SoC02 Tanzania iwe na Vyama vya Siasa vichache ili kuimarisha Taifa

SoC02 Tanzania iwe na Vyama vya Siasa vichache ili kuimarisha Taifa

Stories of Change - 2022 Competition

Manventure

Member
Joined
Jul 16, 2021
Posts
10
Reaction score
4
TANZANIA IWE NA VYAMA VYA SIASA VICHACHE ILI KUIMARISHA TAIFA.​

Mfumo wa vyama vingi vya siasa unaboresha demokrasia ya nchi kwa kuifanya Serikali chini ya chama tawala iliyopo madarakani kutimiza majukumu kwa ufasaha na uangalizi zaidi. Nchini Tanzania mfumo wa vyama vingi vya siasa ulianza mwaka 1992, ambapo kabla ilikuwa ni chama kimoja yaani Chama Cha Mapinduzi (CCM). Mpaka sasa Tanzania kuna vyama vya siasa zaidi ya ishirini. Na kila uchaguzi mkuu Serikali hutenga ruzuku kwa ajili ya vyama vitakavyo shiriki shughuli nzima ya uchaguzi.

Tukiangazia kazi kuu za vyama vya siasa ni pamoja na;

1. Kushawishi watu kushiriki shughuli za maendeleo.

2. Kutoa na kupitisha wagombea wa nafasi mbalimbali wakati wa uchaguzi. Viongozi ambao wataitumikia Serikali na wananchi wake.

3. Kutoa elimu ya siasa, demokrasia na umoja kwa taifa.

4. Kuikosoa na kutoa mapendekezo kwa chama tawala. Katika utendaji chama tawala kitapokosea vyama pinzani vina haki ya kukosoa chama tawala.


Maoni yangu mfumo wa vyama vingi hamna ulazima wa kuwa na idadi kubwa ya vyama. Hata kuwa na vyama viwili hata vinne bado itafahamika kama mfumo wa vyama vingi. Tanzania inaweza kubaki na vyama vichache vitavyoleta ushindani kweli na kupunguza gharama nyingi kwa Serikali, wanachama na wananchi kiujumla.

Tanzania kama taifa linalozidi kukua siku hata siku linatakiwa kuwa na vyama vya siasa chini ya kumi, hata ikiwa vitano tu vinatosha pia. Haya ni maoni yangu tu.


FAIDA YA KUWA NA VYAMA VICHACHE VYA SIASA.

1. Gharama za uendeshaji wakati wa uchaguzi zinapungua.

Serikali hutenga ruzuku kwa kila chama kinachoshiriki uchaguzi mkuu. Mfano, uchaguzi mkuu mwaka 2020 CCM ilipata Tsh bilioni 1.33, CHADEMA Tsh milioni 109.68, ACT-Wazalendo Tsh milioni 14, CUF Tsh milioni 5.7, NCCR-Mageuzi Tsh 316,937. Democratic Party Tsh 63,387.
Mfano tungekuwa na vyama viwili fedha takribani milioni 40 zingetumika kwenye shughuli nyingine. Kwa kuwa Tanzania hatujafikia mafanikio makubwa, tunapaswa kupunguza gharama ili kuendana na hali ya taifa kiuchumi. Njia mojawapo ni kuwa na vyama vya siasa vichache.

2. Taifa linakuwa na sera chache ambazo hazitoleta mkanganyiko kwa wananchi.

Mfano kuwa na vyama zaidi ya ishirini ina maana kila chama kina sera zake kwa wananchi. Wengine wanaweza kuwa na sera za viwanda zaidi, wengine kilimo, wengine utalii, wengine usawa kijinsia na mifano mingi zaidi. Sasa ni mwananchi gani anaweza kufuata sera zaidi ya ishirini ili kuwa mzalendo wa taifa. Lakini kama tukiwa na vyama viwili, vitatu hata vitano ni rahisi mwananchi kuchagua aegemee upande gani ambao utakuwa mtetezi kwake na kuchangia maendeleo yake na taifa zima.

