ChoiceVariable
JF-Expert Member
- May 23, 2017
- 66,537
- 75,687
Mtaani watauwawa na itaishia kuwa kama ilivyoishia huko Kenya.Umemaliza vizuri sana
Ikigoma huko kwenye muujiza watakuja mtaani kusaka vitu kwa nguvu au waanzishe gwaride na serikali.
Kuhusu kupunguza matumizi hiyo pesa inaingia kwenye pato Kama sio kubaki pale na hiyo itafanya kodi zipungue na kupunguza ukali wa maisha.
naona anajaribu kufidia pesa alizotaka awatwishe mzigo wananchiLeo mchana Ruto anajindaa kwa kile kinacho aminika ni hotuba ya kupunguza baadhi ya mawaziri wake na kuunganisha baadhi ya wizara ili kubana matumizi ya pesa za walipa Kodi wa nchi ya kenya ambao ndio wanaoumia na mzigo mkubwa wa kuendesha Serikali.
======
View attachment 3034286
Kwa Tanzania hali ni tofauti, huku tunahimiza kulipa kodi ambayo sana inatumika kuendesha Serikali hasa hasa kununua Magari ya anasa.
Tuna hadi Naibu waziri mkuu cheo cha mchongo ambacho hakipo kikatba ila kimewekwa kwa sababu za siasa na mzigo tunabeba sisi.
Ukiachana na hayo bado tuna Baraza la Mawaziri kubwa sana na sana limekaa kimchongo sana.
Tanzania tuna Baraza kubwa sana la Mawaziri nazani kiliko hata Kenya ilivyo, na baadhi ya wizara zimekaa kimchongo hazina maana yoyote ile zaidi ya kuongeza mzigo kwa wananchi.
Huku tunahimizwa sana hata na mwigulu tulipe Kodi, Ila tusicho kijua hio kodi inatumika kugharamikia anasa za Watawala wa hili Taifa, huku wananchi wakiendelea kuwa masikini.
Na Watawala hawako tayari kupunguza Mzigo wa Baraza la mawaziri kwa sababu limekaa kisiasa hasa kulipana fadhila.
Umechambua vizuri sana, tuna utitiri wa viongozi ambao hawahitajiki na wanafanya kazi mojaKwa mtazamo wako. Ila mimi naamini tukitaka kupunguza ile 60% ya bajeti ambayo inaenda kwenye utawala yaani matumizi ya kawaida basi tunatakiwa kukubaliana kwamba
Mbunge
Mkuu wa wilaya
Mkurugenzi
DAS
Wanafanya kazi moja. Kundi hili inabidi liwe na mtu mmoja tu ambaye hata akitumia Landcruser 300 inakuwa moja tu.
Pale mkoani Kuna
Mkuu wa mkoa
RAS
Na wakuu wa idara
Elimu
Uchumi
Afya
Na wengine ambao bao pia wana wasaidiza wao na staff wanne watano hivi. Hii yote inachangia matumizi kuwa makubwa kuliko kuleta maendeleo.
Hao viti maalumu ndio kabisa hawataki WI kuwepo. Maana kuna
Viti maalumu hawa toka chamani
Wabunge wa kuteuliwa na Rais.
TUJISAHIHISHE.
Khamis yupi???Na Khamis anaombewa na mchungaji huko arudishwe wizara ya mali asili sasa hayo maombi sijui yatakuaje " Baba mtoe aliyepo muweke Khamis babaaa"