Tanzania limekuwa taifa la wacheza kamari (Tanbet)

Tanzania limekuwa taifa la wacheza kamari (Tanbet)

Msimu umeishawa hela..tunaangalia hizi friendly matches.

Njoo kwenye bet na akili na hela usije kijinga kijinga.
 
Jifunze kupambana na hali yako wengne wanasema kla mtu ashinde mechi zake wacha wakubet wabet na ww zako peleka unakojua ni pesa zako
 
Jifunze kupambana na hali yako wengne wanasema kla mtu ashinde mechi zake wacha wakubet wabet na ww zako peleka unakojua ni pesa zako
Mimi sijamkataza mtu kubet bali natoa angalizo tu mkuu; hasa pale serikali na vyombo vyake wanaposhadadia mambo ya betting. Inauma sana.

Hata paketi za sigara zimeandikwa UVUTAJI WA SIGARA NI HATARI KWA AFYA YAKO lakini bado watu wanavuta. Ni uamuzi binafsi. Everyone does whatever s/he feels at his/her own risk. Ngoja kila mtu ajilipue kwa hasara yake mwenyewe.
 
Hali inatisha..
Madhara ya kamari ni makubwa sana mkuu; huchangia hata kwenye ajali za barabarani.
1687725448735.png
 
Watu wanabet roho za watu..
Hakika nchi hii imefika mahali pabaya sana kwenye suala la kamari. Hadi roho za watu zinachezewa kamari. Huku serikali inachezea kamari rasimali za taifa, huku wananchi wachezea kamari roho za watu. Hili ni tatizo kubwa sana.
 
1688141828660.png

Dar es Salaam. Uraibu wa kamari na michezo ya kubeti, wadaiwa kuwa chanzo cha ugomvi uliosababisha mauaji ya Mwanahamisi Pauline (Mwana Mjeshi).

Inadaiwa kuwa Omary Herman (39) maarufu kwa jina la Komi au Mjeshi, jana Jumatano Juni 28, 2023 alimuuwa mkewe ‘Mwana Mjeshi’ kwa kumchoma na kitu chenye ncha kali, na baadaye kujirusha kwenye treni iliyokuwa ikitoke Ubungo kwenda Gerezani, eneo la Ubungo Maziwa na hivyo kupoteza uhai wake.

Jana, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro alithibitisha kutokea kwa tukio hilo kwa kusema: “Taarifa hizo ni za kweli na yeye amejirusha kwenye treni, lakini tunaendelea kufuatilia kwa karibu, taarifa zaidi nitazitoa,” alisema Muliro.

Hata hivyo siku moja kabla ya kutekeleza tukio la mauaji hayo Komi aliandika jumbe mbili tofauti katika mtandao wa kijamii, wa Facebook zilizosema "Ndiyo imeshatokea na imebaki story" na nyingine "Yale maisha ya furaha yamekwisha sasa yamebaki ya huzuni". Leo Juni 29, 2023; Mwananchi Digital ilifika msibani ambapo ilidaiwa kuwa wawili hao walikuwa na ugomvi wa muda mrefu kutokana na kile kilichoelezwa ni malalamiko ya mwanamke huyo kutokana na kitendo cha mumewe kucheza kamari, kubeti kiasi cha kushindwa kuihudumia familia.

Ally Godoro ambaye ni mjomba wa marehemu Mwanahamisi, ameiambia Mwananchi Digital kuwa wawili hao walikuwa na ugomvi wa ugomvi wa muda mrefu hadi kufikia hatua ya kwenda mkoani Morogoro kwa baba mzazi wa mwanamke kupata suluhisho la mgogoro wao. "Mgogoro huu umekuwa wa muda mrefu na ulikuwa ukipelekwa kwa mzee kwa ajili ya kumaliza matatizo yao lakini haikusaidia hadi kufikia hatua ya kupeana talaka," alisema Godoro.

Naye dereva wa bajaji Imani Omary maarufu (Madega) ambaye alimsaidia marehemu Mwanahamisi kuhamisha vitu vyake siku moja kabla ya tukio la mauaji amesema, aliombwa na marehemu kumpeleka katika chumba kipya alichopanga na kuomba asimwambie mumewe Mjeshi mahali alipopanga.

