Tanzania kuanza kununua umeme kutoka Ethiopia

Tanzania kuanza kununua umeme kutoka Ethiopia

Tanzania inalenga kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme nchini kufuatia mpango wa kuanza kununua nishati hiyo kutoka Ethiopia.

Tayari mamlaka za nishati kutoka nchi hizo mbili zipo kwenye meza ya majadiliano kukubaliana kuhusu vifungu, vigezo na masharti ya makubaliana hayo ya miaka 20.

Katika makubaliano hayo, shirika la umeme la Ethiopia litakuwa linaiuzia Tanzania nishati ya umeme, kupitia shirika la TANESCO.

Soma:
Kwa kuanzia, Tanzania inalenga kununua Megawati 100 za umeme kutoka Ethiopia, baada ya kukamiliaka kwa majadiliano ya awali.

"Lengo la mpango huu ni kuunganisha mradi wa umeme wa Afrika Mashariki na ule wa Kusini mwa Afrika, ambapo Tanzania itakuwa katikati ya miradi hiyo miwili. Kukamilika kwa huu mpango kutafanikisha kuuziana umeme kati ya nchi za Afrika Mashariki na zile za Kusini mwa Afrika." anaeleza Mhandisi Innocent Luoga, Kamishna wa Umeme wa Nishati Jadilifu, kutoka wizara ya nishati nchini Tanzania.

"Mambo yote hayo yapo kwenye hatua za majadiliano ambayo hujulikana kitapları kama "Wheeling Charges Agreement." amesisitiza Luoga.

Kulingana na kamishna huyo, mkubaliano yakikamilika, Ethiopia itaanza kuiuzia umeme Tanzania.

Kupitia mradi huo pia Tanzania itakuwa imejitosheleza katika nishati ya umeme na hivyo kuwa na uwezo wa kuiuzia tena Ethiopia au nchi yoyote katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Chanzo TRT Afrika
Wiki iliyopita Biteko alisikika akisema tuna ziada ya megawatt 400, sasa mnatuambia kuwa tutanunua megawatt 100, hivi mnataka tuelewe lipi?!
 
Tanzania inalenga kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme nchini kufuatia mpango wa kuanza kununua nishati hiyo kutoka Ethiopia.

Tayari mamlaka za nishati kutoka nchi hizo mbili zipo kwenue meza ya majadiliano kukubaliana kuhusu vifungu, vigezo na masharti ya makubaliana hayo ya miaka 20.

Katika makubaliano hayo, shirika la umeme la Ethiopia litakuwa linaiuzia Tanzania nishati ya umeme, kupitia shirika la TANESCO.

Soma:
Kwa kuanzia, Tanzania inalenga kununua Megawati 100 za umeme kutoka Ethiopia, baada ya kukamiliaka kwa majadiliano ya awali.

"Lengo la mpango huu ni kuunganisha mradi wa umeme wa Afrika Mashariki na ule wa Kusini mwa Afrika, ambapo Tanzania itakuwa katikati ya miradi hiyo miwili. Kukamilika kwa huu mpango kutafanikisha kuuziana umeme kati ya nchi za Afrika Mashariki na zile za Kusini mwa Afrika." anaeleza Mhandisi Innocent Luoga, Kamishna wa Umeme wa Nishati Jadilifu, kutoka wizara ya nishati nchini Tanzania.

"Mambo yote hayo yapo kwenye hatua za majadiliano ambayo hujulikana kitapları kama "Wheeling Charges Agreement." amesisitiza Luoga.

Kulingana na kamishna huyo, mkubaliano yakikamilika, Ethiopia itaanza kuiuzia umeme Tanzania.

Kupitia mradi huo pia Tanzania itakuwa imejitosheleza katika nishati ya umeme na hivyo kuwa na uwezo wa kuiuzia tena Ethiopia au nchi yoyote katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Chanzo TRT Afrika
Mbona ilisemekana bwawa la Nyerere litazalisha mpaka umeme wa ziada?
 
Ngoja nipite kimya maanake naweza kutukana nikamletea Max Melo matatizo ambayo sio yake wala yeye aliesababisha.
 
Labda anaeelewa atusaidie kufafanua maana nikama tunarudi rivasi
 
Serikali kama chombo !hakina Nia ya dhati ya kutatua changamoto za wananchi kama hili la umeme!

Haiwezekani miaka zaidi ya 40 tunahangaika na umeme TU,Bado afya,elimu mbovu isiyojiajiri n.k!
 
Walisema Sasa hivi umeme unaozalishwa ni mwingi kuliko matumizi,hivyo umeme mwingine utauzwa nje ya nchi ie,Malawi,Zambia,na Kenya,Sasa inakuaje Tena tununue umeme wakati sisi tunauza?
 
Walisema Sasa hivi umeme unaozalishwa ni mwingi kuliko matumizi,hivyo umeme mwingine utauzwa nje ya nchi ie,Malawi,Zambia,na Kenya,Sasa inakuaje Tena tununue umeme wakati sisi tunauza?
Na mimi nilisikia vivyo hivyo!
 
CCM ni majanga!

Ukiwa muongo , usiwe msahaulifu.
images (74).jpeg
 
Kwani ile mitambo yote Tisa haijakwisha kuwashwa...na sisi tuweze kuuza umeme nje ya nchi...?
 
Tuache tu. Hamna hata haja ya kujadili.
Cha muhimu ulipe kodi,pesa zikusanywe,ziende hazina,zichukuliwe na baadhi ya vuongozi wetu,wazitumie watakavyoona INAFAA.
Tuendelee kuhimizana kulipa kodi.
 
Back
Top Bottom