Tanzania isiwe na vazi moja tu la Taifa, tuwe na mavazi rasmi matano kutoka katika makabila yetu

Tanzania isiwe na vazi moja tu la Taifa, tuwe na mavazi rasmi matano kutoka katika makabila yetu

Mambo vp jamiiforums.

Ninashauri sana nchi yetu ya Tanzania isiwe na vazi moja tu la taifa. Tuwe na mavazi rasmi matano (5) kutoka katika makabila yetu yatakayorasimishwa na kupewa hadhi ya utaifa. Yaaani kama inawezekana mpangilio uwe hivi au hata kama kura ya maoni inaweza kupigwa itakuwa sawa tu.

Picha hapo chini ni Rais Mstaafu wa awamu ya nne mzee Kikwete na mkewe Mama Salma wakiwa wamependeza vizuri kabisa katika mavazi ya kabila ya Waha (baba) pamoja na Maasai (Mama)

View attachment 1718602

(1) Kaskazini - Vazi la kimaasai (Mkoa Arusha)

(2) Kusini - Vazi la Kimakonde (Mkoa Mtwara)

(3) Mashariki - Vazi la Kisambaa (Mkoa Tanga)

(4) Magharibi - Vazi la Waha (Mkoa Kigoma)

(5) Kanda ya kati - Vazi la wagogo (Mkoa Dodoma)

Nchini Afrika ya kusini wamefanya hili kwa upande wa lugha rasmi za taifa, ila sisi tunaweza kufanya hivi hivi kwa upande wa vazi rasmi la taifa.

Kwa uhalisia tu ni kwamba, huko nchini Afrika ya Kusini kuna makabila mengi sana yaliyopo katika majimbo tofauti tofauti na matokeo yake lugha zinatawala katika majimbo yao husika ambayo inafanya kuwa lugha mahususi haswa kwa eneo/mkoa husika.

Takribani lugha thelathini na tano (35) zenye asili ya Afrika Kusini huzungumzwa katika nchi hiyo, kumi kati ya hizo ni lugha rasmi za taifa la Afrika Kusini: Ndebele, Pedi, Sotho, Swati, Tsonga, Tswana, Venda, Xhosa, Zulu na Afrikaans.

Lugha rasmi ya kumi na moja ni Kiingereza, ambayo ndiyo lugha ya msingi inayotumiwa katika mazungumzo ya kibunge na kiserikali, ingawa lugha zote rasmi zina uzito sawa katika hadhi ya kisheria na katika ya nchi hiyo.

Kama katika lugha 35 kutoka nchi nzima waliweza kuchagua lugha 11 tu kutambulika kama "official languages" na Tanzania yenye makabila takribani 120 pia inaweza kuchagua mavazi kutoka makabila 5 tu kuwa ndio mavazi rasmi ya taifa ili tumalizane na hili suala kwa maana tangia lianze kujadiliwa ni zaidi ya miaka 15 sasa na bado sijaona solution ya maana mpaka sasa.

Zamani ilikuwa ni Dar es Salaam kwa kabila la wazaramo ila sasa ni Dodoma kwa wagogo ndipo kumepewa hadhi ya makao makuu ya nchi na serikali. Kama mkoa wa Dodoma umeweza kupewa hadhi hiyo na kuacha mikoa mingine, kwanini makabila matano niliyoyaorodhesha hapo juu yasiwakilishe mavazi rasmi ya taifa?

Soma pia>>> Kwanini mitaa ambamo kuna Balozi za nchi tano zenye nguvu duniani isiitwe majina ya vivutio vya utalii vya Tanzania?

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Karne hii ya leo unawaza vazi la kitaifa? Ili iweje? Watu tunahitaji maendeleo hatuhitaji mavazi ya kitaifa ili hali matumbo ya njaa, kila utamaduni umeachwa ukisema hauna maana, leo hii nyumba unayoishi unaishi na kinyesi humo humo ukiita self contained, watoto wako au wadogo zako wanasoma shule kwa lugha ya kiingereza si ungewafundisha lugha ya kabila yako tukuone wewe kweli unajali utaifa wako.
Haya mambo yalishindikana enzi za myerere alipokuja na maduka ya ujamaa, vijiji vya ujamaa nk, hakuna namna utaforce watu wafanane.
 
Ni ngumu kwa tanzania kutambulika kwa vazi rasmi la Asili sababu ya diversity ya mila na tamaduni zetu..makabila yetu mengi asili zao ni za kihamiaji


Nchi ambazo wanatambulika kwa mavazi yao ya Asili utakuta makabila yao machache yameingiliana had lugha yanafana

mfano Burundi na Rwanda watutsi na wahutu ni makabila yanayofautiana kdg kidesturi ila ila
lugha moja tamaduni kias kikubwa zinafanana hadi mavazi.. ndo maana ni rahis kurasimisha

same kwa ethiopia. wanaijeria na wengine hadi west africa.. angalia mavaz ya kiwest africa.. mtu wa senegal, Cameroon .. ghana. na kwingine mavaz yanafanana maana nao wameingiliana makabila. yako machache lakini yameingiliana

sasa sie makabila yetu kiasili yameshabihiana na makabila na tamaduni za watu wa inchi zingine maana kiasili makabila mengi hapa wahamiaji..