"Mama Imani (marehemu) aliniomba nimbebee kitanda na godoro na alisema nisimwambie mumewe alipohamia, licha ya kuwa siku ya kuhamisha vitu vyake alisaidiwa na mumewe wake kubeba hadi barabarani," amesema Madega na kuongeza;

"Mwanamke alikuwa analalamika sana kuhusu tabia ya mumewe ya kuvuta bangi, kucheza kamari alimvumilia kwenye bangi lakini kwenye kubeti waligombana sababu pesa zote za mshahara ziliishia kwenye kubeti.”
Kwa upande wa Jeniffer Java, dada wa Komi; amesema taarifa za msiba wa wifi yao walizipata saa 2 asubuhi, na baadaye walienda eneo la tukio na kukuta mwili wake ukiwa chini umelala.

Hata hivyo licha ya kaka yao kutekeleza tukio hilo, waliweka vikao kwa ajili ya kujua namna ambavyo kama familia wangehusika katika msiba huo, na kwamba wakati wakiwa kwenye maandalizi hayo, alipokea taarifa ya msiba wa mdogo wake kuwa amejirusha kwenye treni.

"Majira ya saa 11 jioni tulipigiwa simu na msamaria mwema, kupitia simu ya wifi yetu (mwanamke aliyeuwawa) ambaye alituambia mwenye simu amefariki kwa kujirusha kwenye treni na kufa papo hapo," alisema na kuongeza;
"Tulipofika kwenye eneo la tukio mashuhuda walituambia, alikaa muda mrefu eneo lile na aliziweka simu zake pembeni, ilipokuja treni aliacha kichwa na behewa la kwanza na la pili lipite ndipo alipojirusha kwenye behewa la tatu," alisema Jenifer.

Jenifer ameliambia Mwananchi Digital kuwa: "Komi alikuwa na ugomvi wa mara kwa mara na mkewe, sababu kubwa ni kubeti kwani pesa zote za mshahara zilikuwa zinaishia huko na mkewe hakuweza kuvumilia na kuamua kuomba talaka ili akanzishe maisha yake."

Aidha baada ya kuachana alisema marehemu (Mwanahamisi) alienda kwao Ngerengere, na alivyorudi Dar es Salaam alipanga chumba maeneo ya Gongo la Mboto na baadae kuamua kurudi Manzese kutokana na shughuli zake za ususi kuwa mbali na wateja wake.

"Wifi yetu ni msusi aliona kutoka Gongo la Mboto hadi Manzese ni mbali, alikuwa akitumia nauli nyingi akaamua kupanga jirani na shughuli zake, alivyopata chumba juzi na kuondoka alisaidiwa na mumewe, lakini jana (juzi) alimpigia simu mkewe aende kwake kuna mteja anahitaji kusuka na ndipo kulipotekeleza mauaji hayo," alisema na kuongeza.

Imeelezwa kuwa, wawili hao kabla ya kutengana; waliishi pamoja kwa miaka tisa, na kwamba wameacha watoto wawili Haiman Omary (7) na Abdulaziz Omary (2).

Chanzo: Mwananchi (30/06/2023)
 
Hivi sasa hivi Tanzania kuna makampuni mangapi ya Kamari. Ninajua kuwa kwa Marekani, kamari imedhibitiwa sana; kuna makampuni machache sana ya kamari Marekani na yana mipaka ya wapi yanafanyia shughuli zao ukiachia yale mawili makubwa bahati nasibu ya Mega Millions na Powerball ambayo shughuli zake zinasimamiwa pia na serikali za state husika. Inaonekana kwa Tanzania yeyote mwenye pesa milioni 300 anaweza kuanzisha kampuni ya kamari na kuwakamua watanzania nchi nzima.
 
😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣🤣
 
Hivi sasa hivi Tanzania kuna makampuni mangapi ya Kamari. Ninajua kuwa kwa Marekani, kamari imedhibitiwa sana; Kuna makampuni mchache sana ya kamari Marekani na yana mipaka ya wapi yanafanyia shuighuli zao ukiachia yale mawili makubwa bahati nasibu ya Mega Millions na Powerball ambayo shughuli zake zinasimamiwa pia na serikali za state husika. Inaonekana kwa Tanzania yeyite mwenye pesa milioni 3000 anaweza kuansisha kampuni ya kamali na kuwakamua watanzania nchi nzima.
Tunatengeneza taifa la ovyo sana. Miaka michache ijayo watanzania 99% watakuwa waraibu wa kamari na mateja wa kubet wa kutupwa!
 
Naingia kwenye mada moja kwa moja pasipo kuwachosha. Inasikitisha kuona kwamba nguvukazi ya taifa inapotea bure kwa kujikita kwenye uchezaji wa kamari. Kwa utafiti mdogo nilioufanya, kamari imekita mizizi kila mahali. Mara nyingi watu wanapobishana kuhusu jambo fulani utawasikia wakiwekeana dau (kamari). Hiki ni kiashiria kuwa kamari imeingia damuni mwa kila mtanzania.

