Tanzania Labour Law (Sheria ya Kazi Tanzania)

Tanzania Labour Law (Sheria ya Kazi Tanzania)

safi safi mtoa uzi sasa tujiulize kwanza humu ndani ya JF wangapi wetu tuna mikataba na wasaidizi wetu kwenye majumba yetu(domestics helpers) je tunawatendea haki ya kuwapa mishahara inayositahili?tunawapa likizo zao?muda wao wa kazi kwa siku upo kisheria?nini marupurupu yao kama chakula ,malazi je vipo above board?tukumbuke wote tumetoka kwa Mungu na tutarudi kwake kumnyanyasa binadamu wenzako kisa hakuwa blessed the way we are ni mbaya mno.

Haa haaa asante kwa kuibua changamoto ambayo hata sisi inatusumbua ktk kazi zetu, ni bahati mbaya kuwa kwa Tanzania bado hatujawa na muongozo mahsusi wa kukagua hii domestic sekta kutokana na changamoto ya hiyo sekta mathalani unaweza kwenda mwenye nyumba asifungue geti, na hata ukienda lazima ushirikishe uongozi wa mtaa usije zuliwa jambo kwamba umeenda kumhoji beki 3 bila boss wake kuwepo ukaambiwa umechukua vitu ama umemfanya jambo...so ni sekta nyeti kidogo. Lakini hii haizuii wao kuwa binded na Sheria za kazi kama kupewa mkataba wa Ajira na stahiki zote

Kwa faida ya wengi, hawa domestic workers nao wana kima chao cha chini cha mishahara kama ifuatavyo;
  • Tsh. 80,0000/= kwa mwezi kwa mfanyakazi ambaye halali kwa mwajiri wake, yaani yule ambaye anakuja kukufanyia kazi halafu jioni anarudi kwake/kwao
  • Tsh. 40,000/= kwa mwezi kwa mfanyakazi ambaye analala kwa mwajiri. Hili kundi ndio lipo kubwa, na iko ndogo kuliko anayerudi kulala kwao kwa sababu tunaamini huyu anayelala kwa mwajiri wake ina maana gharama za chakula, malazi, mavazi na matibabu ni juu ya mwajiri wake na ni nje ya mshahara wake huu.
Hiyo kima cha chini maana yake unaruhusiwa kumlipa kiasi chochote zaidi ya hapo hata ukiamua kumlipa laki ila hauruhusiwi kushuka chini ya hicho kiasi/kiwango elekezi.

Hivi vima vya chini vya mishahara ya kila sekta ni kwa Mujibu wa Tamko la Serikali Namba 196 la mwaka 2013
 
Mkuu nimekusoma asante sana. Sasa hebu nieleze jee tangu niwape maelezo yangu yakuwa Mimi sihuski na swala LA kumpima mtoto ni muda gani walipaswa kunijibu kwani sasa ni Sik 45 wako kimya sijajua hatua gani imechukuliwa dhidi yangu

Sina hakika sana ktk suala la muda wa wao kujibu shauri lako lakini ngoja nipitie pitie vifungu kuona hilo halafu nitajibu mkuu (kama sio ndani siku 14 i stand to be corrected by anyone who is aware of this please)
 
Sina hakika sana ktk suala la muda wa wao kujibu shauri lako lakini ngoja nipitie pitie vifungu kuona hilo halafu nitajibu mkuu (kama sio ndani siku 14 i stand to be corrected by anyone who is aware of this please)
Hicho ndo kimenikwamisha mkuu kwani nimeogopa kuwafuata isije kuwa bado wako ndani ya muda halafu wakanigeuzia kibao kuwa nawapangia cha kufanya, hebu nisaidie kipengere cha muda wa wao kunijibu Mara baada ya mm kuwa nimewajb
 
Hicho ndo kimenikwamisha mkuu kwani nimeogopa kuwafuata isije kuwa bado wako ndani ya muda halafu wakanigeuzia kibao kuwa nawapangia cha kufanya, hebu nisaidie kipengere cha muda wa wao kunijibu Mara baada ya mm kuwa nimewajb

Hili suala lako nimeenda kuonana na R.E.O ili anisaidie ufafanuzi maana tuko karibu karibu kiofisi, anasema kimsingi kwa sababu wewe umeshajieleza kwao kimaandishi, wakiona kuna ulazima utaitwa mbele ya Tume kujieleza halafu wao tume watapima maelezo yako na kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukuliwa, ila kwa sababu mpaka sasa haujaitwa mbele ya tume wala hawajakutumia barua ya kuhitaji maelezo zaidi wewe just sit back and relax mkuu.

