Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hahaha kabisa.Kama wao wanatuuzia na sisi tuwauzie wetu si tunaomwingi tu.
Alooooooh weeeeeh 🤔Shaghalabaghala! watu wanatafuta kula!
Ila hawa rahisi kuwamudu mkishindwana mkataba mnaanza kukamata wahamiaji haramu wa kihabeshi
watasanda.
Wiki iliyopita Biteko alisikika akisema tuna ziada ya megawatt 400, sasa mnatuambia kuwa tutanunua megawatt 100, hivi mnataka tuelewe lipi?!Tanzania inalenga kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme nchini kufuatia mpango wa kuanza kununua nishati hiyo kutoka Ethiopia.
Tayari mamlaka za nishati kutoka nchi hizo mbili zipo kwenye meza ya majadiliano kukubaliana kuhusu vifungu, vigezo na masharti ya makubaliana hayo ya miaka 20.
Katika makubaliano hayo, shirika la umeme la Ethiopia litakuwa linaiuzia Tanzania nishati ya umeme, kupitia shirika la TANESCO.
Soma:
Kwa kuanzia, Tanzania inalenga kununua Megawati 100 za umeme kutoka Ethiopia, baada ya kukamiliaka kwa majadiliano ya awali.
- Ahadi zilizowahi kutolewa na Viongozi kuhusu kuuza Umeme nje ya Nchi
- Mtambo wa pili bwawa la Nyerere kuwashwa, kumaliza kabisa mgao wa umeme nchini
- Waziri Biteko: Tanzania imejipanga vema kuhakikisha inatumia fursa ya uwepo wa soko la pamoja la EAPP la mauziano ya umeme
"Lengo la mpango huu ni kuunganisha mradi wa umeme wa Afrika Mashariki na ule wa Kusini mwa Afrika, ambapo Tanzania itakuwa katikati ya miradi hiyo miwili. Kukamilika kwa huu mpango kutafanikisha kuuziana umeme kati ya nchi za Afrika Mashariki na zile za Kusini mwa Afrika." anaeleza Mhandisi Innocent Luoga, Kamishna wa Umeme wa Nishati Jadilifu, kutoka wizara ya nishati nchini Tanzania.
"Mambo yote hayo yapo kwenye hatua za majadiliano ambayo hujulikana kitapları kama "Wheeling Charges Agreement." amesisitiza Luoga.
Kulingana na kamishna huyo, mkubaliano yakikamilika, Ethiopia itaanza kuiuzia umeme Tanzania.
Kupitia mradi huo pia Tanzania itakuwa imejitosheleza katika nishati ya umeme na hivyo kuwa na uwezo wa kuiuzia tena Ethiopia au nchi yoyote katika ukanda wa Afrika Mashariki.
Chanzo TRT Afrika
Mbona ilisemekana bwawa la Nyerere litazalisha mpaka umeme wa ziada?Tanzania inalenga kuongeza upatikanaji wa nishati ya umeme nchini kufuatia mpango wa kuanza kununua nishati hiyo kutoka Ethiopia.
Tayari mamlaka za nishati kutoka nchi hizo mbili zipo kwenue meza ya majadiliano kukubaliana kuhusu vifungu, vigezo na masharti ya makubaliana hayo ya miaka 20.
Katika makubaliano hayo, shirika la umeme la Ethiopia litakuwa linaiuzia Tanzania nishati ya umeme, kupitia shirika la TANESCO.
Soma:
Kwa kuanzia, Tanzania inalenga kununua Megawati 100 za umeme kutoka Ethiopia, baada ya kukamiliaka kwa majadiliano ya awali.
- Ahadi zilizowahi kutolewa na Viongozi kuhusu kuuza Umeme nje ya Nchi
- Mtambo wa pili bwawa la Nyerere kuwashwa, kumaliza kabisa mgao wa umeme nchini
- Waziri Biteko: Tanzania imejipanga vema kuhakikisha inatumia fursa ya uwepo wa soko la pamoja la EAPP la mauziano ya umeme
"Lengo la mpango huu ni kuunganisha mradi wa umeme wa Afrika Mashariki na ule wa Kusini mwa Afrika, ambapo Tanzania itakuwa katikati ya miradi hiyo miwili. Kukamilika kwa huu mpango kutafanikisha kuuziana umeme kati ya nchi za Afrika Mashariki na zile za Kusini mwa Afrika." anaeleza Mhandisi Innocent Luoga, Kamishna wa Umeme wa Nishati Jadilifu, kutoka wizara ya nishati nchini Tanzania.
"Mambo yote hayo yapo kwenye hatua za majadiliano ambayo hujulikana kitapları kama "Wheeling Charges Agreement." amesisitiza Luoga.
Kulingana na kamishna huyo, mkubaliano yakikamilika, Ethiopia itaanza kuiuzia umeme Tanzania.
Kupitia mradi huo pia Tanzania itakuwa imejitosheleza katika nishati ya umeme na hivyo kuwa na uwezo wa kuiuzia tena Ethiopia au nchi yoyote katika ukanda wa Afrika Mashariki.
Chanzo TRT Afrika
Na mimi nilisikia vivyo hivyo!Walisema Sasa hivi umeme unaozalishwa ni mwingi kuliko matumizi,hivyo umeme mwingine utauzwa nje ya nchi ie,Malawi,Zambia,na Kenya,Sasa inakuaje Tena tununue umeme wakati sisi tunauza?
Cha muhimu ulipe kodi,pesa zikusanywe,ziende hazina,zichukuliwe na baadhi ya vuongozi wetu,wazitumie watakavyoona INAFAA.Tuache tu. Hamna hata haja ya kujadili.