3. Vinapunguza mgawanyiko ndani ya jamii na kuongeza umoja.

Ijapokuwa wengine husema vyama vichache huzalisha makundi machache yenye nguvu zaidi kuliko vyama vingi ambavyo kunakuwa na vikundi vidogo vidogo vingi. Lakini ni rahisi sana kushawishi na kuyaunganisha makundi machache kuchapa kazi kama vile ujenzi wa shule au hospitali. Vikundi vingi na vidogo vidogo ni kazi kwa sababu hadi kuunganisha nguvu kazi inachukua muda mrefu. Vivyo hivyo hata katika siasa kuwa na vyama vya siasa vichache ni rahisi sana kutekeleza sera na mipango ya nchi kuliko vyama vingi ambavyo inachukua muda mrefu kwa sera na mipango kukubaliwa au kuafikiwa na kila mmoja.

4. Ni ishara ya umoja ndani ya jamii.

Vyama vichache vinaashilia watu wake wameridhia na kukubali uwepo wa hivyo vyama pekee. Hivyo watu wake watapendana, pale serikali itapokosea itaweza kukosolewa kwa urahisi zaidi. Lakini vyama kuwa vingi inaweza kuwa ishara ya makundi kadhaa kutoelewana katika jamii na kupelekea kujitenga na kutengeneza chama au kundi jingine. Mtazamo ni kama Taifa tutakuwa na vyama vya siasa vichache pia umoja utakuwa imara zaidi kwa sababu hakuna atayejitenga au kuunda taifa lake. Kila jamii ina kasoro ila ni muhimu kufanyia kazi kasoro hizo.

Maoni.
Yapo mataifa mengi duniani ambayo yanatumia mfumo wa demokrasia pamoja na kuwa na vyama vya siasa vichache. Mfano mzuri ni baba wa demokrasia yaani Marekani kuna vyama vikuu viwili ngazi ya taifa. Mataifa mengine ni pamoja na;

Ujerumani – vyama vikuu viwili (2), vyama vidogo vitatu (3).
Australia – vyama vya siasa vitatu (3).
China – chama tawala cha CPC pamoja na vyama vingine nane (8).

Vivyo hivyo Tanzania tunaweza kuwa na vyama vya siasa vichache na bado taifa likatambullika kama mfuasi wa mfumo wa vyama vingi vya siasa.


Marejeo

https://www.orpp.go.tz/pages-subvention

https://www.bbc.com/habari-59567666
 
Upvote 2
TANZANIA TUNAHITAJI VYAMA VIWILI ILI KULETA MAENDELEO KUPITIA SIASA SAFI NA SHINDANI.
Tangu mfumo wa vyama vingi uanze kutumika hapa nchini imepita miaka mingi lakini mpaka sasa ni chama kimoja kimetawala miaka yote ya uchaguzi tangu mfumo wa vyama vingi uanze kutumika. Nitakuwa sahii nikisema hakuna umuhimu "mkubwa" uliotokana na uwepo wa vyama vingi. Nimetumia neno mkubwa ili kuutambua umuhimu mdogo unaohitaji tochi kuumulika kwani Lengo kuu la kuanzisha chama chochote cha siasa ni kuchukua dola. Hivyo mpaka sasa lengo hili limefanikiwa kwa chama kimoja tu ambacho kipo madarakani hivyo umuhimu mdogo wa vyama vingine umekuwa ni kukokosoa mtawala japo na penyewe ni kwa ufinyu sana. Hakuna ushindani wa kiutendaji kupitia ubadilishanaji wa madaraka.

Kisababishi kinachovinyima nguvu vyama vingine ya kuchukua dola ni kukosekana kwa nguvu ya pamoja/ upinzani imara kwa kuzigawa kura zao kupitia vyama vyao na kumwachia nguvu kubwa ya watu mtawala aliyoitengeneza kutoka vizazi hadi vizazi na kukosesha mabadiliko ya kushindanisha maendeleo yanayohitajika.
HITIMISHO.