Endapo utaitwa mbele ya Tume na ikatokea wakakuchukulia hatua ambazo hautaridhika nazo basi utafuata zile taratibu za kile kifungu nilichokutumia pale juu kukata rufaa ndani ya siku 45. Kwa sasa wee tulia huwezi jua labda maelezo yako yamejitosheleza ndo maana wameona hakuna haja ya hatua zaidi.
 
Hili suala lako nimeenda kuonana na R.E.O ili anisaidie ufafanuzi maana tuko karibu karibu kiofisi, anasema kimsingi kwa sababu wewe umeshajieleza kwao kimaandishi, wakiona kuna ulazima utaitwa mbele ya Tume kujieleza halafu wao tume watapima maelezo yako na kutoa mapendekezo ya hatua za kuchukuliwa, ila kwa sababu mpaka sasa haujaitwa mbele ya tume wala hawajakutumia barua ya kuhitaji maelezo zaidi wewe just sit back and relax mkuu. Endapo utaitwa mbele ya Tume na ikatokea wakakuchukulia hatua ambazo hautaridhika nazo basi utafuata zile taratibu za kile kifungu nilichokutumia pale juu kukata rufaa ndani ya siku 45. Kwa sasa wee tulia huwezi jua labda maelezo yako yamejitosheleza ndo maana wameona hakuna haja ya hatua zaidi.
Asante sana mkuu[emoji112] [emoji112] [emoji112] [emoji115]
 
Ahsante sana Mkuu kwa kutufungua macho. Hapa ninashida moja mimi na mwajiri wangu, yeye hataki kabisa vyama vya wafanyakazi. Tumejiunga na TUICO na mimi nikawa Katibu wa Tawi kila siku ugomvi na kutishiana Maisha. nimejaribu kuwasiliana na Uongozi wa Mkoa naona nao kama wanamuogopa. Issue kama hii Sheria zinasemaje?
 
Ahsante sana Mkuu kwa kutufungua macho. Hapa ninashida moja mimi na mwajiri wangu, yeye hataki kabisa vyama vya wafanyakazi. Tumejiunga na TUICO na mimi nikawa Katibu wa Tawi kila siku ugomvi na kutishiana Maisha. nimejaribu kuwasiliana na Uongozi wa Mkoa naona nao kama wanamuogopa. Issue kama hii Sheria zinasemaje?

Mumekwishasaini Mkataba wa Kutambuana kati na TUICO na huyo Mwajiri?
 
Tulimpelekea asaini hajasaini kauweka offisini kwake!

Hapo sasa Katibu wa TUICO Mkoa wasilianeni naye atimize wajibu wake mkuu, manake hapo ktk swali lako la msingi inaonekana mwajiri anakufanyia ubaguzi wa wazi kwa kuwa wewe ni member/kiongozi wa trade union (hapa inabidi utunze ushahidi ili ikibidi kuja ku-institute case ktk labour court uweze kuwa na evidence).

Sasa hapa cha kukazia kwanza ni Katibu wa Tuico Mkoa akazie utiwaji saini wa hiyo Recognition Agreement, na kama Mwajiri ataweka ubabaishaji basi Huyo Katibu anajua hatua za kuchukua kisheria (kwamba baada siku 30 mwajiri hajafanya hivyo katibu alitakiwa amfungulie case CMA, refer section 67-(5) of ELRA No.6/2004) unless otherwise kama naye ameshatekwa na mwajiri, na ni wajibu wenu kumkazia huyo Katibu wa Mkoa manake mnalipa ada za uanachama (2% mnayokatwa kwenye mshahara) so mnayo haki ya kumkazia kuhusu suala hilo ili sasa ukishasainiwa uweze kuchukua hatua kama kiongozi cha trade union ambayo inatambulika kisheria eneo la mwajiri.

Na mkataba huo ukishasainiwa ikiwapendezeni basi muende mbali zaidi kwa kiungia hata 'Collective Bargaining Agreements' (CBA) nadhani kiswahili chake ni 'Mikataba ya Hali Bora za Wafanyakazi' na usajiliwe kwa Kamishna wa Kazi (Wizara ya Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu).
 
Mkuu asante sana kwa elimu hii. Ni muhimu sana kwa waajiriwa ingawa mara nyingi tunaajiriana kiholela sana na baadae mambo yakiharibika tunaanza kuhaha!!
 
Back
Top Bottom