Tanzania: Mihimili mitatu ya Dola na mwingiliano unaokanganya

Tanzania: Mihimili mitatu ya Dola na mwingiliano unaokanganya

Umenena vema sana
JF palikuwa ni mahali patakatifu kwa kubishana, kukosoana, kuangana mkono kwa hoja. Bahati mbaya, siku zilivyokwenda, waliingia wengi ambao nadhani hawana uwezo wa kujenga hoja au wana uwezo lakini wanafurahia kujitoa ufahamu. Wanachoweza ni kutukana kwa sababu hicho ndicho kilicho rahisi sana kwa mtu ambaye upeo wake na uwezo wake wa kufikiri, ni mdogo. Kutukana, hata mwendawazimu anaweza, lakini hawezi kujenga hoja.

Kuna watu humu, tangu wajiunge, hawajawahi kuleta hoja ya maana wala kutoa mchango wenye hoja. Wao ni kutukana, kukejeli au kuleta mipasho.

Maovu yanayotendwa na watawala na mifumo yetu mibovu, haitawaathiri watu fulani tu, wajue itawaathiri watu wote wa sasa na hata wa vizazi vijavyo.

Magufuli alipoanza kutumia mamlaka yake ya Urais yasiyo na mipaka, hata familia Kikwete na familia yake, Kinana, Makamba, Membe, Lowasa, Sumaye na vigogo wengine wengi waliumizwa hasa mioyoni mwao. Lakini wakiwa kwenye madaraka, waliamini kuwa ubaya wa katiba unagusa kundi fulani tu. Na hata Samia, anaweza kuona hakuna umuhimu wa katiba mpya kwa sababu hii ya sasa inampa uhuru wa kuwa dikteta, asichokijua uhuru huo wa Rais kuwa dikteta, siku moja unaweza kutendeka dhidi yake, wanawe au wajukuu zake.

Jamii Forum, ilistahili pawe mahali pa hoja nzito, siyo majali pa kuleta ushabiki.
Ahsante ndugu kunielewa. Watu humu wengi hawayaelewi hayo na hilo ni tatizo kubwa. Na wanaposhindwa kuyaelewa matusi ndo huwajia haraka. Tuna kazi kubwa sana.
 
Namuamini Mungu wa hayati Chacha Wangwe alieuwawa kwa sababu ya kutaka kugombea uenyekiti wa chama cha mtuhumiwa wetu. RIP Chacha Wangwe Mungu ameanza kukulipia hapa hapa duniani.
Chacha Wangwe alikufa katka utawala ganiwa Chademaa au ccm?? Ina maana ccm wanachoweza ni kudhibiti vyama vya siasa na siyo kudhibiti uhalifu nchini,Ole Sabaya kawaumbua mlikuwa mnafanya matukio mnamsingizia Mbowe na Mtei,lakini leo Sabaya kawaumbua waziwazi kuwa alikuwa ni mtekelezaji wa mfumo dhalimu wa kiutawala unaoongozwa na ccm.
 
Rais aliagiza akina Rugemarila, wakae ndani, wakaa ndani. Rais mwinhine akaagiza akina Rugemarilla watolewe, wakatolewa. Kama tungekuwa na mahakama, Rugemarilla na
Haya mingine yamo ndani ya uwezo wa Rais. Kumbuka kesi za jinai zonaendeshwa na Jamhuri kupitia DPP ambaye ni mteuliwa na Rais. DPP anayo mamlaka kisheria kufuta kesi yoyote. Ikifika mahakamani Rais hana uwezo wa kisheria kuingilia. Kimsingi ikitokea mahakama imetoa uamuzi kwa kufuata maagizo ni udhaifu wa jaji/hakimu kutokujiamini.
 
Kinadharia, Tanzania ina mihimili mitatu ya utawala, SERIKALI, BUNGE NA MAHAKAMA.

Kuanzia awamu ya 5, kimamlaka, mihimili yote mitatu imekufa, umezaliwa mhimili mmoja tu, wa RAIS.

Ndiyo maana unasikia Rais ametoa hela, Rais ameiagiza mahakama, Rais amilikemea bunge.
Mwenye vifaranga vyake amekusikia
 
Hili ni tatizo la siasa kuingia katika mambo ya msingi ya nchi.

UNAFIKI na UCHUMIA TUMBO unaangamiza Taifa.