"Yaani tuwe na chama kimoja pinzani chenye nguvu ya kukipa joto chama tawala kwa kubadilishana nafasi ya kiti cha urasi ili hoja ya kushindanisha maendeleo kupitia hizi pande mbili iwape nafasi wananchi katika kungamua ni yupi ni bora kuliko mwingine ili kumpa ridhaa ya kuongoza kutokana maendeleo yatakayopatikana kupitia pande hizi mbili".
"Mtawala akiboronga mpinzani ampiku ili ajiandae kurekebisha makosa yake huku akimfanya mpinzani aendelee kufanya mazuri yatakayomfanya alinde nafasi aliyonayo.
TANZANIA IWE NA VYAMA VYA SIASA VICHACHE ILI KUIMARISHA TAIFA.​

Mfumo wa vyama vingi vya siasa unaboresha demokrasia ya nchi kwa kuifanya Serikali chini ya chama tawala iliyopo madarakani kutimiza majukumu kwa ufasaha na uangalizi zaidi. Nchini Tanzania mfumo wa vyama vingi vya siasa ulianza mwaka 1992, ambapo kabla ilikuwa ni chama kimoja yaani Chama Cha Mapinduzi (CCM). Mpaka sasa Tanzania kuna vyama vya siasa zaidi ya ishirini. Na kila uchaguzi mkuu Serikali hutenga ruzuku kwa ajili ya vyama vitakavyo shiriki shughuli nzima ya uchaguzi.

Tukiangazia kazi kuu za vyama vya siasa ni pamoja na;

1. Kushawishi watu kushiriki shughuli za maendeleo.

2. Kutoa na kupitisha wagombea wa nafasi mbalimbali wakati wa uchaguzi. Viongozi ambao wataitumikia Serikali na wananchi wake.

3. Kutoa elimu ya siasa, demokrasia na umoja kwa taifa.

4. Kuikosoa na kutoa mapendekezo kwa chama tawala. Katika utendaji chama tawala kitapokosea vyama pinzani vina haki ya kukosoa chama tawala.


Maoni yangu mfumo wa vyama vingi hamna ulazima wa kuwa na idadi kubwa ya vyama. Hata kuwa na vyama viwili hata vinne bado itafahamika kama mfumo wa vyama vingi. Tanzania inaweza kubaki na vyama vichache vitavyoleta ushindani kweli na kupunguza gharama nyingi kwa Serikali, wanachama na wananchi kiujumla.

Tanzania kama taifa linalozidi kukua siku hata siku linatakiwa kuwa na vyama vya siasa chini ya kumi, hata ikiwa vitano tu vinatosha pia. Haya ni maoni yangu tu.


FAIDA YA KUWA NA VYAMA VICHACHE VYA SIASA.

1. Gharama za uendeshaji wakati wa uchaguzi zinapungua.

Serikali hutenga ruzuku kwa kila chama kinachoshiriki uchaguzi mkuu. Mfano, uchaguzi mkuu mwaka 2020 CCM ilipata Tsh bilioni 1.33, CHADEMA Tsh milioni 109.68, ACT-Wazalendo Tsh milioni 14, CUF Tsh milioni 5.7, NCCR-Mageuzi Tsh 316,937. Democratic Party Tsh 63,387.
Mfano tungekuwa na vyama viwili fedha takribani milioni 40 zingetumika kwenye shughuli nyingine. Kwa kuwa Tanzania hatujafikia mafanikio makubwa, tunapaswa kupunguza gharama ili kuendana na hali ya taifa kiuchumi. Njia mojawapo ni kuwa na vyama vya siasa vichache.

2. Taifa linakuwa na sera chache ambazo hazitoleta mkanganyiko kwa wananchi.

Mfano kuwa na vyama zaidi ya ishirini ina maana kila chama kina sera zake kwa wananchi. Wengine wanaweza kuwa na sera za viwanda zaidi, wengine kilimo, wengine utalii, wengine usawa kijinsia na mifano mingi zaidi. Sasa ni mwananchi gani anaweza kufuata sera zaidi ya ishirini ili kuwa mzalendo wa taifa. Lakini kama tukiwa na vyama viwili, vitatu hata vitano ni rahisi mwananchi kuchagua aegemee upande gani ambao utakuwa mtetezi kwake na kuchangia maendeleo yake na taifa zima.