mmakonde kahamia, huko kaskazin ndo yale yale
wachaga na wamburu plus wamasai.. hapo kati wasandawe, wabarbaig wagogo hawana tofauti na watu wa jangwa la namibia na zimbabwe. warangi hawana tofauti na waethiopia

usishangae ukivaa kama mgogo watu wa west africa au ulaya wakahisi umevaa kama watu wa wa Namibia na zimbabwe.. maana wao kule watu wao wabush kwa ujumla wao ndo vazi lao na wanajulikana dunian utaonekana umeiga

ukivaaa kama lubega ya shuka jeupe kama wahaya aidha upelekwe Rwanda , au uganda

kimasai.. tumeingiliana na Kenya so huwezi kuliita vazi asili la tanzania

sie tamaduni na desturi tunashea na watu wa nchi zingine .. so hatuwez tambulika kwa vazi maana makabila yetu kiasili ni wahamiaji tu hapa
 
Ni ngumu kwa tanzania kutambulika kwa vazi rasmi la Asili sababu ya diversity ya mila na tamaduni zetu..makabila yetu mengi asili zao ni za kihamiaji
Ila kumbuka nchi ya South Africa imefanikiwa katika kurasimisha lugha
 
Nchi ambazo wanatambulika kwa mavazi yao ya Asili utakuta makabila yao machache yameingiliana had lugha yanafana

mfano Burundi na Rwanda watutsi na wahutu ni makabila yanayofautiana kdg kidesturi ila ila
lugha moja tamaduni kias kikubwa zinafanana hadi mavazi.. ndo maana ni rahis kurasimisha

same kwa ethiopia. wanaijeria na wengine hadi west africa.. angalia mavaz ya kiwest africa.. mtu wa senegal, Cameroon .. ghana. na kwingine mavaz yanafanana maana nao wameingiliana makabila. yako machache lakini yameingiliana
Hii nimeipenda sana mkuu. Asante kwa kunipa somo zuri.
 
usishangae ukivaa kama mgogo watu wa west africa au ulaya wakahisi umevaa kama watu wa wa Namibia na zimbabwe
Wakihisi ndio tunawapa ufafanuzi kuwa hili ni vazi la Tanzania.

Alafu kwanini wahisi umevaa kama Namibia? Kwanini akivaa mtu wa Namibia wasihisi amevaa kama mtanzania?
 
ukivaaa kama lubega ya shuka jeupe kama wahaya aidha upelekwe Rwanda , au uganda

kimasai.. tumeingiliana na Kenya so huwezi kuliita vazi asili la tanzania

sie tamaduni na desturi tunashea na watu wa nchi zingine .. so hatuwez tambulika kwa vazi maana makabila yetu kiasili ni wahamiaji tu hapa
Kwanini lubega na mavazi ya kimasai yatambulike kuwa ni ya nchi zingine na sio Tanzania? Kwani ni nani amekwambia dunia nzima wanajua wamasai wapo Kenya pekee?
 
Kwani ni nani amekuforce ufanane na mwingine?
Jiulize kwanza ikiwa haukutaji watu wa kufanana na wewe kwa nini usishone la kwako ukavaa?
Ila kumbuka nchi ya South Africa imefanikiwa katika kurasimisha lugha
Kwa hiyo umetoka kwenye vazi umeenda kwenye lugha, na mbona tanzania imerasimisha kiswahili unahitaji lugha gani? ni kijiji gani Tanzania utaenda uongee kiswahili watu washindwe kukuelewa?
 
Wakihisi ndio tunawapa ufafanuzi kuwa hili ni vazi la Tanzania.

Alafu kwanini wahisi umevaa kama Namibia? Kwanini akivaa mtu wa Namibia wasihisi amevaa kama mtanzania?


simple jamii yao kule ni famous tayari.. ni kama vile huko ghana kuibuke kabila wanavaa kama
wamasai.. we unafikir ukiona picha utajuankama ni kabila la ghana.. hapana utajua ni mmasai wa east africa sababu tayar vazi wamasai kwa wingi wao wameshalitawala hilo vazi..

so hata kama kuna kabila dunian wanavaa kama hivyo inabid mvaaji awe anatoa maelezo yanziada vinginevyo anatupwa east africa

so kwa makabila yetu toka enzi na enzi hatujawa popular kwenye mavaz ya asili dunian isipokuwa
wamasai sasa ukianza leo itabid uanze kutoa maelezo ya ziada tena ili wayashike hayo maelezo inabid ufanye kitu unique

masai life style yao ya kuhama hama ni kama
jamii zingine ila ile ya wao kuishi na mavaz yao na silaha popote alipo hata town ndio imefanya vaz likawa famous

wengine sie wagogo au wahaya akija town anatupa lubega anaingia mjini sarawili

halafu pia tunataka dunia itutambue kwa mavaz asili vaz wakat humu ndan wenyewe inatupa shida kujua kabila gani vaz lake la asili ni lipi.
 
Back
Top Bottom