Redio zote nchini Tanzania, ikiwemo TBC, wanachezesha kamari, na nyingine huchezesha kwa saa 24 na kutoa matokeo kila baada ya nusu saa. Tunajenga taifa la wacheza kamari kwa lazima kisa tu serikali inapata mapato. Kibaya zaidi na serikali inaweka mkazo kwenye kamari kuliko kutafuta mbinu mbadala za kujenga ajira kwa vijana ili kuokoa taifa linalotopea kwenye uraibu wa kamari.

View attachment 2665544
Kijana aliyelemewa na uraibu wa kamari (Chanzo: JamiiForums Facebook page)

Niliwahi kutembelea kijiji kimoja ambako wizi wa mazao, mifugo na mali umeshamiri kwa kiasi kikubwa. Nilipofanya utafiti nikagundua chanzo cha wizi ni vijana ambao huiba mali za wananchi ili wapate fedha za kuchezea kamari. Tunajenga taifa la namna gani? Wallah miaka michache ijayo hata serikali nayo itaanza kucheza kamari kwa kutumia kodi za wananchi!

Katika hotuba ya bajeti ya mwaka wa fedha 2023/24, jedwali namba tano linaonyesha mgawanyo wa bajeti kisekta. Sehemu inayoonyesha "Maendeleo ya Uchumi", utaona kuwa Vijana, Kazi na Maendeleo ya Kukuza Ujuzi, fedha ambazo zimetengwa ni Sh20.3 bilioni. Zikiwa zimepungua kutoka Sh31.2 bilioni, mwaka wa fedha unaoishia, yaani 2022-2023.

Taarifa hiyo itakushitua mno ukisoma ripoti ya uchumi wa michezo ya kubahatisha Tanzania. Mwaka wa fedha 2018-2019, mapato ya michezo ya kubahatisha yalikuwa Sh96 bilioni, yakiwa yamepanda kutoka Sh78 bilioni mwaka uliotangulia. Hiyo ni ripoti ya Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania.

Mtandao wa utafiti na takwimu za kibiashara kwenye tasnia mbalimbali duniani, Statista Market Forecast, inaeleza kuwa mapato ya michezo ya kubahatisha Tanzania mwaka 2023 yanatarajiwa kufikia dola 75.09 milioni (Sh180 bilioni).

Kwa mujibu wa Statista, thamani ya soko la michezo ya kubahatisha Tanzania itakuwa dola 110.1 milioni (Sh260.4 bilioni), ifikapo mwaka 2027. Hali ikiwa hivyo, Serikali inapunguza fedha kwenye eneo la upishi wa vijana kuwa wataalamu.

Ukisoma Sheria ya Michezo ya Kubahatisha Sura ya 41 utaona kuwa mkazo mkubwa kwa sasa ni serikali kukusanya mapato kwenye michezo ya kubahatisha. Na pia serikali inakwenda kupunguza maumivu kwa wachezesha kamari kwa kuwapa punguzo la kodi kwenye mapato ghafi kutoka asilimia 25 hadi asilimia 18. Hapa maana yake waendeshaji wa kamari wataona ahueni zaidi. Hivyo, tutarajie makampuni yanayochezesha kamari kuongezeka hapa nchini.

Ukiachana na bajeti kuu ya Serikali, Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Fedha 2023-2024 inaonesha kuwa hadi Aprili 2023 Bodi ya Michezo ya Kubahatisha ilishatoa leseni 8,778 za michezo ya kamari. Hii ni sawa na asilimia 114 ya malengo. Mwaka ujao wa fedha leseni mpya 11,880 zitatolewa.

Ufafanuzi huo unamaanisha kuwa mkazo wa kukuza sekta ya kamari ni mkubwa na wakati huohuo uwekezaji kwa vijana ni mdogo. Maneno ni mengi kuanzia nyumba za ibada hadi kwa wapinzani kwamba vijana wasiwe waraibu wa kamari badala yake wafanye kazi za vipato.

Kamari au michezo ya kubahatisha, kama ilivyo jina lake, inapaswa kuchukuliwa kama michezo ya kujaribu bahati na kujifurahisha. Hivi sasa vijana wengi, tena siku hizi hadi wazee, wamegeuza michezo ya kubahatisha kuwa vyanzo vya mapato.

View attachment 2665539
Vijana wakicheza kamari katika kituo cha kuchezea kamari (Chanzo: Mtandao)

Serikali kwa kutambua hilo inapaswa kuwekeza vizuri kwenye eneo la vijana kwa kuwajengea ujuzi na uwezo waweze kujiajiri au kuajiriwa. Wimbi la vijana kuona michezo ya kubahatisha ni fursa za kimaisha, hadi kuwa mateja wa kamari, ni matokeo ya kukosa machaguo (options) ya kimaisha.