3. Vinapunguza mgawanyiko ndani ya jamii na kuongeza umoja.

Ijapokuwa wengine husema vyama vichache huzalisha makundi machache yenye nguvu zaidi kuliko vyama vingi ambavyo kunakuwa na vikundi vidogo vidogo vingi. Lakini ni rahisi sana kushawishi na kuyaunganisha makundi machache kuchapa kazi kama vile ujenzi wa shule au hospitali. Vikundi vingi na vidogo vidogo ni kazi kwa sababu hadi kuunganisha nguvu kazi inachukua muda mrefu. Vivyo hivyo hata katika siasa kuwa na vyama vya siasa vichache ni rahisi sana kutekeleza sera na mipango ya nchi kuliko vyama vingi ambavyo inachukua muda mrefu kwa sera na mipango kukubaliwa au kuafikiwa na kila mmoja.

4. Ni ishara ya umoja ndani ya jamii.

Vyama vichache vinaashilia watu wake wameridhia na kukubali uwepo wa hivyo vyama pekee. Hivyo watu wake watapendana, pale serikali itapokosea itaweza kukosolewa kwa urahisi zaidi. Lakini vyama kuwa vingi inaweza kuwa ishara ya makundi kadhaa kutoelewana katika jamii na kupelekea kujitenga na kutengeneza chama au kundi jingine. Mtazamo ni kama Taifa tutakuwa na vyama vya siasa vichache pia umoja utakuwa imara zaidi kwa sababu hakuna atayejitenga au kuunda taifa lake. Kila jamii ina kasoro ila ni muhimu kufanyia kazi kasoro hizo.

Maoni.
Yapo mataifa mengi duniani ambayo yanatumia mfumo wa demokrasia pamoja na kuwa na vyama vya siasa vichache. Mfano mzuri ni baba wa demokrasia yaani Marekani kuna vyama vikuu viwili ngazi ya taifa. Mataifa mengine ni pamoja na;

Ujerumani – vyama vikuu viwili (2), vyama vidogo vitatu (3).
Australia – vyama vya siasa vitatu (3).
China – chama tawala cha CPC pamoja na vyama vingine nane (8).

Vivyo hivyo Tanzania tunaweza kuwa na vyama vya siasa vichache na bado taifa likatambullika kama mfuasi wa mfumo wa vyama vingi vya siasa.


Marejeo

https://www.orpp.go.tz/pages-subvention

https://www.bbc.com/habari-59567666
 
Unaonaja kuwa na pande mbili yaani vyama viwili
1. Chama Tawala
2. Chama Pinzani
Uliloondika ni jambo jema huu utitiri wa vyama vya siasa na unazidi kuonhezeka. Kama taifa kwa ujumla kamaslahi ya kodi zetu walifikirie na hili tuwe na vyama viwili tu vya siasa kilicho na madarakani na kingine kijumuishe vyama vya upinzani vyoote
 
Nimekupigia kura ya 2 japo muda umeisha. Na vipi hawajatoa matokeo ya washindi wa hili shindano 2022.?
 
Uliloondika ni jambo jema huu utitiri wa vyama vya siasa na unazidi kuonhezeka. Kama taifa kwa ujumla kamaslahi ya kodi zetu walifikirie na hili tuwe na vyama viwili tu vya siasa kilicho na madarakani na kingine kijumuishe vyama vya upinzani vyoote
"Ni hakika"
Mtawala akibweteka mpinzani ampiku huku mtawala akijiuliza alipofeli ili aweze kujiandaa tena kwa kuwaweka watu makini
Pili hoja iwe kushîndanisha maendeleo.
Mtawala aseme mimi ndani ya miaka mitano nimefanya mambo kadhaa.
Huku mpinzani hakisema mimi nilifanya kadhaa na nitafanya kadhaa, huku atakayeshindwa kutekeleza alichoahidi kiwe kigezo mojawapo cha kumtoa madarakani kupitia kura ya mwananchi.
Pili itasaidiaa katika ukweli na uwazi kama vile makusanyo ya kodi na matumizi kwani kila upande utaweka wazi kiasi kilichokutwa na jinsi kilivyotumika.
 
