya kutengeneza chupa bora zaidi na moja nitaitengeneza kwa shilingi 500 badala ya 1000 kama wewe, na nitakapoanza kuzitengeneza nitaziuza kwa shilingi 1000 badala ya 1500 kama wewe.

Utafanya nini? Kumbuka huyo mtu akianza kuuza chupa moja kwa shilingi 1000 basi wewe itabidi ufunge kiwanda chako, maana watu hawatakubali kununuia chupa zako kwa shilingi 1500 wakati zipo ambazo ni bora zaidi na zinauzwa kwa shilingi 1000 kila moja.

Una mamwili ya kufanya. Itabidi ujitahidi sana upunguze gharama yako ya uzalishaji kutoka shilingi 1000 hadi 500 ili na wewe upunguze bei hadi shilingi 1000 au hata 900 ili kuendelea na biashara. Labda hilo halitawezekana.

Njia ya pili ni kumwambia (au kumlazimisha ukiweza) yule jamaa aliyegundua njia bora na rahisi ya kutengeneza chupa, kwamba sikiliza, katika kila faida ya Shs 500 ninayopta kwa kuuza chupa zangu, nitakupa shs 250 ili usianze kutengeneza chupa zako hadi nitakapofunga kiwanda changu baada ya miaka 10. Nakupa hiyo shs 250 bure bila wewe kufanya kazi na huku rasilimali yako ya kutengeneza chupa za chai ikiendelea kuwapo na utaanza kuitumia siku mie nikiacha. Nipe hiyo mika 10 nijiandae kufunga kiwanda changu bila hasara.

Kumbuka hata ukimpa shs 250 katika faida yako, bado utapata faida, japo itakuwa imepungua, tofauti na hasara ya kufunga kabisa kiwanda chako.

Kuna wakati Bill Gates wa Microsoft aliambiwa aruhusu ushindani katika soko la operating system kwenye computer ili wateja wawe na uhuru wa kutumia operating system zaidi ya Microsoft Windows, la sivyo atapigwa faini ya mamilioni ya dola kila mwaka. Bill Gates alipiga hesabu akakuta hata akipigwa fine bado atapata faida, akaendelea na ukiritimba!

Mfano rahisi ni hivi, nikikwambia nipo hapa Moshi nakusubiri na ukiweza kufika na gari yako kutoka Dar ndani ya masaa matano nitakulipa Tshs 3M, je utajali kupigwa tochi na trafiki? Wakikupiga tochi si utakuwa unawaambia hebu niandikieni faini haraka nina haraka!

Sasa hvyo ndivyo biashara ya kimataifa inavyofanyika. Na kama umenielewa hapo juu utaelewa kwa nini kuna tetesi Tanzania inalipwa kuchelewesha uzalishaji wa Helium, na nani watakuwa wanatoa hela za kuilipa Tanzania.
 
Back
Top Bottom