Tusisahau kuiombea nchi kila mara tusalipo.
 
Ulichoandika ni ujinga mtupu. Sema ndo hivyo unalinda kibarua chako kisiingie mchanga.
Kama alichoandika kwako ni ujinga! Basi wewe aidha ni mpumbavu kabisa! au ni wale policcm yule waziri wa kigogo aliowaita vilaza ambao kazi yao ni kulinda mabenki na kutembea matakoni mwa wanaume na wanawake wenzao. Kama alichoandika ni ujinga wewe ndiyo ambaye hata PGO yako huijui unafanya kazi kama kuku asiye na kichwa!

Siku nyingine ujifunze kupita mbali ukiona thread za wanaume
 
Uchambuzi mzuri sana.hongera.kwa mwenye akili akitafakari sawa sawa lazima aone uzito wa hichi ulichokiandika.ila sasa tunatokaje hapo ilhali kupata katiba mpya kupatikana kwake bado kuko chini ya hisani ya huo muhimili mtu.
 
Hoja za aina hii zilitakiwa zianze wakati wa hukumu ya Sabaya afu ndo wangemalizia katika hii hukumu ya Mbowe. Ila isiwe ile ya kunya anye kuku afu kwa bata ionekane kaharisha.
Mada imekuzidi uzito.rudi fb ndo kunakokufaa.
 
Ulichoandika ni ujinga mtupu. Sema ndo hivyo unalinda kibarua chako kisiingie mchanga.
Kasisi Martin Neomuller wa enzi ya Adolf Hitler aliwahi andika hivi;-
".......Alipowashughulikia Wayahudi sikujali, kwa kuwa mimi sikuwa Myahudi.
Niliposhughulikiwa hakuna aliyejali."
Mifumo ya haki, uhuru na demokrasia ikiharibiwa madhara ni kwa jamii nzima.
 
Mbowe anaita "Hangover" ya ujamaa.
Sijui una mawazo gani hadi unaandika hivi. Kwa taarifa yako familia ya kina Mbowe inaijua hela kwa vizazi visivyopungua vinne nyuma, wakati huo naamini familia yenu hata kujisitiri utupu mlikuwa hajui. Katika watu wasiohamishwa kwa vijiji vya ujamaa ni wa mkoa wa Kilimanjaro. Wewe Mrugaruga unaongea nini?
 
Sijui una mawazo gani hadi unaandika hivi. Kwa taarifa yako familia ya kina Mbowe inaijua hela kwa vizazi visivyopungua vinne nyuma, wakati huo naamini familia yenu hata kujisitiri utupu mlikuwa hajui. Katika watu wasiohamishwa kwa vijiji vya ujamaa ni wa mkoa wa Kilimanjaro. Wewe Mrugaruga unaongea nini?
Una uwezo mdogo sana wa kuchanganua mambo.

Ni hivi, katika kipindi cha SPEAKING OUT WITH TUNDU LISU mbowe alisema hii nchi bado inasumbuliwa na kile kinachoitwa HANGOVER YA UJAMAA inayofanya rais awe ndiyo kila kitu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ulichoandika ni ujinga mtupu. Sema ndo hivyo unalinda kibarua chako kisiingie mchanga.
Ni aibu mnoo na wewe kuwa kwenye jukwaa hili angalau ungempangua kwa hoja.hivyo ndo mwisho wako wa kufikiri!! Bora angenyamaza!!
 
Uchambuzi mzuri sana.hongera.kwa mwenye akili akitafakari sawa sawa lazima aone uzito wa hichi ulichokiandika.ila sasa tunatokaje hapo ilhali kupata katiba mpya kupatikana kwake bado kuko chini ya hisani ya huo muhimili mtu.
Wanaoyafanya haya wanajua kuwa ni ubatili. Lakini wanaushikilia huu ubatili ili wawafanye watu wote waishi kwa hisani yao.

Nini cha Kufanya:

1) Hata siku moja, huwezi kujadiliana na jambazi juu ya njia nzuri za kudhibiti ujambazi. Jambazi anatakiwa kulazimishwa kuacha ujambazi kwa kudhibitiwa.

Je, Watanzania tuna uwezo wa kuwadhibiti watawala ili walazimike kukubali matakwa ya wananchi? Swali lako linanipeleka kwenye hoja mpya.
 
Back
Top Bottom