Unaonaja kuwa na pande mbili yaani vyama viwili
1. Chama Tawala
2. Chama Pinzani
Ni nzuri zaidi sema kwa desturi ya bara letu itakuwa ngumu kupata viongozi wenye weledi kwa wingi kutokana na ufinyu wa nafasi zitazokuwepo.
Sema hii ya vyama vingi then bajeti tusubiri wadhamini inatudumaza
 
Ni nzuri zaidi sema kwa desturi ya bara letu itakuwa ngumu kupata viongozi wenye weledi kwa wingi kutokana na ufinyu wa nafasi zitazokuwepo.
Sema hii ya vyama vingi then bajeti tusubiri wadhamini inatudumaza
Kuhusu nafasi sina shaka nalo kwa upande wangu kwa sababu ya vigezo vifuatavyo:
Ushindani unaangaliwa kupitia nafasi zilizopo kama vile idadi ya majimbo ili kupata wabunge. nk na sio idadi ya vyama.

Pili kuna nafasi za kutopigiwa kula, jambo la kumteua mtu kupitia ufanisi wake kutawakuza wengine watakao kuwa wanamwangalia mtu wao wa mfano.
Hivyo hali ya weledi itakuwa katika hali ya juu.

Pia hizo nafasi nyingi unazohofia kupotezwa zinaweza kuwa ndani ya chama kimoja na cha upande wa pili, ili kumpata mtu mahiri kutoka katika hao walio wengi. Huku hao waliowengi waliobaki wakiendelea kukuza chama chao na kukijinge na kuwazia mbinu sahii za kuyafikia maendeleo hitajika.
 
Utitiri wa vyama unasababisha watu watumie nguvu kubwa katika kuviimarisha vyama vyao kuliko kutumia nguvu hiyo kubwa katika kuwaza ni jinsi gani ya kumkomboa mwananchi waliyemwomba ridhaa ya kumwakilisha na kumpatia maendeleo kupitia huduma za kijamii na kumrahisishia upatikanaji wa mahitaji yake ya msingi.
 
TANZANIA IWE NA VYAMA VYA SIASA VICHACHE ILI KUIMARISHA TAIFA.​

Mfumo wa vyama vingi vya siasa unaboresha demokrasia ya nchi kwa kuifanya Serikali chini ya chama tawala iliyopo madarakani kutimiza majukumu kwa ufasaha na uangalizi zaidi. Nchini Tanzania mfumo wa vyama vingi vya siasa ulianza mwaka 1992, ambapo kabla ilikuwa ni chama kimoja yaani Chama Cha Mapinduzi (CCM). Mpaka sasa Tanzania kuna vyama vya siasa zaidi ya ishirini. Na kila uchaguzi mkuu Serikali hutenga ruzuku kwa ajili ya vyama vitakavyo shiriki shughuli nzima ya uchaguzi.

Tukiangazia kazi kuu za vyama vya siasa ni pamoja na;

1. Kushawishi watu kushiriki shughuli za maendeleo.

2. Kutoa na kupitisha wagombea wa nafasi mbalimbali wakati wa uchaguzi. Viongozi ambao wataitumikia Serikali na wananchi wake.

3. Kutoa elimu ya siasa, demokrasia na umoja kwa taifa.

4. Kuikosoa na kutoa mapendekezo kwa chama tawala. Katika utendaji chama tawala kitapokosea vyama pinzani vina haki ya kukosoa chama tawala.


Maoni yangu mfumo wa vyama vingi hamna ulazima wa kuwa na idadi kubwa ya vyama. Hata kuwa na vyama viwili hata vinne bado itafahamika kama mfumo wa vyama vingi. Tanzania inaweza kubaki na vyama vichache vitavyoleta ushindani kweli na kupunguza gharama nyingi kwa Serikali, wanachama na wananchi kiujumla.

Tanzania kama taifa linalozidi kukua siku hata siku linatakiwa kuwa na vyama vya siasa chini ya kumi, hata ikiwa vitano tu vinatosha pia. Haya ni maoni yangu tu.


FAIDA YA KUWA NA VYAMA VICHACHE VYA SIASA.

1. Gharama za uendeshaji wakati wa uchaguzi zinapungua.

Serikali hutenga ruzuku kwa kila chama kinachoshiriki uchaguzi mkuu. Mfano, uchaguzi mkuu mwaka 2020 CCM ilipata Tsh bilioni 1.33, CHADEMA Tsh milioni 109.68, ACT-Wazalendo Tsh milioni 14, CUF Tsh milioni 5.7, NCCR-Mageuzi Tsh 316,937. Democratic Party Tsh 63,387.
Mfano tungekuwa na vyama viwili fedha takribani milioni 40 zingetumika kwenye shughuli nyingine. Kwa kuwa Tanzania hatujafikia mafanikio makubwa, tunapaswa kupunguza gharama ili kuendana na hali ya taifa kiuchumi. Njia mojawapo ni kuwa na vyama vya siasa vichache.