Mzunguko wa kifedha kwenye michezo ya kubahatisha, unashawishi vijana kuuona utajiri wa ghafla bin vuu kwa kucheza kamari. Bajeti inayoombwa kwa ajili ya Wizara ya Madini kwa mwaka ujao wa fedha ni Sh89 bilioni. Maana yake inazidiwa mbali na mapato ya michezo ya kubahatisha.

Rejea matarajio ya mapato ya michezo ya kamari kuwa Sh260 bilioni ifikapo mwaka 2027 halafu pitia fungu la Biashara na Viwanda kuwa Sh324.2 bilioni. Je, huoni dalili za michezo ya kubahatisha kuelekea kushindana na sekta nyeti ya Viwanda na Biashara?

USHAURI
Baada ya uchambuzi kuhusu sekta ya kamari na kuonyesha jinsi inavyochochewa na serikali, naishauri serikali iache mara moja kuharibu watoto (na wazee) wa watu kwa kuwajengea uraibu wa kamari. Badala yake serikali itafute fursa za ajira kwa vijana ili waache kucheza kamari wafanye kazi halali zenye staha zitakazowaingizia kipato halali.

Nafahamu watoto wa watunga sera hawahusiki kwenye uraibu wa kamari. Watoto wa wanasiasa wanakula maisha mazuri huko waliko. Ni watoto wa walalahoi tu ndio wamejikita kwenye kamari. Ipo haja ya kuwaonea huruma wapiga kura hawa kwa kuwa ndio wanaowaingiza madarakani. Nafahamu wanawaacha wapiga kura wapigike ili iwe rahisi kuwatumia kisiasa kupitia umaskii na kupigika kwao lakini yapaswa watambue kwamba Mungu anawaona. Hata kama hawawaogopi wanadamu, basi wamuogope Mungu.

Nawasilisha
Kama watawala wanafurahia mavuno kwa njia ya kodi bila kufikilia impact inayotokea kwa vijana unategemea nin., maana kuna nguvu kazi kubwa sana inapotea kwa ujinga wa betting.
 
KAMARI ILIVYOMUUA MWANAFUNZI

Mwanafunzi wa kidato cha nne, shule ya Sekondari Nkomolo, Nkasi mkoani Rukwa, Fredy Pupa (19) ameuawa kwa kuchomwa kisu wakati akicheza kamari baada ya kudhulumiana fedha na mwenzake.

Mkuu wa wilaya ya Nkasi amesema kuwa tukio hilo lilitokea Januari 29 majira ya saa 11 jioni wakati mwanafunzi huyo akiwa na kijana mwenzake, Samwel Nkoswe (20) wakicheza kamari.

Amesema mtuhumiwa wa mauaji hayo, alikuwa ameacha shule na alikuwa anaishi mtaani huku akijihusisha na vitendo vya kinyume na sheria kikiwepo cha kucheza kamari.

Imeelezwa kuwa wakiwa wanacheza mchezo huo, mtuhumiwa alikula hela za marehemu lakini alikataa kumpa pesa hizo na kuamua kutoa kisu alichokuwa nacho mfukoni na kumchoma Pupa ubavuni karibu na tumboni.

Baada ya kujeruhiwa mwanafunzi huyo alivuja damu nyingi kitendo kilichompelekea kupoteza maisha muda mfupi baadaye.

Baada ya kuona amefanya tukio hilo, mtuhumiwa alikimbia na kwenda kujificha kwenye mashamba yaliyopo kijijini hapo lakini wananchi walimsaka mpaka kumkamata na kisha kuanza kumshambulia, hadi sasa yupo hospitali akiendelea kupatiwa matibabu.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Rukwa, Justine Masejo, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa mwili wa marehemu umekabidhiwa kwa nduguzake kwaajili ya mazishi baada ya kufanyiwa uchunguzi hospitali.
 
Kama watawala wanafurahia mavuno kwa njia ya kodi bila kufikilia impact inayotokea kwa vijana unategemea nin., maana kuna nguvu kazi kubwa sana inapotea kwa ujinga wa betting.
Hata hii serikali bora tuibetia kwa waarabu tukiliwa tuliwe tu. Nchi imekuwa ya kipumbavu sana hii.
 
Tbc a media state wakihimiza cheza pesa. Sijui madam boss ten sijui djaro arungu.. n.k. for sure tupo kwenye vicious cycle [emoji22]
 
Back
Top Bottom