2. Taifa linakuwa na sera chache ambazo hazitoleta mkanganyiko kwa wananchi.

Mfano kuwa na vyama zaidi ya ishirini ina maana kila chama kina sera zake kwa wananchi. Wengine wanaweza kuwa na sera za viwanda zaidi, wengine kilimo, wengine utalii, wengine usawa kijinsia na mifano mingi zaidi. Sasa ni mwananchi gani anaweza kufuata sera zaidi ya ishirini ili kuwa mzalendo wa taifa. Lakini kama tukiwa na vyama viwili, vitatu hata vitano ni rahisi mwananchi kuchagua aegemee upande gani ambao utakuwa mtetezi kwake na kuchangia maendeleo yake na taifa zima.

3. Vinapunguza mgawanyiko ndani ya jamii na kuongeza umoja.

Ijapokuwa wengine husema vyama vichache huzalisha makundi machache yenye nguvu zaidi kuliko vyama vingi ambavyo kunakuwa na vikundi vidogo vidogo vingi. Lakini ni rahisi sana kushawishi na kuyaunganisha makundi machache kuchapa kazi kama vile ujenzi wa shule au hospitali. Vikundi vingi na vidogo vidogo ni kazi kwa sababu hadi kuunganisha nguvu kazi inachukua muda mrefu. Vivyo hivyo hata katika siasa kuwa na vyama vya siasa vichache ni rahisi sana kutekeleza sera na mipango ya nchi kuliko vyama vingi ambavyo inachukua muda mrefu kwa sera na mipango kukubaliwa au kuafikiwa na kila mmoja.

4. Ni ishara ya umoja ndani ya jamii.

Vyama vichache vinaashilia watu wake wameridhia na kukubali uwepo wa hivyo vyama pekee. Hivyo watu wake watapendana, pale serikali itapokosea itaweza kukosolewa kwa urahisi zaidi. Lakini vyama kuwa vingi inaweza kuwa ishara ya makundi kadhaa kutoelewana katika jamii na kupelekea kujitenga na kutengeneza chama au kundi jingine. Mtazamo ni kama Taifa tutakuwa na vyama vya siasa vichache pia umoja utakuwa imara zaidi kwa sababu hakuna atayejitenga au kuunda taifa lake. Kila jamii ina kasoro ila ni muhimu kufanyia kazi kasoro hizo.

Maoni.
Yapo mataifa mengi duniani ambayo yanatumia mfumo wa demokrasia pamoja na kuwa na vyama vya siasa vichache. Mfano mzuri ni baba wa demokrasia yaani Marekani kuna vyama vikuu viwili ngazi ya taifa. Mataifa mengine ni pamoja na;

Ujerumani – vyama vikuu viwili (2), vyama vidogo vitatu (3).
Australia – vyama vya siasa vitatu (3).
China – chama tawala cha CPC pamoja na vyama vingine nane (8).

Vivyo hivyo Tanzania tunaweza kuwa na vyama vya siasa vichache na bado taifa likatambullika kama mfuasi wa mfumo wa vyama vingi vya siasa.


Marejeo

https://www.orpp.go.tz/pages-subvention

https://www.bbc.com/habari-59567666
CHAMA CHA UPINZANI KIMOJA TU HIVYO VINGINE 14 NA VYAMA TANZU NA CCM
 
Utitiri wa vyama unasababisha watu watumie nguvu kubwa katika kuviimarisha vyama vyao kuliko kutumia nguvu hiyo kubwa katika kuwaza ni jinsi gani ya kumkomboa mwananchi waliyemwomba ridhaa ya kumwakilisha na kumpatia maendeleo kupitia huduma za kijamii na kumrahisishia upatikanaji wa mahitaji yake ya msingi.
It's real a fact. Ni sahihi usemalo.
 
Hakuna chama cha siasa hata kimoja vyote ni vikundi vya wahuni, walafi na wanafki
 
Back
Top Bottom